David Kafulila akamatwa na Polisi

David Kafulila akamatwa na Polisi

Ccm kumkamata kafulila hakutasaidia kitu.
Serikali ya ccm ni sawa na jitu lililotolewa macho linapapasa kila sehemu halijui linapokwenda.
 
HIVI ccm bado wananguvu hata ya kudai mchango??? ama kweli zimwi ni zimwi hata llizeeke vipi
 
Huko hakuna kinga Bunge
Ni kweli hakuna kinga,
Ila burden ya kuonyesha ni sheria ipi inatumika kukusanya elfu mbili za maabara itawanyima fursa ccm na wezi kufikia lengo kwenye kesi mbuzi wanayomtengenezea kafulila
 
Mbona Hawajamkamata Singa singa na badala yake wamkamate Kafulila kama kweli wana nia ya dhati kuhakikisha watu wanaokwamisha maendeleo ya nchi hii wakamatwe na wahojiwe. Polisi wetu hawa akili zao zimeenda likizo tena zimepumzika kwa kuwekwa kwenye kopo kwa kupokea maelekezo ambayo hayana msingi. Unapomkamata Mbunge anayetetea maendeleo ya watanzania tena kwa kusimama kidete kudai pesa za watanzania zirudishwe.

Kati ya singasinga na kafulila nani anayekwamisha serikali ikashindwa kujenga maabara

Ukawa ikikamata madaraka kwanza wasafishe huu uwoza wa ccm ndani ya jeshi la police, usalama, jwtz.

Huku tukiwa na katiba ya wananchi iliyo zingatia mahitaji ya wananchi, na uhuru kwa kila mtu mmoja mmoja. Vyombo vyote vya dola viwe huru kabisa.
 
Hakuna shurti yoyote ya mchango labda iwe kodi...

Hao polisi watakuwa wanatekeleza amri ya mkubwa fulani tu....
 
Tundu Lissu siku nyingi kazuia michango ya kipuuzi jimboni kwake sijasikia wakimkamata,kifo kimewajia maccm,majizi wakubwa
 
Magaidi ndani ya chama cha wahuni na mafisadi wameshatafuta namna ya kumbambikia kesi Kafulila.
 
Wenzenu Kilimanjaro walishachangia maendeleo hadi basi.Sasa hivi wana mashule mazuri na maendeleo kibao sekta za jamii.

Nyie wa kigoma na vumbi na viroboto kwenye miguu mko nyuma kimaendeleo mnahamasishana msichangie maendeleo mtajijua.Wenzenu walishamaliza kuchangia kwenye mikoa yao kama kilimanjaro sasa hivi ni kula kuku na kupiga siasa za bla bla kwenye majukwaa nyumbani kuko vizuri hamna nyumba iliyoezekwa kwa nyasi kama kigoma.

Acheni kuchangia maendeleo mtabaki watumwa wa watu wa kilimanjaro hadi mfe kwa ulofa.

sasa huko kilimanjaro walipokuwa wanachangia walikuwa wanapelekwa polisi
 
Ní kwa kushawishi wananchi wasichangie michango ya maendeleo Uvinza,Kigoma. Anashikiliwa kituo cha Polisi kwa mahojiano.

Chanzo: Jamaa aliye Kígoma

Kafulila achunge anaweza kupakwa ile simu ya polonium mnnae itajataja humu jamvini. Ila nacho amini siku zote ukweli uko juu kabisa kupitia uovu!
 
Wenzenu Kilimanjaro walishachangia maendeleo hadi basi.Sasa hivi wana mashule mazuri na maendeleo kibao sekta za jamii.

Nyie wa kigoma na vumbi na viroboto kwenye miguu mko nyuma kimaendeleo mnahamasishana msichangie maendeleo mtajijua.Wenzenu walishamaliza kuchangia kwenye mikoa yao kama kilimanjaro sasa hivi ni kula kuku na kupiga siasa za bla bla kwenye majukwaa nyumbani kuko vizuri hamna nyumba iliyoezekwa kwa nyasi kama kigoma.

Acheni kuchangia maendeleo mtabaki watumwa wa watu wa kilimanjaro hadi mfe kwa ulofa.

Mkuu...kwanini muuza nguruka achangie ikiwa SINGA SINGA anaiba pesa kwa kishirikiana nawatawala...!
 
aliwashikia mtutu au aliwashawishi mana hata mchango wa harusi kuna wanaoshawishi mtu achangiwe wengine asichangiwe ssa kila mtu anapima achangie nini wapi mfano mwenye uwezo badala ya kuchangia maabara anajenga mabeni nk
 
Michango ni jambo lingine na Escrow ni habari ingine acha akamatwe tuu amegeuza huo mtaji wa kisiasa

ki ukweli hujui A wala B unaonesha wewe ni sahbiki mbumbumbu tu kama wenzio wa sampuli yako, ndio maana mnafaa kwa matumizi ya ccm,
 
mimi sitachangia hata bila ya kushawishiwa na kina Kafulila

waibe KODI halafu nijenge zahanati kwa pesa yangu.NO
 
Back
Top Bottom