KENZY
JF-Expert Member
- Dec 27, 2015
- 26,213
- 56,849
Kaanza mapema mno na hakika anaogopa upepo unaomtikisa!,Tena zaidi anaogopa upepo wakaka yake maana inaonekana upepo wa kaka ni mkali zaidi unampa shida,madira yake yanapeperuka huku na kule!.
Hakika dada hawezi kuvaa viatu vya kaka vimemshinda ndio maana ameanza kuviponda!.. niwaambieni yule mzazi wa kijani aliemzaa dada na kaka sasahivi ameharibikiwa kwani hawana sera tena zaidi ya kupondana wenyewe!,Moto unawaka tena moto wakijani.
Dada unamlaumu kaka kwani hujui sahivi hayupo..? Wakati akiwepo wewe si ulikuwa msaidizi wake..! Jua Kila anguko lake ni lako pia!,picha yake ilikuwa kubwa nawe tengeneza yakwako pasipo kukanyaga picha ya kaka! Adui zako sio waliokufa bali waliohai!.
Umefanya upatanisho na adui zako kwa kuingia mtegoni sasa umekosa adui umeanza kugusa visivyojitetea!. Sasa ni hivi kama alivyopita nawe utapita ila fahamu haya,hata Kama leo Kaka atasemwa vibaya ila hataacha kukumbukwa kwani toka katika ukuaji wake kazi zake nzuri zinafahamika. Asingeweza kukaa miaka kumi na bwana yule kama asingefanya vyema!. Ukweli huonekana dhahiri dada.
Ulipo ndipo kipimo kilipo sasa ni muda wa kufanya kazi na sio masimango,uzuri wa mtu hauji kwa kumponda mwengine tena ambae hawezi kusema!. wanaokupigia makofi hivi sasa wanakudanganya maana usitegemee uliozaliwanao wakakusaliti wakati wanajua umeshika sufuria la pilau na wanataka wazijaze sahani zao!. Tena wanataka ulegeze mikono ili wazijaze vizuri! Kaka yako alikaza mikono kwani alijua tabia za ndugu zake!.
Sisi unaotuona jamaa wa koo nyengine ndio tunaolima na kujaza wali hilo sufuria!,piganeni,gombanieni lakini msijisahau tunawaona na wewe ndio tunakuona vizuri zaidi.
Nikukumbushe ule muda bado haujafika,kazi ya mikono yako itakuja kuhesabika kushinda kazi ya mdomo.
Hakika dada hawezi kuvaa viatu vya kaka vimemshinda ndio maana ameanza kuviponda!.. niwaambieni yule mzazi wa kijani aliemzaa dada na kaka sasahivi ameharibikiwa kwani hawana sera tena zaidi ya kupondana wenyewe!,Moto unawaka tena moto wakijani.
Dada unamlaumu kaka kwani hujui sahivi hayupo..? Wakati akiwepo wewe si ulikuwa msaidizi wake..! Jua Kila anguko lake ni lako pia!,picha yake ilikuwa kubwa nawe tengeneza yakwako pasipo kukanyaga picha ya kaka! Adui zako sio waliokufa bali waliohai!.
Umefanya upatanisho na adui zako kwa kuingia mtegoni sasa umekosa adui umeanza kugusa visivyojitetea!. Sasa ni hivi kama alivyopita nawe utapita ila fahamu haya,hata Kama leo Kaka atasemwa vibaya ila hataacha kukumbukwa kwani toka katika ukuaji wake kazi zake nzuri zinafahamika. Asingeweza kukaa miaka kumi na bwana yule kama asingefanya vyema!. Ukweli huonekana dhahiri dada.
Ulipo ndipo kipimo kilipo sasa ni muda wa kufanya kazi na sio masimango,uzuri wa mtu hauji kwa kumponda mwengine tena ambae hawezi kusema!. wanaokupigia makofi hivi sasa wanakudanganya maana usitegemee uliozaliwanao wakakusaliti wakati wanajua umeshika sufuria la pilau na wanataka wazijaze sahani zao!. Tena wanataka ulegeze mikono ili wazijaze vizuri! Kaka yako alikaza mikono kwani alijua tabia za ndugu zake!.
Sisi unaotuona jamaa wa koo nyengine ndio tunaolima na kujaza wali hilo sufuria!,piganeni,gombanieni lakini msijisahau tunawaona na wewe ndio tunakuona vizuri zaidi.
Nikukumbushe ule muda bado haujafika,kazi ya mikono yako itakuja kuhesabika kushinda kazi ya mdomo.