DC Gondwe unazuiaje mkutano mkuu wa msikiti wakati Katiba yao imekiukwa mwaka wa pili sasa?

Shujaa Mwendazake

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
3,734
6,292
Naelekeza hili swali kama nilivyotumiwa kwa Mkuu mpya wa wilaya ya Kinondoni, Ndg Godwin Gondwe.

Waumini wa msikiti wa Kisumu, Magomeni mikumi wana mgogoro wa kikatiba kuwa Mkutano mkuu haujafanyika kwa miaka miwili sasa.
Hivi karibuni kupitia michango na jitihada zao wamejenga jengo la ghorofa kadhaa na limekamilika kwa upangishaji. Kuna mwekezaji kutoka Uturuki ameamua kupangisha eneo hilo kwa ajili ya matumizi ya shule, lakini kuna mashaka kuwa sehemu ya viongozi waliomleta wana maslahi napo.

Katiba ya msikiti wao ambao inatamka kuwa ni lazima mkutano mkuu ujiridhishe na ndipo kupitia baraza la wadhamini upangishwaji huo ufanyike. Hili suala linashangaza kwani mwanzo wakati mkutano unakaribia OCD alifuatwa na kulishwa matango pori na viongozi wachache akauzuia bila kuja kusikiliza waumini wenyewe, Viongozi wa Bakwata walishauri mkutano mkuu ni takwa la kikatiba hivyo unapaswa kufanyika kila mwaka. wakakubaliana na uongozi na waumini kuwa ufanyike tarehe 27/6/2021 siku ya Jpili.

Lakini katika hali ya kushangaza inasemekana sehemu ya viongozi wanaohangaika na hiyo dili walikuja ofisini kwako na kuwalisha matango pori kuwa kutakuwa na uvunjifu wa amani na ofisi yako bila kutafiti ikaamua kuuzuia mkutano huo tena kwa barua baada ya wao kutuma watu au kwenda kusikiliza waumini wana tatizo gani.

Baada ya uchunguzi mwingine imeonekana kuwa hawa viongozi wachache wanahofia mkutano mkuu utawaondoa na baadhi yao kutokana na kashfa za kusigina katiba yao lakini pia wanataka kwanza upangishaji ufanyike wafanye yao then kama mengine yatokee kwani ofa ya mturuki huyo ni Tshs 6 milioni kwa mwezi. Tayari kuna uthibitisho wa hilo kwani imeonekana katibu wa msikiti huo akimshinikiza Mwenyekiti waendelee na dili hilo bila kuhusisha waumini. Swali ni je, kipi kitaleta uvunjifu wa amani hapo?

Nimeleta hii katika jukwaa hili kwani inaonekana Katibu wa msikiti ambaye pia ni M.kiti wa S.Mtaa ulipo msikiti huu na kwa kutumia nafasi yake ya uenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya mtaa na uhusiano wake wa karibu na viongozi wa kichama na kisiasa ngazi ya kata na wilaya kuwa ndiye anayemastermind harakati zote hziz pamoja na kulisha viongozi wengine matango pori ikiwemo ofisi yako akiamini pia kuwa mkutano mkuu unaweza kumuondoa kwenye nafasi yake kwa sababu ya tuhuma mbalimbali za kifedha na kikatiba.

Nimeshangaa sana kwani nakujua Mh Gondwe ni mtu wa kwenda Field kujiridhisha, imekuwaje ktk hili umekurupuka na kuminya haki ya waumini kikatiba kwa sababu zisizo sahihi. Kumbuka msikiti si jukwaa la siasa bali ni sehemu ya ibada na mambo kama haya ya kuleta siasa ni kunajisi dini ya wenzetu wahusika.

Imani kwetu ni kuwa kupitia jukwaa hili utaupata ujumbe huu na wewe kwenda field kuwasikiliza waumin au pande zote na kufanya maamuzi yanayozingatia natural justice ktk suala hili.
 
Naelekeza hili swali kama nilivyotumiwa kwa Mkuu mpya wa wilaya ya Kinondoni, Ndg Godwin Gondwe
Ustaadhi hebu tulia kwanza ondoa jazba kisha ukae kitako uandike taarifa yako kwa aya.

Imani kwetu ni kuwa kupitia jukwaa hili utaupata ujumbe huu na wewe kwenda field kuwasikiliza waumin au pande zote na kufanya maamuzi yanayozingatia natural justice ktk suala hili .
Halafu nikushauri kitu ustaadhi. DC hawezi kufanyia kazi Mambo yaliyoandikwa jamhuri ya Twitter. Tafuta wawakilishi waende wakawasilishe malalamiko yenu ofini kwa DC.

Taqbir
 
Katiba ya msikiti wao ambao inatamka kuwa ni lazima mkutano mkuu ujiridhishe na ndipo kupitia baraza la wadhamini upangishwaji huo ufanyike
Hii katiba yenu ni ngumu kitekelezeka, mkutano mkuu ni mkutano ambao ni mgumu kupitisha maamuzi.
 
Tatizo ni kuamua kugeuza nyumba ya ibada kuwa eneo la biashara
 
Sasa mnaenda kupitisha nini wakati hata elimu dunia hamna..ndio mana mnaomba tende tani na matani mnashindwa kuomba hata kompyta tesktop mpate kuondoa ujinga..acheni kumsumbua dc ana mambo mengi ya kuwasaidi wana kinondoni.



#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naelekeza hili swali kama nilivyotumiwa kwa Mkuu mpya wa wilaya ya Kinondoni, Ndg Godwin Gondwe.

Waumini wa msikiti wa Kisumu, Magomeni mikumi wana mgogoro wa kikatiba kuwa Mkutano mkuu haujafanyika kwa miaka miwili sasa.
Hivi karibuni kupitia michango na jitihada zao wamejenga jengo la ghorofa kadhaa na limekamilika kwa upangishaji. Kuna mwekezaji kutoka Uturuki ameamua kupangisha eneo hilo kwa ajili ya matumizi ya shule, lakini kuna mashaka kuwa sehemu ya viongozi waliomleta wana maslahi napo.

Katiba ya msikiti wao ambao inatamka kuwa ni lazima mkutano mkuu ujiridhishe na ndipo kupitia baraza la wadhamini upangishwaji huo ufanyike. Hili suala linashangaza kwani mwanzo wakati mkutano unakaribia OCD alifuatwa na kulishwa matango pori na viongozi wachache akauzuia bila kuja kusikiliza waumini wenyewe, Viongozi wa Bakwata walishauri mkutano mkuu ni takwa la kikatiba hivyo unapaswa kufanyika kila mwaka. wakakubaliana na uongozi na waumini kuwa ufanyike tarehe 27/6/2021 siku ya Jpili.

Lakini katika hali ya kushangaza inasemekana sehemu ya viongozi wanaohangaika na hiyo dili walikuja ofisini kwako na kuwalisha matango pori kuwa kutakuwa na uvunjifu wa amani na ofisi yako bila kutafiti ikaamua kuuzuia mkutano huo tena kwa barua baada ya wao kutuma watu au kwenda kusikiliza waumini wana tatizo gani.

Baada ya uchunguzi mwingine imeonekana kuwa hawa viongozi wachache wanahofia mkutano mkuu utawaondoa na baadhi yao kutokana na kashfa za kusigina katiba yao lakini pia wanataka kwanza upangishaji ufanyike wafanye yao then kama mengine yatokee kwani ofa ya mturuki huyo ni Tshs 6 milioni kwa mwezi. Tayari kuna uthibitisho wa hilo kwani imeonekana katibu wa msikiti huo akimshinikiza Mwenyekiti waendelee na dili hilo bila kuhusisha waumini. Swali ni je, kipi kitaleta uvunjifu wa amani hapo?

Nimeleta hii katika jukwaa hili kwani inaonekana Katibu wa msikiti ambaye pia ni M.kiti wa S.Mtaa ulipo msikiti huu na kwa kutumia nafasi yake ya uenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya mtaa na uhusiano wake wa karibu na viongozi wa kichama na kisiasa ngazi ya kata na wilaya kuwa ndiye anayemastermind harakati zote hziz pamoja na kulisha viongozi wengine matango pori ikiwemo ofisi yako akiamini pia kuwa mkutano mkuu unaweza kumuondoa kwenye nafasi yake kwa sababu ya tuhuma mbalimbali za kifedha na kikatiba.

Nimeshangaa sana kwani nakujua Mh Gondwe ni mtu wa kwenda Field kujiridhisha, imekuwaje ktk hili umekurupuka na kuminya haki ya waumini kikatiba kwa sababu zisizo sahihi. Kumbuka msikiti si jukwaa la siasa bali ni sehemu ya ibada na mambo kama haya ya kuleta siasa ni kunajisi dini ya wenzetu wahusika.

Imani kwetu ni kuwa kupitia jukwaa hili utaupata ujumbe huu na wewe kwenda field kuwasikiliza waumin au pande zote na kufanya maamuzi yanayozingatia natural justice ktk suala hili.
Hamkawii kutiana ngeu ninyi.
 
Sajili lain yako ya uwakala kwa MAJINA yako
Tgo pesa 120000/
Airtelmoney 60000/
Halopesa 25000/
M-pesa 145000/
M lipa 50000/
Malipo baada ya kazi
 
Ustaadhi hebu tulia kwanza ondoa jazba kisha ukae kitako uandike taarifa yako kwa aya.


Halafu nikushauri kitu ustaadhi. DC hawezi kufanyia kazi Mambo yaliyoandikwa jamhuri ya Twitter. Tafuta wawakilishi waende wakawasilishe malalamiko yenu ofini kwa DC.

Taqbir
Ushauri mzuri sana huu, ili kuepusha masikhala ya vijana wa kileo hapa, fuata huu ushauri na kisha uufanyie kazi na ufute huu uzi hapa kuepuka ujinga wa vijana baadhi wenye kupenda matukano bila kushauri
 
Sasa mnaenda kupitisha nini wakati hata elimu dunia hamna..ndio mana mnaomba tende tani na matani mnashindwa kuomba hata kompyta tesktop mpate kuondoa ujinga..acheni kumsumbua dc ana mambo mengi ya kuwasaidi wana kinondoni.



#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
Ungeujua uislam na waislam usingesema hivyo, endelea kuropoka maana uwezo wako wa kufikiri umeishia hapo
 
Kuna wanajamvi wanaoamini kuwa viongozi hawapiti humu. Si sahihi, JF inasomwa sana na na watu wa Intelijensia na viongozi
 
Back
Top Bottom