DCI Manumba: Mwakyembe hajalishwa sumu!

DCI Manumba: Mwakyembe hajalishwa sumu!

Ndugu yangu Pasco, kama unajua kuwa lugha ya wageni inakupa shida kimawasiliano kwanini unaing'ang'ania? Kwanza unapowasiliana na sisi wamatumbi wenzio unahaja gani kuchanganya lugha?
Mkuu Gwalihenzi, lugha hiyo ndiyo rahisi kupunguza impact ya maneno mengi ya kiswahili ku drive home what you mean. Mimi ni mtoto wa uswazi hizi ndizo lugha
na ndizo za uswazi zote hata uswazi za huko huko kwenye lugha zao, spelling sio issue saana cha muhimu ni meaning!.
 
Hata bila kumsikiliza Mwakyembe mwenyewe, ni dhahiri kuwa Sitta ni mkweli kuliko Manumba kwa sababu;
  1. Sitta yupo karibu zaidi na Mwakyembe kuliko alivyo manumba.
  2. Sitta alikwenda India kumjulia hali mwakyembe wakati akipatiwa matibabu na bila shaka madaktari walizungumza hilo.
  3. Sitta aliitoa hiyo kauli mbele ya mwakyembe na mwakyembe hakupinga, hiyo ina maana mwakyembe anajua hivyo pia. Kwa upande mwingine, Manumba alitoa kauli hiyo wakt mwakyembe hayupo kabisa nchini.
  4. Sitta alitoa kauli kwa kujiamini, huku akiamini anachokisema wakati Manumba alitoa kauli hiyo kwa woga, bila kujiamini huku akiwa haamini anchokisema.
Kuna memgi ya kulinganisha ili kujua nani mkweli kati yao ila kwa hayo machache tu bila shaka Sitta ana uwezekano mkubwa wa kuwa alichokisema kina ukweli wakati alichosema Manumba hakina sababu ya kuaminika.
 
Hivi hizo YES na NO zinajengwa na background gani

Nani kati yao ni pathologist ????
Si wakati wa yes na no......we need to hear on the genesis n background ya hizi YES na NO otherwise tuwaombee waathirika wapate kuwa na afya na waepushwe na madhila
 
Ngongo, DCI anasema Dk Mwakyembe HAJALISHWA sumu, kwa maneno mengine hajakanusha kuhusu sumu labda Dk Mwakyembe amejilisha sumu mwenyewe; alitaka kujinga?

hajalishwa sumu,amenyweshwa au ametiwa au amenyunyuzia au amepuliziwa au ametegeshewa sumu ! in short sumu imempitia ila hakulishwa lol !
 
huu uwozo wa serikali tutauvumilia mpaka lini siasa mbaya huleta mauti ;kuleta siasa kwenye mambo ya usalama wa watu mwishoe ni kuzikana tu; Manumba analinda ugali wake waungwana
 
wote siwaamini kwa sababu hawajatoa report za madaktari.nina mashaka na kamishna manumba kwa sababu yeye ni mtaalamu na anajua kabisa ili useme mtu amelishwa sumu unahitaji ushahidi kwanza wa kimazingira na pili taarifa ya daktari au mkemia mkuu.sasa iweje akae mbele ya media na kuropoka kama sitta?
 
Namuamini Sitta ndio mkweli kwani uzoefu wangu unaniambia hao watu kina kanumba manumba kayumba hawasemagi ukweli! Si unakumbuka
1.Wao wanasema Daudi balali kafa wakati ye mwenyewe anakula bata
2.Wafanyabiashara wa madini mahenge ni majambazi wkt si kweli
 
Pasco,
Mbona Kiswahili chenyewe tunakosea kila siku hapa? Ila mtu akikosea kidogo kwenye Kiingereza tayari vicheko na maneno mengi. Kasumba ya Ukoloni imejaa vichwani mwetu.

Hao Waingereza wenyewe wenye lugha wanachapia ile mbaya ndio iwe mswahili?

Ni vibaya kufanya makosa kwenye uandishi wowote lakini hii ya makosa ya kiswahili sawa lakini ya Kiingereza vicheko ni yale yale ya kushabikia vya wenzetu.
 
Kwa kiasi fulani inakuwa ngumu ku-judge ukweli ni upi kwenye mkasa huu kwa sababu: Dr.Mwakyembe na Sitta ni wanasiasa wanaokubalika na wanaoheshimika kwa watu wengi(its my opinion).
However Mwakyembe hakuwa tayari kutoa evidence kuwa alilishwa sumu,how comes Sitta anakuwa ndie msemaji wa kunadi ugonjwa wake?Kwa maana Sitta sio msemaji wa familia ya Mwakyembe au msemaji wa jeshi la polisi.
Na kama DCI taarifa alizotoa kazipata wizara ya afya na hospitali India alikotibiwa,kwa nini tusikubali hizi ndio taarifa sahihi,na hizi zinazotolewa na Sitta ni "MINONG'ONO YA MITAANI". Wakati mwingine tusiwe wepesi wa kufata hisia zetu ku-judge ukweli ni upi! Unless kama Robert Manumba katoa taarifa zisizo sahihi kwa umma.
 
Kama Hiyo ndiyo taarifa ya kipolisi basi either Samweli sita ajiuzuru uwazili kwa uzushi ama aje mbele ya vyombo vya habari na kuweka wazi ushahidi wake na kuwaumbua polisi.

ni mtizamo wangu tu!
Tukimtaka Sitta ajiuzuru kwa uzushi tutakuwa tunamwonea, uzushi walianza akina Pinda na Makinda katika posho, tungeanza kuwataka wao wajiuzuru kwanza.

Pia uchunguzi anaousema Manumba kuwa ameufanya kwa umakini mkubwa kimsingi ni kusuma report ya MaDK toka India, hivi kusoma taarifa ndio uchunguzi???Hiyo report aliisoma kwa kutumia Darubini??huyu mzee anaongea nini???walisoma wapi hawa watu mbona wanajifanya MABOGUS???

Ni uchunguzi gan huo wa afya ya mtu unaomalizwa bila kuhusisha analysis ya body samples???kwanini wasingechukua body samples wakapime na waje na majibu ya kueleweka???Kwanini wasilete wataalum wakafanya uchunguzi huru wa afya ya Mwakyembe kama ilivyokatika Auditing?? Kimsingi katika sakata la Mwakyembe kulishwa sumu, Serikali ndiyo inayotuhumiwa, inawezekanaje mtuhumiwa akafanya uchunguzi dhidi yake na uchunguzi huo ukawa na majibu ya kueleweka?????Hawa wanatuona watanzania ni mazezeta kama wao walivyo.
 
Hata bila kumsikiliza Mwakyembe mwenyewe, ni dhahiri kuwa Sitta ni mkweli kuliko Manumba kwa sababu;
  • Sitta yupo karibu zaidi na Mwakyembe kuliko alivyo manumba.
  • Sitta alikwenda India kumjulia hali mwakyembe wakati akipatiwa matibabu na bila shaka madaktari walizungumza hilo.
  • Sitta aliitoa hiyo kauli mbele ya mwakyembe na mwakyembe hakupinga, hiyo ina maana mwakyembe anajua hivyo pia. Kwa upande mwingine, Manumba alitoa kauli hiyo wakt mwakyembe hayupo kabisa nchini.
  • Sitta alitoa kauli kwa kujiamini, huku akiamini anachokisema wakati Manumba alitoa kauli hiyo kwa woga, bila kujiamini huku akiwa haamini anchokisema.
Kuna memgi ya kulinganisha ili kujua nani mkweli kati yao ila kwa hayo machache tu bila shaka Sitta ana uwezekano mkubwa wa kuwa alichokisema kina ukweli wakati alichosema Manumba hakina sababu ya kuaminika.
 
huu bado ni muendelezo wa filamu,japo H.M hajakanusha na bado alikili kulishwa sumu sasa haya manunda sijui kayatoa wapi?kapewa na H.M au ni za kitabibu?na kama ni za kitabibu ina maana SS na H.M wametuhadaa!
 
Nitmwamini zaidi Mwakyembe na Dakitari wake wengine wote mi wasanii.Mwakyembe sasa umefika wakati wa KUZUNGUMZA.
 
nasubiri report ya toxicologists ili tujue ukweli ukowapi.
 
Wewe ni polis unasema Mwakyembe hajalishwa sumu. Sasa kwa nini usimkamate Sitta amusaidie kutoa ushahidi. Au Sitta kusema uongo si kosa la kuudanganya umma?
 
Sitta na DCI Manumba wote ni WAKWELI

MUONGO ni Dr. Mwakyembe ambaye hataki kutueleza UKWELI kama
alivyoficha baadhi ya mambo kwenye report ya Richmond.
 
Nimefurahi jeshi la polisi limemshushua Sitta.

Huyu sita ni mtu wa kuogopwa sana! naona ni mnafiki na mchonganishaji!
Bro Furaha yako inaweza isidumu kwa muda mrefu mana Serikali yako pia ni ya kizushi na kinafiki sana tena zaidi hata ya Sitta. Tusubiri apandishwe kizimbani mana naimani shahidi wake namba 1 atakuwa Dk. Mwakyembe. So nani mnafki/mchonganishi tutamjua muda huo.
 
..DCI Manumba alisema matamshi ya sitta ni matamshi ambayo yana jinai ndani yake na kwamba HAKUMTAJA mtu anaehusika katika swala hilo, wao wanacho fanya ni kuchunguza..Kwa mantiki hiyo sitta hana kosa wala shtaka la kujibu..upo hapo??
 
Hapo sasa tunaongea lugha moja,ukweli utapatikana tu endapo Dr.Mwakyembe atathibitisha kuwa alilishwa sumu from report ya daktari wake aliyemtibu India. On the other hand,tamko la Robert manumba ni hili.....tusije tukawa tunapoteza muda kujishawishi kuna tatizo kumbe tunaumba tatizo!!

"Ukweli kuhusu kauli hiyo inayodai kuwekewa sumu, tumeupata baada ya kuwasiliana na Wizara ya Afya ambayo nayo imewasiliana na hospitali aliyokuwa amelazwa Dk Mwakyembe nchini India. Taarifa zinaonyesha kuwa hakuna sumu katika maradhi yanayomsibu Mwakyembe.''
 
Back
Top Bottom