CUF na Operesheni "Zinduka"

CUF na Operesheni "Zinduka"

Chuma.

Kama Mtei anaona kaonewa awafuate CUF sio hapa JF.mimi bado naamini maneno ya CUF,Nyerere aliondoka madarakani mwaka 1985 lakini miaka kumi mbele 1995 aliweza kumuweka MKAPA kwenye nafasi ya urais wa Tanzania huku akiwa si rais wa nchi wala mwenyekiti wa CCM.

Mtei aliweza kuwaingiza BOT watu wa kabila lake na jamaa zake wengi tu kama Mwenyekiti wa Chadema Taifa hivi sasa ambaye ni mkwe wake na alikuwa hana elimu ya kumfanya aajiriwe BOT.sasa anaposema alikuwa na perfomance ya juu sio kweli kwani aliajiri watu wengi wa kabila lake na ndugu zake.

Mkuu unaonyesha wazi kwamba una-attack personality na sio hoja. Na kama una hoja can you plz summarize hoja yako maana unazungumza zungumza kama wale wanawake wa mipasho. Ukijibiwa hili unazusha lile, na ni kama vile unatafuta sympathy kutoka watu fulani humu JF and all of them in vague formality. Kuhusu suala la kiingereza unachokiita kizungu nadhani hufahamu taratibu za JF, lugha zote hizi i.e kiswahiLi na kiingereza ruksa na kama hufahamu kati ya lugha mojawapo omba utafsiriwe or else kaa kimya......... All in all your arguments are not constructive and it is people like you ambao mnaifanya au kustawisha Tanzania iwe kama ilivyo sasa.
 
kanda2,
Kwanza nenda shule ukajifunze Kiingereza. Pili Mzee Mtei aliachia benki mwaka 1974 wakati huo Freeman akiwa na umri wa miaka 13. Unataka kutuambia kuwa Mzee Mtei alimpa Freeman kazi benki at the age of 13? Come on. Katafute uwongo mwingine.

Mzee Mtei alimpa uanachama wa Chadema Zitto Kabwe akiwa na miaka 14.wakati sheria inasema mtu mwenye miaka 18 ndiyo ana fursa ya kujiunga na chama cha siasa.
 
Kanda2,
Inaonekana uwongo ni mojawapo ya sera zako. Kabwe atakuja hapa kukusuta kama kweli alijiunga na Chadema akiwa na umri wa miaka 14. Na kwa hiyo Freeman alifanya kazi benki akiwa na umri wa miaka 13. Pole sana bwana mdogo.
 
Mkuu unaonyesha wazi kwamba una-attack personality na sio hoja. Na kama una hoja can you plz summarize hoja yako maana unazungumza zungumza kama wale wanawake wa mipasho. Ukijibiwa hili unazusha lile, na ni kama vile unatafuta sympathy kutoka watu fulani humu JF and all of them in vague formality. Kuhusu suala la kiingereza unachokiita kizungu nadhani hufahamu taratibu za JF, lugha zote hizi i.e kiswahiLi na kiingereza ruksa na kama hufahamu kati ya lugha mojawapo omba utafsiriwe or else kaa kimya......... All in all you arguments are not constructive and it is people like you ambao mnaifanya au kustawisha Tanzania iwe kama ilivyo sasa.

mjadala hakuanza kwa kizungu ulikuwa wa kiswahili na mara ya kwanza mzee wenu aliandika kiswahili niliposema hana elimu ya uchumi ndio akaja na kiingereza kama ku JUSTIFY kuwa yeye ni msomi wa uchumi.

mwenzako anataka nikasome kiingereza sio lazima nisome kiingereza.rais wa CHINA,UFARANSA,JAPAN,chile,brazil na nchi nyingi wanaongea lugha zao na wamefanikiwa sana kimaendeleo bila kiingereza.

sihitaji sympathy anayetaka sympathy ni moja wako aliyesema mwache mzee apumzike nisimbugudhi.
Mzee wenu alitegemea yeye aseme na sisi tukae kimya? no way.
 
Chuma.

Kama Mtei anaona kaonewa awafuate CUF sio hapa JF.mimi bado naamini maneno ya CUF,Nyerere aliondoka madarakani mwaka 1985 lakini miaka kumi mbele 1995 aliweza kumuweka MKAPA kwenye nafasi ya urais wa Tanzania huku akiwa si rais wa nchi wala mwenyekiti wa CCM.

Mtei aliweza kuwaingiza BOT watu wa kabila lake na jamaa zake wengi tu kama Mwenyekiti wa Chadema Taifa hivi sasa ambaye ni mkwe wake na alikuwa hana elimu ya kumfanya aajiriwe BOT.sasa anaposema alikuwa na perfomance ya juu sio kweli kwani aliajiri watu wengi wa kabila lake na ndugu zake.

kanda2 thanks kwa Kusimamia Hoja!!!
 
Kanda2,
Inaonekana uwongo ni mojawapo ya sera zako. Kabwe atakuja hapa kukusuta kama kweli alijiunga na Chadema akiwa na umri wa miaka 14. Na kwa hiyo Freeman alifanya kazi benki akiwa na umri wa miaka 13. Pole sana bwana mdogo.

Zitto Kabwe amekwisha eleza kwenye mada yake ya kutogombea ubunge. amekiri alipewa kadi ya chadema akiwa na chini ya miaka kumi na nane.chini ya uenyekiti wa Mzee huyu Mtei aliyeshindwa kuikwamua BOT kama alivyoshindwa hata kusimamisha mgombea urais kwa tiketi ya Chadema kwenye kipindi chake chote cha uenyekiti Chadema.

alishindwa kukipaisha Chadema wakati akiwa na elimu ya POLITICAL SCIENCE NA HISTORIA yaani fani yake.angeweza kuinua uchumi wetu?

vipi mwenyekiti anampa uanachama mtoto wa chini ya miaka 18?
 
kanda2 thanks kwa Kusimamia Hoja!!!
nimegusa pabaya leo nitatengeneza maadui wengi,usishangae nikafungiwa,tayari nimepewa shutuma nzito kuwa ni mdini kwa kumuhoji huyu mzee ambaye ni NGULI WA HISTORY.
 
Hawa CHADEMA tulio nao hapa ni wapiga debe wabaya sana wanaweza kumkwamisha kiongozi wao kwa mambo wasioyajua ,wao wamo tu ,hawaoni hawasikii ,muisilamu akigusia dini tayali ,inakuwa ni adui na analeta udini hapa ,hivi haya mambo ya dini hawaoni yanapo anzia ?
Kuna watu humu utafikiri wanahati miliki ya kuuponda uislamu tena kwa kile wasichokijua lakini ,hawafutiwi wala hawaondolewi mada zao ,jamani huu ni ukandamizaji wa yaliyopo hapa kwamba wa dini fulani tu wawe na uhuru wa kuandika watakacho ,ila mimi kwa upande wangu nalielewa kuwa hilo lipo.

Ukiwambia CHADEMA ni chama kina ukabila ndani yake ,utaona wanavyoshupalia kuwa ni uongo ,aafu kumbe wameozeshana ,afu kumbe Slaa ni mwanachama wa kikundi flani cha Wachaga ,afu kumbe wanamiliki mahoteli makubwa ,sasa watu hawa wakishapewa uongozi huoni kama watajivutia upande wao ? Na inaonekana hivi vita vya ufisadi wamevivalia njuga kutokana na sababu za kimaslahi ,bungeni wanapinga watu kulipwa mishahara mikubwa ,vijijini wananyanganya watu mashamba ,wengine wanawalenga watu risasi halafu mnataka kugombea Uraisi wa Nchi hii ,kwanza jamani jisafisheni kikweli kweli.
Unamfyetulia kizee cha watu risasi ,tena baada ya kuwa keshapigwa na vijana wako,halafu unasema ulilenga juu ? Mzee alikuwa na bakora tu na analilia kuvurugwa kwa kipando chake cha maharage kwa pale alipoamini ni shamba lake ,mlikuwa wapi siku zote tokea alipoanza kulima ? Kuna tofauti gani na serikali inayowavunjia watu majumba yao ? Eti wamejenga kwenye maporomoko,eti wamejenga kwenye sehemu inatakayopita njia ,sasa mkipata ukubwa si mtavunja vijiji ili mjenge mahoteli ? Mtawaharibia konde zao ili muanzishe mashamba makubwa kwa kuwa tu mnamiliki matrekta.............Wacheni hizo ,historia inajirudia pale unapotaka kupanda ngazi ya Uraisi ,ikiwa uliwahi kumlenga mtu risasi basi hufai katika uongozi wowote ule ,wewe ni mtu hatari ,na kesi ile haijulikani iliishia wapi kama mkuu aliomba samahani itakuwa amefanya jambo la kiungwana kabisa.
 
Zitto Kabwe amekwisha eleza kwenye mada yake ya kutogombea ubunge. amekiri alipewa kadi ya chadema akiwa na chini ya miaka kumi na nane.chini ya uenyekiti wa Mzee huyu Mtei aliyeshindwa kuikwamua BOT kama alivyoshindwa hata kusimamisha mgombea urais kwa tiketi ya Chadema kwenye kipindi chake chote cha uenyekiti Chadema.

alishindwa kukipaisha Chadema wakati akiwa na elimu ya POLITICAL SCIENCE NA HISTORIA yaani fani yake.angeweza kuinua uchumi wetu?

vipi mwenyekiti anampa uanachama mtoto wa chini ya miaka 18?
Kwanza ilikuwa 14. Sasa ishakuwa chini ya 18? Lipi ni lipi?
 
Zitto Kabwe amekwisha eleza kwenye mada yake ya kutogombea ubunge. amekiri alipewa kadi ya chadema akiwa na chini ya miaka kumi na nane.chini ya uenyekiti wa Mzee huyu Mtei aliyeshindwa kuikwamua BOT kama alivyoshindwa hata kusimamisha mgombea urais kwa tiketi ya Chadema kwenye kipindi chake chote cha uenyekiti Chadema.

alishindwa kukipaisha Chadema wakati akiwa na elimu ya POLITICAL SCIENCE NA HISTORIA yaani fani yake.angeweza kuinua uchumi wetu?

vipi mwenyekiti anampa uanachama mtoto wa chini ya miaka 18?
Pole sana,
Ila tu unaonyesha ulivyokosa life experience references na world econo-political trends:
- Reagan - Hakuwa Mchumi aliikoa Marekani ilipotaka kuingia recession
- John Major - Alikuwa kondakta wa basi akafikia uwaziri mkuu na kuendesha nchi vizuri tu
- Lula - Brazil hakupata hata kufika elimu ya sekondari - amedalisha Brazil na economy imeenda juu
- Deng Xiaoping- Kitabu hakikupanda lakini ndiyo kabadlisha China leo imefika hapo ilipo
Mifano ni Mingi - kwa taarifa yako tu watawala wengi wa Marekani na nchi za Ulaya hadi Asia hata Mawaziri wao wengi ni Wana-Historia, Siasa, Lawyers etc Unajua Obama kasomea nini?

Sina maana kuwa Elimu si lolote; huwezi Ku-discredit Elimu ya Mr. Mtei; he was a Graduate of high level; and had experinced and also he has pointed the way he used his ecomists below him! Acha kupoint vitu ambavo havieleweki.
In other parts of the world people utilised the same calibre of people and they developed; take another example of Mr. Lee Kwang Ye of Singapore. He studied History together with Mr. Nyerere; and he changed the face of Singapore.
You are saying Mr. Malima was a greatest Economist; yes, but what did he do? We measure our leadership from our achievements!

Remember that, the best cat is the one who catches the mouse!!
 
sina hakika juu ya kauli ya ufisadi wa chadema kaizungumza nani ktk cuf. I hope sio lipumba. Kama maharagande basi tumuonee huruma na matumaini yangu prof.lipumba anaweza kumuweka chini na pia kuwaomba radhi akina hao viongozi walotajwa.

Sijui kwanini cuf au chadema kila mmoja anampiga vita mwezie wakati wote hawana serikali....sijui nani kaanza na mwezie anamaliza!!! Nionavyo ccm ndio wameplay a big role..either ikiwa ccm as a think tank yao au wafanyabiashara wenye "interest ktk siasa" ambao wanapenda kumuona alie madarakani ni mshikaji wao au mwenye ushawishi kwake...!!

Mafisadi either mapapa au nyangumi kila mmoja hapendi kuitwa hivyo...kama wanaona kuna oppurtunity ya kuwatumia wanasiasa ili kuzima au kuwamulika wa upande mwingine kwake yeye ni "mukidy"="poa"..

Atlast wananchi hawajui wanapelekwa wapi...na atlast ccm ndio kitaibuka kidedea!!!

ile theory ya desmond tutu imeshindwa ku-apply hapo?
 
Maskini prof Lipumba,ndio ameishia hapo!
Sijaelewa vizuri,haya matamshi yametolewa na Prof au viongozi wa mitaa wa CUF?
Hana haja ya kupambana na chama bali kuelezea maovu ya wanachama na kueleza plan B ya kuondoa matatizo ya wananchi
 
Maskini prof Lipumba,ndio ameishia hapo!
Sijaelewa vizuri,haya matamshi yametolewa na Prof au viongozi wa mitaa wa CUF?
Hana haja ya kupambana na chama bali kuelezea maovu ya wanachama na kueleza plan B ya kuondoa matatizo ya wananchi
Tatizo mnabwata vibaya sana hivi ,viongozi wenu hawajawahi kushutumiwa mbona mnaonekana kama wageni ndani ya siasa ,yaani mnatisha vibaya sana kuwa viongozi wa CHADEMA wasivutwe ukosi ,wandugu hilo haliwezekani kabisa kabisa na hao viongozi wanalielewa kwa kina jambo hilo.

Sasa jamaa huko vijijini wanazinduliwa ile mbaya yake na sangara wote wamepigwa spray hawaonani 😀
 
Pole sana,
Ila tu unaonyesha ulivyokosa life experience references na world econo-political trends:
- Reagan - Hakuwa Mchumi aliikoa Marekani ilipotaka kuingia recession
- John Major - Alikuwa kondakta wa basi akafikia uwaziri mkuu na kuendesha nchi vizuri tu
- Lula - Brazil hakupata hata kufika elimu ya sekondari - amedalisha Brazil na economy imeenda juu
- Deng Xiaoping- Kitabu hakikupanda lakini ndiyo kabadlisha China leo imefika hapo ilipo
Mifano ni Mingi - kwa taarifa yako tu watawala wengi wa Marekani na nchi za Ulaya hadi Asia hata Mawaziri wao wengi ni Wana-Historia, Siasa, Lawyers etc Unajua Obama kasomea nini?

Sina maana kuwa Elimu si lolote; huwezi Ku-discredit Elimu ya Mr. Mtei; he was a Graduate of high level; and had experinced and also he has pointed the way he used his ecomists below him! Acha kupoint vitu ambavo havieleweki.
In other parts of the world people utilised the same calibre of people and they developed; take another example of Mr. Lee Kwang Ye of Singapore. He studied History together with Mr. Nyerere; and he changed the face of Singapore.
You are saying Mr. Malima was a greatest Economist; yes, but what did he do? We measure our leadership from our achievements!

Remember that, the best cat is the one who catches the mouse!!

wako wengi ZUMA,TSHANGARAI N.K

JOHN MAJOR ALIFELI NDIO MAANA TONY BLAIR AKASHINDA KWA WEPESI MAY 1997.SOMA THE AUTOBIOGRAPHY YA JOHN MAJOR ISBN 0002570041 UKURASA WA 659 ANAKUBALI ALIVYOFELI KIUCHUMI.
Obama kasoma sheria Harvard nimesoma vitabu vyake vyote viwili alivyoandika,namfuatilia toka alipoongea kwa mara ya kwanza kwenye mkutano wa DEMOCTRATIC 2004

Mzee Mtei alishindwa kumshauri Nyerere tutaingia kwenye vita vya Uganda kwa kumdanganya Nyerere kuwa tutakaa na njaa kwa miezi 18 tu na baada ya hapo uchumi wetu utakuwa sawa.toka 1978 uchumi haukukaa sawa hadi alipoingia mzee Mwinyi November 1985.

kipindi cha Nyerere watu waliosomea masomo mengine ndio waliokabidhiwa vyama vya ushirika,RTC,ugawaji n.k na hatimaye kuyaua mashirika na makampuni.

Mtei hana jipya ameshindwa kuiinua Chadema itakuwa na Uchumi?
 
Kwanza nimpe pole Mzee Mtei kwa kushutumiwa bila kuwepo kwa ushahidi, kwani aliyesema maneno hayo ni msemaji wa CUF Maharagande ,hivyo huo ni msimamo wa chama mpaka hapo yatakapotolewa maelezo mengine ya tofauti.

Pili, CUF wanaamini kuwa wao wanaweza kupata wanachama wengi kwa kuitukana CHADEMA na viongozi wake , watu hawa hakuna hata mmoja waliyemuacha wa CHADEMA bila kumtukana .

Tatu, CUF wanasahau kuwa BUSANDA ajenda yao kuu ya mikutano ilikuwa ni kuwatukana CHADEMA na viongozi wake , na walichokumbana nacho kilikuwa ni kipigo kibaya kutoka kwa wananchi wa Busanda kuambulia kura 977 yaani ni miatisa na sabini na saba sawa kura za mtu ambaye anagombea uenyekiti wa Kijiji, ila naona bado hawajaelewa kuwa kuitukana CHADEMA sio mtaji wa kujipatia umaarufu.

Nne, CUF na viongozi wake leo ndio wako mstari wa mbele kumwosha EL NA RA kwenye mikutano yao na bila aibu , wanasema na aliyesema ni LIPUMBA eti LOWASSA alionewa na hili limefanywa baada ya kikao kirefu kati ya Lipumba na Rostam kilichofanyika Kempinski Hoteli.

Tano, Lipumba anapaswa ajue kuwa tangu mwaka 1995 alipokuwa anagombea Urais Home boy wake Rostam ndio alikuwa na ni nguzo kuu ya kuichangia CUF na kuna siku yatawekwa hadharani , sasa kama wao wameingia kwenye mifuko ya mafisadi wasitake kuaminisha umma kuwa kila mtu ni FISADI ama anaweza kununuliwa na Mafisadi.

Ukisoma kitabu cha Lwakatare anasema kuwa aliwaonya CUF wasiende Busanda kwani walikuwa hawajafanya kazi za kisiasa tangu 2005 lakini walimkatalia na wakaambulia aibu ya mwaka ambayo hata kwenye pepa ya Maharagande aliyoiwasilisha kwenye kikao cha Baraza kuu anakiri kuwa BUSANDA imekuwa ni mwiba mchungu kwa chama na ni lazima watafute njia ya kujitopa.

Ukisoma kitabu cha Lwakatare , anasema "Mhe.Mwenyekiti haiwezekani leo chama kitumie Tshs.68,480,000 na tupate kura 977,hii ina maaana katika kile kinachoitwa value for money tumetumia Tshs.78,480 kuipata kura moja .Si ingekuwa vyema hata tukatumia style ya CCM ya kununua kura kwa pesa na kila kura tukainunua kwa Tshs.10,000 tungepata kura nyingi zaidi ya hizi 977. mwisho wa kunukuuu.

Ukiangalia angalizo hili utagundua kuwa tatizo la CUF ni kukosa viongozi wenye muono wa kisiasa ambao naamini wanahitaji kujipanga upya badala ya kubwata bwata kama ambavyo wanafanya sasa kwenye operesheni yao ambayo hata LIPUMBA mwenyewe ameshindwa kuendelea kukaa humo na kurudi dar kwa ajili ya kuja kushiriki semina na makongamano yanayoitishwa na msajili wa vyama na TCD , pasipo kujua ya kuwa wenzake wakina Mbowe, Slaa , Zitto na wengine wanakuwa huko field hata mwezi mzima katika kuendesha Operesheni Sangara na ndio maana leo CHADEMA inafanikiwa na hata siku moja hawajasikika wakiwatukana viongozi wa CUF .

Lipumba , ushauri wangu kwako ni kuwa nenda ukasome kitabu cha Lwakatare vol.003 utaona anavyolalamikia shilingi 300 milioni za chama ambazo mlimpatia mfanyabiashara mmoja ili aweze kuwaletea faida na hajafanya hivyo tangu mwaka 2006 na hakuna anayejua ziko wapi hizo pesa isipokuwa wewe binafsi , Maalim Seif na Juma Duni ambao ni wajumbe wa summit ya chama . Badala ya kuwashambulia watu waadilifu kama wakina Mtei ambao hata maisha yao yanaonyesha kiwango cha uadilifu walichokuwa nacho fanya kazi ya kushughulikia matatizo ya ndani ya chama .

Wana CUF tengenezeni chama kwani mvuto wake kwa jamii unapotea kwa kasi sana na hamtaweza kukijenga kwa kuwatukana viongozi na wanachama wa CHADEMA kwani matatizo ya CUF hayasababishwi na ukuaji wa CHADEMA.

Mzee Mtei huna sababu ya kuendelea kujibizana na hawa ambao hawataki kuelewa , umeshaonyesha uliondoka lini BOT na naamini waliokuwa wanaropoka kama wana akili timamu watajirudi hata kama sio hadharani kwa hatua za sasa.
 
wako wengi ZUMA,TSHANGARAI N.K

JOHN MAJOR ALIFELI NDIO MAANA TONY BLAIR AKASHINDA KWA WEPESI MAY 1997.SOMA THE AUTOBIOGRAPHY YA JOHN MAJOR ISBN 0002570041 UKURASA WA 659 ANAKUBALI ALIVYOFELI KIUCHUMI.
Obama kasoma sheria Harvard nimesoma vitabu vyake vyote viwili alivyoandika,namfuatilia toka alipoongea kwa mara ya kwanza kwenye mkutano wa DEMOCTRATIC 2004

Mzee Mtei alishindwa kumshauri Nyerere tutaingia kwenye vita vya Uganda kwa kumdanganya Nyerere kuwa tutakaa na njaa kwa miezi 18 tu na baada ya hapo uchumi wetu utakuwa sawa.toka 1978 uchumi haukukaa sawa hadi alipoingia mzee Mwinyi November 1985.

kipindi cha Nyerere watu waliosomea masomo mengine ndio waliokabidhiwa vyama vya ushirika,RTC,ugawaji n.k na hatimaye kuyaua mashirika na makampuni.

Mtei hana jipya ameshindwa kuiinua Chadema itakuwa na Uchumi?

Unaona unavyojikanyaga hapo? Obama kasoma Havard na vitabu vyake vyote umevisoma. John Major kwenye biography yake ame-admit kuwa alishindwa - Hivi unajua ile serikali alirithi tu kwa Mama Thatcher? hakuchaguliwa, kama Brown ilivyokuwa kutoka kwa Blair.

Obama kasoma sheria. Sasa hebu ongea kuhusu relevance ya argument yako kuwa Kighoma Malima alisomea UChumi na Mr. Mtei alisomea History.

What is important is the vision, how we utilize our knowledge in real life!
 
Jamani kanda mbili kwenye mambo ya kisomi kama haya mwekeni kando.
Labda kama mnataka kuzungumza naye ebu mpeni thread ya dini. Hapo mtakesha.
Mnamuonea tu kumwambia hoja za kisomi kama hizi. Kwa kajifahamu kake hawezi kuelewa kamwe.
 
najua nakwenda off topic kidogo .........ila zitto kabwe alisema alipewa kadi ya chama akiwa form 3( au form 4?)
kama ni hivyo .....alipewa kadi akiwa chini ya umri wa miaka 18 au zitto kabwe katudanganya?
 
najua nakwenda off topic kidogo .........ila zitto kabwe alisema alipewa kadi ya chama akiwa form 3( au form 4?)
kama ni hivyo .....alipewa kadi akiwa chini ya umri wa miaka 18 au zitto kabwe katudanganya?
Kama unamwamini sana basi atakuwa amekudanganya ,ila kama unafuata siasa hilo lina sehemu yake !
 
Waoneeni huruma CUF jamani.kama mnavyojua wengi mule shule ndogo and for that hawawezi kufanya reseach and analysis za kutosha kupambana na CCM so for that wanaona ngoja tutafute la kusema
Si mnajua mropokaji anweza kujitukana mwenyewe so ndonachofanya
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom