Dar inawapotezea watu muda

Dar inawapotezea watu muda

Duh...kwahio huko mkoani wote mnaishi maisha kama peponi? Hebu tafuta ripori ya NBS ujionee.
Jamaa wanajifariji kweli wanahisi mkoani Kila mtu katoboa wakati sehemu kibao watu wanachangia maji/Dimbwi na Ng'ombe.
Ndiko ambako utakuta wananchi wake Kila siku wanaomba msaada serikali iwasaidie kujenga choo cha zahanati ya Kijiji.Wakitaka kupitisha harambee unakuta vikao wanakuja kufanyia Dar
 
Kwa mujibu wa NBS wakazi wa Dar asilimia kubwa wana unafuu wa maisha kulinganisha na mikoa yote Tanzania. Hizi ni takwimu hizo nyingine ni porojo tu na ndio maana watu wanaongoza kukimbilia Dar na si kinyume chake.
Na Kwa wale waliokuwa wanasikiliza vizuri walimu wao darasani kwenye topic ya migration moja ya sababu kubwa ya migration. Ni watu kutafuta unafuu wa maisha na huduma za binadamu Sasa tujiulize watu wanamigrate kwenda wapi sanasana,kama sio kuja Dar?
 
Hapa tunachanganya vitu viwili kwa wakati mmoja,,mtu anayetafuta maisha DAR,,wakati huo huo wazazi wake wanamijengo dar,,na mtu anayetoka mkoani,,kuja kutafuta,,,,huku wazazi wake wakiwa hawana asset yoyote dar,,hapo kuna tofauti kubwa ya maumivu yautafutaji,,,,,,chamsingi,,nikutokukata tamaaa,,maisha kokote
 
Sijasema wote, ila wengi wao. Cha msingi fanya unachopenda utafanikiwa, yatawale mazingira uliyopo.
Hiyo ndo point kuwa maisha ni popote ambapo wewe unaona unapamudu.Dar kuna matajiri Dar kuna maskini Dar kuna Raha Dar kuna shida zote.Dar pa rahisi Dar pagumu pia,kazi kichwani mwako.Hiyo mikoa ambayo maisha ni mepesi sehemu zote kuzuri tu na kufanikiwa nje nje sijui ni ipi
 
Nimeishi Dar kwa takribani miaka 13,hakuna cha maana nilichokifanya,ila niliporudi mkoani ndani ya mwaka mmoja maisha yalikuwa tofauti kabisa. Niliacha kufikiria mawazo ya muda mfupi mfano nitakula nini kesho,kodi itakuaje na mengineyo ya kipuuzi..

Sasa hivi nawaza itakuaje baada ya mwaka au miaka kumi nitakuwa wapi. Hilo Dar linaishia kwenye maneno tu,maisha ya Dar yanamfanya mtu awe mtumwa,wana wengi wanaogopa kurudi mahome kwao kwa kuhisi watadharaulika.

Acha fikra potovu rudi ubadili namna ya kufikiri,huku mambo yanaenda ukitia nia.
Ukijua kwann maisha ya huko ulipo yamekuwa rahisi utakuja na mrejesho wa kuishukuru Dar kwa kukupa elimu ya miaka mitatu
 
Hapa tunachanganya vitu viwili kwa wakati mmoja,,mtu anayetafuta maisha DAR,,wakati huo huo wazazi wake wanamijengo dar,,na mtu anayetoka mkoani,,kuja kutafuta,,,,huku wazazi wake wakiwa hawana asset yoyote dar,,hapo kuna tofauti kubwa ya maumivu yautafutaji,,,,,,chamsingi,,nikutokukata tamaaa,,maisha kokote
Kwenye kutafuta kuna hitaji kujitoa mhanga
 
Kwa mujibu wa NBS wakazi wa Dar asilimia kubwa wana unafuu wa maisha kulinganisha na mikoa yote Tanzania. Hizi ni takwimu hizo nyingine ni porojo tu na ndio maana watu wanaongoza kukimbilia Dar na si kinyume chake.
Hyo ripoti waifanye na mwaka huu!! Inaweza kuwa vice versa
 
Siyo kwamba Mwanza hakuna Sehemu za changanyikeni,naamini zipo.Tofauti ni population,sehemu yenye population kubwa haiwezi lingana na sehemu population ndogo.Ndiyo maana unalinganisha Tandale tu lkn hujaweza kwenda linganisha zile zenye ubora za Dar maana unajua kabisa kuwa Mwanza itakuwa nyuma.Igogo,Mabaytini,Nyanshana,Iseni,Nyakato Sokoni, ni kwa kisasa Kwa kadiri yako.Unapolinganisha Kwa ubaya linganisha na Kwa uzuri pia.Ni kama mimi niseme Kijijini kwetu hakuna sehemu ya Changanyikeni kama Tandale,sasa itakwepoje wakati kule ni kijijini? Huko Tandale unakokuona Uswahilini ndio sehemu expensive zijazo,
Hahahaaa eti sehemu expensive zijazo , a hell on Earth !
 
Binafsi mi nimeondoka dar mwaka jana mwanzoni na sikuwa na mpango wa kuishi mkoani!! Nilikuwa nimeenda kupiga ishu flani then nigeuze , lkn kadri nilivyozidi kukaa nikashawishika kuwa kuna possibility ya kuishi mkoani na maisha yakawa mazuri tu! Now nipo mwanza na nishahamisha makazi ya kudumu na sina mpango wa kurudi dar tena!!!
 
Dar kwa fursa sawa kwa kuishi No. Naamini kungekua kuna usafiri affordable na realible lets say bullet train kutokea Dar to Arusha au usafiri wa ndege usingekua anasa kwamba hata mtu wa kipato cha kati angeweza kuafford watu wengi wasingeishi Dar.
 
Back
Top Bottom