Baada ya Kusoma hizi quotations za wana-CUF kuhusu mafisadi, niliwasiliana na Mzee Edwin Mtei. Mzee Mtei amesema hajapata nafasi ya kusoma matamshi ya Prof. Lipumba, lakini akakiri kwamba anam-respect sana Lipumba as an economist.
Kuhusu ugavana wake wa Benki Kuu, alisema aliteuliwa mwaka 1966 akkanzisha sarafu (currency) ya kitaifa na Benki Kuu yake. Amesema ali-hand over to Charles Nyirabu kama Gavana mwaka 1974. Charles Nyirabu alikuwa ni Deputy Governor wake na sio Bob Makani.
Baada ya BoT, Mtei alikuwa Secretary General wa East African Community mpaka ilipovunjika mwaka 1977 ambapo alirudi Dar es Salaam na kuteuliwa Waziri wa Fedha na Mipango. Mzee Mtei alijiuzulu uwaziri baada ya kutofautiana na bosi wake, Mwalimu Nyerere juu ya sera, hasa za uchumi na fedha. Ndipo alipoanza shughuli za kilimo.\ 1980.
Mzee Mtei ameeleza kwamba alichaguliwa na Magavana wa English Speaking African countries Oktoba 1982 kuwa Executive Director wa International Monetary Fund, na akahamia Washington D.C. mpaka Novemba 1986. Wakati jengo la BoT alilolisimamia likijengwa lilipoungua kwa moto mwaka 1984, alipigiwa simu akiwa huko Washington. Charles Nyirabu ndiye alikuwa Gavana, na Deputy wake alikuwa Bob Makani. Kama CUF au Lipumba wana ushahidi wa wizi au ufisadi kuhusu chanzo cha ule moto, waulekeze kwa waliokuwa na jukumu kuendesha BoT. Wajifunze pia historia ya BoT.
Mzee Edwin Mtei alikuwa Muasisi wa Chadema mwaka 1992 na alikiongoza kama Mwenyekiti Taifa mpaka 1998 alipo-hand over to Bob Makani. Anasema anafarijika sana kuona CHADEMA chini ya uongozi mpya wa vijana jasiri, wabunifu na wazalendo kinakuwa tishio kwa chama tawala. Badala ya CUF kuunganisha nguvu na Chadema ili kuleta demokrasia ya kweli nchini, inaonekana viongozi wake wanabuni hadithi za ufisadi dhidi ya Mzee Mtei, ambaye by any stretch of the imagination, hahusiki.
Mzee Mtei ameniambia kwamba anatafuta hayo magazeti yaliyomnukuu Lipumba ili aone wamemkashifu kiasi gani. Amesema kwamba hana shida na fedha, eti aende kortini ku-sue misguided wana-Mageuzi kama hilo kundi la CUF. Wakimuomba Mzee Mtei msamaha hadharani hiyo itatosha.
Asante sana mkuu, sasa CUF waje waeleze hizo data zao za kupika wamezitoa wapi? Ama nao walilishwa kasa kama god father wao RA alivo lishwa lile la deni la Mengi na NBC?