CUF sasa wawapigia magoti CHADEMA

CUF sasa wawapigia magoti CHADEMA

cdm tulishasema milango yetu ipo wazi, tuwapokee lkn tuwe waangalifu
 
KAFU mbona wanakua kama ma...laya ...kule zanzibar wameshirikiana na sisiem wakaunda serikali ya mapinduzi ... huku bara wanataka waungane na CDM waunde serikali kivuli ya upinzani.... sasa wachague bwana mmoja tu...sisiem au CDM .... kama wanataka kuungana na CDM waipe talaka sisiem
Nasema CDM iwakaribishe lakini lazima CUF wajue bwana mkubwa ni nani siku CDM ikiandaa maandamano kule zanzibar Seif awe tayari kuyapokea.
 
CDM wasithubutu kabisa kabisa kufanya kosa kama hilo...please CDM! Hivi hamfahamu kama CUF inafadhiliwa na RA -- ambaye ni hasimu mkubwa CDM?

Puuzeni ninalowaambia mtakuja juta. Hili suala la Dowans ndilo RA anataka kuanza nalo Bungeni kwa kuitumia CUF. Watch out!!!!

Wewe unajua kwa nini SABODO kada CCM anawapa Chadema pesa? Muhindi mtu hatari mtakuja juta. Watch out!!
 
Kuwapokea ni vyema. Lakini lazima waseme walivyozitumia kura zao nyingi kuuzofisha upinzani bungeni. Mathalani kura za spika na naibu spika zote walipeleka ccm. Pia kura Mea na naibu mea kule mwanza walipeleka ccm, ni kwa vile tu cdm ilikuwa na wajumbe wengi, vinginevyo wasingeshinda nafasi hzi mbili.
Wajihoji na kujipima kama kweli bado wapo miongoni mwa wanaopigania mabadiliko. Wakati mwingine inaonekana kama washafika vile
 
Wewe unajua kwa nini SABODO kada CCM anawapa Chadema pesa? Muhindi mtu hatari mtakuja juta. Watch out!!
Tujute mara ngapi CCM wameshatujutisha siku nyingi kawashauri kwanza viongozi wako wa CCM ndio uje kuishauri Chadema.
 
Chadema haiwezi kushirikiana na cuf maana cuf sio chama cha upinzani. cuf ina-form part of the govt, hivyo hawataweza kuwa wapinzani kamili!
 
chadema inaviongozi makini na wasomi wanajua upepo wa siasa kwenda nao, hivyo basi wao wataona umuhimu wa kuwakubali au la. tuunge mkono lolote watakaloafiki. tunachohitaji ni mabadiliko. tumechoka usisiemu.
 
Tujute mara ngapi CCM wameshatujutisha siku nyingi kawashauri kwanza viongozi wako wa CCM ndio uje kuishauri Chadema.

Wewe ndugu yangu mtu akiwa tofauti na Chadema lazima ni CCM..
 
Wapinzani wamsihi Mbowe

Kambi ya upinzani isiyo rasmi bungeni imemuandikia barua Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kuomba wachaguliwe kuunda Baraza la Mwaziri Kivuli kwenye Bunge ili waweze kushirikiana kwa dhati kama kambi ya upinzani.

Katika barua ya kambi hiyo iliyosainiwa na mwenyekiti wa kamati hiyo Hamad Rashid na katibu wake David Kafulila kwenda kwa Mwenyekiti wa Chadema wamesema wanaomba ushirikiano huo uanze kwenye Mkutano wa Bunge unaotarajiwa kuanza Februari mwaka huu.

Kambi hiyo ilimsihi Mbowe kuunda kambi ya upinzani imara ikishirikisha vyama vyote vya upinzani ili kuimarisha nguvu ya upinzani bungeni na kuibana serikali ya CCM kwa pamoja.

Vyama vilivyotoa ombi hilo ni CUF chenye wabunge 33, NCCR Mageuzi chenye wabunge wanne, TLP mbunge mmoja na UDP mbunge mmoja wakati Chadema kikiwa na wabunge 47.

Chadema ambacho ndicho chama kikuu cha upinzani kimeunda kambi ya upinzani peke yake huku mwenyekiti wake akichaguliwa kuwa kiongozi wa kambi hiyo na nafasi nyingine za mawaziri kivuli zikijazwa na wabunge wa chama hicho pekee…..


Habari zaidi katika Mwananchi Jumapili.


a friend of our enemy(ccm) is also our enemy(cuf).

CDM. you have Tanzanians backing. Why bother with double-standard parties?
 
Hao CUF ni wakuchinjia baharini tu!!! How can we sleep with the enemy and be safe??? A friend of our enemy is our enemy!!!!!
 
chadema inaviongozi makini na wasomi wanajua upepo wa siasa kwenda nao, hivyo basi wao wataona umuhimu wa kuwakubali au la. tuunge mkono lolote watakaloafiki. tunachohitaji ni mabadiliko. tumechoka usisiemu.
Kweli Chadema viongozi wake ni wasomi? ni viongozi wawili ndio wasomi ZITTO na LISU ndio wamesoma UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM wengine kama watakuwa wamesoma basi vyuo vya kata
 
hapa busara zinahitajika sana..kabla ya kutoa maamuzi mepesi
 
Wewe ndugu yangu mtu akiwa tofauti na Chadema lazima ni CCM..
Unafikiri hamjulikani, ni sawa na nyani kujificha kwenye shamba la karanga huku mgongo wote ukionekana.
 
well said Mbaha, a friend of our Enemy is our enemy indeed
Hao CUF ni wakuchinjia baharini tu!!! How can we sleep with the enemy and be safe??? A friend of our enemy is our enemy!!!!!
 
Si busara kuwadis bila kuangalia ajenda wanayotaka kuileta mezani! Kwa maoni yangu, CDM wakae na watafakari ni ajenda gani wanaileta sasa, inaweza wanufaisha na wao kisiasa zaidi kuliko tunavyofikiria!
 
Una maana maamuzi magumu.
Hawa jamaa walishafunga ndoa na CCM, hapo hapo wanahitaji kujamiiana na CDM, je wana mapenzi kweli na CDM?
iNAWEZEKANA wakawa na nia ya ukombozi lakini approach yao haikuwa nzuri sana, kwani toka mwanzo wamekuwa wakiikandia CDM kama wao sio chama cha Upinzani.
Pili, kuwa kuwakubali kama wakiwa na nia nzuri will be a milestone idea kwa sababu kila hoja itakayoibuliwa bungeni wapinzani watakuwa na nguvu sana wala hawatayumbishwa...
 
CDM mliona body language ya Lipumba na Mama Kombani siku ya kongamano UDASA? Najua kuna intelligent people ndani ya chadema wanaoweza kufanya maamuzi yenye akili.
 
Kweli Chadema viongozi wake ni wasomi? ni viongozi wawili ndio wasomi ZITTO na LISU ndio wamesoma UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM wengine kama watakuwa wamesoma basi vyuo vya kata
Kweli ukipenda chongo utaona kengeza, kama ni hivyo ina maana CCM na wasomi wake wote inahangaishwa na wasomi wawili tu wa CDM, basi mbumbumbu mko wengi sana humo CCM.
 
Back
Top Bottom