CV ya Dr Slaa From Certificate to PhD

Status
Not open for further replies.
Hakuna haja ya kutokwa na povu hii thread ni mpya JF kuna members wapya wanaitaji mijadala kama wewe ulijadili siku nyingi kaa pembeni waachie members wapya hii ndio maana ya forums...halafu nikukumbushe acha kulia lia JF sio mali ya Chadema.


Riz@ nikusaidie kidogo kuelewa:
Chuo cha St. Urban University, Rome, ambacho huchukua wahitimu kutoka vyuo mbalimbali duniani, wanafunzi kutoka vyuo shiriki hasa Seminary huwa kama ifuatavyo:
Vyuo vingi nchini Tanzania kama Kipalapala Major Serinary, Peramiho Major Seminary, Segerea Major Seminary na sasa Morogoro Religious Major Seminary baadhi ya wanafunzi huchukua kozi za moja kwa moja na kufanyia mitihani ya St. Urban University, Rome na kupata shahada za awali, na waendapo huku ni kudeal na PHD tu.

St. Urban University, Rome mfumo wake wa elimu si kama Chuo cha kibongo mlimani au Dodoma Univ. Kule Rome mtu akianza kupiga mbizi kama hakatishi ataendelea hadi kieleweke kupata PHD, si kama bongo, wale jamaa wana mfumo wao.

Kwa taarifa tu kujiunga na chuo kile kuna qualifying test, hata kama una PHD za Marekani au wapi lazima upige hiyo qualifying test yao kupima uwezo wako. Pale haingii mtu kwa kuangalia sura au anatoka wapi ila bongo lifanye kazi. Ujue ni chuo pekee duniani kutoka mataifa yote na hivyo anayetia mguu pale ujue amechujwa vya kutosha.
 
Ritz,

Kwa muda mwingi nimekuwa nikipuuzia post zako kwa sababu wewe mwenyewe umefanya iwe hivyo.

Hata hii nilitaka kupuuzia lakini nimeona nikushauri njia ambayo niliwahi kuitumia. Njia yenyewe ni hii.

Mimi ni mkatoliki. Ninapenda sana kujua mambo ya kanisa langu. Lakini kwa sababu sijawahi kupita Seminary nikadhani kufahamu mambo ya Kanisa langu ingekuwa rahisi kwa sababu mimi ni msomi na ninaelewa mengi.

Nilikwama. Kanisa Katoliki ukiliparamia ovyoovyo unaweza kuishia kuaibika kama inavyokutokea sasa. Labda uniulize ni kwa nini hapa duniani taasisi nyingi zikiwemo nchi kubwa zinaumbuka zinapolivamia Kanisa Katoliki kutaka kushindana nalo kwa hoja yoyote?

Jibu ni kwamba Kanisa katoliki ni taasisi pekee hapa duniani yenye umri mrefu kuliko taasisi yoyote. Hadi sasa ina umri wa miaka 2012.

Hivyo, usidhani kuna swali utalileta halafu Kanisa Katoliki likose majibu. Unaweza kukutana na mkatoliki ukakosa majibu lakini tatizo likawa ni huyo mkatoliki na si lenyewe kama Kanisa.

Ni kweli unaweza kuleta jambo humu JF na ukakuta wote wameshindwa kukujibu na wengine wakaishia kukutukana au kukukejeli. Mimi hao pia nawaonea huruma kwani ukweli ni kwamba majibu yako utashangaa kuona kwamba yalishatolewa miaka 500 iliyopita na wewe unarudia swali leo!

Mimi nilivyoona hivyo, nilicukua kama miaka mitatu najisomea tu mambo ya Kanisa langu. Ritz, nakujibu kiurafiki, kulielewa Kanisa Katoliki unahitajia uvumilivu wa hali ya juu kama umedhamiria kusoma mambo yake.

Mfano wa aibu mnazopata ni mwaka 2009 ambapo Waraka wa Kanisa ulitoka. Watanzania mlishangaa kana kwamba ni mara ya kwanza wakati waraka wa kwanza duniani ulitoka mwaka 1891 ukiitwa Rerum Novarum uliotolewa na Pope Leo XIII. Watanzania mkaaibika duniani kote kwamba ni washamba hawajui nyaraka za Kanisa Katoliki. Tena wakaaibika watu mashuhuri kama Kingunge!



Ona sasa topic unayoileta ya kuuliza Phd ya Dr. Wilbord Slaa. Ni wazi kwamba huelewei kwamba Kanisa Katoliki ndilo mama wa Sheria hapa duniani lakini kubwa zaidi Kanisa Katoliki ndilo mama wa mifumo ya elimu hapa duniani.

Ujerumani iliacha mwaka 1886 kukaguliwa sylabus na majesuit ambao ni mapadri wa Kanisa Katoliki ambao hapa nchini wanaendesha shule maarufu yaani Nyakahoja ya Mwanza na Loyola ya D'Salaam, St. Ignatius ya Dodoma na wamefungua Sekondari hapohapo Dodoma.

Uingereza nayo ilianza shule zake mapema kabla ya Ujerumani na ikafuata mfumo wake.

Lakini kote huko Kanisa likaendelea na mfumo wake mmja uitwao Licentiate au Licenciatura. Nenda kwenye website yoyote halafu soma kwa makini neno Licentiate ndipo utakuta mfumo waliosoma Dr. Slaa na wenzake wengi umejikita humo.

Hebu soma mfumo wa elimu wa nchi zifuatazo yaani Germany, Argentina, France, Australia, Canada, Belgium, Brazil, Bolivia, Costa Rica. Huko kuna vyuo wanafuata mfumo huu wa Licentiate. Huko kukuta mtu kamaliza Diploma halafu anapata Phd ndiyo maisha ya huko.

Sisi hapa Tanzania tuliamua kufuata mtindo wa Uingereza na hasa Oxford. Uingereza waliamua kubuni upya kabisa mfumo wa elimu.

Hivyo, Ritz na wenzako, unpouliza swali kama hili ni wazi kuwa inabidi ujikite maeneo ambayo ni wazi na wao upeo wao ni mdogo. Ungekuwa thread yako umeiandika kwa kiingereza na tukakutana kwenye anga za international threads na tunajadili mataifa mbalimbali ungeumbuka umbuko ambalo hutalisahau, kwani ni wazi wapo ambao wangeuliza umetoka nchi gani huelewi system hiyo ya Eductaion.

Mimi hata leo nikilichukia Kanisa Katoliki na nikaingia katika timu ya watu wanaolichambua kwa kuumbua mambo yake, basi ningekutana na nyinyi kisha nikawapa semina kwamba tubadili mbinu maana hizo mbinu zenu mtaishia kuumbuka tu.

Kawaulize waarabu ambao waliwahi kupiga kelele kuhusu Vatican kupewa ubalozi kwenye nchi kadhaa lakini jinsi wlivyozidisha kelele na wakikaa meza moja na Vatican wanajikuta na wao wanaishi kushawishika kufungua balozi nyingi kama Iran na kwingineko.

Waulize Russia ambako walikejeli sana Ubalozi huo na mwisho nao wakajikuta wanaufungua kwao. Wamarekani tangu mwaka 1871 walikataa ubalozi huo, wakajikuta mwaka 1994 wanaufunguwa kule Washington.

Leo wewe umeuliza swali kuhusu Phd. ya Dr. Slaa. Si mara ya kwanza unauliza hivi. NImesema ukisoma kuhusu Licentiate education system utajikuta umefunguka usichikijua na utashukuru Mungu kwamba unatumia ID ya jina la Ritz na hivyo aibu ya ushamba hutaipata maana hatukujui.

Soma tu utaelewa, document zipo tele. Ni kichwa chako tu.

Riz angejifunza kitu kutoka tu elimu ya shule za seminary ambako mwanafunzi mwenye ufaulu wa chini ya daraja la tatu haruhusiwi kuendelea na kuwepo sekondari za seminary. Wahitimu wenye daraja la kwanza na la pili tu ndio wenye kuruhusiwa kuendelea na masomo ya juu na kipimo hicho si elimu ya biblia bali elimu dunia. Kule si kusoma biblia tu, elimu dunia kwanza ufaulu kwa kiwango hicho ndipo uendelee.
 
A medieval doctorarte, kwa sasa hivi haina maana sana (actually "yoyote"). Unaweza kupata shahada hizi online kwa kusoma biblia na kujibu maswali, baada ya mwaka una Bachelors ya divinity from some church!!, it's bull.
 
Ritz jitahidi kwenda na wakati mwanangu. Watu wanahangaika na mambo mazito wewe unakuja na vitu vya kujitungia. Nini kisichowezekana iwapo jamaa unaambiwa ana certificates nne toka kwenye vyuo vikuu ukiachia mbali advanced diploma toka chuoni. Ni simple wanaotoa PhD wanaweza kufanya cumulative assessment na kuona ni bora mhusika asomee PhD. Nadhani ingekuwa hoja ni kuwa hakuisomea kidogo ingekuwa na mashiko. Mbona Kikwete anayo ya heshima na anaitumia wakati hajui hata dissertation inaandikwaje? Hata kama unamchukia jamaa kidogo kubali kuwa vyeti vyake ni vizito.
 
pro chadema walikuwa wakiikejeli cv ya Vicky kamata.. nkawaambia mbona ya mzee slaa ni kama hivo tu.. wakanambia njiwa wewe mdini.

Ritz shukran kwa kufukua hii kitu..
 
Nilikuwa sitaki kuamini kwamba kuna watu wanalipwa Jf lakini kwa hili Ritz umenifumbua macho,thread imekaa kimipasho sana hii mkuu,yaani baada ya watu kufumua cv ya Vicky isiyokuwa na kichwa wala miguu kwa akili yako ndogo umeileta hii while this has been extensively discussed in here,you should feel shame of yourself ritz.fedha kweli mwanaharamu
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Nyie wasomi wa wapi? Kama mtu ka skip ni kichwaaa! Mark Mwandosya from BSc eng mpaka PhD! Mnadiscuss vise versa!

Daniel Mkude, from BA (Dar) to PhD (London), Mugyabuso Mulokozi BA(Dar), PhD (Dar)..... Hii ni ya Kawaida kabisa..Hawa ni Maprofesa waliobobea katika fani zao pale Mlimani!
 
Hakuna haja ya kutokwa na povu hii thread ni mpya JF kuna members wapya wanaitaji mijadala kama wewe ulijadili siku nyingi kaa pembeni waachie members wapya hii ndio maana ya forums...halafu nikukumbushe acha kulia lia JF sio mali ya Chadema.

Tafuta CV za Professor Amos E. Majule ambaye ni Mkurugenzi wa IRA-(UDSM) na Professor Daniel Mkude, (UDSM) uone kama Ph.D zao zina Masters.
Kama hujui mambo yanayohusu elimu usikurupuke, utaumbuka dogo!
Kwa kukusaidia tu, link ya CV zao iko hapa

 
Haya nime-copy toka kwenye mjadala wa zamani. Huu mjadala ulinzia mwanabidii ukarukia JF. Nanukuu majibu ya mdau,


"Tukianza na Kipalapala, hapa mwanafunzi anasoma form 5 & 6 pamoja na masomo ya Theology na baada ya hapo huunganisha na degrii ya theology.

Kipalapla kama ilivyo Institutions zote za Kanisa Katoliki (kwa level ya Philosophy na Theology) iiko affiliated na vyuo vikuu mbalimbali duniani kutoka nchi moja hadi nyingine.

Mfano, wanaosoma Zomba Theological College Malawi (Theology) na Kachebere Philosophical College (Philosophy) mpakani mwa Malawi na Zambia wanafuata marking scheme ya Chancellor College - University of Malawi. Kuna chuo kingine kiko Balaka Consorsium Philosophical College nadhani kiko affiliated na St Urban University, Rome.

Missionary Institute London (MIL) iko affiliated kwa Middlesex University (chuo cha serikali cha Uingereza) na Luvein University (Belgium). Wanaofuata mfumo wa Middlesex University kupata BA wanasoma miaka 3 na passmark yao ni 40%. Wanaofuata mfumo wa Luvein University kupata BA wanasoma miaka 4 na passmark yao ni 60%. Muhula unaanza Oktoba na kwisha Juni (miezi 8).

Mfumo wa kutoa final mark ni 1) class presentation na participation 2) essay writing 3) oral examination 4) defence of dissertation mbele ya internal & external examiners. Pia mtu anayepata first class, papers zake lazima ziwe marked na internal na external examiners na ajadiliwe kama anastahili first class degree na siyo tu kupata kwenye karatasi. Pia anayeshindwa, paper zake zinasahishiswa na examiners tofauti ili kuonesha kashindwa kweli au kama amepunjwa marks.

Kwa Tanzania, kwa sasa vyuo vyote kwa level ya Philosophy na Theology viko affiliated na St Urban University, Rome. Zamani, falsafa ilikuwa miaka 2 (sasa ni 3) na teolojia ilikuwa miaka 3 (sasa 4).
Mtu akimaliza (Tanzania) alikuwa anapata certificate siyo kwa sababu masomo yalikuwa level ya chini ila kwa sababu maaskofu walikuwa hawajaridhia wahitimu wao kupata digrii licha ya kuwa walikuwa wanaombwa wanafunzi wapewe magamba kama ilivyokuwa kwenye vyuo vingine. Ilichukua muda kidogo.

Lakini kama mtu aliendelea na masomo ya juu walithamanisha masomo yale kwa chuo ambacho mtu anaenda kusoma maana content ya syllabus ya masomo ya falsafa na teolojia ni (universal) kwa vyuo vyote vya Kanisa Katoliki duniani tofauti ni kwa kila nchi wanaongeza mambo yanayohusu cultural understanding ya nchi husika including its legal system.

Uganda mtu akimaliza Jinja Philosophical College (Philosophy) anapata BA katika Philosophy. Akiendelea na Theology chuo kingine, anapata BA katika Theology na kuna vyuo vingine akimaliza Theology anapata MA. Inategemea chuo kina mfumo gani na kinafundisha nini - maana kuna baadhi ya masomo kama mtu hakuyafanya wakati wa philosophy atayafanya wakati wa theology.

Kwa baadhi ya vyuo, mtu mwenye BA ya Philosphy na BA ya Theology, akiendea na masomo ya juu 'specialisation', anaenda moja kwa moja kusoma PhD kulingana na vigezo walivyoweka (mfano, vyuo ambavyo vinafundisha Philosophy na Theology kwa pamoja).
Kwa baadhi ya vyuo masomo haya yanatenganishwa - yaani, mwanafunzi anaamua ku'specialise' kwenye pure philosophy au pure theology. Na katika masomo yote mwanafunzi anafundishwa the secular view na religious view.

Maana ni hasa kumwezesha mwanafunzi kupata "solid and consistent knowledge of man, the world and God... The students should rely on that philosophical patrimony which is forever valid, but should also take account of modern philosophical studies, especially those which have greater influence in their own country, as well as recent progress in the sciences. Thus, by correctly understanding the modern mind, students will be prepared to enter into dialogue with their contemporaries." ( Vatican II, Training of Priests, Paragrapah No 15).

Kuna vyuo kama alikosoma Dr Slaa lecturers wote ni wa level ya profesa na kwenda kusoma huko mpaka uwe 'exceptional student' nadhani kama sikosei wanachukua wale tu wenye 'first class'.

Kitu kingine ninachoona kinampa wasiwasi (jina limehifadhiwa) ni pale anaposoma "Canon Law" au "Catholic Education" kwa kudhani padre anasoma tu biblia au mafundisho ya Kanisa. Mfano, Dr Slaa amespecialise katika Canon Law ambayo ndiyo mother of secular law na kusoma Canon Law ni lazima kuanza na how law developed na mpaka kuja kugawanyika into secular na religious laws.

Advantage ya Dr Slaa si tu kwamba ana'knoweldge' ya Canon Law lakini pia nini kinaitwa secular law na kwa nini - tofauti na similarities. Mfano, definitions of what is an irregurality, malice aforethought, the difference between legality and validity of an act, what is a valid marriage and a legal marriage, etc.

All Catholic Universities undertake secular studies mfano ni Catholic University of East Africa (CUEA), Kenya, ambako hata Waislamu wanasoma huko, St Augustine, Mwanza, Luvein University etc. kwa hiyo mtu akihitimu kwenye vyuo hivyo, huwa haangaliwi kuwa amesoma elimu ya dini bali kwamba ni mtaalamu katika taaluma fulani aliyoisomea.

Tofauti kwa mapadre ni kwamba mfumo wao wa mafunzo unachukua muda mrefu na wanajifunza mambo mengi - maana hadi kufikia upadre ni mpaka uwe walau umesoma miaka 10 baada ya Form VI". (mwisho wa kunukuu)


Ukitaka mjadala mzima. https://www.jamiiforums.com/jamii-intelligence/168414-kuhusu-cv-na-phd-ya-dr-slaa.html

Kuna chuo kilikuwa chini ya shirika la White Fathers (Missionaries of Africa) pale Kahangala, Magu - Mwanza - kilikuwa kinachukua wanafunzi kutoka Tanzania, Uganda, Kenya, Zambia na Malawi kwa masomo ya falsafa. Chuo hiki kilikuwa sawa na chuo kingine Uganda (Jinja Philosophical College) maana wanafunzi wengine walipelekwa Jinja au walikuja Kahangala.

1. Ili kujiunga kwanza upate Division I au II Form IV na VI (Kwa wale waliochukua Arts subjects Division I au II na wale waliochukua science subjects walau Division III).

2. Philosophy ilikuwa miaka 3 (entry qualifications za chuo kikuu) na masomo yote yalikuwa marked under 80 na siyo 100%. Mfano, ukipata 60 (ilikuwa distinction) yaani ni 60/80 kwa wale waliosoma Kahangala. Wale walioenda Jinja walikuwa wanakuwa marked kwa mfumo wa 100%. Kahangala waliokuwa wana mfumo wa y/80 na siyo y/100 pass mark yao ilikuwa 40/80. Kwa wale waliokuwa wanatumia mfumo wa 100% pass mark ilikuwa 50%.


3. Waliomaliza Kahangala walipata diploma ya falsafa. Waliomaliza Jinja walikuwa wanapata BA katika falsafa.


4. Wanafunzi kutoka Kahangala au Jinja walikuwa wanapelekwa kwenye nyuo vingine (kama hatua ya 2). Wale waliochukua masomo ya Kifaransa walipelekwa Fribourg (Uswisi) na waliochukua Kiingereza walipelekwa Kasama, Zambia.


5. Hatua ya 3 - wale wa masomo ya Kifaransa walipelekwa Tolouse, Ufaransa kwa teolojia. Na wale waliochukua Kiingereza walipelekwa Missionary Institute London (MIL). MIL alikuwa affiliated kwa Middlesex University (London) na Louven University (Belgium) na wale wa Tolouse, Louven University.

6. Kule wote walikuwa regarded kama level moja maana walikuwa wame'cover' silabasi moja ingawa wa Kahangala (kutokana na mfumo wa Tanzania wakati ule maaskofu hawakuwa wameridhia mfumo uliokuwa unatumika - ilichukua muda). Uganda mfumo wao ulikuwa tofauti kwani vyuo vyote vilikuwa affiliated kwa Makerere University.

Kwa hiyo, baada ya kumaliza Form VI, ili ujiunge na vyuo vya falsafa au teolojia lazima uwe na entry qualifications za chuo kiukuu na whether chuo fulani kwa sababu zao au utaratibu wao walitoa certificate/diploma/degree, vyote hivi vilikuwa level moja maana silabasi ilikuwa ileile na walimu walikuwa pia wenye qualifications zinazofanana. Baada ya hapo chuo kilichofuata ndicho kilikuwa na jukumu la kuthaminisha mwanafunzi fulani anatoka chuo gani na walikuwa wanapata nini whether certificate/diploma/degree na kwa vile kilicho matter ni pass mark maana kama mtu hajafikia wastani unaotakiwa haruhusiwi kuendelea basi chuo husika kiliamua mwanafunzi apate nini.
 
Shida ya vijana wa sasa kama Ritz hawatumii Akili kabisa kuangaza mifumo ya elimu nje ya nchi .
Nani kasema mfumo wa masomo unaanza primary, secondary, high school,bsc,master,phd
Kuuna nchi nyingi ni diploma , masters,phd. Nchi nyingine, ni diploma the masters na phd zimechanganywa
Jaribu kufanya uchunguzi msikurupuke tu.
 
Haya maneno ni yako CV ya Slaa sio ya kwanza mie kuileta acha watu wajadili kuna members wapya wanaitaji kujua sio wote wana miaka mingi humu JF.
FYI we Dhaifu, DR Slaa siyo mbunge
 
Hapa Dr Slaa alivyokuwa mbunge hana BA wala MA lakini ana PhD

Member of Parliament CV

GENERAL
SalutationHonourableMember picture
1253.jpg
First Name: Dr. Wilbrod
Middle Name:Peter
Last Name:Slaa
Member Type:Constituency Member
Constituent:Karatu
Political Party:CHADEMA
Office Location:P.O. Box 119, Karatu - Arusha
Office Phone: +255 784 666995
Ext.:
Office Fax: +255 22 2668866
Office E-mail: wslaa@parliament.go.tz
Member Status: Current Member
Date of Birth 29 October 1948
EDUCATION
School Name/Location Course/Degree/Award Start DateEnd DateLevel
St. Thomas Aquinas UniversityAdvanced Diploma in Rural Development19801981ADV DIPLOMA
TransWorld Tutorial College, LondonCertificate in Management19851985CERTIFICATE
Kwermusl Primary School(Mbulu)Primary Education19581960PRIMARY
Daudi Primary SchoolPrimary Education19611961PRIMARY
Karatu Primary SchoolPrimary Education19621965PRIMARY
Dung'unyi Seminary SchoolO-Level Education19661969SECONDARY
Itaga Seminary SchoolA-Level Education19701971HIGH SCHOOL
Kibosho Seminary SchoolCertificate in Philosophy19721973CERTIFICATE
St. Urban University, RomePhD (JCD) Law19771981PHD
Kipalapala SeminaryCertificate in Theology19741977CERTIFICATE
International Eye H. CentreCertificate in Eye Health19931993CERTIFICATE
EMPLOYMENT HISTORY

JF Daima...:peace:

ritz endelea kujaza post na wana jf kwa ujumla mpeni sapoti ritz kujaza post iliuendele kujaza post weka cv ya dhaifu na boss wako nape mwisho ukikosa ya kuweka weka yako na ya baba yako mama yako mke wako kama una mke kama una mume weka ya mume wako kila siku una weka cv za watu acha njaa mwanaume anatakiwa kusifiwa kazi cyo umbea majungu MANAMBA WEWE
 
RITZ:WIVU TU UNAKUSUMBUA huwezi kumfananisha dr slaa na dhaifu hata cku moja ***** wewe
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom