..Huyu mzee inasemekana hakuwa muumini wa dini yoyote wakati wa uhai wake (pagan) hata wakati wa kuapishwa enzi za JK Nyerere yeye hakushika bible wala msahafu na mwenzie Kingunge.......RIP M/kawago!!Mungu Ailaze Roho ya Marehemu Mahala Pema Peponi.
Marehemu daudi mwakawago
Habari zimetufikia sasa hivi zinasema balozi daudi mwakawago (71 amefariki dunia ajfajiri leo katika hospitali ya aga khan jijini dar alikokuwa amelazwa kwa takriban siku tisa akisumbuliwa na malaria na baadae nimonia.
Msemaji wa familia, yasini mwakawago, amethibitisha habari hizo na amesema msiba uko msasani maduka mawili jijini dar, na mazishi yanatarajiwa kufanyika jumamosi.
Balozi mwakawago atakumbukwa kama mwanasiasa na mwanadiplomasia mwandamizi aliyeshika nyadhifa mbalimbali ikiwa ni pamoja na waziri wa habari na utamaduni, waziri wa kazi na maendeleo, waziri wa viwanda na biashara.
Balozi mwakawago pia alikuwa balozi wetu huko italia na baadae umoja wa mataifa, kabla ya kusataafu. Aliwahi pia kuchaguliwa na katibu mkuu wa umoja wa mataifa wakati huo, koffi annan kuwa msuluhishi wa mgogoro nchini sierra leone.
wenzako wanaamka wewe unavuta shuka.
he makubwa haya msibani hawapigi hodi we jiunge kwanza, tuko bize na taarifa za msiba na si mda wa kukarishana huu, kwani we huoni bango linasomekaje?I am a new member, do u welcome me wana JF
Mwanasiasa Mkongwe nchini Balozi Daudi Mwakawago amefariki dunia Jijini Dar e salaam.
Mwakawago alipata kushika nyadhifa mabli mbali za Kiasiasa nchini, Ubunge Iringa Mjini, Uwaziri, Balozi wa Kudumu UN