ndugu mwananchi je uko mkoa gani ulikopata hiyo kadhia? kwa upande wa dawasco wasoma mita wetu wanavaa shati la blue au jeupe na huwa na vitambulisho vya kazi au permit job kwa wale vibarua. tafadhali wakati mwingine usisite kuwasiliana nasi kupitia huduma kwa wateja dawasco 0800110064 kama una mashaka na msoma mita wako.Habari za mida hii wanajamvi.
Bila kuwachelewesha niende kwenye mada. Hawa vijana wanaosoma mita kwakweli Mimi binafsi wananichanganya mana juzi nilipata dharura kidogo nikawa nimerudi kwangu mapema, in fact nilirudi baada Tu ya kufika kazini, lakini cha kushangaza mida ya SAA 7 mchana alikuja kijana aliyejitambulisha kama amekuja kusoma mita, Mimi nilikua ndani lakini mke wangu aliyemfungulia aliwahi ndani kuniambia hebu njoo umuone huyu anayedai in msoma mita mbona kama hafananii.
Nilipotoka kwenda kumuona nilielewa mke wangu alichokua anasema maana alikua amevaa jeans na T-shirt na smart phone Tu ndio anatumia, sasa nikashangaa Hamna uniform, Hanna kitambulisho, Hanna chochote, halafu ukiangalia midomo yake niliona ni mtumiaji wa mihadarati maana mdomo umeungua, sasa Mimi sikutaka kuanzisha kitu halafu ikawa tofauti, nikammark halafu akaenda.
Hivi ndivyo wanavyokuwa hawa wasoma mita au huyu wa kesi yangu hakuwa mtu wa idara ya maji kweli
Inabidi idara ya maji wafanye mchakato wa kufanya vijana wao wafahamike vizuri maana Mimi ngeweza kumfungulia mbwa halafu ikaja kuwa kesi
Kula tano mkuu, yale yale ya kufanya kazi kwa mazoea, sidhani toka lianzishwe hili shirika kama limewapa serikali faida! Ni hasara mwanzo mwisho, yote sababu hata wakipata hasara mishahara iko pale pale, lianze kuendeshwa kifaida, watu sales wakae ki commission, hakuna sales, hakuna malipo, wakipata hasara ile kwenye mishahara yao na retrenchment juu, utaona watakavyopiga kazi..Dawasco sio wabunifu kabisa, eti wana afisa biashara, sijui hata kazi yake ni nn wakati kuna nyumba nyingi tuu wangeweza kutuunganishia maji wapate mapato makubwa. Hili shirika sijui kama lina viongozi wasomi, maeneo ya hapa mbezi beach jogoo juu mpaka kinzudi kuelekea goba ni hela ngapi wangepata? Eti tunamtua mwanamke ndoo kichwani, uongo mtupu! Wake up!
Nimetoa maombi/maoni yangu haya tangu tarehe 23/06/17 kuhusu maji Makoka lakini mpaka leo majibu hola. Mtumishi wa DAWASCO anayejibu hoja/maombi anaonekeana anaingia hapa kwenye huu uzi na kutoka lakini hajibu hoja sijui ni kwa nini. Hii inapoteza umuhimu wa uzi. Nafikiri ni muda muafaka sasa kama alivyosema mchangiaji hapo juu kuwa serikali iondoe ruzuku kwenye mashirika kama DAWASCO, NHC, TANESCO, ATCL ili yajiendeshe kibiashara bila kutegemea serikali ndipo wafanyakazi walau watachangamka. Kwa jinsi ilivyo sasa watu wanajua mishahara ipo tu hawawezi kufanya kazi kwa ufanisi.Maji na umeme vikiunganishwa kwa watu wengi zaidi wananchi watalipia hivyo zitapatikana pesa za kuendesha haya mashirika.SISI MAKOKA KISUKURU KWA MKUWA MNATUFIKIRIAJE MAANA TUMEACHWA KAMA KISIWA VILE. MAJI YALIYOTOKEA MAKOKA MWISHO YAMEISHIA KWA KISANGA. MAJI YALIYOTOKA MAJI CHUMVI YAMEISHIA SHULE YA MOUNT ZION YAKAELEKEA JUMBA LA DHAHABU. SISI TULIOBAKI HAPO KATIKATI KWANZA TUPO TAYARI KULIPIA KUUNGANISHIWA BILA HATA YA MKOPO. TUMESHALIPA NA RISITI TUNAZO TOKA MWAKA JANA MWISHONI. SURVEYOR AMESHAPITA MARA KIBAO HAKUNA CHA MAANA. TUMESHAEENDA KWA MENEJA WA TABATA MARA KIBAO LAKINI HAKUNA JIBU LOLOTE LA MAANA. KWA HIYO TUNAOMBA MUKURUGENZI WA DAWASCO ENGINEER LUHEMEJA KAMA YUPO JAMII FORUMS AFIKE MAKOKA KWA MKUWA LABDA TUTAPATA MAJI.
Kwakweli ninyi ni jipu mnastahili kuvunjwa kwa kugeuza maji kuwa ni kitegauchumi na sio necessity kwasababu mmepsndisha bei mara dufu na kuyafaya maji kuwa ni ghali mno, sijui hivyo vigezo vya bei mnavitoa wapi, mdhibiti nae amekuwa mfu asie na memo. Hamkustahili kuyageuza maji kuwa dhahabu. Hivi hii nchi ingekua jangwa ingekuaje? Na hapo ni watanzania wasiozidi asilimia 20 tu ndio wanatumia maji ya bomba, vipi watakapofikia asilimia 95 kama misri.??Ndugu wana JamiiForums,
Tunashukuru kwa maoni yenu mliyoweka hapa juu ya huduma mnazo pata kwenye matawi yetu yaliyo Jijini Dar es salaam , miji ya Kibaha na Bagamoyo Mkoani pwani. DAWASCO inapokea maoni na malalamiko yenu na tuna wahakikishia kuwa tutachukua hatua stahiki kwa haraka zaidi.
Ndugu wana jukwaa, DAWASCO inajipambanua kwa kusimamia maadili ,kutoa huduma iliyotukuka pamoja na kuhakikisha huduma ya Maji inapatikana kwa kila mwananchi.
Kama kutatokea kuharibika kwa bomba, wizi wa Maji, umepata huduma isiyo ridhisha au ufanyaji kazi usiofuata maadili, uaminifu na uadilifu, tafadhali toa taarifa kupitia njia zifuatazo:
1. Kupitia tovuti: DAWASCO - Welcome to new site
2. Kupitia mitandao yetu ya kijamii ikiwa ni pamoja na Twitter|DawascoOfficial..Facebook|DawascoOfficial ...Instagram|DawascoOfficial
3. Kwa mwananchiposta ; Unaweza kutuma barua kwa Afisa Mtendaji kama ifuatavyo:
Afisa Mtendaji Mkuu
DAWASCO
P. O. Box 5340
Sokoine Drive
Dar es Salaam, Tanzania.
4. Au kwa kupiga simu huduma kwa wateja dawasco
0800110064 /022 2164800 ( Kupiga namba hizi ni Bure)