Dar inawapotezea watu muda

Dar inawapotezea watu muda

Maisha huwa hayana formula ni kama vita flani ambayo ushindi unatokana na aina ya silaha ulizonazo za kumpiga adui (umaskini) na ndio maana unaweza ukakaa Dar ukafeli na ukarudi mkoani ukatusua na mwingine anatoka Kilwa Kivunje anakwenda Dar anatua vilevile kutokana na kile kilichompelea Dar. Au mwingine anatoka Dar anarudi mkoani hali inakuwa ile ile kama ilivyokuwa Dar alafu anashuhudia watu wanatoka vijijini wanatusua waati yeye yupo palepale
 
Nimekuuliza tu hio takwimu yako umeipata wapi? Ukinipa mfano wa huyo kibarua ndio unawakilisha wakazi wote wa Dar? Ni sawa na mtu atumie mfano wa Bakhressa kusema Dar au Tz watu wanamaisha mazuri sana.
Hapo nimejaribu kuwazoom raia wa kitaa ninao waona mkuu
 
Nilipomaliza mafunzo yangu ya kininja nilitamani kurudishwa Dar ili kiwe kituo changu cha kazi bahati mbaya sikurudishwa Dar nikaletwa mkoa unaolima mchele aisee huku nimejikuta nafaidi fursa nyingi mno tena ukija huku kijana uliepikwa na jiji la Dar huwezi kuteseka.
 
Nilipomaliza mafunzo yangu ya kininja nilitamani kurudishwa Dar ili kiwe kituo changu cha kazi bahati mbaya sikurudishwa Dar nikaletwa mkoa unaolima mchele aisee huku nimejikuta nafaidi fursa nyingi mno tena ukija huku kijana uliepikwa na jiji la Dar huwezi kuteseka.
Dar ni chuo,maisha yana changamoto sana
 
Asee hilo swali bado sijapata jibu lakini nawaona wanaishi ila naona siku zote mtu huishi maisha yake kuendana na kipato chake
Watu wote hawawezi kuwa na kipato sawa.Hata mikoa vingine kupo hivihivi,uniambie wale wanaofanya kiwanda cha Tumbaku Alliance Morogoro wanalipwa shilingi ngap?
 
Watu wote hawawezi kuwa na kipato sawa.Hata mikoa vingine kupo hivihivi,uniambie wale wanaofanya kiwanda cha Tumbaku Alliance Morogoro wanalipwa shilingi ngap?
Mkuu kubali kataa asilimia kubwa ya wafanyakazi wa viwandani wanalipwa kiduchu wanafanya kazi kwa dhiki tu ili siku ziende na hawana pa kukimbilia
 
Mkuu kubali kataa asilimia kubwa ya wafanyakazi wa viwandani wanalipwa kiduchu wanafanya kazi kwa dhiki tu ili siku ziende na hawana pa kukimbilia
Hiyo ipo kote mkuu na ninakubaliana na wewe kuwa wanalipwa kiduchu.Na hiyo hela Huwa haitoshi hata kufika mwisho wa mwezi lakini maajabu hao watu wanavaa ,wamepanga,na wanacheza kitu inaitwa mchezo Kwa wadada.Haiwezekani watu wote kutoboa iwe Dar au mkoani
 
Penye watu wengi kuna fursa,pesa na matumizi mengi ya pesa. Katika maeneo haya watu wengi hishindana kuona na kuanzisha fursa ili kuendana mtindo wa maisha wa eneo hilo. Wengi wanaotoka nje ya dar hushangaa jinsi vijana wa dar wanaopanga kweny nyumba nzuri ambazo mkoani ni za viongozi na taasisi. Huishia kushangaa acces ya nguo nzuri kwa bei nzuri na vitu vingine vizuri. Kuishi dar unapaswa kuwa mbunifu, mchapakazi na jasiri. Wanaokimbia dar lazima watatunga vijisababu ili kujifariji kwa kushindwa kwao. Kuishi dar tu ukawa na uwezo wa kulipia bills za maisha sio kazi rahisi. Ndo maana tukirudi mikoani tunaheshimika kuliko nyinyi mliorudi na kunyoosha mikono mmeshindwa.
 
**** ukweli flan kwa mtoa mada japo anabezwa sana ,

Binafsi nimezaliwa dar na kuishi hapo kwa zaidi ya miaka 30, mwaka 2015 nikajaribu kwenda mkoani kutafuta fursa , tokea muda huo naichukia sana dar , nikaja kujua kuwa nguvu niliyotumia kutafuta pesa na maisha kwa miaka vote hiyo kama ningekuwa mkoani nadhan ningekuwa mbali sana.

Hao wanaosema kuwa kukaa dar ni uanaume au ujanja , nadhan ni mob psychology, maendeleo hayaji kwa group , ni individual kind of a thing, kila mmoja anaangalia anaweza nn na si wenzake wanataka afanye nini. Just because bakhresa anakaa dar , haimaanishi kuwa na wewe unaeza kuwa kama yeye.
 
Wewe fanya maisha popote penye fursa...nani alikwambia Dar ndo kila kitu?Kama umepata fursa mkoani ni jambo la kheri..na waliotobolea Dar ni jambo la kheri pia.....Sasa mfano wewe unalima mpunga unatarajia uishi Dar kufanya nini?wafugaji etc...
Pambana na hali yako tu bila kelele..mwisho wa siku familia isonge mbele...
 
Nionyeshe mkoa ambao watu wake wanaishi maisha matamu nikuoneshe saiti zenye dhiki katika mkoa huo.
Kwa sasa mimi ni mkazi wa Mwanza , huku pia kuna maeneo ya walalahoi lakini Dar imezidi sasa nionyeshe maeneo ya ajabu ya mwanza halafu tulinganishe na ya Dar
 
**** ukweli flan kwa mtoa mada japo anabezwa sana ,

Binafsi nimezaliwa dar na kuishi hapo kwa zaidi ya miaka 30, mwaka 2015 nikajaribu kwenda mkoani kutafuta fursa , tokea muda huo naichukia sana dar , nikaja kujua kuwa nguvu niliyotumia kutafuta pesa na maisha kwa miaka vote hiyo kama ningekuwa mkoani nadhan ningekuwa mbali sana.

Hao wanaosema kuwa kukaa dar ni uanaume au ujanja , nadhan ni mob psychology, maendeleo hayaji kwa group , ni individual kind of a thing, kila mmoja anaangalia anaweza nn na si wenzake wanataka afanye nini. Just because bakhresa anakaa dar , haimaanishi kuwa na wewe unaeza kuwa kama yeye.
Kwa hiyo watu wote wahame Dar?
 
Back
Top Bottom