dah maisha ya boarding raha sana wadau! Kuna jamaa yeye alikuwa hana bakuli la uji wala sahani, anachofanya akitoka likizo anakuja na ma trunker km matatu hivi, moja la ngun jingine kuna mazagazaga ya breakfast kajaza sugar ten kilos, blueband kubwa km nne hivi, jam, roiko mchuzi mix za kumwaga.
Jingine kajaza samaki flani hivi ni tilapia aka perege hawa wa kawaida lkn kwa sababu wanatoka bwawa la Nguruka Kigoma wakihifadhiwa kwa chumvi nyingi baada ya kukaangwa na mafuta ya mawese, kwa ufupi wanaitwa nguruka, mchizi anajaza trunker lote. Anachofanya yeye wakati wa uji saa nne anatoka na blue band yake na sukari kidogo sana, akiingia mesini watu wanamgombeaje! Anapewa bakuri la uji yeye anawapa sugar kidogo na blueband ya kudabia wengine mliomkosa mnaendelea na uji Sumu wenu kimyamkimya.
Mchana wakati wa makana yaani ugali dagaa mchizi anaibuka na nguruka wake mmoja, hana sahani hapo wala hapangi foleni ya msosi watu wakisikia tu harufu ya nguruka, ugomvi wanamgombea jamaa.
Nilienda na ka kikombe ka chai form one jamaa wa form two walipokiona wakaniuliza kakikombe ka nini niliposema chai jamaa alicheka akasema chai ni dawa ya kutolea mimba kwa hiyo hairuhusiwi kunywewa pale shule km nna pakti lake nimpe akatupe kwa uwoga nikampa, usiku saa tatu natoka kuoga nikawafuma jamaa angle moja bwenini wanachemsha chai kwenye ndoo zile za bati kwa kutumia zile heater za coil pembeni lile boksi langu la green label limeshafunguliwa hahaa jamaa kuniona akakauka kimya. Kesho yake akaja kunipa bakuli kubwa km yale wanayonawishia maji kwenye vitimotoz eti ananikopesha wakati ule eti kila siku ntampa shs hamsini dah boarding si lelemamaa