Asante kiongoziHilo mbona liko wazi? Huyo binti hata kama angetembea kwa miguu hafai kuwa mke, ameonyesha daliliza kuwa mwenye kiburi na majivuno. Hakuna mume atavumilia hayo, labda wale wanaooa kwa ajili ya mali. Mwanamke wa sifa hizo hata akianza kwenda beach akajichanganya na watu maeneo mbali mbali sana ataambulia mimba kama ana uzazi. Mke mwema hatafuti wanaume bali anatafutwa.
Samahani kwa kutumia neno kuzurura, lakini maana yangu ni hii, unaposema binti ajifunze kutoka ili aonekane na wanaume ni kujaribu kujiweka sokoni. Hii ni mbinu inayotumiwa na makahaba pia, ingawa yaweza kuonekana kwamba binti atakuwa na nia njema. Sijaelewa bado mantiki ya huyo mchungaji , lakini kwa mtazamo wangu vitu vinavyovuta hisia za mwanamume anayetafuta ndoa ni pamoja na:
1. Usafi binafsi
2. Mwonekano mzuri na mavazi ya staha.
3. Heshima na adabu kwa watu wa rika zote, mfano awapo kwenye jamii jinsi anavyozungumza na watu mbalimbali, anavyowachukulia wengine, aina ya mazungumzo anayofanya yawe yenye busara za mke, sio mtazamo wa kahaba. Kuna tabia ya binti akitongozwa kuporomosha matusi kama defensive mechanism. Jambo hili ni dalili ya tabia mbaya na mwanamke anayetenda hivi atafanya haya haya kwa mumewe.
3. Aina ya marafiki. Binti akiwa na marafiki wenye sifa mbaya hawezi kukwepa aibu yao. Atahesabiwa kati yao kwa sababu hata aina ya ushauri anaoupanda kwenye ubongo utafuatana na maisha ya hao rafiki zake.
4. Familia aliyotoka. Kama binti anatoka kwenye familia yenye sifa mbaya ni vigumu sana kupata mchumba. Malezi ya binti hufanywa kwa kiasi kikubwa na mama, hivyo kama mama hana sifa njema ni nadra sana kwa watoto wake kuwa tofauti.
Hizi ni baadhi tu ya sifa mabazo kijana yeyote mwenye nia ya mke akizigundua kwa binti, hakika atavutwa nazo na kuamua kumfuatilia jinsi anavyoishi na familia yake, ambapo huko atajua namna gani anayamudu maisha familia.
Mojawapo ya sifa mbaya kabisa ya mke ni kutokujua kupika, na hii imepelekea wanaume wengi kula mahotelini kuliko majumbani. What a shame!!
Mwanamke mwenye sifa hizi hahitaji kujitangaza bali atafuatwa kama nyuki wafuatavyo asali. Atakuwa na wakati mgumu kuamua yupi ni mume sahihi kwa sababu wengi watamtamani.
Ni mtazamo wangu
ninapata maarifa makubwa sana