CV ya Balozi Wilson Masilingi

CV ya Balozi Wilson Masilingi

Jua kuwa huyo balozi ni wale vichwa Nyerere alituachia katika dakika zake za mwisho wa uongozi wake. Inasemekana alikuwa mmoja wa mahakimu vijana waliotingisha enzi hizo kwa kutia hatiani vigogo wahalifu walikuo na uwezo wakununua maisha yako.
Hiyo sio hoja bwana, wewe vipi. Yaani kufunga watu jela ndio umekuwa "Legend". Je kama aliwaonea. Your reasoning reflects shallow thinking and I wish you didn't post this.
 
Uchochezi wa TL umetupelekea vita vya wenyewe kwa wenyewe. Tumeanza na vita vya maneno mitandaoni. Tukikutana uso kwa uso ni ngumi kama ilivyotokea kwa yeye TL na Masilingi. Akitugaia bunduki ndio kabisa vita ya risasi na mitutu ya bunduki. Ndio maana tunawahimiza wenye dhamana ya chukua hatua za makusudi kudhibiti huyu jamaa wafanye hivyo bila kuendelea kuchelewa. TL anatamani siku moja Watanzania walio wengi wafate mkumbo wake na watembelee gongo kama yeye.

Lissu anamudu hoja hahitaji bunduki, jiwe ndio hawezi hivyo ni lazima bunduki itakuwa suluhu yake.
 
Sidhani kama ana muda mrefu kwenye hicho cheo. JPM atakua anaanda mrithi wake.

Hapo Lissu ni wa kumshukuru maana anamsaidia mkulu kuchuja watu wachovu. Je isingekuwa huo mdahalo angejuaje kwamba ni bogus? Na huo ni mfano wa mabalozi wetu wengi kuwa incompetent
 
Masilingi hakupwaya hata kidogo. Ila zipo hoja ambazo hata ungemuweka Lissu kwenye upande wa balozi angepwaya sababu hazina majibu hadi leo. Kama waziri wa mambo ya ndani hana straight answer vipi balozi? Masilingi ni super genius na bingwa wa sheria, pia uzoefu wake ulimsaidia kumtoa Lissu kwenye angle flani ambazo wengi najua hamkuweza kusoma. Rudieni mahojiano yote muone mjadala uliegemea wapi na kwanini! Yule mzee yuko vizuri

Sent using Jamii Forums mobile app

Kutetea upumbavu wa CCM na sirikali yake ni kipaji! Si kila mtu anacho
 
Baada ya kuangalia kipindi cha Straight Talk Africa, ambapo Mh. Tundu Lissu na Balozi Wilson Masilingi walihojiwa, nilishangazwa na jinsi Balozi wetu huko Marekani alivyopwaya na kupata tabu kujielezea kwa Kimalkia na pia kushindwa kudhibiti jazba zake.

Nilidhani pengine ni Kimalkia tu kinamsumbua huyu ndugu yetu, lakini nikagundua kuwa tatizo sio lugha kwani kwenye mahojiano mengine yaliyofanyika kwa kiswahili katika VOA Swahili, hali ni ile ile.
Mbaya zaidi kwenye hii interview ya pili, hata kufuata taratibu ndogo tu za midahalo ya kistaarabu hakuweza.

Haya yote yamenipa hamu ya kufahamu safari ya kiongozi wetu huyu na ni jinsi gani ameweza kufika katika nafasi kubwa kama hiyo pamoja na mapungufu hayo.

Hivyo basi, nawaomba wenye ufahamu juu ya elimu na uzoefu wa Balozi Wilson Masilingi atuhabarishe.
kipindi kilikuwa cha pwagu vs pwaguzi
yani ndo ingekuwa siro vs tundu lisu pale lazima siro angepaniki kama balozi.
shikamoo lisu.watu kama lisu mpo wapi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ww Lissu mi mjanja aliamua kuact in professional way

Mdege mjanja hunaswa na TUNDU bovu. TL kanaswa na tamaa ya malipo ya Fedha haramu. Kabadili gia angani, kajitahidi kukwamIsha juhudi za Rais za kuwashughulikia wezi wa dhahabu za nchi yetu na sasa kalipwa kuendesha uhaini huko ughaibuni.
 
Kwa CCM, CV doesn't matter at all, na ndio maana huwezi kutofautisha anapoongea mtu kama Kibajaji aliyeishia Darasa na Nne na Profesa X aliyebukua mabuku yote hadi yakawa yanakimbia pindi yakimuona!!
Hapo ndipo ELIMU YA DANGANYIKA ilipofikishwa
 
Nilifuatilia ni kawa na shaka sana kuwa katika shule alizopitia hakuwai kuendesha,kuchangia na kusikiliza midahalo mbalimbali kujifunza jinsi ya kujipanga na kuanda data za kutosha pale unapokabiliwa na maswali yenye hoja nzito kama za lissu japo ni yakawaida ila kama balozi wa Tanzania to USA alitakiwa awe amejihanda kwa hili najua ni mzee na binafsi na muheshimu kam mzee na mtu mwenye elimu kubwa tu ila ushauri angetafuta njia nyingine ya darkness njee ya kisiasa kukwepa kujivua nguo na kuidhirisha dunia kuwa anayodai mh tundu antipus lissu ni huhakika usio na uwalakini
Ijumaa njema wadau.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndugu zangu, hiyo mlioiona ndio hulka ya viogozi wa sasa walioko madarakani, hamna cha kushangaza. Rais, wakati anaomba urais alipiga push-up kwa wingi. Hii inawakilisha nini? Misuli na matumizi ya misuli ni nini? Mheshimiwa Job Ndugai alimpinga mgombea mwezie hadjarani hadi akazimia, CCM ikampitisha kuwa mgombea ubunge na akapewa promotion kwa kuteuliwa kuwa spika. Mhe. Tundu Lissu ali[powazidi kwa hoja Bungeni, wakamsubiri atoke nje wakampiga risasi nyingi kuliko alizowahi kupigwa tembo. Ben Saanane alipowasema sana wakampoteza hadi leo sio mwili au nguo alizokuwa amevaa zimeonekana. Na nina uhakika kama mahojiano yangefanyika Tanzania Mhe. Masilingi angepigana.
Nguvu, kiburi na jeuri ndizo sifa pekee za sasa kuwa kiongonzi- jiulize wateule wa rais waliokwisha tumia risasi kutetea hoja zao ni wangapi katika kipindi cha miaka mitatu ya mhe.
 
Angalia na saikolojia yake Kuna watu huwa sio waongeaji hivyo akikutana na muongeaji lzm apigwe chini hii hali ipo kimakundi fatilia sayansi ya saikolojia huyo balozi mnamuonea bure tu hawezi kushindana na lisu hasa kama hana taarifa za kutosha juu ya tukio la lisu
Tatizo tukio l4le la kikatili limechezwa kipumbavu kiasi kwamba mtu yeyote mwenye akili timamu utapata tabu sana kulijibu au kulitetea.
 
Balozi anataka kutumbuliwa uyo wenzake wanaingia mitini yeye anajipeleka mbele lisu anadhani atamfurahisha jiwe, mtu ambaye anaweza kukaa na lisu na kumfurahisha jiwe ni mtu ambaye bongo lala ajui kureason yani mlopokaji mlopokaji mfano bashite na ndungai hao ndio wanaweza mfurahisha jiwe maana watatoka nje ya madam nakuanza matusi kejeli na kebehi sasa balozi msomi hawezi zaidi atatumbuliwa tu save the dat e miezi sita haipiti anatumbuliwa sababu kashindwa muattack lisu[/QUOT
Balozi anataka kutumbuliwa uyo wenzake wanaingia mitini yeye anajipeleka mbele lisu anadhani atamfurahisha jiwe, mtu ambaye anaweza kukaa na lisu na kumfurahisha jiwe ni mtu ambaye bongo lala ajui kureason yani mlopokaji mlopokaji mfano bashite na ndungai hao ndio wanaweza mfurahisha jiwe maana watatoka nje ya madam nakuanza matusi kejeli na kebehi sasa balozi msomi hawezi zaidi atatumbuliwa tu save the dat e miezi sita haipiti anatumbuliwa sababu kashindwa muattack lisu
Kashatumbuliwa.we jamaa noumaa!!!
 
Baada ya kuangalia kipindi cha Straight Talk Africa, ambapo Mh. Tundu Lissu na Balozi Wilson Masilingi walihojiwa, nilishangazwa na jinsi Balozi wetu huko Marekani alivyopwaya na kupata tabu kujielezea kwa Kimalkia na pia kushindwa kudhibiti jazba zake.

Nilidhani pengine ni Kimalkia tu kinamsumbua huyu ndugu yetu, lakini nikagundua kuwa tatizo sio lugha kwani kwenye mahojiano mengine yaliyofanyika kwa kiswahili katika VOA Swahili, hali ni ile ile.
Mbaya zaidi kwenye hii interview ya pili, hata kufuata taratibu ndogo tu za midahalo ya kistaarabu hakuweza.

Haya yote yamenipa hamu ya kufahamu safari ya kiongozi wetu huyu na ni jinsi gani ameweza kufika katika nafasi kubwa kama hiyo pamoja na mapungufu hayo.

Hivyo basi, nawaomba wenye ufahamu juu ya elimu na uzoefu wa Balozi Wilson Masilingi atuhabarishe.
Tofauti na Mtazamo wako....Balozi alikabili vilivyo uzushi uliopitiliza wa Lissu.Amesaidia kuwafahamisha walio nje ya nchi uhalisia wa mambo kama vile Ukweli kuwa akina Mbowe hawajafungwa gerezaani kama anavyodanganya... hao wamelundikwa mahabusu tena kwa kosa la kukiuka masharti ya dhamana, kwa kesi ya jinai na si ya kisiasa. Kuwekwa mahabusu na kufungwa ni mambo mawili tofauti. Big up Masilingi.
 
Back
Top Bottom