Chama cha walimu Tanzania ni chama cha kifisadi kisichokuwa na dhamira ya dhati kuwakomboa walimu. kimetumia zaidi ya Milioni 240 kuitisha mgomo feki kwa kuwafanya Walimu au watanzania ni wapumbavu. Nasema hayo kwa sababu zifuatazo.
1. Wanadai mishara iongezwe kwa 100%, posho walipwe 50%, posho ya mazingiza magumu iwe 30%.
NB: Hii maana yake ni kuwa mwalimu mwenye basic salary ya Tsh. 700,000/= alipwe mshahara mpya wa Tsh. 1,750,000/= [(yaani 700,000/= x 2 = 1,400,000 + 50%(350,000) = 1,750,000]. is it possible?
Kwa maana nyingine ni kuwa, serikali iandae bajeti yenye uwezo wa kuajiri walimu wapya kwa idadi ya walimu waliopo tanzania kwa sasa, hapo ndio itakuwa na uwezo wa kuwatekelezea walimu hao madai yao. Is it possible or just a day dream of CWT?
2. Wametoa Tsh. 1,500,000 kwa wilaya zote za tanzania (Wilaya 134 x 1,500,000/-) = Milioni mia mbili na kumi + Tsh. 1,500,000/= kwa kila CWT Mkoa (kwa mikoa 24)....maana yake hapo ni : Milioni 36; kwa ukijumlisha : MIL:210 + MIL. 36 = MIL. 246. Pesa hizo zote wamesema zitumike katika ngazi hizo kuhamasisha mgomo, je mwalimu wa kawaida anayechangia hizo feza anafaidika na nini katika hayo mamilioni? huo ni ufisadi mkubwa coz hela zote zinaingia kwenye matumbo ya akina mukoba kwa maslahi yao binafsi.
3. Shule zinafungwa tarehe 3, August ( primary na secondary), sasa huo mgomo una nguvu gani/ yaani hauna madhara kwa serikali hata kidogo. rais ni kilaza kwa sababu hajui timed reinforcement/ appropriate time kufanya mgomo.
4. Walimu wote wanaenda kuhesabu sensa kuanzia tarehe 06. August kwa kuhudhuria semina elekezi, sasa ataiathiri vipi serikali ili iweze kumtimizia madai yake.
NB: Naomba mfahamu kuwa viongozi wa CWT wapo kimaslahi zaidi/binafsi na sio kuwatetea walimu.
*Wakufunzi wote wa vyuo vya ualimu wameshastukia hilo, hawaungi mkono mgomo, na wapo mbioni kujitoa CWT ili kuanzisha chama chao ambacho kitakuwa na nguvu kudai haki zao kuliko ilivyo sasa kuburuzwa na CWT.
Habari ndio hiyo.