Dar inawapotezea watu muda

Boss unapoteza muda. Niliacha kujadiliana na nilipogundua najadiliana na watu wanaona tzs 100k per day ndio wamepatia maisha.
 
Ukiegemea kwenye hesabu za probability, uwezekano wa kutoboa ukiwa Dar ni mkubwa kuliko mkoani. Magari na majumba mazuri yako Dar. Mkoani mtu anayetembelea shangingi ni mkuu wa mkoa pekee, whats ur chance of getting one?
Bro wangu yuko mkoa sio mkuu wa mkoa but anamiliki shangingi.
 
Boss unapoteza muda. Niliacha kujadiliana na nilipogundua najadiliana na watu wanaona tzs 100k per day ndio wamepatia maisha.
Doh !!! Kumbe !!!!!
Mi nafanya assumption kuwa mwenzetu upo juu sana kimaisha ie umeyapatia hapo bongo!

By the time naikimbia Dar na kuona napoteza muda hapo, nimeacha nyumba tatu, ambazo valuation ya mwaka Jana hakuna iliyopungua mil 70, shamba hekari mbili huko mpigi magoe , pamoja na Mitsubishi canter mbili za tani tatu ambazo mpaka usiku huu naandika hii thread zinawabebea maji matycoon wa Dar .
Hicho kipato cha laki ambacho wanibeza nacho kwangu mimi kilikuwa ndo kipato changu kwa siku miaka ya 2008-9 hadi 2010,

Just because you are late to the party... It doesn't mean that the party hasn't started yet!
 
Huu Uzi ni maalum kwa waliofanikiwa wakiwa dar na walio shindwa wakiwa dar sasa ngoja niendelee kufuatilia mjadala. Mahakaman anashinda mwenye uwezo wa kujitetea zaidi ya mwenzie. Akishinda wa dar nitatoka mkoan na kwenda huko akishinda aliyerudi home basi ntabaki niliko. Mechi inaendelea
 
achana na huyo anaishi kwa shangazi huyo hajui chochote mbafu huyo
 
Boss unapoteza muda. Niliacha kujadiliana na nilipogundua najadiliana na watu wanaona tzs 100k per day ndio wamepatia maisha.
Unaweza kukuta mkoa mzima watu watatu au wanne pekee wanaingiza 100k per day.
 
Na dunia yenye nchi zilizoendelea wakulima wachache wanalisha nchi nzima.

Nyie mnaoenda kujazana mikoani mbona hatuoni surplus ya uzalishaji hadi muuze nje? Au ndo kuishia kufungua Retail Shop?

Nje ya kilimo (tena cha jembe la mkono na kutegemea mvua) hakuna kitu watu wa mkoani wanamzidi mtu wa dar.

Narudia tena kusema na kusisitiza. Wakulima wakubwa na wanaofaidika na kilimo wanaishi dar (labda na majiji mengine kama mwanza na arusha). Nyie mliobaki mnasindikiza maisha.
 
Upo nyuma sana....hakuna mkulima ata mmoja anayelima kilimo biashara anayetumia jembe la mkono, hapo umebugi. Sehem zote wanazolima kibiashara kuna schemes. Ukiona wapo wanaolima kwa jembe la mkono ujue hao wanalima kwa ajili ya chakula cha nyumban tu. Siku hizi kuna hadi magreen house ya bei ndogo kuanzia milioni moja mikoan yapo kibao. Wew endelea kukalili kile kilimo alicholima babu yako zaman ukazan hadi sasa ni mwendo huo...tembea uone. Siku hizi hawasubir mvua asee na kilimo ni mashine kuanzia mwanzo hadi kuvuna coz kila mtu anakimbizana na mda mzee
 

Kwa hiyo hawa wafanyabiashara/matajiri wa huko mikoani wote ni wakulima/bodaboda sio?
 

Mkuu unapoteza muda tu kuelewesha watu,hapo vijana wa dar wanachojua ni kununua vigari used tena hivi vi bmw 3 series/benz c class za miaka ya 2002 huko+kujua clubs mpya hapo mjini na akijitahidi sana ni kununua kiwanja labda kule Goba kwake hayo ni maendeleo makubwa balaa.

Unavyowaambia una nyumba 3 hapo mjini,viwanja,canter wanaona kama ni uongo flani sababu wao kwao hawawezi kuvipata na waambie wataje assets zao sasa utashangaa wanakutajia magorofa/magari ya ma tajiri wa hapo mjini dar.
 

Mkuu siku hizi umeacha kulima kile kilimo cha maembe kule Tanga ulichokua unalalamika bakhresa anawazingua kununua maembe mpk yanaharibika nje ya geti lake pale kiwandani kwake?
 
Kwani huyaoni maghorofa yaliyojazana Dar? Unadhani yote yanamilikiwa na serikali?
Hapana mengine ni ya kwako. Nikipita tandika , kigogo na mwansnyamala
Dar Dar is complecated. Sii rahisi kama unavoandika hapa.
Dar kulala tajiri na kuamka maskini ni rahisi sana.
 
Kawaida kabisa kwa mkoani...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…