DOKEZO DC Mbinga avunje Hostel Bubu kwenye Shule za Sekondari Mbinga DC na Mbinga TC

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Baadhi ya shule za sekondari wilaya Mbinga zimeanzisha hostel bubu ambazo hazifai kwa matumizi ya wanafunzi hususan wa kike hasa madarasa ya mitihani na hata zile shule zenye hostel za wasichana hazina hadhi ya kuwa hostel.

Baadhi ya shule kama vile Kikolo, Mkwaya,Dr.Shein,Mkoha,Matiri zimegeuza madarasa kuwa hostel ambapo wanafunzi wanalala katika sakafu, wanafunzi wanajipikia wenyewe,hawana muangalizi( matron) n k.

Kwenye shule za sekondari za Ngwilizi,Miparu,Mbangamao,Mahilo,Litembo,Kiamili,n.k zinahostel lakini zinamapungufu makubwa sana, kama vile miundombinu mibovu ya vyoo,baadhi ya wanafunzi kuweka magodoro kwenye sakafu,upungufu wa vitanda,wanafunzi kujipikia wenyewe,ukosefu wa matrons,ukosefu wa ulinzi madhubuti.

Vilevile shule ya sekondari Ndela inatumia majengo ya kilimo kama hostel kwa wanafunzi ambapo majengo haya hayana hadhi ya kuwa hostel, wanafunzi wanalala sakafuni, wanajipikia wenyewe,hawana muangalizi( matron),wala mlinzi.

Baadhi ya wanafunzi kwenye shule hizi wanasema wanakumbana na changamoto nyingi sana ambazo zinapelekea hata kunusurika kubakwa nyakati za usiku wakiwa wenyewe tu,walimu wa kike ambao wameteuliwa kuwa walimu wa mabweni wanaishi mbali na hostel za shule.n.k Vilevile wakuu wa shule wamegeuza hostel hizi kama mtaji kwao kwa kuanzisha michango ambayo baadhi ya wazazi imekuwa ni mzigo kwao.

Mamlaka husika za elimu wilaya ya Mbinga zimekuwa hazifuatiliii kabisa yanayoendelea mashuleni badala yake wanasubiri mpaka DC afanye ziara ......
 
Wanalala shuleni ili kuhakikisha kunakuwepo na ufaulu mzuri Kwa Wanafunzi [mkakati wa Shule].
Mkiwafukuza Wanafunzi msije kuwalaumu walimu Kwa sababu ya matokeo mabaya ya Wanafunzi.
 
Mbna huu utaratibu wa madarasa ya mtihani kukaa hostel shuleni umeanza mda na ulitoa matokeo chanya.

Suluhisho sio kuvunja, ni kutafuta walinzi, wapishi na matrons.
 
Baadhi ya shule za sekondari wilaya Mbinga zimeanzisha hostel bubu ambazo hazifai kwa matumizi ya wanafunzi hususan wa kike hasa madarasa ya mitihani na hata zile shule zenye hostel za wasichana hazina hadhi ya kuwa hostel.

Baadhi ya shule kama vile Kikolo, Mkwaya,Dr.Shein,Mkoha,Matiri zimegeuza madarasa kuwa hostel ambapo wanafunzi wanalala katika sakafu, wanafunzi wanajipikia wenyewe,hawana muangalizi( matron) n k.

Kwenye shule za sekondari za Ngwilizi,Miparu,Mbangamao,Mahilo,Litembo,Kiamili,n.k zinahostel lakini zinamapungufu makubwa sana, kama vile miundombinu mibovu ya vyoo,baadhi ya wanafunzi kuweka magodoro kwenye sakafu,upungufu wa vitanda,wanafunzi kujipikia wenyewe,ukosefu wa matrons,ukosefu wa ulinzi madhubuti.

Vilevile shule ya sekondari Ndela inatumia majengo ya kilimo kama hostel kwa wanafunzi ambapo majengo haya hayana hadhi ya kuwa hostel, wanafunzi wanalala sakafuni, wanajipikia wenyewe,hawana muangalizi( matron),wala mlinzi.

Baadhi ya wanafunzi kwenye shule hizi wanasema wanakumbana na changamoto nyingi sana ambazo zinapelekea hata kunusurika kubakwa nyakati za usiku wakiwa wenyewe tu,walimu wa kike ambao wameteuliwa kuwa walimu wa mabweni wanaishi mbali na hostel za shule.n.k Vilevile wakuu wa shule wamegeuza hostel hizi kama mtaji kwao kwa kuanzisha michango ambayo baadhi ya wazazi imekuwa ni mzigo kwao.

Mamlaka husika za elimu wilaya ya Mbinga zimekuwa hazifuatiliii kabisa yanayoendelea mashuleni badala yake wanasubiri mpaka DC afanye ziara ......
Acha upumbavu, ishinikize serikali ijenge mabweni.
 
Si huwa wanafanya huu utaratibu kipindi mtihani ukikaribia mbona mapema hivi?
 
Wanalala shuleni ili kuhakikisha kunakuwepo na ufaulu mzuri Kwa Wanafunzi [mkakati wa Shule].
Mkiwafukuza Wanafunzi msije kuwalaumu walimu Kwa sababu ya matokeo mabaya ya Wanafunzi.
Kwa hiyo ufaulu mzuri ni kukaa na watoto kwenye mazingira ya hovyo.
Mpeleke mwanao basi..
 
Back
Top Bottom