David Kafulila ahamia CHADEMA akitokea NCCR Mageuzi

David Kafulila ahamia CHADEMA akitokea NCCR Mageuzi

HONGERA MAMA DAVID KAFULILA (Mhe. Jesca Kishoa mb)

Inawezekana kabisaa pasipo shaka Mhe. David Kafulila ukawa umeshawishiwa na Mkeo kuhamia Chadema chama chetu cha zamani ambacho mkeo ni mbunge wake. Kama ndivyo basi napenda kutumia fursa hii kumpongeza Mkeo Mhe Jesca Kishoa Mbunge kwa kukuweka mtu kati hadi ukaamua kurejea mahala ambapo kwa miaka mingi tangu 2009 ukisema sana kwa nyakati tofauti kwamba CDM hawaaminiki, hawafai na hawana shukrani. Pole na hongera kwa uamuzi huo. Vilevile hongereni sana akina mama kwani kupitia Mhe Jesca Kishoa imedhihirika kwamba mna nguvu hadi Mhe David Kafulila Kasarenda misimamo yake. Hongereni sana akina mama, ni wazi mna nguvu na mnaweza kuhamisha hata milima na visiki vya kila aina. Mhe Kafulila Kila laheri kwa kusarenda misimamo yako na Kila laheri ktk kuanza Maisha Mapya na ni haki yako kikatiba. Msalimie sana Shemeji yetu na watoto bila kusahau makamanda. Kwa mala nyingine hongereni akina Mama.

16/12/2016
 
Kafulila ahama NCCR, ahamia Chadema
Dar es Saam. Mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini, (NCCR-Mageuzi) David Kafulila, amekihama chama hicho huku akieleza kuwa anajiandaa kuhamia Chadema.

Kafulila alithibitisha taarifa hizo na kusema tayari ameshawasilisha barua ya kujivua uanachama wa NCCR na kujiunga Chadema leo.

“Nimewashukuru kwa kuwa pamoja katika kujenga chama na nafasi ya uenezi waliyonipa mara zote. Nimeweka wazi kuwa natarajia kujiunga na Chadema. Nimeona kuwa kuna mahitaji ya watu wenye nia ya mabadiliko kuwa katika chama kimoja ili kufupisha safari.” alisema

View attachment 446944

SOURCE: Mwananchi
Karibu kundini
 
Kaenda kwa mkewe, sioni kama ita muimarisha yeye kisiasa bali ita msaidia mkewe zaidi.

Halafu kama wote NCCR na CDM ni UKAWA kuna haja gani ya Kafulila kuhama!? Au ndio umoja wa mashaka wenyewe!!
Mkuu, kuna mambo ya muungano na yasiyo ya muungano. Hili la uanachama siyo la muungano! (Rejea kumbukumbu za muungano).
 
Haiwezekani kwani ujamsikia ktk matukio yaliyopita yakuwa walezi wake na waliomuingiza ktk siasa ni hao hao siem

wewe ndiye unadhani haiwezekani....Na unajiaminisha haiwezekani
 
Msihamishe watu vyumbani bomoeni kuta zinazo tenganisha vyumba muwe na ukumbi mmoja mkubwa.
Hilo ndio wazo langu
Hii shule imewakalia kushoto hawa ukawa. Siku si nyingi pakifukuta , wale Masalia wa Dr. Slaa utasikia wameondoka Chadema na kuhamia NCCR. Siasa zinaendelea.
 
Uzi unakimbia hatari.
Upinzani wamehama toka topik ile kuja huko kwa kasi ya ajabu!!
migration at its best!!
 
unayumba yumba sana,jikite kwenye hoja. Hakikisha kabla kuchangia hutumii viminika au mosho wenye ulevi dogo.

Toka nje mada dogo ....CHADEMA wako busy kukiua NCCR kama ilivyo kwetu tuko busy kuangamiza Taifa kwa kukiuka katiba ya nchi na kutoheshimu Demokrasia na haki za binadam ingawa naona wananchi wanaweka kauzibe asa hii mitandao
 
Back
Top Bottom