CWT kuna uchawi gani mabilioni ya wanachama inaliwa bila maelezo?

CWT kuna uchawi gani mabilioni ya wanachama inaliwa bila maelezo?

dorge

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2025
Posts
235
Reaction score
365
Nini maana ya kuchanga, kutoa michango.
1000084798.jpg


Kwa kawaida michango ikitoka kwa wanachama linafwata jambo lingine. Matumizi ya michango kwenye malengo mliojiwekea.

Hii cwt nilianza kuisikia miaka nenda rudi. Je haijafikia lengo? Je wanachama wanaendelea kuchanga? Kwa nini hawakomi kuchanga na kwanini hawapati nafuu ya michango wanaendelea kukatwa bila ridhaa Yao? Hakuna uhuru wa kuamua kuendelea au kutoendelea, hapa HAKUNA UTAWALA BORA. ni muda mrefu mtu anachangia bila maelezo na uwezo wa kukatwa

Ni watu wengi wamepata kusikia kashfa mablimbali za ufujaji wa fedha za chama. Kwa hiyo inamaana kuna watu wanazitokea macho na kuzitafuna.

Kwanza zimefika shilingi ngapi?
Zinafanyia biashara gani?
Mapato na matumizi yanatolewa wapi?
Matumizi yake ni yapi?
Kuna miradi?
Nani anaifanya auditing?

Maswali ni mengi. Wanaohusika waamke. Mwl anayekatwa 40,000 kila mwezi ni walimu wangapi wanakatwa fedha hiyo nchi nzima?

HAKUNA UTAWALA BORA.
Ni lazima mwajiri angeweza kumsaidia mtumishi asinyanyaswe na wajanja wachache vinginevyo hakuna haki.

 
Nani ambane mwenzake atoe maelezo?

Mimi naona hata ofisi ya CAG ingefutwa tu maana inafanya uchunguzi na ufuatiliaji lakini hakuna anayebana wezi
 
ACHA YALIWE TU WALIMU NI SEHEM YA WATU WANAOFELISHA HII NCHI
 
CAG akinena hakuna mwenye meno
 
Ni kweli hayo MAKATO ni makubwa Serikali iingilie kati kwa kubadili sheria
 
Hivi CWT isipokuwepo walimu watakosa nini ambacho hawawezi kukipata kupitia mifumo mingine iliyopo isipokuwa T sheti tu.
 
Hivi CWT isipokuwepo walimu watakosa nini ambacho hawawezi kukipata kupitia mifumo mingine iliyopo isipokuwa T sheti tu.
CWT ni mradi wa wachache..nilishangaa sana magufuli-aliupotezea,nahisi kuna vitu wanavijua. Jiukize kwa nini maafisa utumishi wanakaataa mwanachana akitaka kuhama?
 
Back
Top Bottom