sinza pazuri
JF-Expert Member
- Aug 16, 2014
- 2,568
- 7,428
Msanii wa kizazi cha leo na kesho aliyetambulishwa recently na lebo namba moja Africa ya WCB Wasafi.
Kwa jina anaitwa D Voice aka Jini aka London Boy au Temeke Boy.
Huyu ndio future ya muziki wa bongo kwa ujumla. Ndio anaenda kuibeba mabegani industry ya muziki wa bongo ni suala la muda tu.
Anakipaji kikubwa sana cha kuimba ana vocal hadimu mno kama unamsikia Issa Matona alafu kama unamsikia Misambano alafu kama unamsikia TX Moshi kwa mbali kama Kassim Mganga.
Anaweza imba kila aina ya muziki lakini nguzo yake kubwa ni muziki wa pwani haswa singeli na lebo inajaribu kutafuta biashara ya singeli nje ya mipaka so dogo atarajie kutembea sana kulitafuta tobo.
Dogo anaandika sana, ameshaandika hitsongs nyingi za singeli za kina mzee wa bwax kina meja kunta na mabongofleva wengine kibao. Ukisikiliza album yake utasikia skills za uhandishi uloshiba na fleva.
Ana star look kitu ambacho ni muhim sana kwenye sanaa na hajapoa kash kash za showbiz anaziweza ni ishu ya muda tu. Umri wake pia ni mdogo kuendana na walaji wakuu wa muziki wa sasa.
Kila la heri mdogo wetu nakutakia mafanikio katika safari yako ya kuwa big supastaa duniani.
Nakushauri tu endelea kuonesha nidhamu kwa kila mtu na kubwa uache tabia yako ya mishangazi ushajipata sasa.
Bongofleva tumepata zawadi kubwa sana, shukran sana kwa Diamond Platnumz na pia kwa Zuchu kwa kuiona hii almasi kwenye mchanga.