CUF sasa wawapigia magoti CHADEMA

Vyama vyote ukipima kwa usomi chama chenye viongozi wasomi ni CUF peke yake

Umekalilishwa vibaya bila kuchambua, unadanganya hadharani kama wanavyosema kuwa, idadi ya waislamu ama ni kubwa au inalingana na idadi ya wakristo nchini.

Chama Cha Mafisadi ndicho chenye wasomi wengi sana ila wameleta maendeleo gani ya maana ukilinganisha na rasilimali tulizo nazo? Zaidi sana wame nyang'anya haki za raia na kuongeza ufisadi nchini.
 
kwenye siasa hakuna rafiki wa kudumu wala adui wa kudumu.tujifunze uvumilivu.Mbowe,naomba uwapokee wana wapotevu.
 
Busara zaidi itumike kupima upepo wa kisiasa, Kama una maslahi kwa Wananchi, na kama wana dhamira ya kweli, ya kubeba dhana ya Upinzani bungeni,
Japo hali ya kuwa amini inapungua na hilo wao wanalifahamu. Kitendo cha Madiwani wa CUF Mwanza kuwapigia CCM inanitoa imani ya kuwa wapinzani wa kweli Inawezakana waliteleza wakagundua wamekosa na wanataka kujirudi.
Heri aliye tambua kosala lake akajutia maana ana weza kuwa mtu wa manufaa.
Kuliko ana bakia kudhani kadhulumia.
No true enemy in politics
 
Naamini cdm hawawezi kuwapa chochote..kwakuwa ni walafi wa madaraka

Hata wakiwapa it does not change anything...in Tanzanian politics..nothing
Wakati Hamad Rashid anasusa alifikiri atabembelezwa leo ndio anaona umuhimu wake, kwa uroho wake akaunda serikali kivuli ndogo akifikiri serikali itampa bajeti ya kuiendesha.

Nashauri CDM wakiwakaribisha CUF, HR asipewe wizara yeyote maana ameonesha shida yake ni uroho wa madaraka, soma signature yangu ujue uroho wake.
 
Yeah -- ni kweli. Kura zote walizopata wabunge wa CUF huko Pemba na Unguja hazizidi kura alizopata Halima Mdee kule Kawe. Uko nami?

yeah-- ni kweli kabisa nakubaliana na wewe. Diwani wa kata ya mwananyamala kura alizopata nyingi kuzidi za mbunge wa Hai Mbowe
 
Wakati Hamad Rashid anasusa alifikiri atabembelezwa leo ndio anaona umuhimu wake, kwa uroho wake akaunda serikali kivuli ndogo akifikiri serikali itampa bajeti ya kuiendesha.

Nashauri CDM wakiwakaribisha CUF, HR asipewe wizara yeyote maana ameonekama shida yake ni uroho wa madaraka, soma signature yangu ujue uroho wake.

I see no impact wapewe wasipewe..nothing

Besides, cdm niwajuavyo hawawezi kuwapa..kwakuwa ni walafi wa madaraka
 
Mimi hapa namsaidia mwanagu hesabu nyie mnatupiana maneno tu. Sawa tu endeleeni kunisumbua j2 yote hii eti wengine wasomi, sijui vimada mapenzi yamechuja sasa wanataka kuwa viruka njia, sawa endeleeni mi nawasikiliza. Bora PJ alitueleza mapinduzi yaliyotokea Makumira!
 
I see no impact wapewe wasipewe..nothing

Besides, cdm niwajuavyo hawawezi kuwapa..kwakuwa ni walafi wa madaraka
Yes you can pretend that you dont see the difference that is up to you but people like HR knows the impact of it.
 
Yes you can pretend that you dont see the difference that is up to you but people like HR knows the impact of it.

Why should i pretend? is it what you do pretending?

HR is nothing to the political equation of Tanzania.

I see no impact, wakipewa au wasipewe...

They are already divided "there is no way watakuwa pamoja" kiseera wala kimtazamo
 
Hawafai kwa tabia zao.
Wamejikomba CCM eti serikali ya umoja. Sasa wanagundua maamuzi makubwa wanatengwa. Si wameona ktk DOWANS chama ndo kinabariki malipo yafanywe!

CUF Muliulizwa? Umoja upi mulionao?
 
Siasa za hivi sasa hapa nchini zinahitaji nguvu kubwa ya pamoja kuweza kutoa msukumo mkubwa wa kuondoa maudhi dhidi ya jamii na kuleta maendeleo. Siasa za kukamiana au kukomoana haziwezi kuleta mafanikio, sana sana zinatoa mwanya kwa walio kwenye dola kuendelea kupeta. Chadema watafakari sana hili ombi kutoka kwa wenzao, maslahi ya nchi kwanza vyama baadaye.

Hakuna ubaya wowote kushirikiana na vyama vingine iwapo wameonyesha nia ya dhati kufanya hivyo. Kumbuka, baraza kivuli sio ndoa ya kudumu. Iwapo itabainika chama au vyama wenziwao wanaonyesha usaliti kwenye kambi basi kwa kuzingatia wingi wao Chadema wanaweza kufanya mabadiliko kulingana na wakati na kusonga mbele.

Wapeni nafasi.
 
Siasa za hivi sasa hapa nchini zinahitaji nguvu kubwa ya pamoja kuweza kutoa msukumo mkubwa wa kuondoa maudhi dhidi ya jamii na kuleta maendeleo. Siasa za kukamiana au kukomoana haziwezi kuleta mafanikio, sana sana zinatoa mwanya kwa walio kwenye dola kuendelea kupeta. Chadema watafakari sana hili ombi kutoka kwa wenzao, maslahi ya nchi kwanza vyama baadaye.

Hakuna ubaya wowote kushirikiana na vyama vingine iwapo wameonyesha nia ya dhati kufanya hivyo. Kumbuka, baraza kivuli sio ndoa ya kudumu. Iwapo itabainika chama au vyama wenziwao wanaonyesha usaliti kwenye kambi basi kwa kuzingatia wingi wao Chadema wanaweza kufanya mabadiliko kulingana na wakati na kusonga mbele.

Wapeni nafasi.
Hebu niambie itasaidie nini kwa mfano?
 
CDM wasithubutu kabisa kabisa kufanya kosa kama hilo...please CDM! Hivi hamfahamu kama CUF inafadhiliwa na RA -- ambaye ni hasimu mkubwa CDM?

Puuzeni ninalowaambia mtakuja juta. Hili suala la Dowans ndilo RA anataka kuanza nalo Bungeni kwa kuitumia CUF. Watch out!!!!

Who is RA by da way? mtajeni sasa. mafumbo ya nn? muungano ni muhimu kwenye mambo ya msingi. 2naitaji nguvu kubwa kuwatoa hawa mafisadi! so kama wana tatizo chadema sio wapuuzi. acha woga wa kitoto.
 
mimi Binafsi sina imani sana na huo Muungano, mi nadhani Cuf wapp kimaslahi zaidi kuna kila haja ya uongozi wa chadema kua makini kbala nya kuamua kushirikiana na Cuf.
 
Chadema kuna wanasheria wa kutosha na wasomi wa darasani. Hapa kifuatacho namuomba mbowe awape nafasi ila tu zile zinazoweza kufutwa na cdm kama kafu watawasaliti. Kama wote watakubali waingie kwa makubaliano ya kutopinga adhima za cdm bungeni. Wakiwa wapinzani wa kweli 96 nahisi hapa msafiri twaweza kumpumzisha. Nakusudia kuwaomba wapinzani wapeleke wazo la kukosa imani na mkwere,na hapo twaweza kuanza kuijenga Tanzania. Najua watatosha kwa zoezi ili.
 
Hebu niambie itasaidie nini kwa mfano?

Mkuu, kwa mfano kupata 20% ya wabunge ku-table motion ya impechment na mengineyo mengi tu.

Najua kuna maudhi mengi tu vyama vingine vya upinzani vimefanya dhidi ya Chadema ndani ya bunge na nje ya bunge lakini pia kuna kujirudi. Mtu akijirudi unafanya tathmini pana kuangalia manufaa na hasara kulingana na wakati husika. Iwapo manufaa yatakayopatikana ni makubwa kuliko hasara basi ombi likataliwe, ila kitu cha msingi tusitumie jazba kufikia maamuzi.
 
CHADEMA walikwishatamka toka mwanzo kuwa wapo tayari kushirikiana na chama chochote alimradi chama hicho kiwe ni chama cha upinzani kweli. CHADEMA isikubali kushirikiana na vyama vingine kwa msukumo wa kuwa na wabunge wengi wa upinzani bungeni bali iwe ni kwa sababu imeridhika kuwa wote nia yao kuu ni moja. Maana ni aheri kuwa wachache wenye lengo moja kuliko kuwa wengi lakini ndani ya huo uwingi ukawa na maadui wa ndani. Vyama vingine vya upinzani vinavyotaka kuingia kwenye umoja wa upinzani vipimwe kwa malengo yao, yakionekana yanawianika na ya CHADEMA, washirikishwe lakini yakionekana kutofautiana sana, basi waachwe, wakae nje ya serikali kivuli. Katika kuwapima, ni lazima waulizwe kwa nini muda wote wamekuwa maadui wa CHADEMA, na kwa nini sasa wanataka kushirikiana na CHADEMA. CHADEMA ikiwakubalia ni lazima kuwepo mwongozo uliokubalika na vyama vyote vilivyokubaliana kuingia katika umoja ili kukiwa na chama chochote kikaenda kinyume na mwongozo huo kifukuzwe kutoka serikali katika umoja.

Kutokana na mwenendo wa CUF na marafiki zake kuwa wa kutatanisha, ni vema wakawekewa masharti na vigezo maalum ili kupima dhamira yao halisi. Wakikidhi, na wote tukaridhika, kunaweza hata kufanyika makubaliano maalum ya ushirikiano kati ya CHADEMA na CUF kwa sababu hivi vyama vyote viwili adui yao mkubwa CCM amewafanyia propoganda nyingi sana za udini ambayo kuweza kuishinda ni lazima vyama hivi, kwa kutumia viongozi wenye busara wanaojua mbinu mbaya ambayo CCM inapandikiza, kuweza kuwa na ushirikiano wa kuaminika, na hiyo iwe ni pamoja na kuangalia uwezekano wa CUF kuvunja ndoa yake na CCM japo CUF Zanzibar inaweza kuendelea kuwa na Makamu wa Rais asiyewajibika kwa Rais, iwe ni hadhi tu lakini siyo katika maana ya ushirikiano na serikali, na wala asiteuliwe na Rais ili aweze kuwa huru kwa sababu hawezi kuwa na ndoa na CCM halafu na CHADEMA ambaye sasa ndiye inayeonekana mpinzani mwenye nguvu dhidi ya CCM. Haya yakishindikana, ni aheri CHADEMA waendelee pekee yao maana kwa na wapinzani wasioeleweka, faida ya kuwa nao itakuwa ni ndogo kuliko hasara inayoweza kupatikana.
 
Mkuu, kwa mfano kupata 20% ya wabunge ku-table motion ya impechment na mengineyo mengi tu.

Najua kuna maudhi mengi tu vyama vingine vya upinzani vimefanya dhidi ya Chadema ndani ya bunge na nje ya bunge lakini pia kuna kujirudi. Mtu akijirudi unafanya tathmini pana kuangalia manufaa na hasara kulingana na wakati husika. Iwapo manufaa yatakayopatikana ni makubwa kuliko hasara basi ombi likataliwe, ila kitu cha msingi tusitumie jazba kufikia maamuzi.

Impeachment kwa sasa haiwezekani kwakuwa hata hukocdm hawako united and organized kuhusu hilo. kwa hiyo hakuna point hapo

hayo megine mengi ni yapi? nothing

Jamani utengano una faida zake..pia..hasa hasa kwenye views ..ili sisi tulioko nje tushibe na views mbalimbali ..
 
Sawa nani kakataa basi undeni serikali kivuli kama mnaweza, wakati huo huo tunaishughulikia barua yenu ya posa tuone kama hamjaolewa sehemu nyingine lakini habari za kiintelijensia tulizo nazo zinasema mmewekwa kinyumba unaweza kanusha hilo.

ume...period eeh
 
Kweli Chadema viongozi wake ni wasomi? ni viongozi wawili ndio wasomi ZITTO na LISU ndio wamesoma UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM wengine kama watakuwa wamesoma basi vyuo vya kata

Ritz, busara kidogo inaweza kuhamisha mlima. Kusoma UDSM sio tija, nimesoma hapo, JK amesoma hapo so what? Viongozi wengi walioko madarakani wamesoma hapo lakini tupo hapa tulipo!!

Usomi sio kigezo pekee cha uongozi bora.
 
Back
Top Bottom