Dar: Wahalifu wadaiwa kutumia jina la ‘Ulinzi Shirikishi’ kufanya uhalifu maeneo ya Tanganyika Packers

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464
images (8).jpeg
Wakazi wa Mtaa wa Kawe Jijini Dar es Salaam, wameliomba Jeshi la Polisi Nchini kuongeza ulinzi hasa nyakati za jioni katika maeneo ya Tanganyika Packers ikidaiwa kuongezeka kwa vitendo vya ukabaji na unyang’anyi wa kutumia silaha mbalimbali hususani za jadi.

Ikidaiwa kuwa wahusika wanaofanya hivyo wanajitambulisha kuwa wanafanya Ulinzi Shirikishi.

Wamedai kuwa ukikutana nao hujitambusha kama Watu wa Usalama na baada ya hapo hutekeleza uovu huo kwa kukutolea mapanga, visu, nondo kisha kufanya uhalifu huo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wakazi wa mtaa huo ambao wawili walikataa kutotajwa kwa majina, wamedai kumekuwepo kwa vitendo hivyo katika eneo Hilo ambalo ni karibu zaidi na Kituo cha Polisi Kawe.

Wadai hivi karibu mmoja wa Askari wa Jeshi anadaiwa kukabwa akiwa na mpenzi wake katika eneo hilo jambo ambalo linaongeza wasiwasi miongoni mwao.

Williams Nashoni ni mmoja wa mkazi wa mtaa huo amesema kuwa kumekuwepo kwa vitendo hivyo kwa kiasi kubwa japo hivi karibuni vimepungua kutokana na baadhi ya walinzi wa Mchungaji Mwamposa kuongeza walinzi, hata hivyo akidai bado jitihada zinatakiwa kuongezwa kutokana na walinzi hao kutokudhi mahitaji.

Nashoni amesema kinachowaumiza ni vitendo hivyo kutokea eneo ambalo si mbali na Kituo cha Polisi Kawe huku akiwaomba wahusika kujitathimini.

Akizungumza kwa njia ya simu Kamanda wa Polisi Mkoa wa kinondoni, ACP Mtatiro Kitinkwi amesema wamejipanga kuendeleza kudumisha ulinzi na usalama eneo nzima la mkoa wa Kipolisi ikiwemo Kawe na Tanganyika Packers.

Amedai kuelekea Mwisho wa mwaka kuna tukio la mkesha eneo la Tanganyika Packers na wao kama Jeshi wamejipanga kuongeza ulinzi na usalama ili kuhakikisha hakuna vitendo viovu vinavyojitokeza hata kwa bahati mbaya.

Amewaomba Wananchi kuendelea kutoa taarifa zote za uhalifu katika mkoa huo ili kuwarahisishia kazi na kuhakikisha vitendo hivyo vinakomeshwa.

Pia soma = IGP Wambura na PT yake wamelishindwa Pori Hatari kwa Uhalifu Tanganyika Packers Kawe!

> Serikali ya Mtaa Kawe: Kweli kuna kundi la Wahalifu wanatumia kivuli cha Ulinzi Shirikishi, wanatuchanganya sana
 
Ulinzi shirikishi ni panya road. Hao jamaa waliwahi kunipiga ubapa wa panga mgongoni bila kosa eti kisa natembea kwa mguu kuelekea nyumbani kutokea sehemu iliyokuwepo pub ya ndugu yangu
 
Ulinzi shirikishi ni panya road. Hao jamaa waliwahi kunipiga ubapa wa panga mgongoni bila kosa eti kisa natembea kwa mguu kuelekea nyumbani kutokea sehemu iliyokuwepo pub ya ndugu yangu
na wewe uka kaa tu kama kunde zinazosubiri kuchemshwa, mpaka unapigwa bapa la upanga....
 
Yote ni miradi ya polisi haohao usidhani hata huyo ijp hajui kinachoendelea eneo hilo!
Tanzania bila polisi hakuna uhalifu!
Siku wakiachwa kutumiwa kisiasa watarudi kwenye mstari na kutenda kazi yao kwa weledi sio kwa sasa ambapo hawatosheki na mishahara na posho nyingi wanazolipwa na serikali, kila askari hata aliyetoka depo juzi anataka kumiliki nyumba gari na maisha mazuri!
 
nakumbuka kamanda siro aliwasihi sana wananchi kwa kusema kuwa ulinzi na usalama unaanzia nyumbani kwako ukiona mtoto wako haeleweki tabia zake peleka katika vyombo vya usalama
akahojiwe anafanya kazi gani kuishi. nadhani tuanzie hapo.
 
Wakazi wa Mtaa wa Kawe Jijini Dar es Salaam, wameliomba Jeshi la Polisi Nchini kuongeza ulinzi hasa nyakati za jioni katika maeneo ya Tanganyika Packers ikidaiwa kuongezeka kwa vitendo vya ukabaji na unyang’anyi wa kutumia silaha mbalimbali hususani za jadi.

Ikidaiwa kuwa wahusika wanaofanya hivyo wanajitambulisha kuwa wanafanya Ulinzi Shirikishi.

Wamedai kuwa ukikutana nao hujitambusha kama Watu wa Usalama na baada ya hapo hutekeleza uovu huo kwa kukutolea mapanga, visu, nondo kisha kufanya uhalifu huo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wakazi wa mtaa huo ambao wawili walikataa kutotajwa kwa majina, wamedai kumekuwepo kwa vitendo hivyo katika eneo Hilo ambalo ni karibu zaidi na Kituo cha Polisi Kawe.

Wadai hivi karibu mmoja wa Askari wa Jeshi anadaiwa kukabwa akiwa na mpenzi wake katika eneo hilo jambo ambalo linaongeza wasiwasi miongoni mwao.

Williams Nashoni ni mmoja wa mkazi wa mtaa huo amesema kuwa kumekuwepo kwa vitendo hivyo kwa kiasi kubwa japo hivi karibuni vimepungua kutokana na baadhi ya walinzi wa Mchungaji Mwamposa kuongeza walinzi, hata hivyo akidai bado jitihada zinatakiwa kuongezwa kutokana na walinzi hao kutokudhi mahitaji.

Nashoni amesema kinachowaumiza ni vitendo hivyo kutokea eneo ambalo si mbali na Kituo cha Polisi Kawe huku akiwaomba wahusika kujitathimini.

Akizungumza kwa njia ya simu Kamanda wa Polisi Mkoa wa kinondoni, ACP Mtatiro Kitinkwi amesema wamejipanga kuendeleza kudumisha ulinzi na usalama eneo nzima la mkoa wa Kipolisi ikiwemo Kawe na Tanganyika Packers.

Amedai kuelekea Mwisho wa mwaka kuna tukio la mkesha eneo la Tanganyika Packers na wao kama Jeshi wamejipanga kuongeza ulinzi na usalama ili kuhakikisha hakuna vitendo viovu vinavyojitokeza hata kwa bahati mbaya.

Amewaomba Wananchi kuendelea kutoa taarifa zote za uhalifu katika mkoa huo ili kuwarahisishia kazi na kuhakikisha vitendo hivyo vinakomeshwa.

Chanzo: Torch Media

Pia soma = IGP Wambura na PT yake wamelishindwa Pori Hatari kwa Uhalifu Tanganyika Packers Kawe!
Hii habari mbona imempita shihata aliyekubuhu GENTAMYCINE ?
 
Back
Top Bottom