Nasema CDM iwakaribishe lakini lazima CUF wajue bwana mkubwa ni nani siku CDM ikiandaa maandamano kule zanzibar Seif awe tayari kuyapokea.KAFU mbona wanakua kama ma...laya ...kule zanzibar wameshirikiana na sisiem wakaunda serikali ya mapinduzi ... huku bara wanataka waungane na CDM waunde serikali kivuli ya upinzani.... sasa wachague bwana mmoja tu...sisiem au CDM .... kama wanataka kuungana na CDM waipe talaka sisiem
CDM wasithubutu kabisa kabisa kufanya kosa kama hilo...please CDM! Hivi hamfahamu kama CUF inafadhiliwa na RA -- ambaye ni hasimu mkubwa CDM?
Puuzeni ninalowaambia mtakuja juta. Hili suala la Dowans ndilo RA anataka kuanza nalo Bungeni kwa kuitumia CUF. Watch out!!!!
Tujute mara ngapi CCM wameshatujutisha siku nyingi kawashauri kwanza viongozi wako wa CCM ndio uje kuishauri Chadema.Wewe unajua kwa nini SABODO kada CCM anawapa Chadema pesa? Muhindi mtu hatari mtakuja juta. Watch out!!
Tujute mara ngapi CCM wameshatujutisha siku nyingi kawashauri kwanza viongozi wako wa CCM ndio uje kuishauri Chadema.
Wapinzani wamsihi Mbowe
Kambi ya upinzani isiyo rasmi bungeni imemuandikia barua Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kuomba wachaguliwe kuunda Baraza la Mwaziri Kivuli kwenye Bunge ili waweze kushirikiana kwa dhati kama kambi ya upinzani.
Katika barua ya kambi hiyo iliyosainiwa na mwenyekiti wa kamati hiyo Hamad Rashid na katibu wake David Kafulila kwenda kwa Mwenyekiti wa Chadema wamesema wanaomba ushirikiano huo uanze kwenye Mkutano wa Bunge unaotarajiwa kuanza Februari mwaka huu.
Kambi hiyo ilimsihi Mbowe kuunda kambi ya upinzani imara ikishirikisha vyama vyote vya upinzani ili kuimarisha nguvu ya upinzani bungeni na kuibana serikali ya CCM kwa pamoja.
Vyama vilivyotoa ombi hilo ni CUF chenye wabunge 33, NCCR Mageuzi chenye wabunge wanne, TLP mbunge mmoja na UDP mbunge mmoja wakati Chadema kikiwa na wabunge 47.
Chadema ambacho ndicho chama kikuu cha upinzani kimeunda kambi ya upinzani peke yake huku mwenyekiti wake akichaguliwa kuwa kiongozi wa kambi hiyo na nafasi nyingine za mawaziri kivuli zikijazwa na wabunge wa chama hicho pekee…..
Habari zaidi katika Mwananchi Jumapili.
Kweli Chadema viongozi wake ni wasomi? ni viongozi wawili ndio wasomi ZITTO na LISU ndio wamesoma UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM wengine kama watakuwa wamesoma basi vyuo vya katachadema inaviongozi makini na wasomi wanajua upepo wa siasa kwenda nao, hivyo basi wao wataona umuhimu wa kuwakubali au la. tuunge mkono lolote watakaloafiki. tunachohitaji ni mabadiliko. tumechoka usisiemu.
Unafikiri hamjulikani, ni sawa na nyani kujificha kwenye shamba la karanga huku mgongo wote ukionekana.Wewe ndugu yangu mtu akiwa tofauti na Chadema lazima ni CCM..
Una maana maamuzi magumu.hapa busara zinahitajika sana..kabla ya kutoa maamuzi mepesi
Hao CUF ni wakuchinjia baharini tu!!! How can we sleep with the enemy and be safe??? A friend of our enemy is our enemy!!!!!
Hawa jamaa walishafunga ndoa na CCM, hapo hapo wanahitaji kujamiiana na CDM, je wana mapenzi kweli na CDM?Una maana maamuzi magumu.
Kweli ukipenda chongo utaona kengeza, kama ni hivyo ina maana CCM na wasomi wake wote inahangaishwa na wasomi wawili tu wa CDM, basi mbumbumbu mko wengi sana humo CCM.Kweli Chadema viongozi wake ni wasomi? ni viongozi wawili ndio wasomi ZITTO na LISU ndio wamesoma UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM wengine kama watakuwa wamesoma basi vyuo vya kata
Naona umepata maneno STAR TV, unayafanyia kaziUnafikiri hamjulikani, ni sawa na nyani kujificha kwenye shamba la karanga huku mgongo wote ukionekana.