DCI Manumba: Mwakyembe hajalishwa sumu!

DCI Manumba: Mwakyembe hajalishwa sumu!

Sasa hata mkubwa akijamba ushuzi ukasika unadhani huwa anakubali kama kajamba??
 
Kwa wale mliofuatilia taarifa ya habari hapo jana ITV Mkurugenzi wa Makosa ya jinai DCI manumba alikanusha yale yaliokuwa yakisemwa na Mh.sitta juu ya kinachomsibu Mh. mwakyembe kwamba alipewa sumu.Sasa kinachotatanisha man jf ni kuwa ni nani mkweli kati ya sitta na manumba?.Je! WATANZANIA WAMUAMINI NANI???..Mh.SITTA au DCI MANUMBA?

umefikia kiwango cha mwisho cha kufikiri au?maana mwenye dhamana ya kutamka hayo mambo kasema hakuna kulishwa sumu au ulitaka apindishe ukweli eti kwa sababu huyo sita kapayuka?
 
Kitendo cha DCI Kukanusha wkt Mkyb yuko India nacno kileta was was mwingine. Anawza asurudi kabsaa na wakasema tulishasema haikua sumu. Mbona Mkyb aliomba ulinzi kabla ma akatoa taarifa polis hata kabla ya hiyo sumu. MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMA
 
Wewe Robert Manumba wacha ubabaishaji!

Hivi unaongoza police wa aina gani? Huyo mtu aliyekuteua kuwa DCI alifanya kosa kubwa sana. Kabla ya kuchukua mike na kuongea ungekaa na jopo la experts wakachukua samples za Mgonjwa Mwakyembe mkazichunguza kipolisi na hata Kama ikibidi utuombe tukupatie majina ya forensic experts FBI au KGB private or active ukatoa taarifa iliyokamilika na kwa kuwa hajafa then ungewatoa matongotongo Askari wako na Public at large useme Mh. Mwakyembe anaugua ugonjwa gani.

Kukaa kimya na kusema polisi hawachunguzi mgonjwa you are damnly lost and for sure sikutegemea kusikia uzushi kama huo ukizungumzwa na DCI katika nchi za Jumuia ya Madola. You are a disgrace to intelligence stop politika. Jibu maswali ya waandishi Mwakyembe anaumwa nini? Wacha kumtishia nyau Sitta. Yeye alizungumza kanisani and for your ignorance you can't prosecute him..?

Kama unakula chauro za akina Manji na Rostam na akina Chenge time is over unaweka a very bad precedence we Mnyanwezi weee!!!
 
Hata bila kumsikiliza Mwakyembe mwenyewe, ni dhahiri kuwa Sitta ni mkweli kuliko Manumba kwa sababu;
  1. Sitta yupo karibu zaidi na Mwakyembe kuliko alivyo manumba.
  2. Sitta alikwenda India kumjulia hali mwakyembe wakati akipatiwa matibabu na bila shaka madaktari walizungumza hilo.
  3. Sitta aliitoa hiyo kauli mbele ya mwakyembe na mwakyembe hakupinga, hiyo ina maana mwakyembe anajua hivyo pia. Kwa upande mwingine, Manumba alitoa kauli hiyo wakt mwakyembe hayupo kabisa nchini.
  4. Sitta alitoa kauli kwa kujiamini, huku akiamini anachokisema wakati Manumba alitoa kauli hiyo kwa woga, bila kujiamini huku akiwa haamini anchokisema.
Kuna memgi ya kulinganisha ili kujua nani mkweli kati yao ila kwa hayo machache tu bila shaka Sitta ana uwezekano mkubwa wa kuwa alichokisema kina ukweli wakati alichosema Manumba hakina sababu ya kuaminika.

nasikia kati ya watu walotumika kumpa sumu mwakyembe ni samuel sita kwa kuwa ndo mtu pekee alokuwa jirani na mwakembe na hivyo kuwa na uwezo mkubwa zaidi wa kumfikia mwakyembe.hapa sita anajikosha ili asijulikane.mnafiki sana huyo
 
Kwa kiasi fulani inakuwa ngumu ku-judge ukweli ni upi kwenye mkasa huu kwa sababu: Dr.Mwakyembe na Sitta ni wanasiasa wanaokubalika na wanaoheshimika kwa watu wengi(its my opinion).
However Mwakyembe hakuwa tayari kutoa evidence kuwa alilishwa sumu,how comes Sitta anakuwa ndie msemaji wa kunadi ugonjwa wake?Kwa maana Sitta sio msemaji wa familia ya Mwakyembe au msemaji wa jeshi la polisi.
Na kama DCI taarifa alizotoa kazipata wizara ya afya na hospitali India alikotibiwa,kwa nini tusikubali hizi ndio taarifa sahihi,na hizi zinazotolewa na Sitta ni "MINONG'ONO YA MITAANI". Wakati mwingine tusiwe wepesi wa kufata hisia zetu ku-judge ukweli ni upi! Unless kama Robert Manumba katoa taarifa zisizo sahihi kwa umma.

Mkuu nashukuru kwa observation yako" No research No right to talk", kwa nini Mwakyembe na 6 hawaelezi scenario ilivyo badala yake wanatoa manung'uniko ambayo hayana nyama (supporting evidence), we all know that Mwakyembe is sick but what is the main problem? wanasema kalishwa sumu; how? watupe maelezo ya kutosha. Manumba kaeleza findings zake kuwa kwa mujibu wa wizara ya afya na hospitali ya India hajalishwa sumu, kama kina 6 wanaona si kweli watupe fact. nafikiri hakuna mwana jf anayependa Mwakyembe auwawe, huyu ni moja ya tools za maendeleo za Tz
wanaoilaumu CCM siwaelewi pia, tusipende kutoa michango ya kufikirika isiyo na ukweli au tija, hii ishu ni sensitive, kwani Mwakyembe ni CUF?
Jamani kuna magonjwa mengi duniani, tuwe tunatembelea mahospitalini tuone watz walivyo na magonjwa ya ajabu, kama mnakumbuka kipindi cha Babu wa Loliondo kuna magonjwa ya kutisha tulikuwa tunayaona, hebu mwak atupe ukweli wa ugonjwa wake(details) kwani Polisi haina nguvu kisheria kufanya hivyo
Inawezekana mtu akawa na sumu mwilini kwa njia mbalimbali, vyakula tunavyotumia na life style inauwezo wa ku accumulate baadhi ya vitu ambavyo ni toxic lakini si lazima uwe umelishwa yote at a time, tunaona watu wakisumbuliwa na saratani mbalimbali (ngozi, damu nk) haya yote ni matokeo ya accumulation ya carcinogenic substances, sasa kwa wengine inawezekana but kwa viongozi kama kina Mwa k tunatafuta sababu za ziada. Mwa K tunakupenda sana pls break the silence kwa kuelezea kwa undani ili kama kuna evidence za kutosha kuwa umelishwa sumu tupambane, hata Libya, Misri na Tunisia ni nguvu ya umma ilitumika, ili na sisi tuindoe serikali itakayokuwa inaua raia wake
 
Kwanini DCI Manumba hakumshirikisha Dr. Ahmed Makatta amchukue samples Dr. Mwakyembe ili aje na scientific explanation?
Dr. Makatta ni qualified pathologist/toxicologist/forensic na Serikali huwa inamtumia sana kwenye issue kama hizi.

Dr. Makatta are you around?
 
..DCI Manumba alisema matamshi ya sitta ni matamshi ambayo yana jinai ndani yake na kwamba HAKUMTAJA mtu anaehusika katika swala hilo, wao wanacho fanya ni kuchunguza..Kwa mantiki hiyo sitta hana kosa wala shtaka la kujibu..upo hapo??

Sasa hilo file la uchunguzi limepelekwa kwa Feleshi kwa kusudi gani?
 
Bosi wake, yaani waziri wa mambo ya ndani alisema kuwa matokeo ya uchunguzi huu hayatawekwa wazi...

Nini kimemsibu Manumba sasa?
 
Wewe ni polis unasema Mwakyembe hajalishwa sumu. Sasa kwa nini usimkamate Sitta amusaidie kutoa ushahidi. Au Sitta kusema uongo si kosa la kuudanganya umma?

pole kaka inaelekea hukuangalia hiyo taarifa ila umesimuliwa, DCI amekwambia wamefungua jalada la uchunguzi, sasa wamkamate bila kuwa na findings za kutosha? polisi hawawezi kukurupuka bila kuwa na enough info, kama 6 an evidence za kutosha inamaana DCI anatakiwa aseme findings zake toka Wizara ya afya na huko India amezipataje na pia wafanye detailed analysis ili kujua ukweli
 
Wanajamvi,

Nchi hii tunafikishwa pabaya muda si mrefu. Hivi kuna shida gani ktk serikali yetu hii? Kwanini kila inapokuja na tamko la tatizo au shida fulani, yaani majibu yake huwa ni tatizo kubwa zaidi au huongeza shida hiyo kuwa kubwa zaidi kuliko tatizo au shida yenyewe? Huko Nyuma niliwahi kusema, tumefika kipindi ambapo sijui tunaviongozi gani sijui, ambao, kila solution ya tatizo wanalotoa huwa ndio tatizo kubwa zaidi. Sasa kwa hili la DCI, limezua tatizo kubwa zaidi badala ya kulipunguza.

Kwanini nasema hivyo:

1. Ripoti ya Madaktari wa Apollo, ilionyesha kuwa Dr, Mwakyembe mwili wake umeathirika na sumu, tena sumu mbaya, tena ni sumu ambayo haipatikani kirahisi, kama hizi za kuulia Panya, au zile za ndugu zake wa Mbeya wanazopiga kwenye Mikahawa. Ni sumu hatarishi sana ambayo upatikanaji wake na mpaka mtu awe na access nayo, basi ni lazima kuwe na kazi ya ziada imefanyika. Na ripoti ikaonyesha Dr. ameathirika na sumu hiyo. Ripoti ikaenda mbali, kuonyesha ni namna gani sumu hiyo inaweza kumpata mtu. Kwa vile ni sumu kali sana basi mtu anaweza kuathirika kwa kuivuta, kuigusa, kunywa, au hata kutumia kitu kilichowekwa sumu hiyo kali. Ripoti hiyo, ilionyesha pia estimation ya time ambayo muathirika anaweza kuwa alikutana na sumu hiyo kwa mara ya kwanza, kitu ambacho kingeweza kusaidia ku narrow down kwa ratiba za Dr. na Kujua possible areas ambazo DR. alikuwepo na kupata tatizo hilo.

2. Kwa vile Dr. ni Kiongozi wa Serikali tena wa kuteuiwa na Rais, na kukabidhiwa mikoba ya siri za Serikali, kulikuwa na utata mkubwa kuwa, kiongozi huyu wa Serikali amekutana wapi na sumu hii kali? Hivyo basi, jukumu likawa kwa ripoti ile kuletwa Serikalini ili Serikali ifanya uchunguzi wake ni vipi mteule huyu wa Rais ameathirika na sumu hiyo. Kwanza kwa kuchuchunguza simu hiyo inawezapatikana wapi, na possible areas ambazo Dr alikuwepo na angeweza kukutana na tatizo hilo. Ndio maana, kwa vile Dr. alijua uzito wa suala lenyewe na kwa vile yeye ni mteule wa Rais, akaona ni vyema aiachie Serikali ifanye kazi yake kwani ndio wajibu wake. Ukiunganisha na malalamiko ambayo Dr. Mwakyembe alikuwa ameshayatoa ktk jeshi la Polisi kuhusiana na mpango wa mauaji juu yake na viongozi wengine, kukawa hakuna ubishi kuwa na hili la sumu ni mbinu zilezile, ndio maana Dr. akawaachia Polisi na hasa Serikali ndiyo ifanye uchunguzi na kumjulisha Dr wabaya wake.

3. Cha kushangaza na kwa mastaajabu makubwa, nadhani hata Dr. Mwakyembe mwenyewe atakuwa ameshanga ni hiyo taarifa ya DCI kuhusu sakata hilo. Taarifa ya DCI inamtwika mteule wa Rais kuwa yeye mwenyewe ndiye anajua amepata wapi hiyo sumu kali, ambayo si rahisi kupatikana kwa mtu wa kawaida, na yeye mwenyewe ndiye labda amejidhuru, kitu ambacho nadhani kinaleta mkakanyiko mkubwa, na kama nilivyosema, kinazua tatizo kubwa zaidi.

4. Sakata hili, linazidi kutuonyesha mpasuko mkubwa ktk serikali yetu, kuwa hata vyombo vya usalama tunavyovitegemea, navyo vimepasuka vipande vipande na kila upande unasema na kufanya litakalo, kitu ambacho ni mwisho mbaya ninao uzungumzia utatukuta muda si mrefu sisi watanzania.

5. Labda nimkumbushe tu DCI kuwa, historia itakuja muhukumu na kuwa yeye ni mtaalamu wa masuala ya upelelezi na si mtalaamu wa field nyingine kama vile Human Psychology. DCI lazima akumbuke, anafanya kazi ktk jamii ya watanzania ambao wamebobea ktk fani mbalimbali, na si mbumbumbu, na kufikiri ni watu wa kukubali kila kitu. Watanzania wa leo na jinsi dunia ya leo ilivyo ktk kiganja, huwezi kuwadanganya kwa kauli zisizo na mshiko, kichwa wa miguu.

6. Sasa tusubiri tamko la kutoka upande wa Dr. Mwakyembe, na mtakubaliana nami hayo niliyoyasema hapo juu.

Source: Personal analysis ya mambo yanavyokwenda Tanzania kwa sasa na hasa Sakata zima la Dr. Mwakyembe.
 
Aisee mambo magumu kweli kweli. Hivi kweli polisi wetu wanaotumiwa wanaubavu wa kusema kuwa mwakyembe kalishwa sumu? Waache ubabaishaji. Je anaumwa nini sasa mbona wanatoa majibu rahisi kwa maswali magumu?
Iko hivi Dr Mwakyembe ni kweli kabisa hakuwekewa sumu kwenye chakula. Sumu iliingiaje kwenye mfumo wa kimwili wa Harrison? Alikuwa akiviziwa sana na jamaa walimwekea sumu kwenye sabuni ya kunawia mikono Dodoma, mara baada ya kuitumia ile sabuni ilitoweka. Cartel ya waliohusika kufanya uharamia huo wa kumtegeshea sumu Mwakyembe inaongozwa na Mbunge wa Monduli, ambaye bunge lilimlazimisha aachie ngazi nafasi ya uwaziri mkuu. Wahusika wote waliisha lipwa kwa kazi hiyo na wana kiapo cha kutosema kwa mtu yeyote.
 
DCI Manumba ameamua kutumiwa na wanasiasa ili kuficha ukweli kuhusu suala la Dr. Mwakyembe. Alama za nyakati zitamuhukumu kwa kutoa hoja zisizo na kichwa wala miguu.
Bosi wake, yaani waziri wa mambo ya ndani alisema kuwa matokeo ya uchunguzi huu hayatawekwa wazi...

Nini kimemsibu Manumba sasa?
 
Umeseama ukweli mkuu. Manumba asitufanye sisi Watanzania ni wajinga. Hivi nani kamtuma kutoa ***** huo.Ametumwa na Rostam nini?
Hata bila kumsikiliza Mwakyembe mwenyewe, ni dhahiri kuwa Sitta ni mkweli kuliko Manumba kwa sababu;
  • Sitta yupo karibu zaidi na Mwakyembe kuliko alivyo manumba.
  • Sitta alikwenda India kumjulia hali mwakyembe wakati akipatiwa matibabu na bila shaka madaktari walizungumza hilo.
  • Sitta aliitoa hiyo kauli mbele ya mwakyembe na mwakyembe hakupinga, hiyo ina maana mwakyembe anajua hivyo pia. Kwa upande mwingine, Manumba alitoa kauli hiyo wakt mwakyembe hayupo kabisa nchini.
  • Sitta alitoa kauli kwa kujiamini, huku akiamini anachokisema wakati Manumba alitoa kauli hiyo kwa woga, bila kujiamini huku akiwa haamini anchokisema.
Kuna memgi ya kulinganisha ili kujua nani mkweli kati yao ila kwa hayo machache tu bila shaka Sitta ana uwezekano mkubwa wa kuwa alichokisema kina ukweli wakati alichosema Manumba hakina sababu ya kuaminika.
 
Hata bila kumsikiliza Mwakyembe mwenyewe, ni dhahiri kuwa Sitta ni mkweli kuliko Manumba kwa sababu;
  1. Sitta yupo karibu zaidi na Mwakyembe kuliko alivyo manumba.
  2. Sitta alikwenda India kumjulia hali mwakyembe wakati akipatiwa matibabu na bila shaka madaktari walizungumza hilo.
  3. Sitta aliitoa hiyo kauli mbele ya mwakyembe na mwakyembe hakupinga, hiyo ina maana mwakyembe anajua hivyo pia. Kwa upande mwingine, Manumba alitoa kauli hiyo wakt mwakyembe hayupo kabisa nchini.
  4. Sitta alitoa kauli kwa kujiamini, huku akiamini anachokisema wakati Manumba alitoa kauli hiyo kwa woga, bila kujiamini huku akiwa haamini anchokisema.
Kuna memgi ya kulinganisha ili kujua nani mkweli kati yao ila kwa hayo machache tu bila shaka Sitta ana uwezekano mkubwa wa kuwa alichokisema kina ukweli wakati alichosema Manumba hakina sababu ya kuaminika.

Kwa maelezo yako...nilitaka kusema hivi hivi sasa mtu mwenye clip ya ITV ya DCI Manumba atuweekee halafu tuipime kwa maelekezo ya mtaalamu huyu wa maswala ya watu waongo
 
Last edited by a moderator:
I beg to differ with DCI Manumba. He is a big liar!

Hivi DCI Manumba anamdanganya nani? Mimi always huwa nawashangaa sana viongozi walioteuliwa na Rais wao Kiwete. Kazi yao ni kuropoka na kuwalaghai Watanzania kama vile ni mazezeta. Kama ni serikali ya kujifunza bila shaka MGOMO WA MADAKTARI NI FUNZO TOSHA. Hakuna mtu anayeweza kukubaliana na taarifa ya uongo ya DCI Manumba. Ni Wizara hii hii ya Afya ambayo imedanganya umma kuhusu mgomo wa Madaktari na sasa viongozi wake wameanza KUTIMULIWA! Sasa ni mjinga gani atakayeamini taarifa za Polisi na Wizara ya Afya kama siyo longolongo tu???

Mimi nafikiri huu ndiyo wakati wa Mhe. Mwakyembe kujitokeza hadharani na kusema ukweli. Namwomba sana Mhe. Mwakyembe atakaporudi toka India for check-up aitishe Press Conference na AMWAGE MBOGA maana serikali ya Kikwete tayari IMESHAMWAGA UGALI. Hivi karibuni tumeshuhudia Mwakyembe akiwa kanisani kwa ajili ya MAOMBI NA ALISIKIKA AKISEMA ANAMSHUKRU MUNGU MAANA MAFISADI WAMESHINDWA!

Kwa akili ya kibinadamu ya kawaida kabisa mtu akisema Mafisadi wameshindwa kwa kuhusisha ugonjwa wake na kupona baada ya matibabu yake kule Apollo,India watu tunapata picha gani kama siyo kwamba MAFISADI ndiyo waliomfanyizia. Mimi siyo mwanasheria wala Polisi lakini najua kina kipengele kinachozungumzia CIRCUMSTANTIAL EVIDENCE kutokana na tukio husika. Kwamba mazingira ya ugonjwa na tuhuma zinazoelekezwa kwa wahusika ambao ni mafisadi zina ukweli wa asilimia 99.99999% kama siyo 100%.

Dr. Mwakyembe hata kabla ya kuanza KUUMWA ALITOA TAARIFA KWA JESHI LA POLISI KWAMBA MAISHA YAKE YALIKUWA HATARINI. KWAMBA KULIKUWA NA KIKUNDI AU KUNDI LA WATU FULANI WALIKUWA WAKIMTAFUTA ILI WAMUUE. Hatukusikia hatua zozote zinzchukuliwa na Jeshi la Polisi na baada ya muda ndipo Dr. Mwakyembe akaanza kuumwa.

Mimi naomba tu kuwa ILE RIPOTI YA MADAKTARI WA APOLLO IWEKWE HADHARANI ili kumaliza ubishi. Kwani kuna siri gani?? Mbona Kiwete alipoanguka Jangwani ripoti ya ugonjwa wake iliwekwa hadharani na madaktari wake???Swala la ugonjwa wa Mhe. Mwakyembe is very case sensitive issue. Siyo swala la kufanyia mzaha maana linaweza kuhatarisha amani na mshikamano wa Watanzania.

Kwako Mhe. SS:

Mhe. Sitta is a very close friend or rather a family freind to Hon. Mwakyembe. SS alisafiri mpaka Apollo Hospital kwenda kumjulia hali Mhe. Mwakyembe na bila shaka kuna siri kubwa anayoijua SS kuhusina na ugonjwa wa Mwakyembe, nafikri ni wakti mwafaka kwa SS naye kutoa taarifa yenye ushahidi,ikiwezekana with evidences from Apollo Doctors' report. Kama SS atashindwa kuwathibitishia Polisi kuhusu Dr. kulishwa sumu basi iajue imekula kwake. SS na Mwakyembe kwa sasa ni wahanga wa Ufisadi lazima wajipange sawasawa kabla HAWAJARIPULIWA MARA YA PILI. SS kwa sasa ni kama amekalia kuti kavu. I predict in the next reshuffle to be announced soonest by JK surely SS and Mwakyembe won't BE AMONG THE MINISTERS. Hili nina uhakika nalo kabisa. Labda utokee muujiza wa Mungu. Alama za nyakati zinaashiria siku za SS na Mwakyembe zina hesabika. Na SS wakishamtema tu basi ajiandae kwa kibano.

Wasaalamu.
 
Back
Top Bottom