Kuombeana ni muongozo tuliopewa na Mungu.Imeelezwa vizuri sana katika Sala ya Baba yetu.Na Mungu anapoombwa hujibu.Rejea maombi ya Mama yake Yesu(Mariamu) kule kwenye harusi ya Kana.Na vile vile alituhakikishia kwa kwa kusema "..ni nani akiombwa na mwanae kitoweo/samaki atampa nyoka au mkate atampa jiwe..."?
Binafsi sina shida na yeye kuomba sala zetu dhidi yake kwa Mungu.Kuna watu toka tu alipoomba tumuombee tukaanza kazi hiyo mara moja.Mimi binafsi katika sala zangu namuombea Mungu ampe afya ya roho na mwili.Mungu amjalie kukua kwa misuli ya mwili sambamba na akili,hekima na busara.Kwamba amuongezee usikivu na utulivu. Na Mungu alivyokwisha kutuambia yumkini maombi yetu yatapokelewa na kujibiwa kadri tunavyoomba.Hatuwezi kumuombea Mungu ampe Magufuli hekima na badala yake Mungu ampe kiburi na kukurupuka.Tumuombee uvumilivu halafu Mungu ampe jeuri ya kuwatambia watu kuwa yeye hajaribiwi!
Kama ilivyo kwa maombi/ sala zetu kwa Mungu dhidi yake kwamba zinatoka kwa watanzania ndivyo ilivyo na kwa majibu ya maombi hayo.Kwamba Mungu atajibu sala/maombi yetu kupitia wale wale waliomba kwa niaba.Yaani kwa kupitia watanzania hao hao.Mungu hatashusha hekima,akili,uvumilivu na fadhila zingine kama Mana ya Jangwani.Hakuna siku Magufuli ataamka tu usingizini na kukuta fadhila tunazomuombea zimejaa kwenye ndoo au mebeseni Ikulu.
Mungu anateremusha fadhila za uvumilivu,ujasiri,upendo,umoja,amani,hekima na mambo mengineyo kupitia watanzania hao hao.Nanukuu" ...katika Agano la Kale Mungu amesema nasi kwa njia za Manabii...sasa katika Agano jipya amesema nasi kwa njia ya Mwanaye(Yesu).Na Mwanaye ametuachia msaidizi wake,Roho Mtakatifu.Roho Mtakatifu yuko kwenye mioyo ya watu.Anafanya kazi kupitia binadamu.
Kwa hiyo swali la kujiuliza ni je Magufuli anapoomba tumuombee anakubali pia tumuletee majibu ya maombi hayo?
Magufuli hawezi kila siku akawa anasema tu tumuombee bila kutupatia mrejesho wa kama anapokea majibu ya maombi.
Mungu ameshajibu maombi yetu.Watu wanamshauri Magufuli aache kukataza mikutano ya kisiasa.Watu wanamuambia aache kuchagua watendaji wa serikali kwa kuangalia tu wanaCCM.Watu wanamshauri aache kujitapa kuwa yeye hajaribiwi.Yesu alijaribiwa yeye inawezekanaje? Tunamtaka apokee majibu ya sala zetu kwa kufanyia kazi.Huwezi kuomba kitoweo ukateletewa halafu ukakacha.