Dereva wa treni ya abiria hupataje taarifa kama kuna dharura au hatari ili aweze kusimama

HOPEfull

JF-Expert Member
Apr 8, 2021
1,722
2,073
Kwenye usafiri wowote kunaweza kutokea hatari au dharura yeyote..Nakumbuka nikiwa Kwenye safari fulani ya gari moshi ilitokea sintofahamu ndani ya mabehewa abiria wakawa wanataka kwenda kutoka nje huku treni iko kwenye mwendokasi lakini bahati nzuri treni ikasimama katikati ya pori na hiyo sintofahamu ikawa 'solved' na safari kuendelea.Sasa wadau nauliza dereva wa treni hupataje taarifa kama kuna hatari na yeye huwa mbali na mabehewa na anakuwa peke yake.
 
Dharura ya abiria kutaka kutoka nje zaidi ya msalani ni dharura gani tena? Treni si zina vyoo mumo kwa mumo?

Kuna wale wahudumu wa ndani, wanawasiliana inapotokea chochote. Lakini kikubwa itakua kuna namna ya mawasiliano kati ya dereva na wafanyakazi wengine wakati wa safari.

Nimevutiwa kujua hiyo ilikua dharura ya aina gani iliyolazimu treni kusimama?
 
Kwenye usafiri wowote kunaweza kutokea hatari au dharura yeyote..Nakumbuka nikiwa Kwenye safari fulani ya gari moshi ilitokea sintofahamu ndani ya mabehewa abiria wakawa wanataka kwenda kutoka nje huku treni iko kwenye mwendokasi lakini bahati nzuri treni ikasimama katikati ya pori na hiyo sintofahamu ikawa 'solved' na safari kuendelea.Sasa wadau nauliza dereva wa treni hupataje taarifa kama kuna hatari na yeye huwa mbali na mabehewa na anakuwa peke yake.
Captain wa train hawezi kuwa mwenyewe. Lazima kuna crew ya watoa huduma, kuna engineers (mafundi) n.k
 
Dharura ya abiria kutaka kutoka nje zaidi ya msalani ni dharura gani tena? Treni si zina vyoo mumo kwa mumo?

Kuna wale wahudumu wa ndani, wanawasiliana inapotokea chochote. Lakini kikubwa itakua kuna namna ya mawasiliano kati ya dereva na wafanyakazi wengine wakati wa safari.

Nimevutiwa kujua hiyo ilikua dharura ya aina gani iliyolazimu treni kusimama?
Nimekupata ni kwamba abiria walikuwa wanataka kutoka nje ya treni na wengine kuruka.Sijataja tukio kwa uwazi kwa sababu sijui linaweza likawa na mgongano fulani labda.
 
Dharura ya abiria kutaka kutoka nje zaidi ya msalani ni dharura gani tena? Treni si zina vyoo mumo kwa mumo?

Kuna wale wahudumu wa ndani, wanawasiliana inapotokea chochote. Lakini kikubwa itakua kuna namna ya mawasiliano kati ya dereva na wafanyakazi wengine wakati wa safari.

Nimevutiwa kujua hiyo ilikua dharura ya aina gani iliyolazimu treni kusimama?
Inaonekana liliibuka Joka ndani ya treni...
 
Kwenye usafiri wowote kunaweza kutokea hatari au dharura yeyote..Nakumbuka nikiwa Kwenye safari fulani ya gari moshi ilitokea sintofahamu ndani ya mabehewa abiria wakawa wanataka kwenda kutoka nje huku treni iko kwenye mwendokasi lakini bahati nzuri treni ikasimama katikati ya pori na hiyo sintofahamu ikawa 'solved' na safari kuendelea.Sasa wadau nauliza dereva wa treni hupataje taarifa kama kuna hatari na yeye huwa mbali na mabehewa na anakuwa peke yake.

Kwenye treni kuna utingo/kondakta au wewe hukuwaona ulipopanda hiyo treni?
 
Kwenye treni kuna wakaguzi wa tiketi jina maarufu matitii,mwisho wa treni kuna behewa huwa wanakaa askari na wahudumu wengine wa treni.
Miaka ya nyuma sana niliwai kuona jinsi mtu aliekua ilo behewa la mwisho akimpa ishara ya kusimama na kuondoka dereva aliyeko mbele,kipindi icho huyo jamaa wa behewa la mwisho alikua anatumia bendera nyekundu na kijani.kwa usiku alikua akiwasha taa ya kijani au nyekundu zipo pembeni ya ilo behewa la mwisho upande wa kulia na kushoto.wakati mwingine alikua akiwasha tochi za kawaida kumpa ishara dereva alieko mbele.
hiyo niliona miaka ya tisini uko.
 
Back
Top Bottom