CUF na Operesheni "Zinduka"

Habarindiyohiyo

JF-Expert Member
Aug 11, 2008
263
13
Chama cha Wananchi(CUF) kimezindua Operesheni yake maarufu kama Zinduka kwa kutoa hadharani siri nzito. Siri hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wake Profesa Lipumba katika mfululilizo wa mikutano ya hadhara iliyofanyika juzi, jana na leo mkoani Mwanza.

Profesa Lipumba akihutubia mikutano hiyo ameeleza kwamba tishio kubwa la amani na maendeleo ya Tanzania ni kundi la watu aliowaita mafisadi nyangumi. Profesa Lipumba ameeleza kuwa watu hao hutumia vyombo vyao vya habari kueneza ubaguzi katika taifa kwa kisingizio cha vita dhidi ya ufisadi.

Katika hatua nyingine, chama cha CUF kimekituhumu chama kingine cha upinzani cha CHADEMA kuwa ni CCM B. CUF imedai kuwa chama cha CHADEMA kinapiga kelele za ufisadi wakati chenyewe kimejaa ufisadi.

Wakieleza ushahidi wa wazi kuhusu ufisadi wa CHADEMA, viongozi mbalimbali wa CUF wameweka wazi kwa wananchi katika hotuba zao katika mfululizo wa mikutano hiyo kuwa viongozi wa CHADEMA ni mafisadi.

Viongozi hao wa CUF wamesema kuwa CHADEMA imeasisiwa na mafisadi wakina Edwin Mtei na Bob Makani ambao waliiba katika benki kuu na kuchoma benki hiyo ili kupoteza ushahidi.

Viongozi hao wameeleza kwamba hata viongozi wa CHADEMA waliofuata wakina Freeman Mbowe, Dr Slaa na Zitto Kabwe wote wana tuhuma mbalimbali za ufisadi zinazowakabili.

Viongozi hao wamewataka wananchi kuzinduka na kuunga mkono chama cha CUF kwani ndio chama pekee cha siasa chenye viongozi safi na walio mstari wa mbele kupambana na CCM.

Chama hicho kimeeleza kuwa ni viongozi wa CUF ndio wana historia ya kufungwa na kusumbuliwa na CCM kutokana na misimamo yao.
 
Huyu naye alikuwa wapi wakati wote? Atueleze vile vile uhusiano wake na RA
 
Mimi nakwambia kuwa CUF ndio inapoteza ulekeo wake na Kuwasema CHADEMA hakuna maana yoyote ile, Narejea makala ya mchambuzi wa kisiasa kuwa CUF katika operetion zinduka adui wao mkubwa ni CCM na Sio CHADEMA, Kamwe CUF hawawezi kusema juu ya hali hii na kupata umarufu kupitia CHADEMA na pia itakuwa vigumu sana kupata support kubwa,
 
kweli RA kawatuma kuja kubomoa upinzani sasa.CUF wamechanganyikiwa mpaka wamekubali kutumiwa.wanachofanya wanazidi kujibomoa.
 
kweli RA kawatuma kuja kubomoa upinzani sasa.CUF wamechanganyikiwa mpaka wamekubali kutumiwa.wanachofanya wanazidi kujibomoa.
Wanajiboa wao mwenyewe na sio siri CUF inabidi wabadilike sana sana na sio kuwasema CHADEMA hata kidogo na pia huku bara sio sawa na kule visiwani hivyo waje na mikakati mikubwa sana na siyo udaku
 
Wanajiboa wao mwenyewe na sio siri CUF inabidi wabadilike sana sana na sio kuwasema CHADEMA hata kidogo na pia huku bara sio sawa na kule visiwani hivyo waje na mikakati mikubwa sana na siyo udaku
Mchambuzi wa Gazeti la Tanzania Daima Mr Kibanda aliwahi kuyasema mambo haya na kwa kuwaonya CUF na CHADEMA pia sasa ndio kuchanganyikiwa kwenyewe na hawajui la kufanya kwa sasa na pia walikuwa wanapoteza muda mwingi sana kuhusu Mwafaka na kuliko active politics kwenye majimbo wao CHADEMA walianza muda mwingi sana kuhusu operation SANGARA
 
mie sikutegemea kabisa kama watatoka hivi.yani "MENGI" ndio wanamuona mbaya wa nchi kuliko wale mafisadi wengine? hii kali ya mwaka.
 
kweli RA kawatuma kuja kubomoa upinzani sasa.CUF wamechanganyikiwa mpaka wamekubali kutumiwa.wanachofanya wanazidi kujibomoa.

Yaani jamaa u-Profesa wake anaudhalilisha si kidogo. Maana hii ni wazi kabisa kuwa katumwa na RA kubomoa upinzani. Na hajui kuwa watu sasa wamechoka ni hizi porojo tu za kurushiana maneno bali wanataka mikakati hasa ya kulinusuru taifa kutoka kwenye lindi la umaskini ikiwemo kudhibiti wizi wa rasilimali za taifa na si hizo porojo za maneno. Arudi akajipange upya maana bara hakuendeshwi kwa jazba za chuki dhiki ya mtu fulani tu.
 
mie sikutegemea kabisa kama watatoka hivi.yani "MENGI" ndio wanamuona mbaya wa nchi kuliko wale mafisadi wengine? hii kali ya mwaka.
So wewe tu pekee yako maana hawa jamaa walikuwa wanapoteza muda mwingi sana kwa ajili ya mwafaka na huku walikuwa wanapoteza pesa za walipa kodi juu wa mwafaka na hakuna mwafaka wala nini sasa wao ndio wamezinduka sasa lakini wao CHADEMA walifanya siku nyingi sana
 
mie sikutegemea kabisa kama watatoka hivi.yani "MENGI" ndio wanamuona mbaya wa nchi kuliko wale mafisadi wengine? hii kali ya mwaka.

Kweli inasikitisha sana. Watu walioifilisi nchi yetu ndo wanaonekana bora na huyu Mangi wa watu ndo anaonekana kuwa mbaya wao. Lol! Kazi ipo. Hii nchi yetu hii, mhhhhh! Ngoja tusikilizie.
 
Chama cha Wananchi(CUF) kimezindua Operesheni yake maarufu kama Zinduka kwa kutoa hadharani siri nzito. Siri hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wake Profesa Lipumba katika mfululilizo wa mikutano ya hadhara iliyofanyika juzi, jana na leo mkoani Mwanza.

Profesa Lipumba akihutubia mikutano hiyo ameeleza kwamba tishio kubwa la amani na maendeleo ya Tanzania ni kundi la watu aliowaita mafisadi nyangumi. Profesa Lipumba ameeleza kuwa watu hao hutumia vyombo vyao vya habari kueneza ubaguzi katika taifa kwa kisingizio cha vita dhidi ya ufisadi.

Katika hatua nyingine, chama cha CUF kimekituhumu chama kingine cha upinzani cha CHADEMA kuwa ni CCM B. CUF imedai kuwa chama cha CHADEMA kinapiga kelele za ufisadi wakati chenyewe kimejaa ufisadi.

Wakieleza ushahidi wa wazi kuhusu ufisadi wa CHADEMA, viongozi mbalimbali wa CUF wameweka wazi kwa wananchi katika hotuba zao katika mfululizo wa mikutano hiyo kuwa viongozi wa CHADEMA ni mafisadi.

Viongozi hao wa CUF wamesema kuwa CHADEMA imeasisiwa na mafisadi wakina Edwin Mtei na Bob Makani ambao waliiba katika benki kuu na kuchoma benki hiyo ili kupoteza ushahidi.

Viongozi hao wameeleza kwamba hata viongozi wa CHADEMA waliofuata wakina Freeman Mbowe, Dr Slaa na Zitto Kabwe wote wana tuhuma mbalimbali za ufisadi zinazowakabili.

Viongozi hao wamewataka wananchi kuzinduka na kuunga mkono chama cha CUF kwani ndio chama pekee cha siasa chenye viongozi safi na walio mstari wa mbele kupambana na CCM.

Chama hicho kimeeleza kuwa ni viongozi wa CUF ndio wana historia ya kufungwa na kusumbuliwa na CCM kutokana na misimamo yao.


Kweli mimeamini kwamba akili ya Lipumba ni Pumba kama huko aliko.Anataka wazinduke yeye analala .Yeye anaweza kusimama na ajenda dhidi ya Chadema akafanikiwa kweli huyu jamaa ? Hajui kwamba Bara CUF haina nguvu na ushahidi ni huo kwamba hata pale walio waislam wengi kama Dar bado CUF hata seikali za mtaa haina kiongozi .Kwa nini asianzie kule Pemba ambako ndiko kuna mizizi yao na watu wana nyanyasika ? CUF kweli tu ndiyo waaga hivi hivi .
 
Tupe ushahidi wa hayo unayosema...kabla hatujaita ni umbea

Tumanini unataka ushahidi wa namna gani wakati maneno ya Lipumba yanajieleza? Hivi wewe unafurahi tu unapoona hawa akina Rostam wanazidi kuifilisi hii nchi? Usianze kuleta element za udini tena kwenye jambo hili yatupasa tupambane na mafisadi bila kujali dini zetu.
 
Kweli mimeamini kwamba akili ya Lipumba ni Pumba kama huko aliko.Anataka wazinduke yeye analala .Yeye anaweza kusimama na ajenda dhidi ya Chadema akafanikiwa kweli huyu jamaa ? Hajui kwamba Bara CUF haina nguvu na ushahidi ni huo kwamba hata pale walio waislam wengi kama Dar bado CUF hata seikali za mtaa haina kiongozi .Kwa nini asianzie kule Pemba ambako ndiko kuna mizizi yao na watu wana nyanyasika ? CUF kweli tu ndiyo waaga hivi hivi .
Kweli amechanganyikiwa kweli, Inabidi aseme ni kwanini mwaka 2005 walikosa hata mbunge mmoja huku Bara?? Then ni kwanini alikuwa anapoteza muda mwingi sana kwenye mwafaka na CCM huku akijua kuwa haliwezekani kabisa?? Lipumba kusema CHADEMa bara ni makosa makubwa sana
 
Kweli amechanganyikiwa kweli, Inabidi aseme ni kwanini mwaka 2005 walikosa hata mbunge mmoja huku Bara?? Then ni kwanini alikuwa anapoteza muda mwingi sana kwenye mwafaka na CCM huku akijua kuwa haliwezekani kabisa?? Lipumba kusema CHADEMa bara ni makosa makubwa sana

Lipumba kesha katiwa , anaonyesha yale madai ya watanzania kwamba CUF kuna udini mie naongezea anasimama kumtetea Rostam kwa mshiko na kwa kuwa wote wanatoka Tabora .Mtu mwenye heshima na akili timamu hata ndani ya CCM they will never stand for Rostam trust me and at least not in the open like this .Lipumba kweli pumba .Kesha jua CIF imekufa visiwani sasa anaisaidia CCM bara .
 
CUF wakitaka ku-protect credibility yao waeleze ufisadi wa hao waliotajwa. Si blah blah tu. Ukiangalia kwa makini CUF sasa inaanza kukosa mwelekeo baada ya kupigwa danadana ya MUAFAKA. Kama siasa zimekushinda acha kupiga blah blah bali toa FACTS.
 
CUF wakitaka ku-protect credibility yao waeleze ufisadi wa hao waliotajwa. Si blah blah tu. Ukiangalia kwa makini CUF sasa inaanza kukosa mwelekeo baada ya kupigwa danadana ya MUAFAKA. Kama siasa zimekushinda acha kupiga blah blah bali toa FACTS.
Kweli hata mimi nashangaa sana kusikia maneno kama haya, Hata hiyo operation Zinduka ni kuiga tu kwa CHADEMa ambao walianza muda mwingi, kwanza aje na kuomba samahani kwa Watanzani kwa kupoteza kodi za wananchi Watanzania na pia muda kwa ajili ya mwafaka na pia nyinyi Ndugu zangu mtaona wenyewe baada ya uchaguzi wataanzisha MWafaka 5 na 6 na 7 ni ulaji hakuna jipya juu ya CUF bara, Walipoteza hata jimbo la TEMEKE, Bukoba na kule maswa sijui, Maana inatia shaka msimamo wa huyu jamaa au ndio kwa ajili wanatoka sehemu moja na wakina RA?? CUF mkitaka kupata watu acha kuwasema CHADEMA na Pia Lipumba ni mmoja wa JF aje kusoma humo ndani alama za nyakati juu ya hilo
 
Tumanini unataka ushahidi wa namna gani wakati maneno ya Lipumba yanajieleza? Hivi wewe unafurahi tu unapoona hawa akina Rostam wanazidi kuifilisi hii nchi? Usianze kuleta element za udini tena kwenye jambo hili yatupasa tupambane na mafisadi bila kujali dini zetu.
Kivipi mbona unataka kukwepa hoja nakuingiza udini?? labda wewe ndiyo umeanza udini??
Lipumba anaongelea mafisadi wote either wako chadema, wako CCM it doesn't matter?? ,Masikio yangu yako huru nasubiria kusikia chadema wakijibu hizo tuhuma kwa faida ya nchi!!
 
Kweli mimeamini kwamba akili ya Lipumba ni Pumba kama huko aliko.Anataka wazinduke yeye analala .Yeye anaweza kusimama na ajenda dhidi ya Chadema akafanikiwa kweli huyu jamaa ? Hajui kwamba Bara CUF haina nguvu na ushahidi ni huo kwamba hata pale walio waislam wengi kama Dar bado CUF hata seikali za mtaa haina kiongozi .Kwa nini asianzie kule Pemba ambako ndiko kuna mizizi yao na watu wana nyanyasika ? CUF kweli tu ndiyo waaga hivi hivi .

Viongozi wa mitaa wanaoo Buguruni vingunguti kiwalani mbagala lakini ukweli ni kwamba wanafanya kosa kubwa mno lakuanza kubomoana wenyewe kama wapinzani nataka kujua walikuwa na vielelezo kama wenzao wanavyokuwa navyo
Nadgani wangeacha kulaumiana wakatafuta mbinu za kutowachanganya wananchi ndio maana wanashindwa kuamua na kususia mambo ya kisiasa kwa vile wanapewa taarifa za kuwachanganya
 
Back
Top Bottom