CV ya Balozi Wilson Masilingi

CV ya Balozi Wilson Masilingi

Baada ya kuangalia kipindi cha Straight Talk Africa, ambapo Mh. Tundu Lissu na Balozi Wilson Masilingi walihojiwa, nilishangazwa na jinsi Balozi wetu huko Marekani alivyopwaya na kupata tabu kujielezea kwa Kimalkia na pia kushindwa kudhibiti jazba zake.

Nilidhani pengine ni Kimalkia tu kinamsumbua huyu ndugu yetu, lakini nikagundua kuwa tatizo sio lugha kwani kwenye mahojiano mengine yaliyofanyika kwa kiswahili katika VOA Swahili, hali ni ile ile.
Mbaya zaidi kwenye hii interview ya pili, hata kufuata taratibu ndogo tu za midahalo ya kistaarabu hakuweza.

Haya yote yamenipa hamu ya kufahamu safari ya kiongozi wetu huyu na ni jinsi gani ameweza kufika katika nafasi kubwa kama hiyo pamoja na mapungufu hayo.

Hivyo basi, nawaomba wenye ufahamu juu ya elimu na uzoefu wa Balozi Wilson Masilingi atuhabarishe.

Hata simlaumu yule balozi. Jaribu kuvaa viatu vya Balozi na uone ugumu wa kuutetea udhalimu wa serikali. Alionekana balozi kuwa ill - informed. Ninavyoamini alijitayarisha sana lkni ni kwa vipi angewezea ku-defend uovu wa serikali ktk international media? Nafkr si rahisi kutetea . Mwenzake TL alijiamini kwa kuwa alikuwa na ushahidi ikiwa yeye mwenyewe ni shahidi namba moja. TL was very confident. Points zake zilikuwa evidence based kinyume chake balozi alionekana kutoa hoja ambazo hata mtoto wa kindergaten angeweza kusema.
 
Jua kuwa huyo balozi ni wale vichwa Nyerere alituachia katika dakika zake za mwisho wa uongozi wake. Inasemekana alikuwa mmoja wa mahakimu vijana waliotingisha enzi hizo kwa kutia hatiani vigogo wahalifu walikuo na uwezo wakununua maisha yako.

Masilingi ni simba wa kuchora
 
Baada ya kuangalia kipindi cha Straight Talk Africa, ambapo Mh. Tundu Lissu na Balozi Wilson Masilingi walihojiwa, nilishangazwa na jinsi Balozi wetu huko Marekani alivyopwaya na kupata tabu kujielezea kwa Kimalkia na pia kushindwa kudhibiti jazba zake.

Nilidhani pengine ni Kimalkia tu kinamsumbua huyu ndugu yetu, lakini nikagundua kuwa tatizo sio lugha kwani kwenye mahojiano mengine yaliyofanyika kwa kiswahili katika VOA Swahili, hali ni ile ile.
Mbaya zaidi kwenye hii interview ya pili, hata kufuata taratibu ndogo tu za midahalo ya kistaarabu hakuweza.

Haya yote yamenipa hamu ya kufahamu safari ya kiongozi wetu huyu na ni jinsi gani ameweza kufika katika nafasi kubwa kama hiyo pamoja na mapungufu hayo.

Hivyo basi, nawaomba wenye ufahamu juu ya elimu na uzoefu wa Balozi Wilson Masilingi atuhabarishe.
Ni kweli mkuu, Lakini huyo ni nafuu humo, kuna wabovu zaidi yake! Huwa najiuliza sijui hao watu walifikiaje hizo nafasi? Au ni mambo ya ubaguzi?🤔
 
Jua kuwa huyo balozi ni wale vichwa Nyerere alituachia katika dakika zake za mwisho wa uongozi wake. Inasemekana alikuwa mmoja wa mahakimu vijana waliotingisha enzi hizo kwa kutia hatiani vigogo wahalifu walikuo na uwezo wakununua maisha yako.
Hizi stori za kizamani sana hazina maana karne hii. Unataka kusema anamzidi Propesa?
 
Ni kweli mkuu, Lakini huyo ni nafuu humo, kuna wabovu zaidi yake! Huwa najiuliza sijui hao watu walifikiaje hizo nafasi? Au ni mambo ya ubaguzi?🤔

Ni kama kumsifu Maradona enzi hizi za Messi. Mla mla leo mla jana kaka nini?
 
Hakika, Masilingi alionyesha kupwaya na ilikuwa ni lazima kupwaya maana hata maswali aliyoulizwa na shaka achilia mbali ya Hama Mwamoyo hakuweza kuyajibu ipasavyo. Na watendaji wengi wataendelea kupata shida kwa kuwa wanajaribu kusema uongo ili kumridhisha bwana Mkubwa.
 
Uchochezi wa TL umetupelekea vita vya wenyewe kwa wenyewe. Tumeanza na vita vya maneno mitandaoni. Tukikutana uso kwa uso ni ngumi kama ilivyotokea kwa yeye TL na Masilingi. Akitugaia bunduki ndio kabisa vita ya risasi na mitutu ya bunduki. Ndio maana tunawahimiza wenye dhamana ya chukua hatua za makusudi kudhibiti huyu jamaa wafanye hivyo bila kuendelea kuchelewa. TL anatamani siku moja Watanzania walio wengi wafate mkumbo wake na watembelee gongo kama yeye.
Out of the topic
 
TL mwenyewe alichachawa na kila wakati akimwita a very senior lawyer in Tanzania which means TL na misifasifa yake yote anakubali ni jr kwa mh Masilingi.
Hujasaidia kujibu na au unakubaliana nami kuwa siyo competent kwenye fani yake mwenyewe! What to do with seniority!? Haibadili lolote siyo? So hoja yako ni mfu!
 
mbona hard talk ya lissu hamkuizungumzia/wakati na yeye alipuyanga.
Jifunze kutofautisha basi ili twende sawa. Kwanza ni vyombo viwili tofauti vya habari na pili waongoza mdahalo ni watu tofauti na ndio maana hata maswali yaliyoulizwa BBC hayakuulizwa voa!
Kwa taaluma ya habari utakuwa uliona kama mwendesha mdahalo wa BBC alimbana Lissu lakini kiuhalisia alimsaidia kuyatoa mengi ya moyoni ambayo mlikuwa hamyajui. Alimuongoza vyema ili aweze kuongea zaidi na hiyo ni mbinu ya kisaikolojia ya kuondoa trauma.
 
Back
Top Bottom