Daudi Mwakawago afariki Dunia

Status
Not open for further replies.
Mungu Ailaze Roho ya Marehemu Mahala Pema Peponi.
..Huyu mzee inasemekana hakuwa muumini wa dini yoyote wakati wa uhai wake (pagan) hata wakati wa kuapishwa enzi za JK Nyerere yeye hakushika bible wala msahafu na mwenzie Kingunge.......RIP M/kawago!!
 
Jamani Mungu akulaze mahali pema peponi. hichi kifo jamani.... juzi tu tumemwona kwenye kipindi cha Mayrose show star tv, alikuwa akituaga jamani.
 
According to michuzi blog Balozi Mwakawago hatunaye tena

Marehemu daudi mwakawago

Habari zimetufikia sasa hivi zinasema balozi daudi mwakawago (71 amefariki dunia ajfajiri leo katika hospitali ya aga khan jijini dar alikokuwa amelazwa kwa takriban siku tisa akisumbuliwa na malaria na baadae nimonia.

Msemaji wa familia, yasini mwakawago, amethibitisha habari hizo na amesema msiba uko msasani maduka mawili jijini dar, na mazishi yanatarajiwa kufanyika jumamosi.

DaudiMwakawago_000.jpg

Balozi mwakawago atakumbukwa kama mwanasiasa na mwanadiplomasia mwandamizi aliyeshika nyadhifa mbalimbali ikiwa ni pamoja na waziri wa habari na utamaduni, waziri wa kazi na maendeleo, waziri wa viwanda na biashara.

Balozi mwakawago pia alikuwa balozi wetu huko italia na baadae umoja wa mataifa, kabla ya kusataafu. Aliwahi pia kuchaguliwa na katibu mkuu wa umoja wa mataifa wakati huo, koffi annan kuwa msuluhishi wa mgogoro nchini sierra leone.
 
Wanajamii forum

Kuna taarifa kwamba ndugu yetu mkongwe, Comrade Daudi Mwakawago alifariki leo asubuhi katika Hospital ya Aga Khan jijini Dar es Salaam. Mazishi ni siku ya Jumamosi katika makaburi ya Kisutu
 
RIP Mzee Mwakawago, kwa wale tuliokuwa Freetown enzi hizo akiwa USG-UNAMSIL, tutamkumbuka kwa kuitisha vikao vya watanzania nyumbani kwake maeneo ya Aberdeen, kwa kweli alituunganisha vizuri sana, ni majonzi makubwa
 
Mwanasiasa Mkongwe nchini Balozi Daudi Mwakawago amefariki dunia Jijini Dar e salaam.

Mwakawago alipata kushika nyadhifa mabli mbali za Kiasiasa nchini, Ubunge Iringa Mjini, Uwaziri, Balozi wa Kudumu UN

Msiba uko wapi angalao watakaopata nafasi wahudhurie??
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom