gharama zote ni milioni 10 kwa ujenzi wa kawaida kisha unahamia nyumba yako. Kwa anayetaka complicated finishing na installations ya vitu vya pesa ndefu basi ni 25-30 milioni.
kwa uzoefu wangu mdogo naona kama unawadanganya wananchi wa kawaida.....kwamba 10m ujenzi wa kawaida nyumba imeisha unahamia kwako...duhh. Sio kweli aisee. Nimepiga hisabati zangu naona kama msingi au hiyo unayoita substructure ukijibana sana itagharimu kama 7.326 milion kwa mchanganua huu hapa chini
1- tofali 1206 @ 1000/= = tshs 1,206,000/=
2- cement 30bags @13,000/= =tshs 390,000/=
3- mchanga 5 lories @ 150,000/= =tshs 750,000/=
4- chuma 30pcs y12 @ 16,000/= = tshs 480,000/=
5- zege 13.2 cubic metre @ 225,000/= =tshs 2,970,000/=
6- labour charges =tshs 1,000,000/=
7- gharama nyinginezo =tshs 500,000/=
hapo nimejaribu kuchanganua gharama za ujenzi wa msingi...na ikizingatiwa nyumba ni msingi ndugu yangu...sasa tunafikia milion 7...hatujanunua bati, hatujanunua mbao, hatujanunua milango na madirisha, bado wiring, bado plumbing installations, bado plastering nje na ndani, bado ceiling brandering, bado ceiling boards, bado skimming, bado painting, bado magrill ya milango na madirisha.
Kaka unawadanganya watu...waambie ukweli wakiingia waingie kiume au wawe wamejipanga kujenga.
Kwa uzoefu wangu hicho kijumba cha vyumba viwili kwa hizo sq metre 88 hakuna jinsi utakimaliza kukijenga kwa standard ya kawaida kikawa chini ya mill 44. Na ukizingatia muonekano wake kwenye 3d au perspectives...kinaweza kuzidi gharama iwapo anasa zitazidi kwenye finishing.
Ni hayo tuu....