Jibu la haraka haraka.
Hii ina maana katika kuhitimu mafunzo (shahada) yake ameshika nafasi ya tatu.
Shahada zipo kwenye viwango hivi na nitavifafanua baadae:
- 1st class honors au (Summa cum laude): Nafasi ya juu kabisa (ya kwanza)
- Upper 2nd class honors au (Magna cum laude): Nafasi ya pili
- Lower 2nd class honors au (Cum laude): Nafasi ya tatu
- Pass (au Thank-you Oh Lord degree a.k.a. gentleman degree)
- Fail (umefeli au kushika mkia)
​
LOWER SECOND WITH HONORS inamaana gani?
Inamaanisha kuwa katika masomo ya kozi yake amejitahidi na kupata
GPA (Grade Point Average) ya wastani wa
B+ kwa masomo yote. Hii
GPA sio kiashiria cha mafanikio yake kwenye maisha au kazini. Kwa mwajiri hii ina maana huyu kijana akimpa jukumu unaweza kutegemea ufanisi mzuri zaidi ya wastani (better than average performance). Aina ya shahada iliyopo kwenye cheti chako itakusaidia tu kufungua milango katika kutafuta ajira.
Inawezakana kabisa mwanafunzi mwenye
pass (B) degree akawa na
ufanisi wa A+ kazini na
1st class honor (A+) degree holder akawa na
ufanisi duni kazini.
Hii GPA inakokotolewaje?
Nitakupa mfano hai ninaoufahamu mimi kwa hapa nilipo. (Utaratibu huu unaweza kutofautiana na sehemu nyingine).
Kuanzia mwaka wa kwanza mpaka mwanafunzi anamaliza shahada yake kila somo akilimaliza atapewa alama ya
A, B, C, D, F kufuatia na ufaulu wake. Kila alama ina uzito wake (huu uzito unatofautiana kutoka shule hadi shule) kama ifuatavyo:
A+ = 5.0
A =4.5
A- =4.0
B+ =3.5
B =3.0
B- =2.5
C+ =2.0
C =1.5
C- =1.0
D+ =0.5
F =0
Zaidi ya kila alama kuwa na uzito wake, pia kila somo linapewa uzito kulingana na ugumu au umuhimu wake katika hiyo shahada.
Kwa mfano: Kama unafanya shahada ya uchumi
(Economics), basi somo linalochambua sera za kiuchumi
(MONETARY/FISICAL policies) litakuwa na uzito mkubwa kuliko somo la mwaka wa kwanza kama
Introduction to Microeconomics. Uzito wa somo pamoja na uzito wa alama aliyopata mwanafunzi ndivyo vinavyotumika kukokotoa (weighted average)
GPA.
(Kama utataka mfano wa kukokotoa weighted average nitonye nitakuwekea)
Hivi ndio viwango vya shahada kufuatia
GPA yake atakapomaliza shahada yake:
4.00-5.00 - 1st class honors au (Summa cum laude): Nafasi ya juu kabisa (ya kwanza)
[A-, A, A+]
3.80-3.99 - Upper 2nd class honors au (Magna cum laude): Nafasi ya pili
[upper B+]
3.5-3.79 - Lower 2nd class honors au (Cum laude): Nafasi ya tatu
[lower B+]
2.5-3.49 - Pass (Thank-you Oh Lord degree a.k.a. gentleman degree)
< 2.5 - Fail