Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,565
- 7,988
Mbunge wa Viti Maalumu(CUF), Mkiwa Kimwaga amemwanika mbunge wa jimbo la Karatu, Dr Slaa kuhusu unafiki wake. Mheshimiwa Kimwaga aliyasema hayo katika mkutano wa hadhara wa chama chake juzi kwenye operesheni zinduka katika mkutano uliofanyika katika uwanja wa furahisha katika wilaya ya Nyamagana.
Akihutubia mamia ya wakazi wa Mwanza mbunge huyo amesema kwamba Dr Slaa ni mtu anayeongoza kwa unafiki kwa kuwasema mafisadi wa CCM wakati ambapo yeye mwenyewe ameoa mke ambaye ni diwani wa CCM.
Kutokana na hali hiyo mbunge huyo aliwataka wananchi kuzinduka na kukichagua chama cha CUF kwa kuwa kina viongozi ambao hawana doa lolote la ufisadi.
Katika hatua nyingine, Mkurugenzi wa siasa wa chama hicho, Mbarara Maharagande amewataka watanzania kuipuuza Operesheni Sangara inayofanywa na CHADEMA kwa kuwa haina maslahi yoyote kwa taifa.
"Hao CHADEMA wanapita na kuwaita wananchi kuwa ni Sangara. Wana dharau sana na hawana maslahi yoyote kwenu hivyo ni vyema mkawapuuza", alisema Maharagande.
Hata hivyo mkutano huo ulikaribia kuingia dosari baada ya kikundi kimoja cha wahuni kilichokuwa kinahudhuria mkutano huo kuanza kuzomea kila viongozi hao wa CUF walipokuwa wakianika ukweli kuhusu Dr Slaa.
Wakizungumzia hali hiyo, viongozi hao wa CUF walisema kuwa chama cha CHADEMA ni chama cha wahuni ambao hawataki kusikiliza sera za vyama vingine badala yake wapita wakivuruga mikutano ya vyama vingine. Viongozi hao walilitaka jeshi la polisi kuimarisha ulinzi na kupiga marufuku wavamimizi wa mikutano ya vyama vingine ili kila chama kipate fursa ya kueneza sera zake.
Mikutano ya Operesheni Zinduka inaendelea katika mkoa wa Mwanza ambapo kwa sasa inaelekea katika wilaya ya Ilemela.
.....ndiyohiyo
kwa jinsi nilivyoisoma hii habari sijaona mahalim kokote panapoonyesha kuanikwa kwa Dr. Slaa, isipokuwa mleta habari ndiye kaweka heading ya kuonyesha kuwa Dr. Slaa ameanikwa. Sijui kama HNH amefanya hivyo makusudi au kwa bahati mbaya.
hata hivyo suala la iktikadi ya kisiasa haliwezi lufungamana na ndoa yao.
Au huyo mbunge wa CUF anataka Dr. Slaa awe kama wapemba?manake huko ndiko hawaelewi somo la mke na mume kuwa na itikadi tofauti za kisiasa, huko ndiko imeshuhudiwa wanawake wakiachika kwa kuwa na itikadi tofauti na waume zao. Yaani kama mume ni CUF marufuku mke kuwa CCM, akithubutu tu, talaka.