LHRC yafungua kesi ya kikatiba kupinga adhabu ya viboko shuleni kufuatia kifo cha mwanafunzi Simiyu

LHRC yafungua kesi ya kikatiba kupinga adhabu ya viboko shuleni kufuatia kifo cha mwanafunzi Simiyu

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,934
Reaction score
16,573
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimeunga mkono na kufungua kesi ya kikatiba katika Mahakama Kuu ya Tanzania (Kanda Kuu Dodoma) kupinga uhalali wa matumizi ya adhabu ya viboko shuleni. Kesi hii imewasilishwa kwa niaba ya Samwel Maduhu Mangu, mlezi wa marehemu Mhoja Wilson Maduhu, mwanafunzi wa Kidato cha Pili katika Shule ya Sekondari Mwasamba mkoani Simiyu. LHRC inamwakilisha mlalamikaji kama sehemu ya jitihada zake endelevu za kulinda haki za watoto na kuhakikisha mazingira ya kujifunzia yanakuwa salama na yenye heshima.

Kesi hii inapinga Kanuni ya 2, 3 na 6 za Kanuni za Elimu (Adhabu ya Viboko), GN. Na. 294 ya 2002, kwa hoja kwamba zinakiuka Katiba hususan haki ya heshima na utu, haki ya kusikilizwa, na haki ya kuwa huru dhidi ya mateso au adhabu au matendo ya kikatili au ya kudhalilisha. Shauri hili linatokana na tukio la kusikitisha ambapo Mhoja na wenzake waliadhibiwa kwa kutokamilisha kazi ya somo la Jiografia kinyume na maelekezo ya walimu. Mhoja alipigwa mara kadhaa kwa fimbo, zikiwemo viboko viwili kichwani alipokuwa akijaribu kujikinga. Alianguka chini, hali yake ikazidi kuwa mbaya, na licha ya kulia kwa maumivu, mwalimu aliendelea kumsukuma kichwani ili amnyamazishe. Alikimbizwa hospitalini lakini alifariki dunia. Ripoti ya uchunguzi wa mwili ilionyesha kuwa alikufa kutokana na kutokwa na damu ndani ya fuvu la kichwa baada ya kupigwa na kitu butu.

Mwalimu aliyempiga marehemu alifikishwa Mahakamani kwa kosa la kuua bila kukusudia katika Shauri la Jinai Na. 16680 la mwaka 2025 (Mahakama Kuu - Kanda Ndogo ya Shinyanga), ambapo alikiri kosa na kuhukumiwa adhabu ya kutotenda kosa lolote ndani ya kipindi cha miezi 12.

Kesi ya kikatiba imepewa namba Shauri Na. 32373 la 2025, na imepangiwa kusikilizwa na Majaji Mruma, Hassan na Musokwa. Kesi imepangwa kutajwa tarehe 16 Machi 2026 saa 3:00 asubuhi. LHRC itaendelea kufuatilia shauri hili kwa karibu, kuhakikisha haki inapatikana kwa Mhoja na kuendeleza msukumo wa mageuzi ya kisheria yanayolinda watoto dhidi ya adhabu za kikatili na za kudhalilisha shuleni.

Soma

SnapInsta.to_617120800_18402243160133657_5981706513625596969_n.jpg
 
Nimejifunza kuwa wazazi na walezi wakifikia kutoa kinacjoitwa adhabu kuna vitu hawafikiri.
1. Lengo la adhabu unayotaka kutoa ni kupunguza hasira au kufundisha?

2. Adhabu ninayotoa inalingana na kosa na kuwa inatolewa kwa kufuata kanuni na sheria?

Ukiyabaini haya, utafikiri mara mbili kati ya adhabu na nidhamu.
 
Ningewaelewa Sana kama wangefungua KESI kupinga matumizi ya RISASI kwa Askari polisi, maana wameshudia mamia ya raia wakiuawa kwa mtutu wa bunduki, Oct, 29!
 
Hadi leo tunatumia viboko kama adhabu aisee! Hakuna tafiti zenye suluhu mpya?
 
Mimi bila mboko nisingefika hapa...

Hivi hawa watu wa haki za kibinadamu wanachaguaga kipi wakilalamikie na kipi wasikilalamikie?
Zipo njia nyingi za kumuadhibu mtoto bila kutumia fimbo. Kwa mfano, unaweza kumpa kazi ya kusafisha mazingira ya shule wakati wenzake wamepumzika. Adhabu kama hii sio tu inarekebisha tabia lakini pia inanufaisha school community.
 
Zipo njia nyingi za kumuadhibu mtoto bila kutumia fimbo. Kwa mfano, unaweza kumpa kazi ya kusafisha mazingira ya shule wakati wenzake wamepumzika. Adhabu kama hii sio tu inarekebisha tabia lakini pia inanufaisha school community.
Africa bado hamjafikia hatua hii... Mtoto wa kiswahili, vyake viboko.

Ningekuelewa kama ungesema uchapaji ulenge kumrekebisha mtoto na sio kumkomoa.

Walimu wengine humalizia hasira zao kutoka nyumbani kwa watoto wa wengine.
 
Me kuna mwalimu alinichapa fimbo za mkononi kisa sijamaliza kuandika Notes na wakati ananichapa utazani anauwa nyoka....notes zenyewe hata haieleweki aliandikia ubao gani ila wao kazi yao nikwambia nendeni mkachukue Nots Darasa fulani unaenda nao wanakwambia hawajamaliza...anyway walimu wa Shule za Kata wanamatatizo pia wanavisasi vya ajabu sana hawa maskini wenzetu...alijisema Dr Slaa kwamba tunakoelekea haya mashule ya Kata yatakufa kisha majengo tutafugie Kuku.
 
Africa bado hamjafikia hatua hii... Mtoto wa kiswahili, vyake viboko.

Ningekuelewa kama ungesema uchapaji ulenge kumrekebisha mtoto na sio kumkomoa.

Walimu wengine humalizia hasira zao kutoka nyumbani kwa watoto wa wengine.
That’s too subjective. Atakayeamua kwamba huu ni uchapaji wa kumrekebisha mtoto na sio kumkomoa ni nani?
 
Back
Top Bottom