Daudi Mwakawago afariki Dunia

Status
Not open for further replies.
kwa tunavyomjuwa mkwere na visasi ..bahati hiyo asingeweza kuipata asilani...mkulu huyu alipokuwa mtendaji mkuuu pale Lumumba miaka ya 80.....alimdemote Jamaa ...kutoka idara ya usalama kwenye chama..hadi wilayani tabora,singida,na lindi,,,etc....katika lile kongamano ni kati ya walio piga mawe saana...

- Mkuu PM sawa sawa tena 100%, hiyo revenge mode ilianza siku nyingi na ndio waliomzungukia kwa Kimiti hao, anyways ngoja msiba utulie kwanza Mzee arudi tulipotokea ndio tuchambue pumba na mchele, inasikitisha sana!

Respect.

FMEs!
 
kwa tunavyomjuwa mkwere na visasi ..bahati hiyo asingeweza kuipata asilani...mkulu huyu alipokuwa mtendaji mkuuu pale Lumumba miaka ya 80.....alimdemote Jamaa ...kutoka idara ya usalama kwenye chama..hadi wilayani tabora,singida,na lindi,,,etc....katika lile kongamano ni kati ya walio piga mawe saana...

JF kwa data, I like the place!
 
Kumbe kweli kesi ya Babu Seya ina utata sana.

Anyway, muosha huoshwa.

RIP Mtani wangu Mwakawago. Huyu Mzee nilimuona alipokuja Sikonge chuo cha FDC kama katibu wa CCM. Kutoka hapo sijawahi muona tena. Kuna kipindi nilikuwa nawasiliana na mtoto wake wakati nikiwa Tanzanet. Anyway, wazee wenye maadili wanaisha, sijui tutaenda wapi maana naanza kupata wasiwasi siku si nyingi tutakuwa kama Wakenya..........

- Sikonge hapa mkuu wangu umepiga msumari mzito sana, hawa ni wazee ambao wamelitumikia taifa with honors infact akiwa CCM boss alimuwajibisha hata mkuu wa kaya wa sasa, ndio maana walimfaulo sana mwishoni, lakini malipo hapa hapa duniani!

Respect.


FMEs!
 
Inasikitisha kuna watu bado wanaona ni sawa kwa viongozi kusafirishwa kwenda kutibiwa nje huku mamilioni ya Watanzania hawana hata Asprin.

Ni mawazo mufilisi kweli na aibu kwa taifa letu. Lini tutaelewa kwamba lazima tutengeneze vyetu kwanza kabla ya kukimbilia kwenye vya wenzetu?
 
Inasikitisha kuna watu bado wanaona ni sawa kwa viongozi kusafirishwa kwenda kutibiwa nje huku mamilioni ya Watanzania hawana hata Asprin.

Ni mawazo mufilisi kweli na aibu kwa taifa letu. Lini tutaelewa kwamba lazima tutengeneze vyetu kwanza kabla ya kukimbilia kwenye vya wenzetu?

- Mawazo mufilisi ni kuacha kuwapeleka nje kabla ya kutengenza vyetu kama unavyoshauri it is simply insane yaani kuacha kazi moja kabla ya kutafuta nyingine kwanza, ndio tabia za vijana wengi wabongo majuu siku hizi, sijui hili taifa tumelogwa na nani!

Respect.


FMEs!
 
- Balozi Mwakawago, alikuwa na dini, alikuwa muumini mkubwa sana wa dini ya Islam, ukifika nyumbani kwake hicho kilikuwa ni kitu cha kwanza kuki-notice ndani ya nyumba yake na besides alikuwa ni mtu wa swala tano kwa siku, ninakuomba sana umuombe Mungu wako akusamehe kwa hayo maneno ya hapo juu.

- Marehemu, Balozi Mwakawago alikuwa ni mtu wa watu on a personal level, alikuwa ni mtu wa kujichanganya sana na watu wote bila kujali uwezo wala nafasi zao katika jamii. Alihudhuria sherehe yoyote aliyoalikwa, ninakumbuka siku moja akinilalamikia kwamba kwanini wananchi wa kawaida hawamualiki lakini wanamfahamisha later kwamba walikuwa na sherehe! au kilio.

- On the leadership level alikuwa ni mzalendo, mmoja wa the chosen one wa Mwalimu, he was a very respected leader huko Iringa, lakini ilipotokea ishu ya Mwamwindi wananchi wengi wa huko waliwakaba koo yeye na Chifu Adam Sapi, ambaye Marehemu ameoa dada yake, kwamba wafanye kila wawezalo ili asinyongwe na serikali ya awamu ya kwanza. Kwa vile sheria ni msumeno walishindwa ku-secure his realese na akaishia kunyongwa kama alivyohukumiwa na sheria, wananchi wengi wa Iringa hawakuridhishwa na juhudi zake pamoja na shemeji yake Chifu Sapi za kumuokoa Mwamwindi, na wakaishia kumnyima kura za ubunge mpaka anafariki he was very unpopular na home political base.

- Alikuwa ni mmoja wa viongozi waliomuamini Mwalimu na itikadi zake na kuzitimiza kwa matendo, infact hata nyumba yake aliyoijenga hapa mjini ilikuwa ni baada ya kuingia UN, otherwise aliondoka serikalini akiwa kama alivyo. Na knowing him on a close range he was not very happy na the way he parted ways na taifa letu baada ya kulitumikia kwa karibu nusu ya maisha yake he felt kwamba hakupewa heshima aliyostahili. Na Mtandao made very clear to him kwamba they wanted nothing to do with him na hii ilikuwa ni through Marehemu Kawawa, ambaye alimsaidia sana katika dakika zake za mwisho mwisho na ajira yake kwenye taifa letu.

- Huyu hakuwa fisadi, hakuiba wala hakuwa na kitu ninarudia ametoka serikalini akiwa mtupu sana, thanks to the UN na hasa Mzee Kofi Anan. Ninakumbuka sana baada ya kutoka kwake serikalini, nilikuwa NY nikashiriki kumfanyia sherehe kubwa sana ya kumuaga ambapo binafsi nili-specialize na financial ya ile hafla, pamoja na wananchi wengi sana kujitokeza kushikiri, pia tuliweza kuwashawishi Mabalozi karibu 20 wa nchi zingine za Africa kuja kushirki nasi kwenye kumuaga. It was a suprise party masikini ya Mungu hakujua, he cried alipofika ukumbini, siku moja baada ya sherehe he took a time akanitafuta personally na in a very humble way akaniamibia "....kijana you made my day, hujui how down I was hujui jinsi nilivyokuwa ninajisikia worhtless, kumbe kuna wanaothamini niliyoyafanya hapa duniani...", miezi mitatu later akiwa UN ninakumbuka kumualika tena kwenye sherehe moja iliyokuwa na wakuu wengi wa taifa, he came na again akanishukuru sana kwa kumkumbusha enzi zake, ingawa mwanzoni alisita sana kukubali mwaliko kwa wasi wasi kwamba labda wale wakuu wa taifa wasingependa awepo pale.

- Again this was a good man, ninajua kwamba kama bin-adam alikuwa na mapungufu, lakini ninaamini kwamba hayakuwa makubwa sana kiasi cha kuliltetea hasara taifa, au kulifisadi as opposed na hawa maviongozi magoi goi mengi tulionayo sasa. Kwa jinsi alivyokuwa akinisimulia experience zake na uongozi wa taifa hata Mwalimu alimuheshimu sana, infact hata ndani ya UN alikuwa aki-command heshima kubwa sana na ya juu sana, na he was a family man devoted in a very serious ways to his family, I mean hata watoto wake ni mfano mzuri sana wa who was Marehemu as a person.

- Again nimeandika hiki kipande na roho nzito sana, I am mourning this good man na a good leader, ninawatakia heri familia yake nzima na hasa watoto wake, Mungu awape nguvu na hasa busara za kupita hiki kipindi kigumu sana.

Respect.

FMEs!

Sometimes umuhimu wa mtu haujulikani hadi akiondoka duniani na hii ndio mifano yake. Mara nyingi watu wema hufa maskini lakini majitu majizi hufa wakasindikizwa na mali zao. Inasikitisha sana lakini sishangai kwani Tanzania imegeuka sasa kama Italy (i.e. mafia style leadership) kufanyiziana tu ndio maana waswahili wanasema fanya wema uende zako usingojee shukrani maana unaweza kuambulia matusi bure!!!
 
Inasikitisha kuna watu bado wanaona ni sawa kwa viongozi kusafirishwa kwenda kutibiwa nje huku mamilioni ya Watanzania hawana hata Asprin.

Ni mawazo mufilisi kweli na aibu kwa taifa letu. Lini tutaelewa kwamba lazima tutengeneze vyetu kwanza kabla ya kukimbilia kwenye vya wenzetu?

Ni mawazo gani muflis kumpeleke kiongozi mgonjwa nje kama Tanzania hawana tiba. Mbona nyerere, ,mwinyi na mawaziri wengineo wanaenda nje sembuse kumpeleka kiongozi aliyelitumikia taifa kwa uzalendo akatibiwe nje. Mh naona ndugu utawachafua watu humu JF rekebisha kauli yako mzee
 
- Wakuu wa New York City na vitongoji vyake ni kwamba kuna tunaojitayarisha kwenda Boston this weekend kuwafariji na kulia na watoto wa marehemu ambao baadhi yao wapo kule na ndiko msiba hasa hapa US ulipo, sasa kwa wanaotaka kwenda tuwasiliane jamani,

- Na habari nilizozipata hapa mjini kutoka kwa Mwalimu, ni kwamba Balozi wetu hapa UN, naye atakwenda huko mwisho huu wa wiki kuwaona wafiwa na tarehe 6 mwezi ujao kutakuwa na kumkumbuka marehemu nyumbani kwa balozi, kuanzia saa Nane mchana.

Mungu amlaze pema marehemu na awafariji wafiwa.

Ahsante.


William.
 
Mwanasiasa Mkongwe nchini Balozi Daudi Mwakawago amefariki dunia Jijini Dar e salaam.

Mwakawago alipata kushika nyadhifa mabli mbali za Kiasiasa nchini, Ubunge Iringa Mjini, Uwaziri, Balozi wa Kudumu UN

Ama hakika sisi ni wenye kurejea kwake Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu amlaze mahala pema peponi Amina
 
FMES,
Nimekusikia mkuu wangu. Ndiyo maana nimesema Mwakawago alikuwa a class act.
Alipomaliza muda wake UN aliomba kuonana na Mkapa Ikulu Mkapa akakataa eti anakuja kuomba kazi. Kumbe jamaa alikuwa kishapata kazi ya UN. Hawakumtendea haki, lakini sishangai kwa sababu hakuwa fisadi mwenzao. Kuna wakati nilikuwa nasaka interview na Mwalimu Nyerere bila kufanikiwa. Niliongea na Mwakawago akaniambia nimuandikie maswali, nikadhani utani. Niliandika maswali matano, akampelekea Mwalimu. Baadaye akanipigia simu akisema Mwalimu amekubali interview yako. That is the kind of man he was.
Jaribu kumwandikia Makamba uombe interview na JK...lol
 
kwi!kwi!kwi!
Hawa viongozi wetu wa kwanza walikuwa class act. Hawa waliofuata ni utapeli tu.
Lakini naamini Tanzania bado kuna vichwa.

Ebana Jasusi...hiyo interview yako unayo kwenye audio? Kama unayo tuwekee basi hapa....
 
Poleni wafiwa wote. Nimesikia watamzika hapa Dar. Mzee mzito kama huyu wameshindwa kumzika Iringa kwa nini? Tunaifuta historia ya Nchi hii kwa kuwazika wazee kama hawa kwenye makaburi ya jumla hapa Dar ambayo baadaye yatakuja fukuliwa kuwapisha wawekezaji.
 
Poleni wafiwa wote. Nimesikia watamzika hapa Dar. Mzee mzito kama huyu wameshindwa kumzika Iringa kwa nini? Tunaifuta historia ya Nchi hii kwa kuwazika wazee kama hawa kwenye makaburi ya jumla hapa Dar ambayo baadaye yatakuja fukuliwa kuwapisha wawekezaji.

- Mkuu sasa hivi nimemuuliza mzito mmoja kuhusu hii hoja nzito sana, akaniambia kijana Dodoma kuna sehemu imetengwa kwa ajili ya maziko ya marais na viongozi wa juu wa taifa, lakini hakuna familia hata moja ya kiongozi wa taifa aliyewahi kufariki iliyowahi kuomba kuzika kwenye hilo eneo.

- Kwanini hakuzikwa Iringa, ni very complicated ishu ambayo katika hii hali ya msiba na bado hajazikwa sio polite kwenda hiyo avenue!

Respect.


FMEs!
 
Ebana Jasusi...hiyo interview yako unayo kwenye audio? Kama unayo tuwekee basi hapa....
Julius,'
Ninayo kwenye cassette. Nikishatulia nitaiweka kwenye cd. Lakini si mkisikia sauti yangu identity yangu itajulikana? kwi!kwi!kwi!
 
Julius,'
Ninayo kwenye cassette. Nikishatulia nitaiweka kwenye cd. Lakini si mkisikia sauti yangu identity yangu itajulikana? kwi!kwi!kwi!

Sauti yako si inajulikana na watu wanaokujua?Ama kuna watu wanaokujua lakini hutaki wajue kama ni wewe?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom