Habarindiyohiyo
JF-Expert Member
- Aug 11, 2008
- 263
- 13
Chama cha Wananchi(CUF) kimezindua Operesheni yake maarufu kama Zinduka kwa kutoa hadharani siri nzito. Siri hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wake Profesa Lipumba katika mfululilizo wa mikutano ya hadhara iliyofanyika juzi, jana na leo mkoani Mwanza.
Profesa Lipumba akihutubia mikutano hiyo ameeleza kwamba tishio kubwa la amani na maendeleo ya Tanzania ni kundi la watu aliowaita mafisadi nyangumi. Profesa Lipumba ameeleza kuwa watu hao hutumia vyombo vyao vya habari kueneza ubaguzi katika taifa kwa kisingizio cha vita dhidi ya ufisadi.
Katika hatua nyingine, chama cha CUF kimekituhumu chama kingine cha upinzani cha CHADEMA kuwa ni CCM B. CUF imedai kuwa chama cha CHADEMA kinapiga kelele za ufisadi wakati chenyewe kimejaa ufisadi.
Wakieleza ushahidi wa wazi kuhusu ufisadi wa CHADEMA, viongozi mbalimbali wa CUF wameweka wazi kwa wananchi katika hotuba zao katika mfululizo wa mikutano hiyo kuwa viongozi wa CHADEMA ni mafisadi.
Viongozi hao wa CUF wamesema kuwa CHADEMA imeasisiwa na mafisadi wakina Edwin Mtei na Bob Makani ambao waliiba katika benki kuu na kuchoma benki hiyo ili kupoteza ushahidi.
Viongozi hao wameeleza kwamba hata viongozi wa CHADEMA waliofuata wakina Freeman Mbowe, Dr Slaa na Zitto Kabwe wote wana tuhuma mbalimbali za ufisadi zinazowakabili.
Viongozi hao wamewataka wananchi kuzinduka na kuunga mkono chama cha CUF kwani ndio chama pekee cha siasa chenye viongozi safi na walio mstari wa mbele kupambana na CCM.
Chama hicho kimeeleza kuwa ni viongozi wa CUF ndio wana historia ya kufungwa na kusumbuliwa na CCM kutokana na misimamo yao.
Profesa Lipumba akihutubia mikutano hiyo ameeleza kwamba tishio kubwa la amani na maendeleo ya Tanzania ni kundi la watu aliowaita mafisadi nyangumi. Profesa Lipumba ameeleza kuwa watu hao hutumia vyombo vyao vya habari kueneza ubaguzi katika taifa kwa kisingizio cha vita dhidi ya ufisadi.
Katika hatua nyingine, chama cha CUF kimekituhumu chama kingine cha upinzani cha CHADEMA kuwa ni CCM B. CUF imedai kuwa chama cha CHADEMA kinapiga kelele za ufisadi wakati chenyewe kimejaa ufisadi.
Wakieleza ushahidi wa wazi kuhusu ufisadi wa CHADEMA, viongozi mbalimbali wa CUF wameweka wazi kwa wananchi katika hotuba zao katika mfululizo wa mikutano hiyo kuwa viongozi wa CHADEMA ni mafisadi.
Viongozi hao wa CUF wamesema kuwa CHADEMA imeasisiwa na mafisadi wakina Edwin Mtei na Bob Makani ambao waliiba katika benki kuu na kuchoma benki hiyo ili kupoteza ushahidi.
Viongozi hao wameeleza kwamba hata viongozi wa CHADEMA waliofuata wakina Freeman Mbowe, Dr Slaa na Zitto Kabwe wote wana tuhuma mbalimbali za ufisadi zinazowakabili.
Viongozi hao wamewataka wananchi kuzinduka na kuunga mkono chama cha CUF kwani ndio chama pekee cha siasa chenye viongozi safi na walio mstari wa mbele kupambana na CCM.
Chama hicho kimeeleza kuwa ni viongozi wa CUF ndio wana historia ya kufungwa na kusumbuliwa na CCM kutokana na misimamo yao.