CUF waishambulia CHADEMA

Asante mkuu. Litakuwa kosa kubwa kwa CHADEMA kushirikiana na CUF ambao wanamakubaliano ya siri na wakubwa zao CCM. CHADEMA wakishirikiana na CUF basi by default CHADEMA itakuwa ni CCM. Dhama za chama kimoja tutarudi huko. Kazi kubwa ya CUF kwenye yale makubaliano yao ni kuuwa upinzani na CHADEMA. Nafurahi viongozi wa juu wameliona hili. CUF imepoteza identity ya upinzani nadhani tamaa ya viongozi wao imewafikisha huko. 2015 CUF itakuwa imefutika kabisa

Mch Masa K
Uko sahihi, CUF sio chama cha upinzani tena hivyo hakiwezi kuungana na Chadema, ukiangalia Ndugu Mrema wa TLP kwenye kampeni alikuwa anampigia kampeni JK, hivyo binafsi simwamini hata kidogo kuingia kambi ya upinzani kwani anaweza kuwa chanzo cha migogoro na kuturudisha nyuma zaidi. Ukiangalia pia NCCR Mageuzi pia hawaaminiki ukianzia na kukuru kakara za mwenyekiti wake wakati wa kampeni hata sasa juu ya Chadema na wabunge wake, hivyo ni bora Chadema kusimama kama wao ili kuepuka migororo ambayo ingetokana na wao kuungana na vyama vingine.

Naafikiri baadae tutawaelewa viongozi wa Chadema nini wanachokifanya sasa hivi.
 
Wakuu zangu hili sio swala la kupuuza hata kidogo. Chadema acheni uchu wa madaraka kuunda kambi ya Upinzani na haitawasaidia chochote zaidi ya kujenga fitna zaidi.
Kweli kabisa Chadema kulingana na katiba inayo haki ya kufanya kila kitu watakavyo isipokuwa mjue tu kinachozungumziwa zaidi na katiba ni jinsi ya kumpata kiongozi wa kambi hiyo ya Upinzani, kuliko uundwaji wa kambi yenyewe.

Vipengele vyote vinazungumzia nani atakuwa kiongozi wa kambi hiyo lakini haikatazi chama kuunda umoja na vyama vingine kwani maana ya kuunda kambi hiyo ni kutoa fursa kwa vyama vingine vipate nafasi ya kuzungumzia hoja walizokuwa nazo dhidi ya chama tawala. Kinyume cha vyama hivyo havitakuwa na nafasi hiyo isipokuwa kuuliza maswali ya nyongeza tu.

Leo hii wakuu zangu nimeamka vibaya na hakika sipendi kuzungumza mengi isipokuwa nasema Mkuu wangu Mbowe, ile tabia ya kuwatumia watu kisha ukawaacha mataani iache.. sii nzuri hata kidogo na wala sii uungwana kwa sababu siasa sio biashara ni maelewano ambayo yanahitaji uaminifu na makubaliano ambayo hayawezi vunjika mara tu unapofanikiwa na kutaka kuvuta asilimia yote 100 wewe.

Hizi tabia za kusema CUF wana wivu ni tabia za kishenzi tu, ni tabia zisizokuwa na shukranii kutofikiria ulitoka wapi na leo umefika wapi ukasahau kwamba pasipo ushirikiano wa mwenzako pengine usingefika hapo ulipo. Alichozungumza Rashid ndiyo hali halisi na sioni sababu kwa nini watu mlitaka afiche hali ndicho kilichotokea hadi kutokuwepo ushirikiano baina ya vyama kuunda kambi ya Upinzani. Sasa kama Chadema mnafikria mnaweza kwenda solo baada ya mafanikio mloyapata uchaguzi huu, sawa endeleeni kufurahia matunda hayo lakini amini maneno yangu malipo yake yatakuja jitokeza muda sii mrefu... Itakula kwenu.

Mkuu,
Nilikuwa nimeanza kupata wasiwasi kama kweli ni wewe ndio umeandika hii maneno manake inaonekana kiwango chake kiko chini sana kwa mtu kama wewe lakini nilipofika hapo kwenye red bold nikaamini kwamba ni wewe mwenyewe Bob.
Nadhani ukirudia hali yako ya kawaida utakuja na mawazo mazuri zaidi kuliko haya mkuu. CUF wana muafaka na CCM na hakuna anayejua nini kilichomo kwenye makubaliano yao. Kwahiyo sio suala la kuamka tu na kuunda umoja usioeleweka kwa kuwa tu chadema iwafurahishe CUF(CCM). NCCR, TLP na UDP wanajulikana wako upande gani sasa mkuu bado tu hulioni hilo? unataka tu chadema iungane nao ili ufurahi? hapana bana, hebu itendee haki chadema kwa hili japo kidogo.
 
Wakuu zangu hili sio swala la kupuuza hata kidogo. Chadema acheni uchu wa madaraka kuunda kambi ya Upinzani na haitawasaidia chochote zaidi ya kujenga fitna zaidi.
Kweli kabisa Chadema kulingana na katiba inayo haki ya kufanya kila kitu watakavyo isipokuwa mjue tu kinachozungumziwa zaidi na katiba ni jinsi ya kumpata kiongozi wa kambi hiyo ya Upinzani, kuliko uundwaji wa kambi yenyewe.

Vipengele vyote vinazungumzia nani atakuwa kiongozi wa kambi hiyo lakini haikatazi chama kuunda umoja na vyama vingine kwani maana ya kuunda kambi hiyo ni kutoa fursa kwa vyama vingine vipate nafasi ya kuzungumzia hoja walizokuwa nazo dhidi ya chama tawala. Kinyume cha vyama hivyo havitakuwa na nafasi hiyo isipokuwa kuuliza maswali ya nyongeza tu.

Leo hii wakuu zangu nimeamka vibaya na hakika sipendi kuzungumza mengi isipokuwa nasema Mkuu wangu Mbowe, ile tabia ya kuwatumia watu kisha ukawaacha mataani iache.. sii nzuri hata kidogo na wala sii uungwana kwa sababu siasa sio biashara ni maelewano ambayo yanahitaji uaminifu na makubaliano ambayo hayawezi vunjika mara tu unapofanikiwa na kutaka kuvuta asilimia yote 100 wewe.

Hizi tabia za kusema CUF wana wivu ni tabia za kishenzi tu, ni tabia zisizokuwa na shukranii kutofikiria ulitoka wapi na leo umefika wapi ukasahau kwamba pasipo ushirikiano wa mwenzako pengine usingefika hapo ulipo. Alichozungumza Rashid ndiyo hali halisi na sioni sababu kwa nini watu mlitaka afiche hali ndicho kilichotokea hadi kutokuwepo ushirikiano baina ya vyama kuunda kambi ya Upinzani. Sasa kama Chadema mnafikria mnaweza kwenda solo baada ya mafanikio mloyapata uchaguzi huu, sawa endeleeni kufurahia matunda hayo lakini amini maneno yangu malipo yake yatakuja jitokeza muda sii mrefu... Itakula kwenu.
Mkuu Mkandara...nakubaliana na ulichosema kwa 110% lakini validity yake nadhani imekuwa overtaken na time (or rather events).
Bond iliyopo kati ya CUF na CCM is just too strong to reverse. NCCR/TLP ndio hao, nao ni kama mouthpiece ya CCM.
Beats common sense how can Chadema fit into such chemistry without compromising their opposition stature.
 
Nadhani CUF inatumiwa na CCM ili kui-keep Busy CHADEMA huku CCM wakiwalaghai watanzania kua upinzani hauna lolote ila kulumbana tu kila siku. Huu ndio Mchezo unaochezwa sasa hivi. Ni Muhimu Chadema kuwa makini na CUF sana kwa sababu wako kwenye payrol ya CCM ili kuidhoofisha CHADEMA ambacho kimekua tishio kwa CCM.

Ni muhimu CHADEMA kutoa Msimamo wao wa Mwisho kuhusu hili swala na kuendelea mbele na shughuli yao ya kuwatumikia wananchi, Wasijisahau na kuingia katika Malumbano na CUF kwa sababu hawa wanafiki wako Kazini.

Kuhusu Kumkataa/Kumkubali JK, sijui kwanini CUF wanajiingiza katika hili wakati haliwahusu. inatakiwa awepo mtu wa kuwaambia CUF usoni kwamba hayawahusu na waache kuingilia mambo ambayo si ya kwao.

CUF should not interfere with how CHADEMA runs its affairs.Its none of their business, they should keep their comments and advices to themselves
:A S angry:
 
MBONA MNAVURUGA AKILI KAMA PUNGUWANI JAPO NAJUA ITS CONTRARY? KWANI CUF YA ZANZIBAR NA CUF YA BARA NI TOFAUTI? IWEKE IVI: kwani wajumbe (wabunge) wa Baraza la Uwakilishi visiwani, na wabunge wa hili la jamhuri ya muungano (bara & visiwani) wanaowakilisha CUF, ni CUF hiyo hiyo au kuna ya bara na visiwani? NI CHAMA KIMOJA CHENYE MRENGO/MWELEKEO MMOJA. SASA KAMA WAO VISIWANI NI WAMOJA NA CCM, itakuaje bara wawe tofauti....... KAMA HUIELEWI IYO KUMBUKA KUELIMIKA NI KULE KUBAKI MUELEWA BAADA YA KUSAHAU ULIYOFUNDISHWA SHULENI... Yule injinia (kingereza mbofu mbofu) aliegombea unaibu spika alijitoa amwachie CCM, ili akija kugombea uwakilishi SADEC CCM wampe kimahaba!!!! Sasa huo ni mwanzo tu... CUF si wapinzani tena, hamwelewi nini sasa? Sema wao ndo hawajielewi.... hau wanaelewa lakini wanataka watufanye hatwelewi... na sisi tunakaa tunawaskiliza....nafikiri ni ujinga mtupu huu....
 
mkuu tukiangalia hivyo na tukienda down that road utaanza kuona kwamba wote wana makosa. Maana cuf wanaonekana ni waislamu na chadema wakatoliki/wachaga. Udini upo na ukabila upo sikatai. Hata katika hali ya kawaida mtu ukiwa na nafasi uka kutana na mtu wa kabila lako au dini yako una kuta ni rahisi zaidi kuwasaidia ila haimaanishi wewe ni mkabila au mdini.

Ila mkuu hamna haja ya mimi na wewe kubishana. Unaweza kuwa sahihi kusema udini umechangia nami nasema muafaka nao kwa kiasi kikubwa umechangia. Mbona wakati cuf ndiyo wameunda baraza kivuli bunge lililo pita wali washirikisha chadema? Wakati huo udini haukuepo? Kwa mantiki hilo swala la kwanza linalo kuja kichwani mwangu ni kwamba it's not a matter of "udini" per se bali inferiority complex inayo izuia cuf kuwa chini ya chadema kwenye baraza kivuli ndani ya bunge.

hapo umenena mkuu
 
Mundo, you have nailed it all mkuu; kama kweli Hamad Rashid anaiponda CHADEMA kwa kutotaka kushirikisha vyama vingine vya upinzani zaidi ya CUF wao CUF na CCM wangeshirikisha vyama vingine pia kuunda serikali huko Zanzibra, kitu ambacho CUF hawakukifanya huko Zanzibar kwa nini wanalazimisha kifanywe na CHADEMA huku Bara? UNAFIKI!

Hapa ninachoona, na kipo wazi ni kuwa CUF kipo kwa manufaa ya Wazanzibari zaidi na si Watanzania, wao wamepata huko Zanzibar ambapo ndipo walipopapigania hadi kumwaga damu basi hawana haja na ukombozi wa Watanganyika!

Sio Kwa ajili ya Zanzibar... Kwa ajili ya Pemba...
 
NITARUDIA KUSEMA TENA NA TENA CUF NI WANAFIKI WAKUBWA NA NI WAFITINI.
Nasema hivyo kwa sababu CUF wameunda serikali ya ummoja wa kitaifa na CCM Zanzibar bila kuwashirikisha TADEA, UPDP, JAHAZI ASILI, NRA na vyama vingine. Kama wao wanaona CHADEMA ni wabaguzi kwa kuto kuwashilikisha NCCR MAGEUZI, UDP, na TLP kuunda serikali ya upinzani Bungeni kwanini wao wasinge kataa kuunda serikali ya umoja wa kitaifa kwa kushirikisha vyama vyote vya upinzani Zanzibar. Kuunda serikali ya ukweli wanashirikiana na chama kimoja (CCM) na kubagua wapinzani wengine, lakini kuunda serikali kivuli wanataka uwepo ushirikiano wa wapinzani wote si kuwa na chama kimoja (CHADEMA) mbona msimamo wao ni kwa serikali kivuli lakini kwa serikali halisi msimamo huo haupo?

Wanasema wapinzani wengine hawana wabunge au wajumbe wa baraza la wawakilishi ndio maana hawamo ktk serikali, si wangewateua hata wawili au mmoja kuwapa nafasi ya ujumbe wa baraza la wawakilishi na kumuingiza ktk serikali ya mapinduzi ili kuonyesha huo umoja wa kitaifa?

Ubaguzi wao umeanza toka ktk kujadili muafaka kwa kutoshirikisha vyama vingine, kama kweli wao si wabaguzi kwa nini ktk majadilianao ya muafaka walikuwa na CCM pekee na hawakuwashinikiza CCM kuwa na vyama vingine ili uwe muafaka wa Taifa la Zanzibar na si muafaka wa CCM na CUF. Inapofika sehemu kuna maslahi CUF wanataka kuwa peke yao na kuwatenga wenzao (mf serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar) hila linapofika swala hambalo halina maslahi ya kifedha (serikali kivuli ya muungano) CUF wanataka ushirikiano wa pamoja. Waache unafiki na ubaguzi wa ubara na upemba. kwanza wao ndio wabaguzi wakubwa kuliko CCM huko Zanzibar. KTK chaguzi wa mwaka huu wameibiwa ushindi wao lakini kwa kuwa wameahidiwa kuwemo serikalini wanacheka tu na kujifanya hawaoni wizi uliofanyika. waache CHADEMA waendeshe mapambano yao kwa kutumia mikakati yao na wao waendelee na uswahiba na CCM.

Mwaka 1995 walipokuwa wengi bungeni waligoma kuunda serikali kuvuli ya pamoja na NCCR leo wanajifanya wamesahau na kuwakumbatia NCCR ili wajue ni wanzao. kupoteza nafasi ya kuwa chama kikuu cha upinzani Tanzania kinawauma sana na wataumia sana hadi ifike 2015 watateseka kweli mioyoni mwao
 
Wakuu zangu,
yawezekana kweli bado sijaamka lakini yanitisha sana kuona huu muafaka baina ya CUF na CCM umekuwa kidonda kikubwa cha Upinzani hasa tukizingatia kwamba CUF wameyafanya yote haya kwa faida ya Wazanzibar. Labda tunachoshindwa kuelewa ni kwamba bado tupo ktk mfumo wa chama kimoja na CCM ndiye anaamua kila kitu kulingana na mustakabali wa Taifa letu kama wanavyoliangalia wao.

Ikumbukwe tu kwamba Muafaka baina ya CUF na CCM umefanyika wakati bunge letu lipo na hakuna chama wala kiongozi yeyote wa Upinzani aliyesimama na kupinga Muafaka huo kulingana na sheria. Kama kweli Upinzani upo nadhani la muhimu ilikuwa kupinga muafaka huo kwanza kisheria kwani binafsi ingawa sii mwanasheria lakini nadhani CCM na CUF walipindisha sheria kuunda muundo mpya wa serikali ya Zanzibar kinyume cha katiba hivyo kuwanyima fursa hiyo vyama vingine kushiriki kikamilifu, kiasi kwamba vyama vingine havitakuwa na nafasi ya kuunda serikali isipokuwa CCM na CUF au kutakuwepo na aina mbili ya serikali ile ya kikatiba na hiyo ya CCM na CUF..

Kwa hiyo, nachozungumzia mimi ni Upinzani ktk serikali ya Muungano na laukama CUF wameungana na CCM na mnaamini kwamba wameungana kutokana na muafaka ulofanyika Zanzibar basi nadhani ipo kila sababu kupinga muafaka huu kisheria kwanza kuliko kuweka madai haya na kuyapa uhalali. Kama kweli hii ndio sababu iliyotangulia kwa nini Chadema waliwafuata CUF na kutaka kuunda Upinzani nao hali wakijua kwamba CUF ameungana na CCM? kwa nini Chadema wasiwafuate vyama vingine badala ya CUF na kama wote hawa hawaaminiki Chadema anapungukiwa kipi ikiwa ushirikiano wenyewe ni wa bungeni tu...

Sasa labda nizungumzie Political strategic hateful attitudes...
Kwanza niwape mfano wa kimaisha ili mpate kunifahamu vizuri where do I come from..na mifano yangu ni ile ile asoipenda Mwanakijiji..

CCM na CUF wameklubaliana Unyumba pasipo ndoa na CUF kama mwanamke malaya ametaka unyumba na Chadema lakini Chadema hawataki kwa sababu CUF kawekwa kinyumba na CCM ili apate kujengewa nyumba yake huko Unguja. Lakini kuwepo sababu hizo Chadema hawataki tena mahusiano na CUF pamoja na kwamba Chadema wanajua sababu ya CUF kukaa na CCM hivyo kuhofia matokeo ya relation baina yao.

Sasa mimi nasema hivi huu ni wivu wa kijinga ikiwa Chadema anafahamu fika kwamba CUF anafanya umalaya wa kisiasa ili afanikishe sera zake ndani ya utawala wa CCM. Na maadam mbaya wa Chadema ni CCM strategically Chadema anatakiwa kumuumiza CCM kwa kila nafasi anayopata na moja wapo ni hii ya kushirikiana na CUF na vimada wake wote ktk baadhi ya maswala. Nikirudi ktk mfano wangu pale juu, mtu yeyote mwenye mahusiano na ametumia fedha na muda wake kumjenga, akisikia kuna mhuni anapiga kwa pembeni pasipo gharama itamuuma zaidi na pengine kuwa na wasiwasi zaidi na mahusiano baina yao.

Kwa maana hiyo Chadema kama chama wanatakiwa kuwa na mbinu za kuwaangusha CCM na mojawapo ni kuendelea ushirikiano na CUF pale inapohitajika kukidhi haja za Chadema kama ilivyokuwa toka mwanzo. CCM wanajulikana ni mafisadi tena ktk hili ndio kabisa wamemchukua mke wa mtu na kumweka kinyumba..Chadema wasifanye hasira kama kweli mufaka huo ndio unawauma zaidi basi wafikishe mashataka yao mahakamani ili kupata sheria. Lakini tunapoendelea kudai kwamba CUF nbdio walikuwa hawataki ushirikiano hali Chadema ndio tumewapa nafasi hiyo kwa masharti nadhani ni bora tuwe wakweli. Tukubali kwamba Chadema imekataa ushirikiano na CUF kwa sababu CUF imetaka vyama vingine vishirikishwe lakini hili halikubaliki na Chadema na kwa sababu zifuatazo.

Again, nashindwa kuelewa kwa nini tuwakaribishe CUF ktk ushirikiano na tuwaache wengine hali CUF amekaa vibaya zaidi ya NCCR -Mageuzi au TLP ukichukulia muafaka uliopo baina ya CUF na CCM. Wakuu zangu sintapenda kuendelea na ubishi huu lakini utetezi wa wana Chadema hauna mantiki hata kidogo ikiwa Chadema waliwafuata CUF kisha leo tunasema hatuwataki CUF kwa sababu ya ushirika wake na CCM...Je, Chadema hawakuona ubaya wa mahusiano hayo toka mwanzo kabla hawajawafuata CUF?

Nazidi kuwaumiza vichwa!
 
- Well, hii ni nothing but cheap politics halafu you wonder who is immature here Mwenyekiti wa Chadema aliyeongea naye huyu kiongozi wa CUF in private, au huyu kiongozi wa CUF aliyeyaleta mambo ya Private kwenye Public? Sasa unaunda vipi umoja wa Upinzani bungeni na viongozi kama hawa wasioelewa kutenganisha maana ya ishus za private na ishus za public!

- I mean mambo kama haya yataishia kurudisha nyuma tu momentum ya ari ya wananchi waliyoionyesha kwenye huu uchaguzi kwamba wanataka mabadiliko, sasa kama CUF hawaelewi basi dawa ni kuachana nao tunachotaka ni upinzani wa kweli bungeni ili taifa liweze kunufaika na uwajibikaji utakaoletwa na Upinzani kweli bungeni hata kama ni mdogo, maana sasa itakwua nguvu ya hoja zaidi kuliko uwingi wa wabunge wa chama,

- CUF someni mabadiliko ya nyakati wananchi hawana tena muda wa kupoteza na hizi habari zisizo na anything good kwa taifa, zaidi tu ya kutafuta cheap popularity ambayo kama imeshindikana kupatikana kwenye kura, haiwezi kupatikana kwa kulumbana kwenye public na wapinzani wengine!, it stinks!


William.
Hivi tuongeze ukweli upi zaidi ya huu? Thanks William. Be Blessed a million times.
 
Loud and clear... CUF wameamua kuwa wanafiki... lakini cha maana ni chadema kurudi kambini na kupanga upya mambo yao

Thanks for the post
Have you seen post number 3 Mh. Acid? It is so clear that Chadema will never surrender to CUF.
Kama wanadhani bado wao wanaweza kuunda kambi yao waendelee tu lakini wajue haina nguvu kwa namna yoyote ile. Wataishia kuwa wanahama viti siku Chadema waki boycott hotuba za Kikwete! No way!
 
HIYO HABARI YENYEWE NAONA UMEITOA KWENYE GAZETI LENYE KINYESI CHA NGURUWE HABARI LEO GAZETI LINALONAJISIWA KILA KUKICHA,JANA MHARIRI WAKE KAANDIKA TAHARIRI YAKE AKISEMA HIVI chadema acheni kurudisha maendeleo ya watanzania nyuma. JAPO KUWA SINA KIPATO CHA KUNUNUA GAZETI NA MAGAZETI NAYASIKILIZIA YAKISOMWA REDIONI.NALICHUKIA HABARI LEO KAMA MATAPISHI
Nilikuwa nalisoma mtandaoni lakini nimeliondoa hata kwenye cookies zangu! Silitaki kabisa kama nisivyotaka Uhuru na magazeti yote ya Rostam.
 
Loud and clear... CUF wameamua kuwa wanafiki... lakini cha maana ni chadema kurudi kambini na kupanga upya mambo yao

Thanks for the post

I secondyou mkuu!! Ni wakati wa kuwa careful na kila move!! Thanks mkuu!!:smile-big:
 
Kikwete na sera ya udini
Hivi leo nimesikia kikwete anasema kuna udini mkubwa sana hapa Tanzania na akaongea kwa msisitizo kabisa,guys is it true?
 
Acid, Hivi kweli unafikiri kwa hali ya kawaida, CHADEMA wanaweza kuungana na CUF ambao wameungana na CCM? Japo CHADEMA waliextend hiyo invitation, do you realy think it can work. Kwamba CHADEMA wa team up na Mapandikizi ya CCM na washirika wakuu CCM (CUF)? How do you real expect CHADEMA to share political secrets and strategies without feeling vulnerable. Well they are aloneand have kept their doors open. Ndo wameanza let's wait and see what will become of the opposition in the paliament.
 
Hapo ndo inajulikana kuna upinzania au kuna kutafuta sifa na vyeo thanks kwa wachangiaji kama @Nikupateje. Hawa cuf ndo Bure bureshi hamna kitu kabisaa wacha wabwabwaje maana hawana jipya kwishinei hoja zao zimemezwa sasa wanakimbilia kushabulia upande wao!!!
 
Eti CHADEMA WAMEWAKWAZA MBATIA NA LIMBUKA HIVYO INABIDI WAENDE WAKAONGEE NAO NY.................O!! KWA LIPI HASA LA KUWABEMBELEZA NYIE WAPINZANI FAKE? KWANZA YA NINI KUPOTEZA MUDA WA BURE WAKATI CUF NI CCM NA IKO SERIKALINI TAYARI TENA SERIKALI HARAMU NA BANDIA ISIYOCHAGULIWA NA WANANCHI SASA WATAKUWAJE WAPINZANI WA KWELI? MBOWE ALICHOFANYA NI KUONDOA LAWAMA NDIO AKAMWITA HUYO ASIYEJUA KUTUNZA SIRI CHEMBA NA SIYO KAMA HAMAD ANAVYOTAFSIRI KUWA CHADEMA HAWANA UWEZO WA KUJIONGOZA BILA WAPINZANI WENGIE, HAHAHAHAHAHAHAH LOOOOOOOOO HUYO MPINZANI NANIIIIII...MREMAAA, MBATIAAAA, CUF WANAOKULA KUKU SAIVI NA MAFISADIII.. TUACHE UNAFIKI JAMANI CHADEMA NDIO CHAMA CHA WANANCHI NA NDIO WAPINZANI WA KWELI BUNGENI..CHADEMA MMOJA NI KAMA ELFU MOJA HAHAHAHAHAHA
 
- Well, hii ni nothing but cheap politics halafu you wonder who is immature here Mwenyekiti wa Chadema aliyeongea naye huyu kiongozi wa CUF in private, au huyu kiongozi wa CUF aliyeyaleta mambo ya Private kwenye Public? Sasa unaunda vipi umoja wa Upinzani bungeni na viongozi kama hawa wasioelewa kutenganisha maana ya ishus za private na ishus za public!

- I mean mambo kama haya yataishia kurudisha nyuma tu momentum ya ari ya wananchi waliyoionyesha kwenye huu uchaguzi kwamba wanataka mabadiliko, sasa kama CUF hawaelewi basi dawa ni kuachana nao tunachotaka ni upinzani wa kweli bungeni ili taifa liweze kunufaika na uwajibikaji utakaoletwa na Upinzani kweli bungeni hata kama ni mdogo, maana sasa itakwua nguvu ya hoja zaidi kuliko uwingi wa wabunge wa chama,

- CUF someni mabadiliko ya nyakati wananchi hawana tena muda wa kupoteza na hizi habari zisizo na anything good kwa taifa, zaidi tu ya kutafuta cheap popularity ambayo kama imeshindikana kupatikana kwenye kura, haiwezi kupatikana kwa kulumbana kwenye public na wapinzani wengine!, it stinks!


William.

Hivi ni Malecela kweli kaandika haya? Nashangaa. Congrats!!!!!!!
 
Back
Top Bottom