Dar to Mtwara, mdogo wangu kafariki kwa basi gani?

Dar to Mtwara, mdogo wangu kafariki kwa basi gani?

Nimepata sms asubuhi hii mdogo wangu amefariki kwa ajali ya basi lililokuwa linatokea Dar kwenda Mtwara. Maiti ziko hospital gani, aliyenipigia nimeshindwa hata kumuuliza sehemu ilipotokea ajali na jina la basi.

Hivi sasa simpati kwenye simu, simu ya bwana mdogo tangu jana haipatikani japo mchana akitoka Dar waliwasiliana na dada. Ma rafiki zake walioko Mtwara hata wao wanadai mawasiliano yalikata gafla.

Nisaidieni mlioko huko na tushamtuma dada yetu yuko njiani kwenda huko Mtwara na huku tukielekea stand kuanza safari.

Bwana mdogo!!! Tangulia ndugu yangu
 

Attachments

  • 1445243277681.jpg
    1445243277681.jpg
    55.4 KB · Views: 618
Baraka ni basi litokalo Lindi kwenda Dar na kurudi tena Lindi, haliendi Mtwara. Ni mini bus! R.I.P mdogo wetu!

Mkuu kuna moja ni basi sample ya hizi Yutong
 
Ajal iltokea majira ya saa tisa alasr maeneo ya mto matandu ambapo shughul za ukarabati wa barabarani znafanyika . Chanzo ni mwendo mkal, ambapo gar liliacha njia na kuingia ktk calvat. Daily route ya bus ni dar lindi mjn to nachingwea, awali lilikuwa dar kilwa masoko


Pole sana kwa msiba
 
Pole sana mkuu.

Pole sana Kamanda..

Poleni sana kwa msiba huu ,Mungu awatie nguvu muweze kufanikisha yote katika kumpumzisha katika Nyumba ya milele!

Pole sana mkuu, R I P mwalimu

Pole sana ndugu yangu, Mungu awafariji na kuwatia nguvu, huu ulimwengu siyo mahali salama kabisa kwetu sisi cha kufanya tumche Mungu kwa akili zetu zote, kwa nguvu zetu zote, kwa mioyo yetu yote na kwa roho zetu zote, Mungu ampumzishe ndugu yetu na wote waliofariki katika ajali hii amen

pole sana mkuu kwa msiba huo

pole sn, r i p mwlm tegemeo la vijana.

Poleni Sana

pole sana mkuu

Pole sana mkuu

Dahh Inaumiza Sana Mkuu.....inaumiza sana sana! Pole sana Mkuu...Mungu akupe wepesi katika kipindi hiki kigumu! Mungubail

Mungu awabariki sana ndugu zangu kwa busara zenu. Tawajulisha maiti ikifika.
 
Pole ndugu Mungu akupe moyo wa uvumilivu kipindi chote hiki
 
Duuu!! Mkuu bro amefariki akiwa na basi liitwalo: Baraka Bus, maiti iko Kilwa Kivinje Hospital wamefariki sita!! Nimempata kwenye simu aliyenijulisha ajali.
Jamani so sad! Poleni sana Mkuu. Mungu awape faraja katika wakati huu Mgumu wa majonzi.
 
Duuu!! Mkuu bro amefariki akiwa na basi liitwalo: Baraka Bus, maiti iko Kilwa Kivinje Hospital wamefariki sita!! Nimempata kwenye simu aliyenijulisha ajali.

pole sana mkuu.
Mungu awape wepesi.
 
Ajal iltokea majira ya saa tisa alasr maeneo ya mto matandu ambapo shughul za ukarabati wa barabarani znafanyika . Chanzo ni mwendo mkal, ambapo gar liliacha njia na kuingia ktk calvat. Daily route ya bus ni dar lindi mjn to nachingwea, awali lilikuwa dar kilwa masoko


Pole sana kwa msiba

Maskini!!!!! Liliingia kwenye calvat!!? Mungu alipanga mdogo wangu afariki kwa style hiyo. Mungu ndiye mwamuzi.
 
Pole sana. Kwani sisi ni wamwenyezi mungu na kwake tutarejea sema tu hatujui saa wala muda wa sisi kuondoka na yeye pekee ndiye anayejua kuja kwetu na kuondoka kwetu na wala hatuna hiyana wala kipingamizi. Allah amuweke mahali pema peponi. Pumzika salama mdogo wetu. Amii
 
Back
Top Bottom