Dhana ya kuombewa

Dhana ya kuombewa

Watu wanatishwa kila siku, watu hawaruhusiwi kukosoa, watu hawaruhusiwi kumchallange, watu wanakosa haki zao, wanafunzi wamefukuzwa km mbwa na wazazi wao wakalia machozi, wengne wamebomolewa nyumba zao, mama ntilie wanavunjiwa vyombo vyao na kumwagiwa vyakula. Hao wote wanalia machozi. Hakika machozi yao hayatakuwa bure.

Alafu unakuja kuwaambia hao hao wakuombee? Mungu anaona na anasikia kilio chao. Labda tumuombee hiki kilio kisije kikageuka laana kwake.
 
Wenye Afya Hawahitaj Daktari Bali Wale Walio Wagonjwa.Yesu Hakuja Duniani Kwa Ajili Ya Walio Watakatifu.Bali Alikuja Duniani Kwa Ajili Ya Wote Wenye Dhambi i.e Wezi, Waongo, Wafiraji, Wasagaji, Wauaji, Wasengenyaji, Wenye Choyo, Wenye Wivu, Wala Rushwa, Nakadharika Ili Wapate Kutubu.Kwahiyo Ni Wajibu Wetu Kuzidi Kuwaombea Watu Hawa Ili Waziache Njia Zao Zilizo Mbaya.Kondoo Mmoja Aliepotea Ni Bora Kuliko Kondoo Tisini Na Tisa Walio Kundini.
Tafsiri ya mkuu sio hii...tafsiri yake ni kwamba anapambana na mfumo wenye nguvu kubwa hivyo tumuombee apate nguvu zaidi za mapambano pia tumuombee ulinzi kwakuwa anaziba na kuua mirija ya upigaji
Lakini je ni kweli hiki ndio anachokifanya kwa asilimia mia moja? Mbona kuna ishu nyingine very sensitive zimefunikwa chini ya kapeti? Naona makengeza kila pahala kuanzia huko kwenye kuombewa mpaka kwenye utendaji na hata maamuzi. ..naona rangi nyingi kama za kinyonga kwamba anabadilika kulingana na rangi ya mazingira aliyopo, ni ngumu na kwa hakika kuijua rangi halisi ya kinyonga..kwenye uongozi hili ni jambo baya sana....
 
Ktk viumbe aliowaumba Mungu ni binadamu pekee ndiye aliyempa utashi zaidi..
Lakn kwa bahati mbaya Sana binadamu huyohuyo ndiye kiumbe hatar zaidi na ndiye anajitengenezea uadui zaidi kwa Mungu..

Hata Jesus pamoja na kuwatendea mema na kuwafufua wafu, kuwaponya viwete, vipofu wenye pepo mbaya bado hawakuutambua wema wake ule wema waliugeuza ukawa ubaya..

Hata walipo mkamata simon peter alipomkata sikio mmoja Wa waliokuja kumkamata Yesu alimponya huyo mtu lakn bado hawakuweza kumtambua Bali hasira na chuki ndio ziliwajaa..

Huyo ndio binadamu
 
Umeongea point moja ya maana sana ivi kweli unamuombea mfalme badala ya kumuombea maskini anayelala bara barani apate tahafifu ya mwenyezi mungu inashangaza
Mtu anayeitwa maskini kwa mujibu Iman unamjua?
 
Usidanganyike Mungu adhihakiwi chochote mtu apandacho ndicho avunacho..Anataka aombewe wakati anapanda visasi,uonevu,uadui,vitisho na ubabe daah ngoja tusubiri mavuno yake
 
Hapa sikosoi dressing code na jinsi shati lilivyokaa vibaya..fulana ya blue na si vest nyeupe... bali ile dhana nzima ya kuombewa
1469940345572.jpg
kwamba mgonjwa ndie anamuombea mzima ubinafsi wa kiwango chake
 
Kumuombea asiyetenda haki ni sawa na kupaka upepo rangi, bora kuiombea familia yako ipate mkate wa kila cku, mtu hajui atakula nini kesho, akiugua hajui ka atapata huduma bora badala ajiombee mwenyewe anahangaika na mwenyewe ulinzi twenty four seven. Yesu aliwaambia wanawake wasimlilie yeye walilie shida zao na watoto wao. At the end kila MTU ataubeba msalaba wake.
Nchi hii wajinga hawatakaa waishe ..kuna watu hawataelewa ulichoandika mijitu haijionei huruma..Upuuzi huu nimeukataa Kanisani Mchungaji wangu anamkubali sana huyo jamaa sasa ikawa kila Ibada hakosi kulazimisha kumuombea asee Tangu uchaguzi wa Mwaka Jana tena ilitengwa siku maalum ya J5 sikuwahi kwenda...Honestly Watz%kubwa ni watu wapuuzi sana Asante mshana jr kuleta mada fikirishi
 
Itafika hatua tutaelewana tu..
Kwakuwa hatujui tukitakacho lakn pindi tukijua tutakuwa sawa
 
Halafu ni wachafu wazandiki waongo. ..mdomo mmoja unaomba kuombewa mdomo wa pili unatoa vitisho kuwa wewe hujaribiri
Hilo nalo neno... Mungu ameruhusu kujaribiwa kwa zaka...

Sasa mkulu hataki hata kujaribiwa kwa maandamano tuu.... Je ukimjaribu kwa kodi si ndio balaa kabisa.

Naunga mkono hoja ya kumuombea abadilike aliongoze taifa la mungu kwa HEKIMA zikiisha atumie BUSARA na aenende Katika HAKI na kuzishika SHERIA za BWANA na kuheshimu KATIBA tulilojiwekea watu wa MUNGU.

Mungu ibariki Tanzania Mungu mmbadili mkulu ku mwamo.

AMEN
 
Inafika wakati maombi yanageuka laana kama uadilifu hauzingatiwi..!
Hapa dunian ukitaka upendwe na uwe maarufu ww kuwa mnafki na muongo lakn ukiwa mtenda haki watu watakuchukia na kukuzushia kila aina ya ubaya..
Hata kwenye maandiko hayo yapo
Rejea akina petro na akina yohana
 
Ni neno la kawaida la kiimani kwa wale waamini na waaminio. Lakini awamu hii ya tano linaelekea kupata umaarufu
Nimejikuta napitia makabrasha mbalimbali ya kidini kuona ni nani wanaopaswa kuombewa na kwanini
.wagonjwa
.yatima
.Wajane
.wenye shida za kiroho
.wenye shida za kimwili
Hawa ndio tmefundishwa kuwaombea kwa imani ya kikristo
Lakini vile vile tuna maombi na sala maalum za kuombea Taifa na viongozi wake wote ...tuna maombi na sala rasmi kila siku ikianza na kila siku ikiisha
Napatwa na ukakasi mkubwa kuendelea kuombwa nimuombee mtu mwenye kila aina ya ulinzi kuanzia wa mitambo mpaka wa majeshi na usalama
Napatwa na mshangao kuendelea kuombwa nimuombee mtu ambaye hajui bajeti yake ya mahitaji ya kila siku kuanzia chakula usafiri ada za watoto shule , mahitaji ya ndugu na jamaa nk nk..vyote hivi anavipata bure na ziada
Hii ni aina fulani ya uchoyo na ubinafsi uliopitiliza...! Hivi yule mgonjwa pale Hospitali ataombewa na nani? Je yule mjane aliyedhulumiwa nyumba na mirathi yake yeye ataombewa na nani?
Nchi imezungukwa na matatizo na shida kila mahali ni vilio na maumivu...maisha magumu hela hakuna kazi hakuna....hawa ndio waombe? Wamuombee asiye na dhiki wala changamoto za maisha yetu haya???jamani mbona mnatuonea na kututia majaribu ni tumkufuru Muumba wetu
Yani kweli kabisa nitoke Muhimbili kumuangalia mgonjwa wangu ninayetakiwa kutafuta pesa ili aweze kutibiwa huku nadaiwa kodi ya nyumba na ada za watoto na mengine mengi...na uchovu wote na changamoto zote hizi halafu niombwe kumuombea mtu ambaye hata nilitaka kuonana naye siwezi? Kweli dunia ina mengi
Uongozi wa nchi ni uongozi wa kisiasa...michezo ya kisiasa inajulikana pote duniani ni michafu tena huku Africa ndio kabisa...kumhusisha Mungu kwenye mambo ya kisiasa ni kumdhihaki
Mtu Hapaswi kuwa na wasiwasi...kama una imani kwa Mungu wako na utendalo ni sahihi hata Mungu anajua , hupaswi kuwa na wasiwasi kwakuwa yeye hachagui wala habagui...na ukitenda kwa haki mkono wake utakuepusha na mabaya yote na malaika mlinzi atakuwa nawe bila hata maombi ya mzinifu, muongo, mtenda dhambi zote....
Mkuu hiyo dozi yako si haba.
 
Hapa sikosoi dressing code na jinsi shati lilivyokaa vibaya..fulani ya blue na si vest nyeupe... bali ile dhana nzima ya kuombewa View attachment 373692kwamba mgonjwa ndie anamuombea mzima ubinafsi wa kiwango chake
I sometimes fail how to comment and term you Mr Mshana jr. You are so challenging and analytical on faith matters. You speak openly, if ironically the truth is apparently. You are the one of the great thinkers in jf.
 
Back
Top Bottom