Wakuu,
Habari hii imesambaa kwenye mitandao ya kijamii, kwamba huyu Daktari baada ya kumkosoa Rais wa Burkina Faso Kpt. Ibrahim Traore kuhusu kushindwa kupambana na magaidi, alikamatwa, akavishwa magwanda kwenda kupambana na magaidi hao kwakuwa yeye analiweza suala hilo kuliko jeshi.
Hii taarifa ni ya kweli au tunapigwa kamba tu?
Habari hii imesambaa kwenye mitandao ya kijamii, kwamba huyu Daktari baada ya kumkosoa Rais wa Burkina Faso Kpt. Ibrahim Traore kuhusu kushindwa kupambana na magaidi, alikamatwa, akavishwa magwanda kwenda kupambana na magaidi hao kwakuwa yeye analiweza suala hilo kuliko jeshi.
Hii taarifa ni ya kweli au tunapigwa kamba tu?
- Tunachokijua
- Kapteni Ibrahim Traore ni Rais wa Sasa wa Burkina Faso. Rais huyu aliingia madarakani mnamo Septemba 30, 2022 baada ya kufanya mapinduzi ya kijeshi dhidi ya Serikali iliyokuwa madarakani wakati huo.
Tangu kuingia madarakani Nchini Burkina Faso, yameibuka makundi mbalimbali pinzani ndani na nje ya yakipinga mambo mbalimbali katika Utawala wa Rais Ibrahim Traore.
Nchi nyingi zinapinga serikari ya Rais huyu hasa sababu ya kuingia madarakani kwa njia ya mapinduzi. Ndani ya nchi yake baadhi ya wadau wanapinga namna mambo mbalimbali yanavyoendeshwa ndani ya nchi hiyo ikiwamo namna Rais huyu anavyoongoza mapambano ya vikosi vyake dhidi ya magaidi.
Sakata Daktari Kumpinga Rais
Kumekuwapo picha mbili zinasambaa katika mitandao mbalimbali ikiripoti Daktari wa Burkina Faso aliyemkosoa Rais kuhusu anavyopambana na Ugaidi kupelekwa kwenye Jeshi la Ulinzi.
Picha ya kwanza inamuonesha mwanaume huyo akiwa ndani ya mavazi ya kidaktari huku nyingine akiwa katika mavazi ya kijeshi ameshika silaha kama ilivyoletwa na mleta mada hapo juu.
Mathalani Blogu ya Spectacle inaandika:
Mtaalamu wa Afya Daktari Ahmed Diallo alikuwa akikosoa kwa uwazi Rais Kapteni Ibrahim Traoré, akijiuliza uwezo wake wa kupambana kwa ufanisi na tishio linaloendelea la ugaidi ndani ya nchi.
Serikali ya nchi hiyo imemjibu kwa vitendo kwa kumpa mafunzo ya kijeshi Kisha kumfanya mtu anayesimama mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya Ugaidi yanayoendelea.
Nao, Nairaland hawatofaitiani na Blogu ya Spectacle ambao pia wanaandika:
Daktari wa matibabu wa Burkina Faso ambaye alikosoa Rais wa Burkina Faso, Kapteni Ibrahim Traoré, amepelekwa mstari wa mbele.
Daktari huyo aliikosoa vikali serikali ya Traoré kwa jinsi jeshi lilivyokuwa likishughulikia hali ya kutokuwa na usalama nchini, hivyo rais alimkamata na kumtia katika jeshi la ulinzi.
Kwa mujibu wa mtaalamu wa usalama, Zagazola, Traoré alimpeleka daktari huyo mstari wa mbele ili aone kwa karibu ukweli wa ugaidi.
Ukweli wake upoje?
Baada ya kufuatilia suala hili kwa undani wake, JamiiForums imekosa ushahidi mahsusi kuthibitsha madai haya ambayo hayajaandikwa na chombo chochote cha kimataifa wala kutolewa kauli na mamlaka rasmi kutoka Burkina Faso.
Hata hivyo, ni muhimu kuufahamisha umma kuwa picha zinazooneshwa ni halisi, na daktari husika yupo. Isipokuwa sababu za kwenda vitani sio kama zinavyobainishwa mitandaoni.
Kwa mujibu wa Waziri wa Habari na Mawasiliano wa nchi hiyo, Jean Emmanuel Ouédraogo, ni wajibu wa kila mwananchi wa Burkina Faso kuhakikisha kuwa nchi hiyo inakuwa salama, pia ni jambo la kujivunia kusimama mstari wa mbele kupigania dhidi ya magaidi.
Vyanzo vya kuaminika vinabainisha kuwa kama ilivyo kwa wananchi wengine walio mstari wa mbele kukabiliana na magaidi nchini humo, daktari huyu pia alijiunga na jeshi kama sehemu ya kuilinda nchi yake na sio kwa kuwa alimkosoa Rais.
Aidha, kuna tofauti kubwa ya majina ambapo baadhi ya vyanzo vinamtaja kama Daktari Ahmed Diallo huku vingine vikimtaja kama Daktari Arouna Loure.
Katika hatua nyingine, JamiiForums haijapata andiko, sauti au ujumbe wowote wa daktari huyu akiituhumu Serikali na Rais wa nchi hiyo kushindwa kushughulikia kikamilifu suala la magaidi.