Jacobus
JF-Expert Member
- Mar 29, 2011
- 4,708
- 1,733
Wakuu,
Naomba kufahamu nini maana ya mlango wa 'nane'. Hii imekuja baada ya dada mmoja kutaka kumfahamu bosi wake kama ni mlango wa nane, nilipomuuliza ana maana gani alinishangaa sana.
Pamoja na kufahamu maana ya mlango wa nane pia nitafurahi pamoja na milango mingine kwa idadi na maana yake.
Naomba kufahamu nini maana ya mlango wa 'nane'. Hii imekuja baada ya dada mmoja kutaka kumfahamu bosi wake kama ni mlango wa nane, nilipomuuliza ana maana gani alinishangaa sana.
Pamoja na kufahamu maana ya mlango wa nane pia nitafurahi pamoja na milango mingine kwa idadi na maana yake.
Disclaimer:
Mimi nilikaa darasani kujifunza elimu ya nyota (Astrology) lakini si-practice na wala siiamini. Hapa nitakumegea kidogo nilichojifunza.
Katika utabiri wa nyota (Astrology) kuna nyumba au milango 12 jumla (au kwa kizungu zinaitwa HOUSES).
Hii milango inashabihiana na zodiac signs (makundi ya nyota kwenye njia ya jua au ecliptic kama vile Virgo (Mashuke), Leo, Scorpion, nk.)
Sasa wakati unapozaliwa ile nyumba (au mlango) ambao jua ndipo lilipo, kwa mfano Germini (au mapacha) ndio mlango wako wa kwanza (First House). Mlango huu wa kwanza unakupa personality yako. Sayari na mwezi (hasa mwezi) zilivyojipanga kwenye huu mlango wako wa kwanza ndio una-finetune hiyo personality yako (mtu wa aibu au machachari au mpendwa na watu burebure tu, nk.)
Hii milango (houses) ni hii
Aires, Taurus, Germini, Cancer, Leo, Virgo, Libra, Scorpion, Sagittarius, Capricorn, Pisces, Aquarius
Sasa kwa mfano: Kama umezaliwa chini ya nyota (Mlango, au house) ya Germini, basi
Germini ni mlango wako wa kwanza
Cancer ni mlango wako wa pili
Leo ni mlango wako wa tatu
.
.
Capricorn ni mlango wako wa nane
.
.
Taurus ni mlango wako wa kumi na mbili
Kila mlango unatawala kitu fulani maishani mwako (kama ulivyo mlango wa kwanza kutawala personality yako)
Sasa mlango wa nane unatawala uzazi na kifo. Lakini huu ndio mlango ambao, kutegemea ni sayari gani zilikuwepo kwenye huu mlango na zilijipangaje wakati unazaliwa unaweza kukufanya uwe na bahati au mikosi.
Kwa hiyo watu wakisema kuwa mtu huyu ni wa mlango wa nane wanamaanisha kuwa mipangilio wa sayari na mwezi kwenye mlango wake wa nane wakati anazaliwa umempa haiba ya nuksi, mikosi, bahati mbaya, na si mtu wa kushirikiana nae kwa sababu atakuangamiza.
Hapa chini nitaweka link itakayokueleza hii milango (Houses) na ni mambo gani yanatawaliwa na hii milango.
Enjoy.
The 12 Astrological Houses: their Meaning