Em jifunze kupitia kwangu,
Nina mchumba wangu tayari nimemtolea posa kipindi anamimba ya miezi mitatu hivyo najulikana kwa baadhi ya ndugu zake ila sasa kishajifungua na mtoto ana mwaka na miezi mitano, sijamuoa sababu ni mjeuri na kiburi pia anajiona ananipelekesha sababu mimi huwa napenda kutumia busara, ila kuna siku nilimwonyesha jinsi nilivyo, aliniaga anataka kwenda kusalimia ndugu zake na angerudi siku ya pili,
Nikaenda nae mpaka kwa Bibi yake MBande ndani ndani hukooooo
Kisha nikageuza nikamwambia kesho awahi kurudi (hapo kwenye smartphone yake nahack mawasiliano yake yote)
Kesho yake nikawa nawasiliana nae mpaka saa tisa alasiri, kufika saa kumi ikawa nikipiga simu anapokea jamaa nikamuuliza wewe unayepokea hiyo simu ni nani kwake akajibu kaka yake, nikaendelea kusumbua baadae akaniblock, nikapiga kwa namba nyingine akapokea nikamwambia mpe mwenye simu niongee nae akanijibu hayupo, nikamuuliza alipo nikajibiwa yupo kwa mjomba, bahati mbaya mjomba wake simfahamu nikampigia simu mdogo wake wa kike ye akasema hajaonana nae, nikamwambia anipe namba za mjomba wake akasema ye hana,
Nikatulia nikawa nafikiria cha kumfanya akirudi, nikapiga simu mpaka kwao Tanga huko, nikawaambia ujinga alioufanya binti yao wakanijibu wanamtafuta kwenye simu, nikapiga kimya, kufika saa mbili anaingia home kakuta nimekasirika,
Swali la kwanza, "nahitaji kumjua uliyempa simu kisha akawa ananiblock ni nani?" Jibu, mdogo wake
Swali la pili, " kwa nini umuachie yeye simu?" Akajibu nilimpa akaniwekee chaji kisha alipoipeleka umeme ulikuwa umekatika,
Nikamuuliza kwa nini usiingeenda nayo kwa mjomba wako ukachajie huko? Akajibu huko hakuna umeme,
Nikamuuliza kwa nini umechelewa kurudi wakati jana nilikwambia uwahi? Akajibu nilicheewa kwa bibi tulikua tunamsaidia kuchota maji, nikamjibu OKAY, mara nyingi nikitoa hili jibu ye huwa anajuwa namaanisha nini na anajua lazima kuna kitu nataka kumfanyia
Hapo nimefuatilia mawasiliano yake tayari sikuona simu yoyote ile zaidi ya mjomba wake aliyembipu na mdogo wake wa kike maana hata maongezi walikuwa wakisalimiana tu,
Pia huyu ni mshamba hajui maswala ya technolojia maana kuacha nafasi tu kati ya neno na neno kwenye msg alikuwa hajui ndo nimemfundisha mimi,
Pia sa hivi ndo namfundisha na kutumia Laptop
Nilishawahi kufuma text zake akijaribu kuchepuka nikampiga biti nikamwambia chochote utakachokifanya hata uwe wapi mimi lazima nitajua tu
MPAKA HII LEO ANAJUA SIMUAMINI NA HUWA ANANIAMBIA KABISA KWAMBA MIMI SIMUAMINI NAMI NINAMJIBU HAITATOKEA HATA SIKU MOJA NIKAKUAMINI
Huyo wako ulipaswa kumzukia hadi kwa huyo wifi yake sijui uhakikishe kama kafika au la
Pia mwanamke si wa kumwamini hata siku moja
KAMWE MWANAUME HAWEZI KUWA MALAYA