Dar: Maandamano makubwa katikati ya Jiji

Dar: Maandamano makubwa katikati ya Jiji

Status
Not open for further replies.
...Mkuu Zogwale ngoja chama yetu CDM iandae maandamano makubwa katika mikoa ifiuatayo Dar, Mwanza, Mbeya, Ruvuma na Tabora ili kuwashinikiza "Nikijiuzulu hamtapata waziri mzembe/goi goi kama mimi" alias Nchimbi, IGP na RPC wa Iringa wajiuzulu kufuatia mauaji mbali mbali yanayoendelea nchini yakiwemo yale ya Mwangosi. Natumai polisi magamba hawatazuka na silaha zao za moto kama walivyofanya jana katika maandamano yaliyofanyika jijini Dar.


Mkuu BAK,
Nakuhakikisha hao hawatapigwa mabomu, Mkuu wa Nchi, IGP Said Mwema, na Kova hawawezi kuwadhuru wenzao. Thubutu ungekuta ni CDM au Wakristu, leo tungepata misiba mingi maana mji wenyewe posta ni kitovu na watu ni wengi!!!! Tanzania haina udini!!!!!! Ha ha ha ha!!!! Haya ni mambo ya awamu ya nne.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu wangu unajiaibisha bure kwa majibu yasiyofanyiwa utafiti japo kiduchu.
Tunaojua historia wala tusingethubutu kusema "PWANI YOTE ILIKUWA INAKALIWA NA WAISLamu, BABU YENU NYERERE NDIO ALIWAVUTA NYIE".
Unafahamu Ukristo ulianzia wapi TZ? Ni Bagamoyo, kisha ukaenda Zanzibar na bara kote.

Na sababu kubwa ni za kijiografia (jinsi walivyokuwa wanakuja kutoka kwao kwa merikebu) na watawala wa kwao (wenyeji wao-wakoloni) waliowakuta wakati wanawasili.

Kwani Waislam ni kabila gani hapa Tanzania? Uislam ni dini ya Waarabu tena Ukristo ni dini ya wazungu iweje leo tunaanza kusahau asili zetu tunajifungamanisha na wageni? Watanzania tuamke tuijenge nchi yetu.
 
Nadhani hakuna haja ya kueleza zaidi, Watz wote leo wameona unafiki, uongo na undumila kuwili wa policcm. Maandamano ya Waisilamu leo hayakuingiliwa kabisa, hayakudhibitiwa wala hayakuwa halali kufuatana na wanachodai polisi kuwa kuna sensa inaendelea.

Lazima Nchimbi atoe maelezo.

usifananishe uislam na cdm! .. uislam siyo chama cha siasa chadema ni chama cha siasa..

waislam hawakutanguliza sms za vitisho slaa alitanguliza

waislam walichagua watu watao control fujo yoyote itakayo tokea... cdm wanapandikiza waanzilishi wa fujo .


 
Kwani Waislam ni kabila gani hapa Tanzania? Uislam ni dini ya Waarabu tena Ukristo ni dini ya wazungu iweje leo tunaanza kusahau asili zetu tunajifungamanisha na wageni? Watanzania tuamke tuijenge nchi yetu.
Mkuu, watu walishazibwa akili hawawezi kufikiria nje ya dini!! Mwarabu na mzungu alituweza na hii ndiyo itatuchelewesha kuendelea. Watu wenye ufahamu wa mambo ya dini ndiyo wa kwanza kuwpotosha watu. Acha tuendelee kusuguana hivyo hivyo, utafika muda wetu utaisha tutawaachia watoto wetu watayamaliza nao wakishindwa watayaacha kwa watoto wao ...Mie nimeamua kutokuhangaika na haya mambo nafanya kile kinachotakiwa nifanye kusaidia wote (muislam, mkristo, hindus, budhist na hao wasiokuwa na dini).
 
Tatizo ni udhaifu. Leo wamefanya dogo, kesho watafanya kubwa.
Amewakubalia leo, atawakatalije kesho?

Tafakari.
 
Penye nia pana njia. Kesho wakristo nao wataandamana, je wataruhusiwa?

Ah kwani wakristo wanaandamana? Askofu si anaenda ikulu kama kwake bana, akisema waachiwe wanaachiwa hakuna pingamizi
 
Ni kweli maandamano yanafanyika kushindikiza kuuachiwa Waislam wenzao waliokamatwa kutokana na kukataa kuandikishwa sensa.

Wanataka waachiwe bila kufuatwa kwa utaratibu wa kisheria?au wanataka serikali iendeshwe kisultani sultani au kiislam islam?
 
Kuwa na heshima wewe mpuuzi, huna hadhi ya kumuona mtume, ata yesu humuoni utabaki kuchorewa picha zake tu ignorant. Huwezi kuona wanawake hapo bcz wanawake wanatakiwa wakae nyumbani, wewe hujui kama mwanaume ndo wa kwenda vitani? Au wewe utakaa ndani umwache mkeo anaenda vitani wewe wavadilisha channel??

Mkuu hao ndio wafuasi wa Chadema wanataka eti Watanzania tuungane tuwape nchi mtu kama huyo mwenye dharau na kejeli dhidi ya dini ya mwenzake kuna haja ya kuungana naye kweli, hawa ndio wanayoialibia Chadema mbele ya jamii ya kiislam.
 
Hao wote wanaofanya maandamano pamoja na familia zao wote hawajaandikishwa sensa.

Ni hasara yao wenyewe na vizazi vyao kwa kuwa baadaye watakuwa wanalalamikia ufinyu wa uduma za kijamii!!!!
 
Wanataka waachiwe bila kufuatwa kwa utaratibu wa kisheria?au wanataka serikali iendeshwe kisultani sultani au kiislam islam?

Kuna sheria gani ambayo inasema usipojiandikishwa sensa ni kosa? Vipi kupiga kutokupiga kura nalo ni kosa au sensa tu?
 
Sasa hiyo sensa imekwisha? Kwa nini wanaandamana tena hapa Dar ndo polisi wapo kibao na bado wamewaacha? Km kweli nchimbi unao ubavu sogelea hao waislamu na vipolisi vyako ndo utaijua nguvu ya Jihadi kwani hapo ni JK,Bilali na raisi wa Zanzibar ndo watatoa matamko.

Hayo matamko ya hawa viongozi watayatolea msikitini au serikalini?mbona wameshindwa kuanzishi mahakama ya kadhi inayogharamiwa na serikali?Mbona wameshindwa kuiwezesha nchi kujiunga na OIC ilihali wenyewe ni viongozi wenye nguvu serikalini?
 
Ni hasara yao wenyewe na vizazi vyao kwa kuwa baadaye watakuwa wanalalamikia ufinyu wa uduma za kijamii!!!!

Kwa hiyo wewe baada kuhesabiwa umepata huduma za jamii? Hongera sana kwa maendeleo.
 
Kuna sheria gani ambayo inasema usipojiandikishwa sensa ni kosa? Vipi kupiga kutokupiga kura nalo ni kosa au sensa tu?
Mkuu fuatilia sheria ya sensa utajua ni kufungu gani kinachofanya kosa hili kuwa la jinai au wasiliana na mkurugenzi wa sensa Hajat Amina Mrisho kwa maelezo zaidi!
 
Kwa hiyo wewe baada kuhesabiwa umepata huduma za jamii? Hongera sana kwa maendeleo.
Maendeleo yatakuja tu mkuu kwa sera nzuri ya serikali ya Magamba!!au wewe leo umeamia CUF au umesahau ile kauli mbiu yetu!
 
Wanaandamana katika mambo yenye kipaumbele kidogo na kuacha yenye kipaumbele kikubwa.

wangeandamana kudai kuongeza majengo ya chuo kikuu cha Waislamu morogoro hawa jamaa wangekuwa mbali sana kielimu. tangu Mkapa alipowapa majengo hayo ya serikali miaka 10 iliyopita hawajaongeza darasa hata moja.
Mkuu watajengaje wakati muda mwingi wanautumia kulalamika tu?
 
Mkuu fuatilia sheria ya sensa utajua ni kufungu gani kinachofanya kosa hili kuwa la jinai au wasiliana na mkurugenzi wa sensa Hajat Amina Mrisho kwa maelezo zaidi!

Mkuu sheria za nchi zipo wazi azikai kwa mtu ni bunge peke yake ndio linatunga sheria za nchi, sheria zote za jinai zinafahamika, sheria za sensa ni upuuzi mtupu ndio maana umeona waliokamatwa wote wameachiwa hakuna sheria ya kuwatia hatiani.
 
Maendeleo yatakuja tu mkuu kwa sera nzuri ya serikali ya Magamba!!au wewe leo umeamia CUF au umesahau ile kauli mbiu yetu!

Kwa hiyo wewe umeamia CCM rasmi baada ya sera nzuri za sensa.
 
Mkuu sheria za nchi zipo wazi azikai kwa mtu ni bunge peke yake ndio linatunga sheria za nchi, sheria zote za jinai zinafahamika, sheria za sensa ni upuuzi mtupu ndio maana umeona waliokamatwa wote wameachiwa hakuna sheria ya kuwatia hatiani.
Sawa mkuu,lakini kwa kuwa nchi hii inaendeshwa kwa utawala wa kisheria kwa nini wasisubili wafikishwe mahakamani na huko ingejulika mbichi na mbivu?badala ya kutumia njia ya mkato?
 
Kwa hiyo wewe umeamia CCM rasmi baada ya sera nzuri za sensa.

Mimi siku zote nipo CCM nakushangaa wewe unavyoamia CUF kwa sababu ya jambo dogo tu la sensa na mbaya zaidi unasahau zile sera zetu nzuri za chama chetu chini ya mwenyekiti wetu mchapakazi JK Kikwete!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom