David Kafulila akamatwa na Polisi

David Kafulila akamatwa na Polisi

Mkuu,nikiri kwanza kuwa mimi ni Wakili ingawa sijui kama ni mzuri au la. Mkuu,masuala la kijamii huongozwa na sheria. Zaweza kuwa Sheria zitungwazo na Bunge au zile ndogondogo. Masuala haya hayapaswi kuendeshwa kwa kauli za viongozi.

Kimsingi,serikali ina wajibu wa kujenga miundombinu mbalimbali kwa wananchi. Kisheria,mwananchi hana wajibu wa kujenga miundombinu kwa njia ya kuchanga. Sababu ni kuwa mwananchi si mkusanya kodi,mtunza fedha na mpanga mipango.

Hatahivyo wananchi wanaweza kuridhia kuchanga michango mbalimbali. Si kwa njia ya kushurutishwa. Wanapaswa kushawishiwa na kuombwa kuchanga.

Asante Mkuu
Siyo mtu mmoja mmoja anyeruhusiwa kuwahamasisha wanachi kutotii sheria ndogondogo huo ni uhaini
 
hivi ni haki kuchangia maendeleo wakati tunalipa kodi,vip na hii kisheria imekaa vipi mahakamani

Inategemea kama unataka maendeleo ya haraka au la kama ikiwa kodi hazitoshi.

Kigoma inabidi wachangie.Ni katika mikoa inayonyonya sana mikoa mingine.Nenda kaangalia mkoa mzima wa kigoma unachangia kodi zote shilingi ngapi TRA halafu angalia huduma kama mabarabara,madaraja n.k waliyojengewa yamegharimu shilingi ngapi.Hizo zilizozidi zimetoka kwa walipa kodi wa mikoa mingine.

Iko haja ya kupitisha sheria kuwa kila mkoa utumie kodi zake tu halafu tuone kigoma watakuweje kimaendeleo.
Hapo tu wameshatunyonya vya kutosha mikoa mingine wasitupandishe hasira hawalipi kodi au kodi wanayolipa kidogo halafu halafu hata kuchangia maendeleo yao hawataki.

Hapo alipokuwa akihamasisha kafulila watu wasichangie maendeleo pana walipa kodi wangapi na wamelipa shilingi ngapi kama kodi?
 
Mbona hawajamkamata Tundu Lissu aliyegomesha wananchi wake kuchangia tangu ameingia madarakani?
 
chezea pengine,tunataka kugawana hiyo keki,siyo wengine wanawekewa milioni 800,halafu wengine tunaambiwa tuchangie maabara.David usivunjike Moyo
 
Nchi ya wajinga huku wanachabgishwa halafu wanagawana wachache.Atskae hoji anakamwatwa.ujue hata moshi haitaachwa wameibia sana nchi hii.soma unabii wa Nyerere utajua nini kinainyemelea Tz
 
Hapo alipokuwa akihamasisha kafulila watu wasichangie maendeleo pana walipa kodi wangapi na wamelipa shilingi ngapi kama kodi?
Nafikiri suala si la wananchi wa pale wanalipa kiasi gani,uzuri VAT unalipa kadri ya uwezo wako kifedha,kuwa kama matumizi yako ni makubwa basi na VAT yako itakuwa kubwa...wananchi wa kule huwezi kuwafananisha na wananchi wa Dar,Mwanza au hata Arusha,then kuna suala la viwanda kama tutaangalia uchangiaji wa kimkoa.Dar viwanda ni vingi na ni nani anatakiwa ahamasishe ili na mikoa ya pembezoni kiuchumi nayo iwe na viwanda vingi?
 
Inategemea kama unataka maendeleo ya haraka au la kama ikiwa kodi hazitoshi.

Kigoma inabidi wachangie.Ni katika mikoa inayonyonya sana mikoa mingine.Nenda kaangalia mkoa mzima wa kigoma unachangia kodi zote shilingi ngapi TRA halafu angalia huduma kama mabarabara,madaraja n.k waliyojengewa yamegharimu shilingi ngapi.Hizo zilizozidi zimetoka kwa walipa kodi wa mikoa mingine.

Iko haja ya kupitisha sheria kuwa kila mkoa utumie kodi zake tu halafu tuone kigoma watakuweje kimaendeleo.
Hapo tu wameshatunyonya vya kutosha mikoa mingine wasitupandishe hasira hawalipi kodi au kodi wanayolipa kidogo halafu halafu hata kuchangia maendeleo yao hawataki.

Hapo alipokuwa akihamasisha kafulila watu wasichangie maendeleo pana walipa kodi wangapi na wamelipa shilingi ngapi kama kodi?
Una maana ya mfumo wa majimbo?
 
.... Mimi Hata Hao Wanajeshi Waje Na Vifaru Siwezi Kuchangia Hiyo Michango Ya Mafisadi
 
.Dar viwanda ni vingi na ni nani anatakiwa ahamasishe ili na mikoa ya pembezoni kiuchumi nayo iwe na viwanda vingi?

Ni kazi ya mbunge kuhamasisha hilo .Mbunge anasafiri anakutana na wengi tu wakiwemo wawekezaji ni wajibu wake kufanya lobbying na kwa kushirikiana na madiwani na halmashauri kwenye jimbo lake kuweka sera na mazingira na vivutio watu wawekeze kwenye jimbo lake.

Mkoa wa morogoro ulipata viwanda vingi kwa sababu ya mbunge wake Amir Jamal alikuwa very active kwenye hilo.Kazi ya mbunge si kelele bungeni na kwenye mikutano ya hadhara tu! Kigoma imepata wabunge wengi tatizo wanaongea sana kwenye bunge na mikutano ya hadhara hawana mbinu za uhamasishaji upatikanaji viwanda kigoma!
 
Una maana ya mfumo wa majimbo?

Kwa jinsi tunavyonyonywa na mikoa inayochangia kodi kidogo TRA ya hawa akina Kafulila naona iko haja ya kukubaliana na sera ya majimbo ya CHADEMA ili kila mtu ale chake.Jimbo lofa kama la Kafulila libakie na ulofa wake forever sababu hela za Kodi watakazokusanya zitakuwa hazitoshi hata kulipia vikao vya madiwani au kumlipa mbunge hayo mamilioni anayolipwa Kafulila sasa.
 
Mbona wezi kama akina muhongo, singasinga, maswi, na escrow yao hawawakati, hao polisi ni wa TZ kweli no I doubt. Labda ni jiroboti tu limetumwa na mafisadi
 
Badala ya kukamatwa kina chenge anakamatwa kafulila! Duh hii nchi ilishauzwa kwa mafisadi zamani sana!
 
Inategemea kama unataka maendeleo ya haraka au la kama ikiwa kodi hazitoshi.

Kigoma inabidi wachangie.Ni katika mikoa inayonyonya sana mikoa mingine.Nenda kaangalia mkoa mzima wa kigoma unachangia kodi zote shilingi ngapi TRA halafu angalia huduma kama mabarabara,madaraja n.k waliyojengewa yamegharimu shilingi ngapi.Hizo zilizozidi zimetoka kwa walipa kodi wa mikoa mingine.

Iko haja ya kupitisha sheria kuwa kila mkoa utumie kodi zake tu halafu tuone kigoma watakuweje kimaendeleo.
Hapo tu wameshatunyonya vya kutosha mikoa mingine wasitupandishe hasira hawalipi kodi au kodi wanayolipa kidogo halafu halafu hata kuchangia maendeleo yao hawataki.

Hapo alipokuwa akihamasisha kafulila watu wasichangie maendeleo pana walipa kodi wangapi na wamelipa shilingi ngapi kama kodi?
hapo ulichoandika ni upuuzi mtupu, ina maana hapo kigoma wananchi hawalipi kodi? Yaani mafisadi waibe mabilioni halafu wananchi wanyanyaswe kwa mchango wa maabara, hilo sio sawa kamwe.
 
Back
Top Bottom