Haifai kufyatuka namna hii.Hili ni onyo la awali kwa mamlaka za Tanzania.
Kwa ilipofikia Chadema Kwa sasa kitendo chochote cha kuua viongozi wake hakitanyamaziwa na haraka sana kisasi kitalipwa pakubwa
Jumbe, Mtu Mwema na Mtulivu, ambaye ni msaidizi wa Lissu ametekwa n.a. maofisa usalama Kwa lengo la kumuua, baada ya kutoa siri ya Lissu kulishwa sumu gerezani, hili jambo litavuruga Armani ya Nchi
Soma Pia: Tetesi: - David Djumbe Msaidizi Wa Tundu Lissu Ametekwa
Kwa nini wamuue; "lengo la kumuua" limetangazwa wapi?
Hakuna asiyejuwa uovu wa watu hawa, lakini haimsaidii yeyote kufyatuka tu namna hii jukwaani humu.
Inamsaidia nani hasa kwa maneno kama haya yaliyotumika; kama siyo hao hao waovu.
Huu siyo wakati wa kubwatuka tu hovyo hovyo na maneno ambayo waovu wanayachukulia kutokuwa na uzito wowote!
Samia yupo kwenye hali mbovu sana, ndiyo maana ya haya yote yanayofanyika. Anatafuta kila aina ya njia kupenya kikombe kinachomkabili; haitulazimu na sisi tuanze kuonyesha dalili za kutojiamini juu ya kinachosubiri kumwandama mwovu huyu.