Daudi Mwakawago afariki Dunia

Daudi Mwakawago afariki Dunia

Status
Not open for further replies.
duh.. siku nyingine ya huzuni kwa taifa letu. Mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi. Amina.
 
Inna lillah wa inna 'ilayhi raji'un.
'Surely we belong to Allah and to Him shall we return'
'Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu na kwake tutarejea'.​
 
R.I.P Daudi Ngelautwa Mwakawago , Naona pale Kitanzini patakuwa Hapatoshi.
Poleni sana wafiwa.
 
Aliwahi pia kuwa katibu mkuu wa CCM. A class act. Huwezi kumfananisha na Makamba.Hata kidogo.
RIP, brother Mwakawago.
 
..Huyu mzee inasemekana hakuwa muumini wa dini yoyote wakati wa uhai wake (pagan) hata wakati wa kuapishwa enzi za JK Nyerere yeye hakushika bible wala msahafu na mwenzie Kingunge.......RIP M/kawago!!

- Balozi Mwakawago, alikuwa na dini, alikuwa muumini mkubwa sana wa dini ya Islam, ukifika nyumbani kwake hicho kilikuwa ni kitu cha kwanza kuki-notice ndani ya nyumba yake na besides alikuwa ni mtu wa swala tano kwa siku, ninakuomba sana umuombe Mungu wako akusamehe kwa hayo maneno ya hapo juu.

- Marehemu, Balozi Mwakawago alikuwa ni mtu wa watu on a personal level, alikuwa ni mtu wa kujichanganya sana na watu wote bila kujali uwezo wala nafasi zao katika jamii. Alihudhuria sherehe yoyote aliyoalikwa, ninakumbuka siku moja akinilalamikia kwamba kwanini wananchi wa kawaida hawamualiki lakini wanamfahamisha later kwamba walikuwa na sherehe! au kilio.

- On the leadership level alikuwa ni mzalendo, mmoja wa the chosen one wa Mwalimu, he was a very respected leader huko Iringa, lakini ilipotokea ishu ya Mwamwindi wananchi wengi wa huko waliwakaba koo yeye na Chifu Adam Sapi, ambaye Marehemu ameoa dada yake, kwamba wafanye kila wawezalo ili asinyongwe na serikali ya awamu ya kwanza. Kwa vile sheria ni msumeno walishindwa ku-secure his realese na akaishia kunyongwa kama alivyohukumiwa na sheria, wananchi wengi wa Iringa hawakuridhishwa na juhudi zake pamoja na shemeji yake Chifu Sapi za kumuokoa Mwamwindi, na wakaishia kumnyima kura za ubunge mpaka anafariki he was very unpopular na home political base.

- Alikuwa ni mmoja wa viongozi waliomuamini Mwalimu na itikadi zake na kuzitimiza kwa matendo, infact hata nyumba yake aliyoijenga hapa mjini ilikuwa ni baada ya kuingia UN, otherwise aliondoka serikalini akiwa kama alivyo. Na knowing him on a close range he was not very happy na the way he parted ways na taifa letu baada ya kulitumikia kwa karibu nusu ya maisha yake he felt kwamba hakupewa heshima aliyostahili. Na Mtandao made very clear to him kwamba they wanted nothing to do with him na hii ilikuwa ni through Marehemu Kawawa, ambaye alimsaidia sana katika dakika zake za mwisho mwisho na ajira yake kwenye taifa letu.

- Huyu hakuwa fisadi, hakuiba wala hakuwa na kitu ninarudia ametoka serikalini akiwa mtupu sana, thanks to the UN na hasa Mzee Kofi Anan. Ninakumbuka sana baada ya kutoka kwake serikalini, nilikuwa NY nikashiriki kumfanyia sherehe kubwa sana ya kumuaga ambapo binafsi nili-specialize na financial ya ile hafla, pamoja na wananchi wengi sana kujitokeza kushikiri, pia tuliweza kuwashawishi Mabalozi karibu 20 wa nchi zingine za Africa kuja kushirki nasi kwenye kumuaga. It was a suprise party masikini ya Mungu hakujua, he cried alipofika ukumbini, siku moja baada ya sherehe he took a time akanitafuta personally na in a very humble way akaniamibia "....kijana you made my day, hujui how down I was hujui jinsi nilivyokuwa ninajisikia worhtless, kumbe kuna wanaothamini niliyoyafanya hapa duniani...", miezi mitatu later akiwa UN ninakumbuka kumualika tena kwenye sherehe moja iliyokuwa na wakuu wengi wa taifa, he came na again akanishukuru sana kwa kumkumbusha enzi zake, ingawa mwanzoni alisita sana kukubali mwaliko kwa wasi wasi kwamba labda wale wakuu wa taifa wasingependa awepo pale.

- Again this was a good man, ninajua kwamba kama bin-adam alikuwa na mapungufu, lakini ninaamini kwamba hayakuwa makubwa sana kiasi cha kuliltetea hasara taifa, au kulifisadi as opposed na hawa maviongozi magoi goi mengi tulionayo sasa. Kwa jinsi alivyokuwa akinisimulia experience zake na uongozi wa taifa hata Mwalimu alimuheshimu sana, infact hata ndani ya UN alikuwa aki-command heshima kubwa sana na ya juu sana, na he was a family man devoted in a very serious ways to his family, I mean hata watoto wake ni mfano mzuri sana wa who was Marehemu as a person.

- Again nimeandika hiki kipande na roho nzito sana, I am mourning this good man na a good leader, ninawatakia heri familia yake nzima na hasa watoto wake, Mungu awape nguvu na hasa busara za kupita hiki kipindi kigumu sana.

Respect.

FMEs!
 
RIP Mzee Mwakawago, kwa wale tuliokuwa Freetown enzi hizo akiwa USG-UNAMSIL, tutamkumbuka kwa kuitisha vikao vya watanzania nyumbani kwake maeneo ya Aberdeen, kwa kweli alituunganisha vizuri sana, ni majonzi makubwa

- This was him, kila mahali alipowahi kuishi hata wale walioishi naye Italy watakubaliana na mimi kwamba hii ya kuwaunganisha wananchi ilikuwa ni kwenye damu yake.

Respect.


FMEs!
 
FMES,
Nimekusikia mkuu wangu. Ndiyo maana nimesema Mwakawago alikuwa a class act.
Alipomaliza muda wake UN aliomba kuonana na Mkapa Ikulu Mkapa akakataa eti anakuja kuomba kazi. Kumbe jamaa alikuwa kishapata kazi ya UN. Hawakumtendea haki, lakini sishangai kwa sababu hakuwa fisadi mwenzao. Kuna wakati nilikuwa nasaka interview na Mwalimu Nyerere bila kufanikiwa. Niliongea na Mwakawago akaniambia nimuandikie maswali, nikadhani utani. Niliandika maswali matano, akampelekea Mwalimu. Baadaye akanipigia simu akisema Mwalimu amekubali interview yako. That is the kind of man he was.
 
FMES,
Nimekusikia mkuu wangu. Ndiyo maana nimesema Mwakawago alikuwa a class act.
Alipomaliza muda wake UN aliomba kuonana na Mkapa Ikulu Mkapa akakataa eti anakuja kuomba kazi. Kumbe jamaa alikuwa kishapata kazi ya UN. Hawakumtendea haki, lakini sishangai kwa sababu hakuwa fisadi mwenzao.
.

- Mkuu wangu, ni kwamba walikuwa wanamtafuta siku nyingi sana kumuondoa, lakini Kawawa alikuwa anawazuia kwa sababu hakuona sababu ya msingi, lakini hawa wajanja wakamzungukia kwenye bajeti ya Wizara ya nje, wakamtumia Kimiti aliyedai specifically kwenye kamati ya nje kwamba Mwakawago, Nyag'anyi na Sarakikya wasiporudishwa, bajeti haipiti,

- Mkuu Jasusi hili taifa tuna mafia sana wa kichini chini can you imagine hizi schemes utafikiria wanauchungu na taifa kumbe ni ujanja ujanja tu! Aliniambia jinsi walivyomkatalia kabisa kumuona Mkapa na huyu wa sasa yeye Marehemu ndiye aliyempeleka Tunduru kutoka Dodoma, yaani alikuwa hataki kabisa hata kumsikia, sasa subiri uwaone kwenye mazishi na unafiki wao!

Respect.


FMEs!
 
FMES.. si unakumbuka majuzi tulipokuwa tunazungumza nikawa naulizia mzee huyo ameishia wapi tena.. sasa wazee wenyewe ndio hao wanaondoka taratibu..
 
FMES.. si unakumbuka majuzi tulipokuwa tunazungumza nikawa naulizia mzee huyo ameishia wapi tena.. sasa wazee wenyewe ndio hao wanaondoka taratibu..

- Mkuu MMJ, ni kweli lakini knowing him as I do, afya yake haikuwa nzuri sana siku zote na serikali haikuwa na utaratibu wowote wa kumsaidia, hata ule msaada mdogo sana aliokuwa nao through ubalozi wake, uliiisha pale pale alipotolewa kazi, inasikitisha sana maana hawa ndio dhahabu ya taifa. I mean hakuwa mzee kabisa, alikuwa bado saaana!

- Unajua nilinasa dataz za siri sana toka Jumanne kwamba huko magogoni kulikuwa na a big debate among the powers kama marehemu awe airlifted to Nairobi au ney!, sasa kama amefia Agha Kan ina maana the neys! zilikuwa nyingi zaidi ya the Isss!, ni aibu sana!

Respect


FMEs!
 


The late H.E Balozi Mwakawago

RIP

Mwenyezi mungu airehemu roho yake na kuwapa nguvu wanafamilia wakati wa kuomboleza msiba huu.



 
- Mkuu MMJ, ni kweli lakini knowing him as I do, afya yake haikuwa nzuri sana siku zote na serikali haikuwa na utaratibu wowote wa kumsaidia, hata ule msaada mdogo sana aliokuwa nao through ubalozi wake, uliiisha pale pale alipotolewa kazi, inasikitisha sana maana hawa ndio dhahabu ya taifa. I mean hakuwa mzee kabisa, alikuwa bado saaana!

- Unajua nilinasa dataz za siri sana toka Jumanne kwamba huko magogoni kulikuwa na a big debate among the powers kama marehemu awe airlifted to Nairobi au ney!, sasa kama amefia Agha Kan ina maana the neys! zilikuwa nyingi zaidi ya the Isss!, ni aibu sana!

Respect

FMEs!

FMES, hiyo hapo bolded ni partially true.
Kweli kulikuwa na mjadala na haukuwa siri, ulikuwa wa wazi tu. Familia yake kupitia kwa vigogo wenzie akina Mungai, Kitine, Mkwawa, etc walikuwa katika utaratibu wa kumpeleka aidha Nairobi au India kwa matibabu zaidi. Nadhani walihusisha Magogoni pia, sina hakika sana na hili.
Akiwa ICU pale Aga Khan juzi j'pili, ilionekana kuwa isubiriwe hali yake iwe nzuri kidogo kabla ya kusafirishwa. Mapenzi ya Mungu yametangulia mipango ya wanadamu.

Anategemea kuzikwa Ijumaa makaburi ya Kisutu.

Peace. Naingia mitini tena.
 
FMES, hiyo hapo bolded ni partially true.
Kweli kulikuwa na mjadala na haukuwa siri, ulikuwa wa wazi tu. Familia yake kupitia kwa vigogo wenzie akina Mungai, Kitine, Mkwawa, etc walikuwa katika utaratibu wa kumpeleka aidha Nairobi au India kwa matibabu zaidi. Nadhani walihusisha Magogoni pia, sina hakika sana na hili.
Akiwa ICU pale Aga Khan juzi j'pili, ilionekana kuwa isubiriwe hali yake iwe nzuri kidogo kabla ya kusafirishwa. Mapenzi ya Mungu yametangulia mipango ya wanadamu.

Anategemea kuzikwa Ijumaa makaburi ya Kisutu.

Peace. Naingia mitini tena.

- Mkuu Kiungani heshima yako sana mkuu, unajua kua siku zote you have my respect, kwamba hii debate ilikuwa ya wazi labda huko kwenye familia, mimi nimezisikia hizo dataz Jumanne asubuhi kutoka line ya Magogoni in a very ugly debate na haikuhusisha anyone kutoka familia, isipokuwa the powers tu na I happen to be karibu na the power mmoja ambaye alitakiwa kutoa ushauri wake kutokana na kutokuwepo huko Magogoni, eti unasema familia ndio walihusisha magogoni haya mkuu, bado tuko kwenye msiba for now.

- Ya kusubiri hali yake iwe nzuri ndiyo asafirishwe, siyajui maana by the time ninazisikia hizi dataz yaani Jumanne asubuhi ni kwamba alikuwa na hali mbaya sana sasa kumbe kabla ya kuwasafirisha wagonjwa wa dharura huwa wanasubiri kwanza ili hali yao iwe nzuri? Duh!

Ahsante mkuu kwa hizi habari na wasalimie sana huko mitini!

Respect.

FMEs!
 
- Mkuu MMJ, ni kweli lakini knowing him as I do, afya yake haikuwa nzuri sana siku zote na serikali haikuwa na utaratibu wowote wa kumsaidia, hata ule msaada mdogo sana aliokuwa nao through ubalozi wake, uliiisha pale pale alipotolewa kazi, inasikitisha sana maana hawa ndio dhahabu ya taifa. I mean hakuwa mzee kabisa, alikuwa bado saaana!

- Unajua nilinasa dataz za siri sana toka Jumanne kwamba huko magogoni kulikuwa na a big debate among the powers kama marehemu awe airlifted to Nairobi au ney!, sasa kama amefia Agha Kan ina maana the neys! zilikuwa nyingi zaidi ya the Isss!, ni aibu sana!

Respect


FMEs!

.........Sio Siri serikali inawasahau sana hawa wazee wa zamani.Marehemu Chief Adamu Sapi Mkwawa kipindi alivyokuwa mgonjwa alikuwa anakuja pale Amana hospital na kutibiwa.Kweli kiongozi kama Adam Sapi Mkwawa aje kutibiwa Amana, hebu angalia serikali isivyowajali hawa viongozi wa zamani.

.......Bwana alitoa na Bwana ametwaa,jina la Bwana lihimidiwe.
RIP Mzee Daudi Mwakawago.
 
mwanga wa milele bwana akuangazie na upumzike kwa amani...RIP mzee wangu Mwakawago
 
-

- Unajua nilinasa dataz za siri sana toka Jumanne kwamba huko magogoni kulikuwa na a big debate among the powers kama marehemu awe airlifted to Nairobi au ney!, sasa kama amefia Agha Kan ina maana the neys! zilikuwa nyingi zaidi ya the Isss!, ni aibu sana!

Respect

FMEs!


kwa tunavyomjuwa mkwere na visasi ..bahati hiyo asingeweza kuipata asilani...mkulu huyu alipokuwa mtendaji mkuuu pale Lumumba miaka ya 80.....alimdemote Jamaa ...kutoka idara ya usalama kwenye chama..hadi wilayani tabora,singida,na lindi,,,etc....katika lile kongamano ni kati ya walio piga mawe saana...
 
kwa tunavyomjuwa mkwere na visasi ..bahati hiyo asingeweza kuipata asilani...mkulu huyu alipokuwa mtendaji mkuuu pale Lumumba miaka ya 80.....alimdemote Jamaa ...kutoka idara ya usalama kwenye chama..hadi wilayani tabora,singida,na lindi,,,etc....katika lile kongamano ni kati ya walio piga mawe saana...

Kumbe kweli kesi ya Babu Seya ina utata sana.

Anyway, muosha huoshwa.

RIP Mtani wangu Mwakawago. Huyu Mzee nilimuona alipokuja Sikonge chuo cha FDC kama katibu wa CCM. Kutoka hapo sijawahi muona tena. Kuna kipindi nilikuwa nawasiliana na mtoto wake wakati nikiwa Tanzanet. Anyway, wazee wenye maadili wanaisha, sijui tutaenda wapi maana naanza kupata wasiwasi siku si nyingi tutakuwa kama Wakenya..........
 
Kwa masikitiko makuu na hudhuni nyingi naipokea taarifa hii. Nilimfahamu Daudi tangu siku za ujana wake akiwa TANU mpaka katika uzee akiwa UN. Alikuwa mchapa kazi mahiri sana, mcheshi na mkarimu.

Mungu ampe makazi mema yanayomstahili na awape nguvu wafiwa ya kustahimili msiba huu mkubwa. Ameen!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom