DECI Tanzania: Ilivyoanza, ilipo na hatma yake

MwanaHaki;424182]Mungu ashukuriwe kwa lipi ndugu yangu?

Kwa sababu hatimaye dawa ya ujinga imepatikana. Ni hatari watu wenye akili kukaa kimya wakati mambo ya kipuuzi yanayoiumiza jamii yakiachwa yaendelee

DECI haikuanzishwa ili IKOPESHE wanachama wake, kwani waanzilishi wake, ambao ni watu wa KANISA, walitambua kwamba kufanya hivyo kungekuwa ni kuzidi kuwakandamiza watu maskini, mafukara, wasiokopesheka, wasio na hata hati ya kibanda, ambao wakienda benki wanarudishwa nyuma, na wakienda PRIDE na FINCA wanaambiwa wajiunge vikundi vya watu 5 kila kikundi, na wanageuzwa kuwawatumwa wa kufanya kazi kwa bidii ili WALIPE RIBA ya mkopo, hatimaye kushindwa kulipa mkopo!

Kama kweli wewe na wenzio wa DECI na baadhi ya Watanzania mnataka utajiri bila kutoka jasho basi mmepotea njia. Labda mkaishi sayari nyingine, kwa sababu hiyo ni laana toka kwa Mungu, kwamba kila mwanadamu atakula baada ya kutokwa jasho. Sasa wale wanaotaka faida ya 100% huku wakicheza bao mchana kutwa haya, hiyo adhabu ya DECI ndiyo haki yao wanayoistahili.

Kama ninayoyasema ni uongo, waulizeni PRIDE na FINCA wawambie wana wanachama wangapi mpaka sasa na DECI wana wanachama wangapi?

Najiuliza sana kama unajua unalolisema. Kwani kati ya wafanyabiashara wa kawaida na mafisadi wa EPA, akina nani wanatajirika haraka? Na kama hizo shughuli zote zingekuwa wazi ili kila mtu aingie ni wapi ungepata wafuasi wengi? Huwezi kulinganisha wizi na kazi halali.
 
Je pale ambapo mwenye njaa anataka kumsaidia mlala hoi mwenzake asiibiwe lakini isikilizwi inakuwaje? Kwani tuliyoyasema humu kuhusu huo wizi ni kidogo? Sikio la kufa..... Na sasa wauguze majeraha tu!

Na je, ukiwa masikini ndo unapoteza hata akili za kawaida tu za kutambua mema na mabaya? Naona kama mengine ni visingizio tu vya kuhalalisha ujuha. Siyo wote waliokwenda kupanda DECI ni masikini au wasiosoma, ingawa si kila aliyesoma ameelimika!

Dark City mkuu, naomba nikupe mkono! Umeongea, Visingizio wanavyojaribu kuleta are PATHETIC! MAfisadi ni nani? NI hao watu walioanzisha DECI na wamewaibia pesa zao watu maskini! Wewe unayetoa ushauri mzuri na tahadhari unaambiwa eti kwa vile huna shida. Nobody should judge you mkuu! DECI ni pyramid scheme ... PERIOD ...the rest is just noise!
 
Mungu ashukuriwe kwa lipi ndugu yangu? 1) Ashukuriwe kwa ufisadi waliofanyiwa watu maskini, ambao sasa wanalia na kusaga meno, wakiwa na hofu kuu juu ya usalama wa fedha zao? au 2) Ashukuriwe kwa ufisadi waliofanyiwa watu maskini, ambao kila uchao wanadanganywa na wanasiasa (soma Watawala) kwamba wataletewa maendeleo, ambayo mpaka leo yamekuwa ni ndoto. Nafasi pekee waliyoipata wananchi ya kujipatia maendeleo ya kweli imezimwa kama mshumaa uliozimika kwa upepo mkali... Upepo hauna muamana na kila kilichoko kwenye njia yake... Wanasiasa nao vile vile, hawana muamana na yeyote yule aliyeko kwenye njia yao, wanamuona kila anayetaka kuleta maendeleo ya kweli kuwa hatari kwa uhai wao, kwani, maendeleo yakija, wanasiasa watakosa kazi... watamwambia nani juu ya maendeleo ambayo tayari YAPO? Mmeshabikia kufutwa kwa DECi bila kupambanua kwa kina nini kinachoendelea. 1) Mwaka 2007, PRIDE Tanzania ilichukua mkopo wa USD 1.2 million kutoka Hivos-Triodos Fund. Kwa mujibu wa taarifa zilizoko kwenye Internet (nenda uka-google utapata), PRIDE Tanzania "is the largest microfinance institution in Tanzania". Haya, hii taasisi ya microfinance iliyo kubwa kuliko zote, iliyoanzishwa miaka ya 90, ina wanachama 75,000 (takriban), mpaka sasa. DECI, iliyoanza shughuli zake 2006 ina takriban wanachama 500,000! Mjiulize: Kwa nini DECI imefanikiwa mapema haraka kiasi hicho? Ina maana watu wote hao ni wajinga na mbumbumbu, wasiojua kwamba wanatapeliwa? 2) Kuanzia 2006, wakati DECI ilipoanzisha Tushikamane Revolving Fund, haikukopesha, lakini mwaka 2007 ilipoomba kibali cha kuwakopesha wanachama wake huko Wizara ya Biashara na Viwanda ILIKATALIWA. Haya, LEO hii Gavana Benno Ndulu anasema DECI isajiliwe ili IWAKOPESHE wanachama wake. 3) Mojawapo ya kundi la wanachama wa DECI ni wafanyakazi wa Benki (kama vile NMB, CRDB na nyinginezo...). Hawa, baada ya kuona hawatapata faida ya maana kwenye benki zao, wamekuwa wakichukua mikopo ya muda mfupi, wakipanda mbegu zao na kuvuna, kisha kurejesha mikopo hiyo na kuendelea na kupandikiza mbegu hizo, kwenye mfumo huo wa revolving fund. Wale walioanzia 2006 sasa wamekuwa wakivuna zaidi ya Shs. 10 million kwa mara moja. 4) Matatizo ya upatikanaji wa pesa yameanza tu mara Serikali ilipoingilia kati mpango huu, kwa kuwa nia ilikuwa kuhakikisha kwamba DECI INAKUFA KWA HALI YOYOTE ILE. Mikakati iliyopangwa ilikuwa ni pamoja na (i) kujenga hoja potofu kwamba DECI ni utapeli, bila hata ya kutaja ni aina gani ya utapeli unaofanyika, (ii) kujenga hoja kwamba wasimamizi wa DECI ni watu matapeli, bila kusema ni watu wa aina gani (ukweli ni kwamba hawa ni watu wa Kanisa, kama sikosei, Kanisa la Kibaptisti... MIMI NI MUISLAM, na si mwanachama wa DECI... lakini kama ningejua kuhusu undani wa DECI singeangalia UDINI wa walioianzisha, ningejiunga nao...), (iii) kujenga hoja kwamba DECI itakufa, bila hata ya kusema itakufa kwa namna gani. 5) Kuna tofauti kubwa kati ya "Pyramid Scheme" na "Revolving Fund". Mkitaka niwafafanulie, hiyo ni mada pekee, inayojitosheleza. BOT, kwanza ninashangaa, jinsi ilivyojazwa na ufisadi inapataje uhalali wa kusema kwamba DECI ni matapeli, imetoa tangazo kwamba DECI inakwenda kinyume na sheria. Mbona haikutangaza ni sheria gani (na vifungu vyake) iliyokiukwa? Unapomshtaki mtu, tena kosa la jinai, ana haki ya kujua anashtakiwa kwa kosa gani. DECI hawakuambiwa wameshtakiwa kwa kosa gani, mbaya zaidi, wananchi/wanachama wa DECI wametishwa na BOT waondoe fedha zao kule, au wasiwe na imani na DECI, ili DECI ife! 6) Kama DECI - na hiki ndicho kiini cha matatizo - ingeachwa iendelee, watu wangeendelea kuvuna, na kuvuna, kiasi kwamba benki za kawaida zingekosa uhalali wake. Watu wangeondoa amana zao kwenye benki (NMB, CRDB, NBC, BARCLAYS, STANBIC, etc.), kisha kuzipeleka DECI, ambapo wangepata faida kubwa zaidi, kwa kuwa DECI HAIKOPESHI. Wote mnajua (na hili si kwa Uislam pekee) kwamba vitabu vya Mungu vimeharamisha RIBA! Mikopo yote inayotolewa kwa minajili ya kutoza RIBA ni haramu. Lakini tumezaliwa na kukuukuta mfumo huu, ambao ndio umeanza kuhatarisha mfumo wa kiuchumi wa dunia... si mmeyaona wenyewe? 7) DECI haikuanzishwa ili IKOPESHE wanachama wake, kwani waanzilishi wake, ambao ni watu wa KANISA, walitambua kwamba kufanya hivyo kungekuwa ni kuzidi kuwakandamiza watu maskini, mafukara, wasiokopesheka, wasio na hata hati ya kibanda, ambao wakienda benki wanarudishwa nyuma, na wakienda PRIDE na FINCA wanaambiwa wajiunge vikundi vya watu 5 kila kikundi, na wanageuzwa kuwa watumwa wa kufanya kazi kwa bidii ili WALIPE RIBA ya mkopo, hatimaye kushindwa kulipa mkopo! Kama ninayoyasema ni uongo, waulizeni PRIDE na FINCA wawambie wana wanachama wangapi mpaka sasa na DECI wana wanachama wangapi? Benki huwa zinaikopesha Serikali ili iweze kuendesha shughuli zake za kiserikali (soma kifisadi), na kama watu wakitoa amana zao kwenye hizo benki, hakutakuwa na pesa za kuikopesha Serikali, hatimaye Serikali itaporomoka na kukosa uhalali wa kuitwa "Serikali", kwani, kadri jinsi watu wanavyoneemeka na kuwa na uwezo mkubwa wa kiuchumi, viongozi wa kuchaguliwa wanakosa watu wa kuwasimamia. Wananchi wakijenga Shule zao wenyewe, Hospitali zao wenyewe, mifumo yao wenyewe, na (asilani!) mitambo yao wenyewe ya kuzalisha nishati ya umeme, ili waweze kuwa na (a) nyumba bora, (b) lishe bora, (c) elimu bora, (d) afya bora, hapo ndipo kutakuwa na MAENDELEO! DECI waliwapa nuru Watanzania wanyonge - maskini - walio wengi. Lakini Serikali yetu hii - ya kifisadi - imediriki kwenda kuwakandamiza na kuizima nuru hiyo ya matumaini! Kumbe zile ahadi za "Maisha Bora kwa Kila Mtanzania" zilikuwa danganya toto? Sasa mmeamini wenyewe! Mmeshabikia DECI kufungwa, haya, nendeni, kama kondoo mnaotaka kuchungwa, mkaweke pesa zenu kwenye benki (NMB, NBC, CRDB, BARCLAYS, STANBIC, PRIDE, FINCA, etc.) tuone kama mtayapata hayo "Maisha Bora"! Kumbukeni, PRIDE ilikuwa na wanachama 75,000. Sasa wamepungua, na kuwa takriban 50,000! Ina maana, 25,000 waliondoka na kwenda DECI. Sasa Iddi Simba aliona hatari, atarudishaje mkopo wa USD 1.2 million huko kwa Wadachi wa Hivos-Triodos Fund? Ukitaka kusoma habari hizo, just Google "Pride Tanzania", utaona link mojawapo! Wala si siri! Ama kweli, wajinga ndio waliwao! Nimetoa somo... atakayekwazwa, aniwie radhi! Sasa kilichobaki, Uchaguzi Mkuu! 2010 ni keshokutwa! Tutaona itakavyokuwa, au sio? Umejiandikisha kupiga kura? ./Mwana wa Haki

MWANaHAKI you remain ''FIRM ON ISSUE"
Umeona mwenyewe walivyoilewa hoja yako na wanapotosha TENA umma kwa kusema ni pyramid scheme!
This is fantastic...! Nikirudi kwenye nadharia yangu mwenyewe kuwa "USOMI UMESHINDWA KUTATUA MAFUMBO YA MAISHA" pia nakumbana na kitu kama hiki ambacho kimewababaisha WASOMI PAMOJA NA NADHARIA ZAO ZA KIUCHUMI ambazo zinasisitiza KUTOKUWEZEKANA KWA JAMBO HILI AMBALO LIMEWEZEKANA ( wengine huita muujiza)
Chukulia mafano pale ambapo YESU alikwenda kinyume na kanuni za kifizikia.....KUTEMBEA JUU YA MAJI & KUPAA....!
LEO HII DECI IMETEMBEA JUU YA MAJI WASOMI HAWATAKI....!
 
MWANaHAKI you remain ''FIRM ON ISSUE"
Umeona mwenyewe walivyoilewa hoja yako na wanapotosha TENA umma kwa kusema ni pyramid scheme!
This is fantastic...! Nikirudi kwenye nadharia yangu mwenyewe kuwa "USOMI UMESHINDWA KUTATUA MAFUMBO YA MAISHA" pia nakumbana na kitu kama hiki ambacho kimewababaisha WASOMI PAMOJA NA NADHARIA ZAO ZA KIUCHUMI ambazo zinasisitiza KUTOKUWEZEKANA KWA JAMBO HILI AMBALO LIMEWEZEKANA ( wengine huita muujiza)
Chukulia mafano pale ambapo YESU alikwenda kinyume na kanuni za kifizikia.....KUTEMBEA JUU YA MAJI & KUPAA....!
LEO HII DECI IMETEMBEA JUU YA MAJI WASOMI HAWATAKI....!

Hahaha hela zinashushwa kwa miujiza kumbe!!! Sasa mbona miujiza haijazuia Pyramid Scheme kuvunjika?
 
MWANaHAKI you remain ''FIRM ON ISSUE"
Umeona mwenyewe walivyoilewa hoja yako na wanapotosha TENA umma kwa kusema ni pyramid scheme!
This is fantastic...! Nikirudi kwenye nadharia yangu mwenyewe kuwa "USOMI UMESHINDWA KUTATUA MAFUMBO YA MAISHA" pia nakumbana na kitu kama hiki ambacho kimewababaisha WASOMI PAMOJA NA NADHARIA ZAO ZA KIUCHUMI ambazo zinasisitiza KUTOKUWEZEKANA KWA JAMBO HILI AMBALO LIMEWEZEKANA ( wengine huita muujiza)
Chukulia mafano pale ambapo YESU alikwenda kinyume na kanuni za kifizikia.....KUTEMBEA JUU YA MAJI & KUPAA....!
LEO HII DECI IMETEMBEA JUU YA MAJI WASOMI HAWATAKI....!

Please mkuu!!! Usitake kuchanganya udini na uchumi! Eti kutembea juu ya maji????? This is blasphemy! Una-compare miujiza ya Bwana wetu Yesu Kristo na dhuluma, wizi na ujangili uliofanywa na watu wa DECI???!!! As a Christian naomba unitake radhi mara moja! Bwana wetu hakuzungumzia hata siku moja kujipatia mali na utajiri kwa kuiba, in fact hata mtajiri halali aliambiwa ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita tundu la sindano kuliko mtu tajiri kuingia mbinguni.

Ukitaka analogy nzuri hebu refer kwa yaa zile ambapo Yesu alienda kanisani na aliwakuta watu wanafanya biashara na aliwatimua akiwaambia Mmegeuza nymba ya Baba yangu kuwa pango la wezi! That is what DECI has done, SHAME on YOU!!! Huwezi kuuhodhi ukristo na kusema eti DECI ni ukristo! Kama mnafanya biashara zenu fanyeni, kama mnakubali kudanganywa na pyramid schemes, endeleeni lakini usimwingize Yesu Kristu, Mungu, au udini!
 
MWANaHAKI you remain ''FIRM ON ISSUE"
Umeona mwenyewe walivyoilewa hoja yako na wanapotosha TENA umma kwa kusema ni pyramid scheme!
This is fantastic...! Nikirudi kwenye nadharia yangu mwenyewe kuwa "USOMI UMESHINDWA KUTATUA MAFUMBO YA MAISHA" pia nakumbana na kitu kama hiki ambacho kimewababaisha WASOMI PAMOJA NA NADHARIA ZAO ZA KIUCHUMI ambazo zinasisitiza KUTOKUWEZEKANA KWA JAMBO HILI AMBALO LIMEWEZEKANA ( wengine huita muujiza)
Chukulia mafano pale ambapo YESU alikwenda kinyume na kanuni za kifizikia.....KUTEMBEA JUU YA MAJI & KUPAA....!
LEO HII DECI IMETEMBEA JUU YA MAJI WASOMI HAWATAKI....!

Mkuu mbona hiyo DECI yenu wameifunga kama inaweza kufanya mambo ya miujiza? Wangeacha iendelee kwa miujiza miujiza tu. Lakini kwa ujinga wetu nadhani bado kuna watu wanaweza kuamini hadithi za Kinje Kitile na vita ya maji maji katika karne hii ya 21!! Huwezi jua, labda wanachama wanaendelea kupelekewa mavuno kwa miujiza.
 
Sakata la Richmond liliitwa RICHMONDULI

Napendekeza ishu ya DECI iitwe DECIMALI kwani desimali ni hesabu za mafumbo ya kukokotoa ambapo ili upate jibu ni shurti ubadili namba katika desimali au sehemu. sasa Watanzania wenzangu hawakutaka kukaa chini na kukokotoa kupata majibu ya vijisenti wala sehemu ambazo fedha zao hupelekwa ili kutotoleshwa kwa hizo aslilimia lukuki.
 
Sakata la Richmond liliitwa RICHMONDULI

Napendekeza ishu ya DECI iitwe DECIMALI kwani desimali ni hesabu za mafumbo ya kukokotoa ambapo ili upate jibu ni shurti ubadili namba katika desimali au sehemu. sasa Watanzania wenzangu hawakutaka kukaa chini na kukokotoa kupata majibu ya vijisenti wala sehemu ambazo fedha zao hupelekwa ili kutotoleshwa kwa hizo aslilimia lukuki.

Mimi si mtaalamu wa hesabu ila nadhani ukiita DECIMALI inapoteza maana ambayo wanachama wangependa kusikia. Nijuavyo mimi decimali ni ndogo kuliko kitu kamili. Sasa hii ni muujiza wa kuzalisha vitu kutoka kitu kamili kimoja au viwili (exponential amplification). Kwa hiyo tutafute jina lingine ili watu waendelee kuomboleza miujiza yao vizuri.
 
MWANaHAKI you remain ''FIRM ON ISSUE"
Umeona mwenyewe walivyoilewa hoja yako na wanapotosha TENA umma kwa kusema ni pyramid scheme!
This is fantastic...! Nikirudi kwenye nadharia yangu mwenyewe kuwa "USOMI UMESHINDWA KUTATUA MAFUMBO YA MAISHA" pia nakumbana na kitu kama hiki ambacho kimewababaisha WASOMI PAMOJA NA NADHARIA ZAO ZA KIUCHUMI ambazo zinasisitiza KUTOKUWEZEKANA KWA JAMBO HILI AMBALO LIMEWEZEKANA ( wengine huita muujiza)
Chukulia mafano pale ambapo YESU alikwenda kinyume na kanuni za kifizikia.....KUTEMBEA JUU YA MAJI & KUPAA....!
LEO HII DECI IMETEMBEA JUU YA MAJI WASOMI HAWATAKI....!

Ningeshauri ubadili nick name ... hakuna miujiza kwenye hesabu ... tehe tehe :)

Na hata kama unaamini kwenye miujiuza, huu hapa haukuwa. Kwa wasioelewa mchezo huo unafanyaje kaza, na wale wasiotaka kuelewe, ni rahisi kuuchukulia kama ni muujiza.

Mimi pengine ningeshawishika kwamba wanauwezo wa kufanya miujiza kama ningeona hao maaskofu wenu wanawaambia mkavune tu bila kupanda.

Yesu alizidisha mikate, lakini hakuitoa kwa watu wengine. Na ingekuwa ameiba hiyo mikate ya nyongeza kutoka kwa watu wengine na kuwaacha hao wengine na njaa wangemuua kabla ya siku zake.
 
Please mkuu!!! Usitake kuchanganya udini na uchumi! Eti kutembea juu ya maji????? This is blasphemy! Una-compare miujiza ya Bwana wetu Yesu Kristo na dhuluma, wizi na ujangili uliofanywa na watu wa DECI???!!! As a Christian naomba unitake radhi mara moja! Bwana wetu hakuzungumzia hata siku moja kujipatia mali na utajiri kwa kuiba, in fact hata mtajiri halali aliambiwa ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita tundu la sindano kuliko mtu tajiri kuingia mbinguni.

Ukitaka analogy nzuri hebu refer kwa yaa zile ambapo Yesu alienda kanisani na aliwakuta watu wanafanya biashara na aliwatimua akiwaambia Mmegeuza nymba ya Baba yangu kuwa pango la wezi! That is what DECI has done, SHAME on YOU!!! Huwezi kuuhodhi ukristo na kusema eti DECI ni ukristo! Kama mnafanya biashara zenu fanyeni, kama mnakubali kudanganywa na pyramid schemes, endeleeni lakini usimwingize Yesu Kristu, Mungu, au udini!

Hao ndiyo mashahidi wa uwongo na mpinga kristo. Wanafanya kazi ya bwana Yesu ikataliwe na watu waliofungwa na minyororo ya ibilisi. Neno la Mungu linasema zipimeni roho. Si kila mtu asemaye bwana bwana yuko kwenye ufalme wa mwana wa pendo lake. Huwezi kuwa mwizi at the same time mwana wa mungu na neno la injili halihitaji enticing words of the matapeli liweze kusimama.

Watu wote alioambiwa wapande mbegu walionyeshwa na udongo/ardhi ya kupandia i.e physical seed to physical substrate sasa vipi upande physical (carnal) uvune ki spirit? If it would have been wamepewa neno (idea) wakaambiwa that small they have would multiply to multiples through idea ningeamini iko in line with neno la Mungu kwani those who are led by spirit see things which are not seen by carnal man and they later manifest into physical after they profesy. Hii ndiyo kanuni ya neno la Mungu spirit to physic and not physic to spirit.

Kama yesu alivyosema yeyote anaekataa kuwa yesu alizaliwa akakua akahisi njaa; akalala; akachoka na akafa kisha akafufuka na kurejea katika mwili wake na siyo ghost huyo ni mpinga kristo. Inamaana watu wanao shindwa kumanifest their ideas into reality wote ni matapeli. Our God is not mystery is real we talk with him we see him for he is alive and has once lived amongst us even now is yaani Emanuel Mungu katikati ya wanadamu. Devil is mysterious everthing which is not clear and can not be substantiated comes from devil for he is the author of confusion.
 
Mimi si mtaalamu wa hesabu ila nadhani ukiita DECIMALI inapoteza maana ambayo wanachama wangependa kusikia. Nijuavyo mimi decimali ni ndogo kuliko kitu kamili. Sasa hii ni muujiza wa kuzalisha vitu kutoka kitu kamili kimoja au viwili (exponential amplification). Kwa hiyo tutafute jina lingine ili watu waendelee kuomboleza miujiza yao vizuri.

asante mkuu
unajua tena ulevi mwingine ni mzuri tu. nshabugia chupa kadhaa hapa nakosa balansi.
Wacha tuiite DECI-Kimeo
 


Labels: DECI, UPATU, WATUMISHI


[h=3]DECI[/h]
Hii ni DECI au Desimali? Je nnani mkweli ktk hili kati ya BOT, Soko la Mitaji CMSA, VIONGOZI wa DECI na wanaodai ni WANUFAIKA? Lakini zaidi ni nani antuongopea (anawaongopea) au hatwambii ukweli hapa?
You might also like:
 
DUH hakika JF kiboko yao kwa kuangalia michango ya wanajf hapo juu nimegundua kua wanajf wana upeo wa hali ya juu kwani wanaona mbali.
 
Kwa mtu yeyote mwenye kukifahamu vizuri hiki chombo kinachojishugulisha na biashara ya pesa wao wasema kupanda na kuvuna atuhabarishe.

Kila kona ya Dar na baadhi ya Mikoa hapa nyumbani TZ DECI wanakusanya pesa na kurudisha kwa faida kubwa.

Tunaomba kuwafahamu vizuri ili tukiamua kujiunga nao tusiwe na mashaka kama yale yaliyowahi kutukuta ya UPATU.

Plz wenye data zitakazo tusaidia msisite.
wakuu JamiiForums Mod 1 Mod 5 kwa taarifa nilizonazo kama schoolmate mwenzangu huyu member mwezetu Kasungura alifariki mwaka jana mwezi wa 12 na kuzikwa huko kwao Rorya mkoani Mara.....

R.I.P Kasungura
 
Hawa jamaa naskia wapo toka zamani ni kama inamilikiwa na dini ya kikristo sijajua dhehebu gani....wanacho fanya unaingia uanachama kwa sh.20,000/= kwa sasa ukipanda 200,000/= ambayo ndo maximum kwao unakuja kuvuna 300,000/= baada ya wiki 16 kwa hiyo jumla unakabidhiwa 500,000/= ila kuna riba wanakata pesa ndogo sana katika hiyo 300,000/= utakayo pewa.Kwa hiyo ukiamua kuvuna zote ni wewe au ukiamua kupanda tena ni wewe.Wao hawapokei zaidi ya 200,000/= kwa kupanda lakini unaweza ukapanda zaidi na zaid kwa interval tofauti.

Ni kweli watu wanavuna wengi nimewashuhudia wamevuna pesa kibao pale.
Swali la kujiuliza hawa DECI wakipokea hiyo 200,000/= wao wanafanyia nini?wanabiashara gani?faida wanapataje?

Hawa jamaa walikuwepo toka miaka kama 3 nyuma watu walicho kuwa wakifanya walikuwa wanafanya siri kwa hiyo ilikuwa vigumu kwa mtu kugundua kama wana operate kwani mtu alikuwa anapanda kisha anasikilizia asije akatapeliwa kwa hiyo anafanya siri sana.....Kwa sasa wana wanachama wengi wengi mno ukienda pale Mabibo utakumbuna na bonge la foleni watu wanataka kupanda wengine wanavuna fedha hizo.

My take
Hawa jamaa kweli wamedhamilia kuinua hali duni ya Mtanzania kwani unapanda kidogo unavuna pesa kibao.Hata Mabank nao wangeiga mfano wa hawa jamaa ingekuwa faraja sana kwa wateja ukiweka pesa zinazaa pesa ingekuwa safi sana.Lakini Bank ukiweka 1M utashangaa unapata faida 10,000/= kwa mwaka.

DECI kwa sasa wamefungua matawi sehemu mbali mbali kama Morogoro,Mbeya kwa hapa Dar hata Gongo la Mboto napo wapo.

Your take though
 
JamiiForum back then ilikua na watu wenye akili sana aisee

Hata uandishi wao na namna wanavyoargue ni tofauti na wakina "Xaxa,xo etc"
 
Back
Top Bottom