David Kafulila ahamia CHADEMA akitokea NCCR Mageuzi

David Kafulila ahamia CHADEMA akitokea NCCR Mageuzi

Tuchukukie mfano una nyumba kubwa yenye vyumba vingi (UKAWA)...
Kwanini ulale chumba kimoja miaka yote?
Kuna ubaya kuhamia chumba kingine ndani ya nyumba hiyohiyo moja?
mna tengeneza umoja usio na balance, na mkisha kuwa hivo ni bora mumshauri na Mbatia amaliziea aje CDM
Ila ni kama Kafulila kamvizia Mbatia anavo umwa ndio kahama, angesubiri apone.
 
Au tuchukulie mfano nyumbani kwako unakaa na wanawake watatu.. Mkeo, mdada wa kazi na mdogo wake mkeo!
Kuna haja gani kila siku ulale chumbani kwako tu wakati nyumba ina vyumba vingi

Weeeeeee mfano gani huu unaleta?
Like serious baby umekosa kabisa mfano mwingine wa kufanania wangu?

Thubutu yako ndio utajua kwanini ni lazima ulale chumbani kwako tu
 
Huu umoja wa kufanyiana udukuzi....yani Mbowe kamvizia Mbatia anaumwa kamfanyia udakuzi juu kwa juu,, noma sana

Mi.mwenyewe ni mewaza mbona jamaa kama wana fanya hivi wakati mzee Mbatia ni mgonjwa!!
Kibusara wangesubiri afya yake itengemae.
 
Baadae CCM watajuta kwanini wameunda mgogoro ndani ya CUF maana CUF (ya <Maalim Seif) ikihamia CHADEMA, mchezo wa bao utakuwa umeisha. Ukichanganya nguvu ya CUF ZNZ na CHADEMA Bara, utamu unakolea!
Hapo nio utakuwa mwisho wa upinzani...kutawaka moto...mafia wa kaskazini na mafia wa Pemba hapatatosha.
 
Kafulila ahama NCCR, ahamia Chadema
Dar es Saam. Mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini, (NCCR-Mageuzi) David Kafulila, amekihama chama hicho huku akieleza kuwa anajiandaa kuhamia Chadema.

Kafulila alithibitisha taarifa hizo na kusema tayari ameshawasilisha barua ya kujivua uanachama wa NCCR na kujiunga Chadema leo.

“Nimewashukuru kwa kuwa pamoja katika kujenga chama na nafasi ya uenezi waliyonipa mara zote. Nimeweka wazi kuwa natarajia kujiunga na Chadema. Nimeona kuwa kuna mahitaji ya watu wenye nia ya mabadiliko kuwa katika chama kimoja ili kufupisha safari.” alisema
View attachment 446944
SOURCE: Mwananchi
Rekebisho kidogo, David Kafulila hajahamia Chadema, bali amerejea Chadema, NCCR Mageuzi ndio alihamia na sasa amerejea nyumbani, ataisaidia sana Chadema kuziba pengo la ZZK kama ata team up na JJ. Mnyika. Kafulila is good so does JJMNYIKA na wengine wachache. Pengo la ZZK ndani ya Chadema halijazibwa so does pengo la Dr.Slaa, na Bavicha ya sasa haina big impact so does Bawacha.

Mimi kama ningekuwa mshauri wa Chadema ningemshauri Mbowe his time it's time up. Ameifanyia Chadema mengi na makubwa but amefikia optimum take. Kama night solution, it is a saturated solution, it can take no more than it can.

Chama makini kinatakiwa kuanza jana kujipanga kwa kesho, kwa uchaguzi wa 2020 hata yule jamaa yangu atakuwa ni spent force unless Chadema imeridhika kuendelea kuwa msindikizaji tuu na sio mshindani.

Hongera sana Kafulila, welcome back home kwako ulikotoka na kugeuka mwana mpotevu aliyerejea nyumbani kwa baba take.

Paskali
 
Kafulila ahama NCCR, ahamia Chadema
Dar es Saam. Mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini, (NCCR-Mageuzi) David Kafulila, amekihama chama hicho huku akieleza kuwa anajiandaa kuhamia Chadema.

Kafulila alithibitisha taarifa hizo na kusema tayari ameshawasilisha barua ya kujivua uanachama wa NCCR na kujiunga Chadema leo.

“Nimewashukuru kwa kuwa pamoja katika kujenga chama na nafasi ya uenezi waliyonipa mara zote. Nimeweka wazi kuwa natarajia kujiunga na Chadema. Nimeona kuwa kuna mahitaji ya watu wenye nia ya mabadiliko kuwa katika chama kimoja ili kufupisha safari.” alisema
View attachment 446944
SOURCE: Mwananchi
Rekebisho kidogo, David Kafulila hajahamia Chadema, bali amerejea Chadema, NCCR Mageuzi ndio alihamia na sasa amerejea nyumbani, ataisaidia sana Chadema kuziba pengo la ZZK kama ata team up na JJ. Mnyika. Kafulila is good so does JJMNYIKA na wengine wachache. Pengo la ZZK ndani ya Chadema halijazibwa so does pengo la Dr.Slaa, na Bavicha ya sasa haina big impact so does Bawacha.

Mimi kama ningekuwa mshauri wa Chadema ningemshauri Mbowe his time it's time up. Ameifanyia Chadema mengi na makubwa but amefikia optimum take. Kama night solution, it is a saturated solution, it can take no more than it can.

Chama makini kinatakiwa kuanza jana kujipanga kwa kesho, kwa uchaguzi wa 2020 hata yule jamaa yangu atakuwa ni spent force unless Chadema imeridhika kuendelea kuwa msindikizaji tuu na sio mshindani.

Hongera sana Kafulila, welcome back home kwako ulikotoka na kugeuka mwana mpotevu aliyerejea nyumbani kwa baba take.

Paskali
 
wakati huo mm nakimbia namfuata polepole coz anajua kujenga hoja
[HASHTAG]#katika[/HASHTAG] maisha usimfuate mtu maarufu coz hawezi kukushawishi uache hiki na ufuate hiki but tunashauriwa tuwafuate watu wenye ushawishi wa hoja kama polepole
 
Baadae CCM watajuta kwanini wameunda mgogoro ndani ya CUF maana CUF (ya <Maalim Seif) ikihamia CHADEMA, mchezo wa bao utakuwa umeisha. Ukichanganya nguvu ya CUF ZNZ na CHADEMA Bara, utamu unakolea!
Inatakiwa wafanye hivo

Lakini pia kama chadema wana taka umoja wangemshawishi na Mbatia ahamie au ahamishe chama chote waende kwa CDM ila si kwa kuchumoa wanachama wake.
 
Kahamia kwa mkewe si unajua mkewe ni mbunge wa viti maalumu Chadema.Mama akiwa na kazi au nyumba mwanaume Ukawa huna kazi au nyumba kuhamia kwa mke ili maisha yaendelee si kitu cha ajabu.Na kila ukiamka huko ulikohamia lazima kila asubuhi umwamkie mke Shikamoo mke wangu maana ndie anakuweka mjini.
we hushangai watu wachafu km chenge na tibaijuka ambao hawanafaida yotote kwa taifa wanapata ubunge lkn mtu wa maana km Kafurila anakosa nafasi ambaye ilitakiwa hata awe waziri mkuu? Lazima atafute atakako kutana na watz wanaojielewa na kuelewa mchango wake kwa taifa.....Eti hana kazi hujielewi ww dogo
 
Hongera sana Kafulila, welcome back home kwako ulikotoka na kugeuka mwana mpotevu aliyerejea nyumbani kwa baba take
umekaribisha nyumbani kwake? wewe ni mwenyeji wa huko?
Mimi kama ningekuwa mshauri wa Chadema ningemshauri Mbowe his time it's time up. Ameifanyia Chadema mengi na makubwa but amefikia optimum take. Kama night solution, it is a saturated solution, it can take no more than it can.
Hapa utaishia kutukanwa matusi lakini ndio ukweli.
Chama makini kinatakiwa kuanza jana kujipanga kwa kesho, kwa uchaguzi wa 2020 hata yule jamaa yangu atakuwa ni spent force unless Chadema imeridhika kuendelea kuwa msindikizaji tuu na sio mshindani
Mhh raisi wa mioyo yao? kweli?
 
Kwanini chadema inaibomoa NCCR?
Alitoka Mrema NCCR-Mageuzi haikubomoka itakuwa akitoka Kafulila? Nyie wabomoaji huwa mnadhani watu fulani fulani wakitoka vyama vya upinzani vitakufa.

Mlianza kumtoa Masumbuko Lamwai, akaja Kilonzo Mporogomnyi, mkambeba Walid Kabour, mkamchomoa Festus Limbu hamkuridhika naye mkamvuta Anna Senkoro huyo naye hakutosha akaja Stephen Wasira, mkawazoa kina Shonza na wenzake mkaunda CCJ ilipowatisha mkaiua mkaileta CCK ambayo wala hamna habari nayo, mkaunda uhasama ndani ya CHADEMA kwa misingi ya Udini na Ukanda mkampa hela "Kiongozi Mkuu" akaanzishe chama na baadaye kidogo mkampa wazimu Dr. Slaa atoke ili CHADEMA ife lakini hamkufanikiwa!! Naye Lipumba hata kumuongelea kwenye vikao vyenu vya kahawa pale Lumumba mmeshaacha!

Kama nyie kwa kutumia nguvu zenu zote pamoja na zile za kuazima toka kwenye dola mmeshindwa kuviua vyama vya upinzani ndiyo NCCR-Mageuzi itakufa kwa kutoka kwa Kafulila na kujinga na chama rafiki CHADEMA?
 
Kila Mtu Anakimbilia CHADEMA,Very Nice!Mwisho wa Siku Tuwe na Vyama Viwili Vikubwa!
 
Back
Top Bottom