Kwanza kabisa uache wivu. Naona wanaume wengi wa kibongo wanachukia sana wakiona mabinti wa kiafrika wanaopenda wazungu. Kwa nini? Kufanya uamuzi ni haki ya kila mtu.
Pili ukitaka kujua kwa nini wadada hawapendi wabongo, ujue ni kwa sababu ya vifuatavyo...
1) Kwa ujumla wanaume wa kizungu hawana tabia za nyumba ndogo, wanapenda kuridhika na wake zao
2) Wanaume wa kizungu hawana tabia ya kutelekeza familia zao na watoto wao. Wabongo ndo ni balaa, wanazaa watoto ovyo halafu hawataki hata kuwatambua. Tabia chafu kabisa
3) Wanaume wa kizungu hawana tabia za ukatili, wanawaheshimu wake zao. Mbongo anaona ni haki kabisa kupiga mke
4) Wanaume wa kizungu wanaona kuna usawa kati ya jinsia zote. Wabongo wanawafanyia wake zao kama ni housegirl, wanaenda kukaa kwenye baa mpaka usiku na wanarudi nyumbani kwa ajili ya kula chakula na kulala tu
5) Kwa ubaya wadada wengi wanafikiri kila mzungu anazo hela nyingi. Nadhani unajua siku hizi wasichana wengi hawataki upendo, wanataka pesa tu
Najua nitatukanwa lakini sijali, wanaume wetu wakiendelea na tabia zao za kijinga wasichana wataendelea kuwakimbia.