CUF sasa wawapigia magoti CHADEMA

CUF sasa wawapigia magoti CHADEMA

CUF tangu uchaguzi uishe kazi yao kubwa imekuwa moja tu. Kuishambulia CDM kushoto na kulia.
Hata humu JF, wapenzi wa cuf (wakiongozwa na Mwiba) badala ya kuisapoort CDM, wamekuwa ndio wapinzani wakubwa wa CDM.
Sasa najiuliza, ghafla haya mapenzi kwa CDM yametoka wapi????
Cheyo naye aliponda sana CDM walipotoka bungeni na alimponda Marando eti hafai kuwa spika, na kusema ni afadhali yule mama wa ccm.
Mrema ndio usiseme, yeye imebaki achukue kadi ya ccm tu.

Can you really believe watu hawa wana interest za upinzani in their hearts?

Lazima ipo ajenda imesukwa na ccm na hawa makanjanja ya kutaka kuihujumu CDM.
 
let CUF go to hell...! pesa za RA zinanuka inbidi zitakaswe kwanza ndo zifae kwa matumizi halali....!
 
Kwenye mdahalo na Mbowe, Hamadi Rashidi alionekana kuumia roho zaidi kuhusu bajeti ya ofisi ya kambi ya upinzania bungeni, kwamba sasa itakuwa inakwenda chadema peke yake.

kule zanzibar walipotupiwa mpunga kidogo wakaharakisha kukubali kuingia kwenye serikali ya umoja wa kitaifa. tukumbuke awali, maalim seif hakuamini kwamba serikali ya umoja wa kitaifa ikiundwa kwamba atapata ulaji na hivyo alizunguka akihamasisha wananchi wamuombe Karume aendelee kuongoza (kwa sababu tu Karume alianza kumwalika kwenye workshop za serikali)

inawezekana kwa kipindi kifupi ambacho wamekuwa kwenye ndoa ya mashaka na ccm wameona hawatapata chochote kwa hiyo sasa wanataka kurudi kwenye kambi rasmi ya upinzani angalau waambulie mgao kidogo.

hivyo mimi naona maombi yao yanasukumwa zaidi na njaa kuliko nia ya dhati ya kuimarisha upinzani bungeni. naomba mnikosoe please.
 
Jamani mtu akikosa na akajua kuwa amekosea akiomba msamaha huwa anasamehewa kwa nianjema kabisa. Hawa wamegundua walikosea kwa hiyo wanataka kurudi kundini. simbaya tuwaruhusu. Angalizo wasije wakawa na tamaa ya madraka makubwa matokeo yake walete mtafaruku. Nakumbuka Hamad alipewa hadi ofa na Zito ya kuachiwa nafasi akagoma kwahiyo inabiditu akubaliane na nafasi atakayo pewa hatakama ataona haina masilahi kihiiivyo. Chadema wanapenda kushirikiana sema jamaa maringo sana hadi waliboaaaaaaaaa.
 
Hamad hajasema ishirikishwe CUF bali vyama vyote vya upinzani. Huo ndio msimamo wake siku zote. Kwanini hamkuwi vijana wa chadema na still mnaamini mngeshinda umeya Arusha.
 
No intelectual inputs in this thread, sijaona sababu ya Chadema kutokuwa pamoja na CUF, unless otherwise mtu u-nullify kuwa CUF si wapinzani.

we have a long way to the real politics.........CUF kuunda serikali ya umoja na CCM then sio wapinzani!!! what a shame

mabadiliko tunataka kwa vitendo vyetu tunayachelewesha!!! yaani wapinzani wenyewe wanaanza kupingana hivyo kuipa CCM nguvu, jamani umoja ni nguvu..mpaka sasa madhara ya kutokuwa wamoja yameishaonekana msitake kujifanya hamuoni!!!
 
cdm wawasamehe cuf na vyama vingine japo walikuwa upande wa ccm wakati wa mchakato wa kupiga kura ya kumchagua spika na naibu wake.vyama vingine vilionesha tabia isiyo ya kipinzani kwa kukiunga mkono ccm lakini kwa vile katika siasa hakuna adui wa kudumu, basi inabidi cdm wafikirie ombi hilo.
 
CHADEMA msisahau uchaguzi wa spika na naibu spika! CUF hawakuwaunga mkono kwa wagombea wenu, hiyo inaweza kuwapa ishara ya walichonacho moyoni na akilini mwao! Lakini pia hata bunge lililopita CUF ilikuwa na wabunge wengi lakini hawakuwa na la maana! Kambi ya upinzani siyo idadi ya wabuge, ni uwezo wa kuchambua na kuwasilisha hoja makini! Wabunge 31 kati ya 33 wa CUF wanatoka zanzibar na huko CDM haina mvuto, hvyo wanakosa uelewa mpana wa matatizo ya watanganyika! CUF wana lao! Kwanini wanalilia sana hiyo kambi? Waondoke CUF wajiunge CDM ndo waingizwe kambini! Kama hawataki waendeleze muafaka wao na CCM!
 
Spika wa bunge, Anne Makinda, amesema kwamba haiwezekani kuwa na kambi mbili za upinzani bungeni kwa sababu siyo sheria.

Source: TBC1 taarifa ya habari usiku huu
 
Back
Top Bottom