DCI Manumba: Mwakyembe hajalishwa sumu!

Tukimtaka Sitta ajiuzuru kwa uzushi tutakuwa tunamwonea, uzushi walianza akina Pinda na Makinda katika posho, tungeanza kuwataka wao wajiuzuru kwanza.

Pia uchunguzi anaousema Manumba kuwa ameufanya kwa umakini mkubwa kimsingi ni kusuma report ya MaDK toka India, hivi kusoma taarifa ndio uchunguzi???Hiyo report aliisoma kwa kutumia Darubini??huyu mzee anaongea nini???walisoma wapi hawa watu mbona wanajifanya MABOGUS???

Ni uchunguzi gan huo wa afya ya mtu unaomalizwa bila kuhusisha analysis ya body samples???kwanini wasingechukua body samples wakapime na waje na majibu ya kueleweka???Kwanini wasilete wataalum wakafanya uchunguzi huru wa afya ya Mwakyembe kama ilivyokatika Auditing?? Kimsingi katika sakata la Mwakyembe kulishwa sumu, Serikali ndiyo inayotuhumiwa, inawezekanaje mtuhumiwa akafanya uchunguzi dhidi yake na uchunguzi huo ukawa na majibu ya kueleweka?????Hawa wanatuona watanzania ni mazezeta kama wao walivyo.

Wafanye uchunguzi wa nini wakati majibu ya Apolo yanasema hakuna sumu?
 
Taarifa ya Dr. Mwakyembe kutokana na taarifa ya Jeshi la Polisi juu ya afya yake
Dk. Harrison G. Mwakyembe (Mb), NW-UJ

Dar es Salaam

18/02/12





TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Nimelazimika leo Jumamosi, tarehe 18 Februari, 2012 kutoa taarifa hii kwa vyombo vya habari kufuatia mkutano wa DCI Robert Manumba na waandishi wa habari jana (17/02/12) kuongelea, pamoja na mambo mengine, hali yangu ya afya na kuhitimisha, kienyejienyeji tu kuwa "sikunyweshwa sumu" ila naumwa tu ugonjwa wa ngozi bila kufafanua ugonjwa huo wa ngozi umesababishwa na nini!
Napenda nisisitize mapema kabisa kuwa msimamo huo wa Jeshi la Polisi umenikera sana katika hali niliyonayo ya ugonjwa, kwanza kwa kuingilia mchakato wa matibabu yangu na uchunguzi wa kina kuhusu kiini chake unaoendelea hospitali ya Apollo nchini India ambako bado sijahitimisha matibabu yangu; pili kwa ufinyu wa uelewa unaojitokeza bayana kwenye tamko la Jeshi la Polisi unaosisitiza kuwa "sikunyweshwa sumu" wakati sumu si lazima unyweshwe ili ikudhuru, inaweza kudhuru hata kwa kugusishwa tu; na tatu kwa Jeshi la Polisi kujiingiza kwenye suala ambalo kwa takriban mwaka mzima halijawahi kuwa na dhamira ya dhati ya kulielewa au kulichunguza mbali na kulifanyia mzaha kupitia magazetini.
Itakumbukwa kuwa tarehe 9 Februari, 2011 nilimwandikia barua IGP Said Mwema kumtaarifu kuhusu njama za kuondoa maisha yangu na ya viongozi wengine. Kwa kutambua kuwa Jeshi la Polisi la Tanzania daima husisitiza kuletewa ushahidi kwanza ndipo lifanyekazi, nilihakikisha nimeainisha katika barua hiyo kila ushahidi nilioupata au kupewa. (Utaratibu huu wa Jeshi la Polisi kusubiri kuletewa ushahidi mezani, kama ambavyo mahakimu wanavyosubiri ushahidi mahakamani, haupo popote pale duniani (ila Tanzania tu) kwani kazi ya msingi ya Polisi si kuletewa, ni kutafuta ushahidi. Polisi wanachohitaji duniani kote ni kupata clue au tetesi tu. Hiyo inatosha kufukua ushahidi wote unaohitajika). Pamoja na kujitahidi kuanika kila aina ya ushahidi niliokuwa nao, mambo manne yalijitokeza ambayo yalionyesha wazi kuwa Polisi hawakuwa na dhamira ya dhati ya kupeleleza suala hilo:

(i) Siku chache baada ya kumkabidhi IGP barua hiyo, nilitumiwa timu ya "wapelelezi" ofisini kwangu kuja kuchukua maelezo yangu ya ziada. Timu hiyo ilikuwa inaongozwa na ACP Mkumbo, afisa wa polisi ambaye wiki chache zilizokuwa zimepita alikuwa miongoni mwa askari waliotuhumiwa kupokea rushwa kwa lengo la kumbambikizia madawa ya kulevya mtoto wa Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi, suala ambalo mpaka leo hii uongozi wa Polisi umeshindwa kulitolea maelezo ya kuridhisha. Kwa msingi huo, nilikuwa nimeletewa mtuhumiwa wa rushwa/ ujambazi kuendesha uchunguzi wa watuhumiwa wengine wa ujambazi! Nikatambua mara moja kuwa zoezi zima lilikuwa la mzaha, tena mzaha mkubwa!

(ii) Wiki chache baada ya barua yangu kuwasilishwa kwa IGP na timu ya ACP Mkumbo "kuanza kazi", Jeshi la Polisi likachukua hatua ya kuwapongeza na kuwazawadia askari niliowatuhumu kushirikiana na majambazi! Huhitaji kuwa profesa wa falsafa kuelewa kuwa huo ulikuwa ujumbe tosha wa kunipuuza.

(iii) Hivi karibuni tuhuma za askari polisi kujihusisha na vitendo vya ujambazi mkoani Morogoro zilipopamba moto na kuwagusa askari "wale wale" niliowatuhumu kwenye barua yangu, IGP alichukua hatua ya kuwahamishia mikoa mingine!

(iv) ili kunikatisha tamaa kabisa, barua yangu ya "siri" kwa IGP ikavujishwa kwa makusudi kwenye vyombo vya habari na kuchapishwa kama habari ambayo ilikebehi na kukanusha taarifa nzima niliyotoa, sijui kwa faida ya nani! Lakini huu ni mchezo wa kawaida kwa polisi kwani hivi karibuni Mhe. Waziri Samuel Sitta alipohojiwa na ofisa mwandamizi wa Jeshi la Polisi ofisini kwake, wakiwa wawili tu, taarifa ya kikao hicho ikawa magazetini ikikebehi ushahidi aliotoa Sitta! The integrity of the police force leadership is on the line.
Nimeelezea vizuri katika barua yangu kwa IGP kuwa kundi hilo la mauaji lilikuwa limeelekezwa kuniua kwa kutumia sumu, taarifa ambayo kwa karibu mwaka mzima Polisi hawakutaka kuifuatilia kwa sababu wanazozijua wenyewe. Sasa huu msukumo mpya wa Jeshi la Polisi kutaka kujua kama nilipewa sumu au la na kukurupuka kutoa tamko hata kabla ya kunichunguza nilivyo, kunihoji mimi na wasaidizi wangu ofisini na hata kuongea na mabingwa wa Kihindi wanaonifanyia uchunguzi, umetokea wapi?

Aidha napata taabu kuamini kama DCI Manumba na wenzake waliisoma taarifa halisi ya matatibabu yangu au walisoma taarifa "nyingine", na kama waliisoma taarifa hiyo wenyewe au "walisomewa"! Nasema hivyo kwa kuwa alichokisema DCI Manumba kwa wandishi wa habari hakifanani kabisa na picha iliyo kwenye taarifa halisi ya Apollo ambayo inatamka wazi kuwa kuna kitu kwenye bone marrow kinachochochea hali niliyonayo, kitu ambacho mabingwa wanahangaikia kukidhibiti/ kukiondoa huku vyombo vyetu vya dola vikipelekeshwa na mafisadi kusema bila msingi wa kisayansi na bila aibu: "hakulishwa sumu", "hakulishwa sumu"!

Nimesoma darasa moja Kitivo cha Sheria Mlimani na DCI Manumba. Baadaye IGP Mwema alikuwa mwanafunzi wangu wa sheria Mlimani. Vigogo hawa wawili wa usalama wa raia nchini hawajanitendea haki, nao wanajua. Wanajua vilevile kuwa sitakaa kimya au kumung'unya maneno come what may pale ambapo haki inakanyagwa.
Tuendelee kuombeana afya na uhai ili kutendeane haki na vilevile tuitendee nchi yetu haki kwa kuvimalizia viporo vinavyokera vya Dowans, EPA, Kagoda n.k. kwa maslahi mapana ya Taifa letu.

Mungu Ibariki Tanzania.​
 
Dk. Harrison G. Mwakyembe (Mb), NW-UJ

Dar es Salaam
18/02/12

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Nimelazimika leo Jumamosi, tarehe 18 Februari, 2012 kutoa taarifa hii kwa vyombo vya habari kufuatia mkutano wa DCI Robert Manumba na waandishi wa habari jana (17/02/12) kuongelea, pamoja na mambo mengine, hali yangu ya afya na kuhitimisha, kienyejienyeji tu kuwa “sikunyweshwa sumu” ila naumwa tu ugonjwa wa ngozi bila kufafanua ugonjwa huo wa ngozi umesababishwa na nini!
Napenda nisisitize mapema kabisa kuwa msimamo huo wa Jeshi la Polisi umenikera sana katika hali niliyonayo ya ugonjwa, kwanza kwa kuingilia mchakato wa matibabu yangu na uchunguzi wa kina kuhusu kiini chake unaoendelea hospitali ya Apollo nchini India ambako bado sijahitimisha matibabu yangu; pili kwa ufinyu wa uelewa unaojitokeza bayana kwenye tamko la Jeshi la Polisi unaosisitiza kuwa “sikunyweshwa sumu” wakati sumu si lazima unyweshwe ili ikudhuru, inaweza kudhuru hata kwa kugusishwa tu; na tatu kwa Jeshi la Polisi kujiingiza kwenye suala ambalo kwa takriban mwaka mzima halijawahi kuwa na dhamira ya dhati ya kulielewa au kulichunguza mbali na kulifanyia mzaha kupitia magazetini.
Itakumbukwa kuwa tarehe 9 Februari, 2011 nilimwandikia barua IGP Said Mwema kumtaarifu kuhusu njama za kuondoa maisha yangu na ya viongozi wengine. Kwa kutambua kuwa Jeshi la Polisi la Tanzania daima husisitiza kuletewa ushahidi kwanza ndipo lifanyekazi, nilihakikisha nimeainisha katika barua hiyo kila ushahidi nilioupata au kupewa. (Utaratibu huu wa Jeshi la Polisi kusubiri kuletewa ushahidi mezani, kama ambavyo mahakimu wanavyosubiri ushahidi mahakamani, haupo popote pale duniani (ila Tanzania tu) kwani kazi ya msingi ya Polisi si kuletewa, ni kutafuta ushahidi. Polisi wanachohitaji duniani kote ni kupata clue au tetesi tu. Hiyo inatosha kufukua ushahidi wote unaohitajika). Pamoja na kujitahidi kuanika kila aina ya ushahidi niliokuwa nao, mambo manne yalijitokeza ambayo yalionyesha wazi kuwa Polisi hawakuwa na dhamira ya dhati ya kupeleleza suala hilo:

(i) Siku chache baada ya kumkabidhi IGP barua hiyo, nilitumiwa timu ya “wapelelezi” ofisini kwangu kuja kuchukua maelezo yangu ya ziada. Timu hiyo ilikuwa inaongozwa na ACP Mkumbo, afisa wa polisi ambaye wiki chache zilizokuwa zimepita alikuwa miongoni mwa askari waliotuhumiwa kupokea rushwa kwa lengo la kumbambikizia madawa ya kulevya mtoto wa Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi, suala ambalo mpaka leo hii uongozi wa Polisi umeshindwa kulitolea maelezo ya kuridhisha. Kwa msingi huo, nilikuwa nimeletewa mtuhumiwa wa rushwa/ ujambazi kuendesha uchunguzi wa watuhumiwa wengine wa ujambazi! Nikatambua mara moja kuwa zoezi zima lilikuwa la mzaha, tena mzaha mkubwa!

(ii) Wiki chache baada ya barua yangu kuwasilishwa kwa IGP na timu ya ACP Mkumbo “kuanza kazi”, Jeshi la Polisi likachukua hatua ya kuwapongeza na kuwazawadia askari niliowatuhumu kushirikiana na majambazi! Huhitaji kuwa profesa wa falsafa kuelewa kuwa huo ulikuwa ujumbe tosha wa kunipuuza.

(iii) Hivi karibuni tuhuma za askari polisi kujihusisha na vitendo vya ujambazi mkoani Morogoro zilipopamba moto na kuwagusa askari “wale wale” niliowatuhumu kwenye barua yangu, IGP alichukua hatua ya kuwahamishia mikoa mingine!

(iv) ili kunikatisha tamaa kabisa, barua yangu ya “siri” kwa IGP ikavujishwa kwa makusudi kwenye vyombo vya habari na kuchapishwa kama habari ambayo ilikebehi na kukanusha taarifa nzima niliyotoa, sijui kwa faida ya nani! Lakini huu ni mchezo wa kawaida kwa polisi kwani hivi karibuni Mhe. Waziri Samuel Sitta alipohojiwa na ofisa mwandamizi wa Jeshi la Polisi ofisini kwake, wakiwa wawili tu, taarifa ya kikao hicho ikawa magazetini ikikebehi ushahidi aliotoa Sitta! The integrity of the police force leadership is on the line.
Nimeelezea vizuri katika barua yangu kwa IGP kuwa kundi hilo la mauaji lilikuwa limeelekezwa kuniua kwa kutumia sumu, taarifa ambayo kwa karibu mwaka mzima Polisi hawakutaka kuifuatilia kwa sababu wanazozijua wenyewe. Sasa huu msukumo mpya wa Jeshi la Polisi kutaka kujua kama nilipewa sumu au la na kukurupuka kutoa tamko hata kabla ya kunichunguza nilivyo, kunihoji mimi na wasaidizi wangu ofisini na hata kuongea na mabingwa wa Kihindi wanaonifanyia uchunguzi, umetokea wapi?

Aidha napata taabu kuamini kama DCI Manumba na wenzake waliisoma taarifa halisi ya matatibabu yangu au walisoma taarifa “nyingine”, na kama waliisoma taarifa hiyo wenyewe au “walisomewa”! Nasema hivyo kwa kuwa alichokisema DCI Manumba kwa wandishi wa habari hakifanani kabisa na picha iliyo kwenye taarifa halisi ya Apollo ambayo inatamka wazi kuwa kuna kitu kwenye bone marrow kinachochochea hali niliyonayo, kitu ambacho mabingwa wanahangaikia kukidhibiti/ kukiondoa huku vyombo vyetu vya dola vikipelekeshwa na mafisadi kusema bila msingi wa kisayansi na bila aibu: “hakulishwa sumu”, “hakulishwa sumu”!
Nimesoma darasa moja Kitivo cha Sheria Mlimani na DCI Manumba. Baadaye IGP Mwema alikuwa mwanafunzi wangu wa sheria Mlimani. Vigogo hawa wawili wa usalama wa raia nchini hawajanitendea haki, nao wanajua. Wanajua vilevile kuwa sitakaa kimya au kumung’unya maneno come what may pale ambapo haki inakanyagwa.
Tuendelee kuombeana afya na uhai ili kutendeane haki na vilevile tuitendee nchi yetu haki kwa kuvimalizia viporo vinavyokera vya Dowans, EPA, Kagoda n.k. kwa maslahi mapana ya Taifa letu.

Mungu Ibariki Tanzania
 
Hata bila kumsikiliza Mwakyembe mwenyewe, ni dhahiri kuwa Sitta ni mkweli kuliko Manumba kwa sababu;
  1. Sitta yupo karibu zaidi na Mwakyembe kuliko alivyo manumba.
  2. Sitta alikwenda India kumjulia hali mwakyembe wakati akipatiwa matibabu na bila shaka madaktari walizungumza hilo.
  3. Sitta aliitoa hiyo kauli mbele ya mwakyembe na mwakyembe hakupinga, hiyo ina maana mwakyembe anajua hivyo pia. Kwa upande mwingine, Manumba alitoa kauli hiyo wakt mwakyembe hayupo kabisa nchini.
  4. Sitta alitoa kauli kwa kujiamini, huku akiamini anachokisema wakati Manumba alitoa kauli hiyo kwa woga, bila kujiamini huku akiwa haamini anchokisema.
Kuna memgi ya kulinganisha ili kujua nani mkweli kati yao ila kwa hayo machache tu bila shaka Sitta ana uwezekano mkubwa wa kuwa alichokisema kina ukweli wakati alichosema Manumba hakina sababu ya kuaminika.

Mkuu MARQ nimekukubali kwa point namba 4! DCI alikuwa anaongea bila kujiamini!
 
Jamani,uongozi ni sehemu tu ya majukumu,siyo kwamba viongozi wanaakili sana kushinda watu wote,Dr huthibitisha tatizo la mtu,je polisi wanapima afya ya watu siku hizi?Mwakembe anaumwa nini,waseme,polisi hawawasemei wataalamu wa afya,tunaweza amini ni kwelilisemwalo.
 
Haya wanajamvi,
Taarifa ya Mwakyembe hiyo hapo! kila tulichokijadili na kudhaniwa ni conspiracy kakisema mwenyewe.
Tume question integrity ya jeshi kama alivyofanya Mwakyembe kuanzia matukio ya mwanzo
Tumehoji taarifa ya DCI kama alivyofanya, tumehoji kama Mwakyembe alishirikishwa kwenye uchunguzi, amekana!
Tumekataa kuchukua upande na kulishwa maneno 'hakuna sumu' bila kufikiri

Narudia kusema kama hatutatafuta ukweli na kuusimamia ili haki itendeke, itafika mahali tutapoteza uhuru wetu wa kuongea, kujadili n.k
Nimesema awali kuwa serikali inahaha kulinda kundi fulani, swali ni kuwa kwanini sheria, taratibu na heshima ya taifa itawaliwe na kundi hili la watu wasiozuidi 50?

Bado nashawishika kuwa kwa jinsi serikali inavyojikanyaga, kuna watu wanamkono mkubwa ndani yake. Kama kuna kundi la watu lenye nguvu kuliko serikali basi hatupo salama kabisa.

Kwa wanaotetea uhalifu kwa mgongo wa serikali badala ya kutafuta ukweli , taarifa ya Dr hiyo hapo!
 
Mwakyembe bado hujasema kuwa umelishwa au umepakwaa sumu au umenyinyiziwa au umegusishwa.

Wewe mwenyewe unakiri kuwa "taarifa halisi ya Apollo ambayo inatamka wazi kuwa kuna kitu kwenye bone marrow kinachochochea hali niliyonayo"

Kuwa na kitu kwenye bone marrow hakumaanishi umegusishwa sumu au umenyweshwa sumu. Hata Julius Kambarage Nyerere alikuwa na kitu kwenye bone marrow kilichosabisha kuumwa kwake na ugonjwa huo kupelekeaa kifo chake.

Hapo unajaribu kupata huruma lakini hukuonesha report kuwa umepewa, umelishwa, umegusishwa sumu. Manumba mpaka sasa hivi yupo sahihi.

Ungeonesha kinaga ubaga kuwa hii hapa ripoti ya madaktari wa India au wa Tanzania au wa nchi nyingine yoyote ile. Hapo ungetukinaisha. Kwa sasa bado unacheza na maneno na hakuna mahalai ulipothibitisha kuwa maradhi yako yanatokana na sumu.

Kumbuka kuwa Sumu si lazima upewe, ulishwe, ugusishwe., upakwe. Hata madawa tu yakukutibu yanaweza kuwa toxic na kugeuka sumu, kwa maana hiyo, hata kama ni sumu ndio inasababisha hali yako inawezekana ni sumu inayosababishwa na madawa unayotumia au uliyotumia kabla ya hiyo hali kukutokea, hiyo kitaalam huitwa "medicine toxicity".

Mpak uttuthibitishie kitaalam na watu wenye fani yao wathibitishe kuwa sumu inayomdhuru ni hii na hii imesababishwa na hiki (ioneshe ni kuwa sumu ya kupewa, kupakwa, kunyunyiziwa, kunyweshwa) Hapo kidogo tutakuamini, isitoshe tuoneshwe na motive ya wewe kupewa sumu, kuna kesi za watu kupewa sumu na wake zao, kwa wivu, ugomvi wa nyumbani, kutaka mirathi na mengine mengi. Mpaka tutakapainishiwa kuwa ni sumu na motive ya kupewa sumu, hapo tutakuamini. Kwa sasa bora ungekaa kimya tu.

Tafadhali Dr. Mwakyembe usicheze na akili za waTanzania, inahusu nini kuwafundisha kumfundisha kwako Saidi Mwema na kusoma kwako pamoja na Manumba kuingizwe kwenye hii issue? huo si usomi ni upunguani wa hali ya juu.
 
Dk. Harrison G. Mwakyembe (Mb), NW-UJ

Dar es Salaam
18/02/12

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Nimelazimika leo Jumamosi, tarehe 18 Februari, 2012 kutoa taarifa hii kwa vyombo vya habari kufuatia mkutano wa DCI Robert Manumba na waandishi wa habari jana (17/02/12) kuongelea, pamoja na mambo mengine, hali yangu ya afya na kuhitimisha, kienyejienyeji tu kuwa “sikunyweshwa sumu” ila naumwa tu ugonjwa wa ngozi bila kufafanua ugonjwa huo wa ngozi umesababishwa na nini!
Napenda nisisitize mapema kabisa kuwa msimamo huo wa Jeshi la Polisi umenikera sana katika hali niliyonayo ya ugonjwa, kwanza kwa kuingilia mchakato wa matibabu yangu na uchunguzi wa kina kuhusu kiini chake unaoendelea hospitali ya Apollo nchini India ambako bado sijahitimisha matibabu yangu; pili kwa ufinyu wa uelewa unaojitokeza bayana kwenye tamko la Jeshi la Polisi unaosisitiza kuwa “sikunyweshwa sumu” wakati sumu si lazima unyweshwe ili ikudhuru, inaweza kudhuru hata kwa kugusishwa tu; na tatu kwa Jeshi la Polisi kujiingiza kwenye suala ambalo kwa takriban mwaka mzima halijawahi kuwa na dhamira ya dhati ya kulielewa au kulichunguza mbali na kulifanyia mzaha kupitia magazetini.
Itakumbukwa kuwa tarehe 9 Februari, 2011 nilimwandikia barua IGP Said Mwema kumtaarifu kuhusu njama za kuondoa maisha yangu na ya viongozi wengine. Kwa kutambua kuwa Jeshi la Polisi la Tanzania daima husisitiza kuletewa ushahidi kwanza ndipo lifanyekazi, nilihakikisha nimeainisha katika barua hiyo kila ushahidi nilioupata au kupewa. (Utaratibu huu wa Jeshi la Polisi kusubiri kuletewa ushahidi mezani, kama ambavyo mahakimu wanavyosubiri ushahidi mahakamani, haupo popote pale duniani (ila Tanzania tu) kwani kazi ya msingi ya Polisi si kuletewa, ni kutafuta ushahidi. Polisi wanachohitaji duniani kote ni kupata clue au tetesi tu. Hiyo inatosha kufukua ushahidi wote unaohitajika). Pamoja na kujitahidi kuanika kila aina ya ushahidi niliokuwa nao, mambo manne yalijitokeza ambayo yalionyesha wazi kuwa Polisi hawakuwa na dhamira ya dhati ya kupeleleza suala hilo:

(i) Siku chache baada ya kumkabidhi IGP barua hiyo, nilitumiwa timu ya “wapelelezi” ofisini kwangu kuja kuchukua maelezo yangu ya ziada. Timu hiyo ilikuwa inaongozwa na ACP Mkumbo, afisa wa polisi ambaye wiki chache zilizokuwa zimepita alikuwa miongoni mwa askari waliotuhumiwa kupokea rushwa kwa lengo la kumbambikizia madawa ya kulevya mtoto wa Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi, suala ambalo mpaka leo hii uongozi wa Polisi umeshindwa kulitolea maelezo ya kuridhisha. Kwa msingi huo, nilikuwa nimeletewa mtuhumiwa wa rushwa/ ujambazi kuendesha uchunguzi wa watuhumiwa wengine wa ujambazi! Nikatambua mara moja kuwa zoezi zima lilikuwa la mzaha, tena mzaha mkubwa!

(ii) Wiki chache baada ya barua yangu kuwasilishwa kwa IGP na timu ya ACP Mkumbo “kuanza kazi”, Jeshi la Polisi likachukua hatua ya kuwapongeza na kuwazawadia askari niliowatuhumu kushirikiana na majambazi! Huhitaji kuwa profesa wa falsafa kuelewa kuwa huo ulikuwa ujumbe tosha wa kunipuuza.

(iii) Hivi karibuni tuhuma za askari polisi kujihusisha na vitendo vya ujambazi mkoani Morogoro zilipopamba moto na kuwagusa askari “wale wale” niliowatuhumu kwenye barua yangu, IGP alichukua hatua ya kuwahamishia mikoa mingine!

(iv) ili kunikatisha tamaa kabisa, barua yangu ya “siri” kwa IGP ikavujishwa kwa makusudi kwenye vyombo vya habari na kuchapishwa kama habari ambayo ilikebehi na kukanusha taarifa nzima niliyotoa, sijui kwa faida ya nani! Lakini huu ni mchezo wa kawaida kwa polisi kwani hivi karibuni Mhe. Waziri Samuel Sitta alipohojiwa na ofisa mwandamizi wa Jeshi la Polisi ofisini kwake, wakiwa wawili tu, taarifa ya kikao hicho ikawa magazetini ikikebehi ushahidi aliotoa Sitta! The integrity of the police force leadership is on the line.
Nimeelezea vizuri katika barua yangu kwa IGP kuwa kundi hilo la mauaji lilikuwa limeelekezwa kuniua kwa kutumia sumu, taarifa ambayo kwa karibu mwaka mzima Polisi hawakutaka kuifuatilia kwa sababu wanazozijua wenyewe. Sasa huu msukumo mpya wa Jeshi la Polisi kutaka kujua kama nilipewa sumu au la na kukurupuka kutoa tamko hata kabla ya kunichunguza nilivyo, kunihoji mimi na wasaidizi wangu ofisini na hata kuongea na mabingwa wa Kihindi wanaonifanyia uchunguzi, umetokea wapi?

Aidha napata taabu kuamini kama DCI Manumba na wenzake waliisoma taarifa halisi ya matatibabu yangu au walisoma taarifa “nyingine”, na kama waliisoma taarifa hiyo wenyewe au “walisomewa”! Nasema hivyo kwa kuwa alichokisema DCI Manumba kwa wandishi wa habari hakifanani kabisa na picha iliyo kwenye taarifa halisi ya Apollo ambayo inatamka wazi kuwa kuna kitu kwenye bone marrow kinachochochea hali niliyonayo, kitu ambacho mabingwa wanahangaikia kukidhibiti/ kukiondoa huku vyombo vyetu vya dola vikipelekeshwa na mafisadi kusema bila msingi wa kisayansi na bila aibu: “hakulishwa sumu”, “hakulishwa sumu”!
Nimesoma darasa moja Kitivo cha Sheria Mlimani na DCI Manumba. Baadaye IGP Mwema alikuwa mwanafunzi wangu wa sheria Mlimani. Vigogo hawa wawili wa usalama wa raia nchini hawajanitendea haki, nao wanajua. Wanajua vilevile kuwa sitakaa kimya au kumung’unya maneno come what may pale ambapo haki inakanyagwa.
Tuendelee kuombeana afya na uhai ili kutendeane haki na vilevile tuitendee nchi yetu haki kwa kuvimalizia viporo vinavyokera vya Dowans, EPA, Kagoda n.k. kwa maslahi mapana ya Taifa letu.

Mungu Ibariki Tanzania

Nilisema, taarifa ya upande wa Dr. Mwakyembe ikija hapa patakuwa hapatoshi...In summary Jeshi la Polisi linatumiwa na Mafisadi na kwa mantiki hiyo, watanzania hatuna Jeshi la Polisi.... What Next??
 
Yasema sasa imekamilisha uchunguzi
headline_bullet.jpg
Kupeleka jalada kwa DPP



DCIManumba(1).jpg

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Kamishina Robert Manumba akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana.


Sakata kuhusu madai kuwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe, amelishwa sumu, limeingia katika hatua mpya, kufuatia Jeshi la Polisi nchini kusema tayari limemaliza uchunguzi na linaandaa jalada kwa ajili ya kulipeleka kwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP).
Dk. Mwakyembe aliugua ugonjwa wa ngozi Oktoba 9, mwaka jana na kupelekwa nchini India kwa ajili ya matibabu na kulazwa katika Hospitali ya Andraprasta Apollo iliyopo mjini China na kurejea nchini Desemba 11, mwaka jana.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Kamishina Robert Manumba, alisema katika uchunguzi wao waliwasiliana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ili kupatiwa taarifa kuhusiana na ripoti ya ugonjwa wa Dk. Mwakyembe kama inaonyesha alilishwa sumu au la.
Hata hivyo, Manumba alisema wizara hiyo iliwajulisha kuwa maradhi ya Dk. Mwakyembe, ambaye pia ni mbunge wa Kyela hayahusiani na kulishwa sumu.
Alisema waliwahoji watu mbalimbali kuhusiana na tuhuma hizo na kusisitiza kuwa kwa sasa hayupo tayari kuwataja.
Alisema kuhusiana na madai aliyoyatoa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta ni matamshi ambayo yana jinai ndani yake na kwamba Jeshi hilo liliamua kuyafuatilia ili kubaini kama kuna ukweli au la.
Manumba alisema kwa kuwa Waziri Sitta katika matamshi yake hakumtaja mtu ambaye amehusika katika suala hilo, wao wanachokifanya ni kuchunguza.
Aidha, alisema Dk. Mwakyembe aliwahi kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi kuwa anatishiwa maisha yake na kuzifanyia uchunguzi.
Aiongeza kuwa walipokuwa wanakaribia kukamilisha uchunguzi ndipo Dk. Mwakyembe alipoanza kuugua na kupelekwa India kwa matibabu.
Alisema wanaendelea na uchunguzi wao kuhusiana na taarifa alizopeleka Dk. Mwakyembe kuwa alikuwa anapata vitisho.
"Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii imetupatia taarifa hiyo kwa sasa tunachokifanya ni kuandaa jalada hilo na hatutatumia muda mrefu kuliwasilisha kwa DPP," alisema Manumba.
Hivi karibuni, Waziri Sitta alisema taarifa ya ugonjwa wa Dk. Mwakyembe kutoka kwa madaktari wa Apollo iko Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, na akashangaa kwa nini inaona ugumu wa kuitangaza wakati mwenyewe (Dk. Mwakyembe) ameridhia.
Sitta pia alisema uchunguzi aliofanyiwa Dk. Mwakyembe nchini humo kwa kuchukua sehemu mbalimbali za mwili, zikiwemo kucha na ngozi, umeonyesha kwamba alilishwa sumu.
Waziri huyo alisema Dk. Mwakyembe anatarajiwa kwenda tena India kesho (Februari 19), na atakaporejea nchini ameahidi kupasua jipu juu ya ugonjwa wake.
Sitta alililaumu Jeshi la Polisi kupuuza madai ya vitisho vya kuuawa kwa baadhi ya viongozi, akiwamo yeye pamoja na watu binafsi.
Akitolea mfano, alisema aliwahi kupeleka taarifa za kutishiwa kuuawa mjini Dodoma wakati huo akiwa Spika wa Bunge, lakini Jeshi la Polisi mkoani humo hadi leo halijazifanyia kazi taarifa hizo wala kumpa majibu ya kuridhisha.
Alisema kuwa mbunge mmoja aliwahi kunasa mazungumzo ya watu fulani Dodoma wakipanga kuligonga gari lake na kwamba alipeleka taarifa hizo Polisi, lakini hawakuzifanyia kazi.
BIASHARA YA DAWA ZA KULEVYA
Wakati huo huo, Manumba alisema kuwa bado kumekuwa na tatizo la ongezeko la kiwango cha uingizaji wa dawa za kulevya nchini ingawa takwimu zinaonyesha kuwa mwaka 2010 matukio ya kukamatwa kwa dawa hizo yalikuwa 707 ikilinganishwa na ya mwaka jana 604.
Alisema pamoja na kupungua kwa idadi ya makosa hayo, kumekuwa na ongezeko la kukamatwa kwa kiwango kikubwa zaidi cha dawa hizo ikilinganishwa na kipindi cha nyuma.
“Kutokana na kukamatwa na kiwango hicho kikubwa na watuhumiwa ambao ni raia wa nchi za nje, kuna kila dalili kwamba ukanda wa pwani ya Afrika Mashariki unatumika kama kituo cha kusafirisha dawa hizo kwenda nchi nyingine na kiwango kidogo kutumika nchini,” alisema Manumba
Alisema ili kumaliza tatizo hilo wamejipanga kuimarisha doria katika viwanja vya ndege, bandari zote pamoja na maeneo ya mipaka ya nchi.
UCHAGUZI WA ARUMERU
Akizungumzia uchaguzi mdogo wa ubunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki, mkoani Arusha, ambao unatarajia kufanyika Aprili 1 mwaka huu, alisema wamejipanga kuhakikisha usalama unakuwepo na hawapo tayari kuona vitisho vyovyote vinatokea kwa wananchi.
Manumba, alisema wanategemea kuona uchaguzi huo unafanyika kwa amani na vyombo vya dola vitafanya kazi yake ya kuhakikisha vinawalinda wananchi na amani kuwepo.
Alisema viongozi ambao wanagombea wawaache wananchi wachague watu wao wanaowapenda bila kuwepo kwa vitisho wala kuwapiga watu.



CHANZO: NIPASHE

 
Lakini hata uchunguzi unasema Mwakyembe hakulishwa sumu.. sasa ikiwa mnasema kalishwa kuna kosa gani kusema hakulishwa... Na kikubwa zaidi hakusema wala kukataa kama sumu imetumika..
 
Mkuu Mchambuzi, nimependa unavyochambua, ki ukweli unazama deep!.
Nimeupitia uchambuzi wako kuna kitu sijakiona ukikizungumza kuhusu sumu.
Kuna sumu za aina tatu,
1. Intentions or delibarate poisoning, hii ndio ile dhana ya mtu kulishwa sumu, kutiliwa, kushikishwa au hata kutumiwa kwa barua kama 'anthrax', hii ni mtu kupewa sumu be it first poisoning or slow poisoning ila mwisho wa siku mhusika hudhurika!.
2. Food poisoning, hii ni aina ya pili ya sumu ambayo hutokana na kula chakula chenye sumu, mfano kuna baadhi ya mihogo ina sumu, uyoga, na baadhi vya vyakula vya proteion in nature kama nyama, samaki, maziwa, mayai etc ambapo aliyekula vinamdhuru ama instantly kwa kupata rushes, kuwashwa au kupata mafindofindo wanaita 'alergy' au slow reaction ambapo inaibuka baada ya kipindi kirefu na ineweza kuibuka kama kansa etc!.
3. Medical Reaction, japo sumu zote ni chemical reaction, hii sumu ya medical reaction ni sumu inayotokana na reaction ya madawa fulani fulani kwenye mwili wa binadamu mostly kutokana na prolonged use!. Hii humpata mtu ambaye kuna kitu ameugua na ni ugonjwa wa muda mrefu, mtu huyo anakuwa anatumia combination ya madawa fulani kwa muda mrefu imefikia muda madawa hayo yamereact from each other na kugeuka sumu na wakati huo huo mwili unakuwa umetengeza 'antigen' za kukabiliana na hiyo reaction na matokeo huwa ndiyo kama hiyo hali ya Mwakiyembe!.

Wanabodi nilishauri huko nyuma na hapa nashauri tena, tupunguze conspiracy theories tusubiri tamko la Mwakiyembe mwenyewe!.

Japo naye ili kumlindia Sitta heshima, anaweza kusema "Nimesha Muachia Mungu, hivyo naomba nisizungumze chochote"! hivyo kutosema anaumwa nini!.
Akiwa Kyela rais Magufuli amethibitisha Dr. Mwakyembe alitiliwa sumu. Tangu kuibuka kwa kadhia ya sumu ya Mwakyembe, hii ndio kauli from the highest authorities kuwa Mwakyembe alitiliwa sumu. Kutiliwa sumu ni criminal offence ya attempted murder, kama rais anathibitisha Waziri wake alitiliwa sumu na wahusika anawajua na hakuna sio aliyekamatwa, bali aliyehojiwa!, what are the chances kwa wasiojulikana wa Shambulio la Lissu ambao hawajulikani kabisa?.

Hivi katika hili sakata la sumu ya Mwakyembe, iliwahi kuthibitishwa na authorities zozote kuwa ni kweli Mwakyembe alitiliwa sumu, au uthibitisho ndio huu wa leo wa rais Magufuli?.

P.
 
Back
Top Bottom