Asprin
Platinum Member
- Mar 8, 2008
- 68,272
- 96,398
![]()
Mambo huweza nitinga, niisakapo riziki,
Mkahisi nawatenga, mkahisi siwataki,
Juweni nasaka mpunga, ili niishinde dhiki,
Niwapo kimya wapendwa, msidhani siwapendi.
Najua mnaumia, kwani hamwishi lalama,
Nami ninawasikia, huku moyo kiniuma,
Najaribu kuzuia, kwa maneno ninasema,
Niwapo kimya wapendwa, msidhani siwapendi.
Salamu kweli muhimu, daima kukumbukana,
Huleta mashamshamu, nayo mapenzi kufana,
Ukimya unayo sumu, kama utazidi sana,
Niwapo kimya wapendwa, msidhani siwapendi.
Nipo nanyi ndugu zangu wana JF, hakika nitakuja Dar siku hiyo ya MKODOBWE
Wewe unatuchukia, Mimi nimeshatambua,
Vikao wavikimbia, Kazi unasingizia,
Hakika watubania, Nduguzo watukimbia,
Kimya chako cha mashaka, Nduguzo watuchukia
Surayo watubania, Kutingwa wasingizia,
Kila mara wakimbia, Vikao vya jumuia,
Kazi wazisingizia, watukimbia jamaa,
Kimya chako cha mashaka, Mduguzo watukuchukia.
Sababu waturushia, Tena za kuongopea,
Surayo twatamania, wewe unaifichia,
Kwanini watuchukia, tena unatukimbia?
Kimya chako cha mashaka, Mduguzo watukuchukia.
Na Babu ODM
Kaunta ya Juu, Mfalme Nyota,
Fyatanga Bar
Boko Basihaya.
Nakala: Mtambuzi, gfsonwin, lara 1, amu, Paloma, Jiwe Linaloishi, cacico, snowhite, Madame B, Fidel80, Naniliyu, Zion Daughter KakaKiiza, Ruttashobolwa, Superman naaaaa........... well well well charminglady, Nicas Mtei.
Last edited by a moderator: