Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,599
MwanaHaki;424182]Mungu ashukuriwe kwa lipi ndugu yangu?
Kwa sababu hatimaye dawa ya ujinga imepatikana. Ni hatari watu wenye akili kukaa kimya wakati mambo ya kipuuzi yanayoiumiza jamii yakiachwa yaendelee
DECI haikuanzishwa ili IKOPESHE wanachama wake, kwani waanzilishi wake, ambao ni watu wa KANISA, walitambua kwamba kufanya hivyo kungekuwa ni kuzidi kuwakandamiza watu maskini, mafukara, wasiokopesheka, wasio na hata hati ya kibanda, ambao wakienda benki wanarudishwa nyuma, na wakienda PRIDE na FINCA wanaambiwa wajiunge vikundi vya watu 5 kila kikundi, na wanageuzwa kuwawatumwa wa kufanya kazi kwa bidii ili WALIPE RIBA ya mkopo, hatimaye kushindwa kulipa mkopo!
Kama kweli wewe na wenzio wa DECI na baadhi ya Watanzania mnataka utajiri bila kutoka jasho basi mmepotea njia. Labda mkaishi sayari nyingine, kwa sababu hiyo ni laana toka kwa Mungu, kwamba kila mwanadamu atakula baada ya kutokwa jasho. Sasa wale wanaotaka faida ya 100% huku wakicheza bao mchana kutwa haya, hiyo adhabu ya DECI ndiyo haki yao wanayoistahili.
Kama ninayoyasema ni uongo, waulizeni PRIDE na FINCA wawambie wana wanachama wangapi mpaka sasa na DECI wana wanachama wangapi?
Najiuliza sana kama unajua unalolisema. Kwani kati ya wafanyabiashara wa kawaida na mafisadi wa EPA, akina nani wanatajirika haraka? Na kama hizo shughuli zote zingekuwa wazi ili kila mtu aingie ni wapi ungepata wafuasi wengi? Huwezi kulinganisha wizi na kazi halali.