CUF iko wapi?

CUF ipo na ipo ngangari kinoma ,kwanza tukubaliane kuwa katika CUF hakuna alie juu ya sheria ,Hamadi huyo alietimiliwa juzi ni mmoja kati ya waasisi wa CUF lakini kwa usiri na ujuaji wake leo hii akienda Zenji ni aibu tupu.

CDM (Chama Duni Mitaani) ni Chama kisicho na dira kwani nia na dhamiri yake ya kuleta fujo hapa Tanzania zimejulikana na zinazimwa kwa ustadi mkubwa sana ,mtakuja kushangaa hapo baadae ,msiseme hamkuambiwa.

CUF ipo na hazina ya wanachama wake ipo tena inaongezeka kwa hali ya kutisha ,wanachama ambao wanaamini kabisa kuwa wao ndio wenye Chama na sauti yao ndio ya MWISHO.

Chadema ilikuja na hoja ya kulipua mabomu pale bungeni ,wakajaza majungu hadi serikali na bunge wakawa hawasikilizani ,bahati nzuri au mbaya ykapita ya kupita mambu yakatulizwa na leo hii hatuwasikii CHADEMA kulipua mabomu wala kutega jipya ,hapa nasema wamezimwa vibaya sana.

Chadema walitaka kuisambaratisha nchi kwa kutumia uchaguzi wa Arusha kwa kweli wakasambaratishwa na wengine kuwekwa lockup ,eti wakakusanyana kwenda kituoni maji waliita mee ,nia na lengo lao likazimwa kiurahisi kabisa.

Haya hivi karibuni wamejaribu kuchokonoa katika idara za serikali na kuwashawishi madaktari na walimu wanafunzi ,nalo hilo halikufanikiwa leo limezimwa kiurahisi kabisa kwa kuahidiwa kuwa mambo yatatulizwa.

Sasa angalieni tifu la CUF kule Zanzibar leo hii CUF imo kwenye serikali moja kati ya serikali za MUUNGANO ,mnabaki kubeza eti ndoa ,mmeona eei !
CUF imeshafukuza wanachama wake wakuu akina Mapalala ,Salum Msabah ,Jidawi ambao hawajulikani hata wapo wapi na juzi tu Hamadi ,nae miezi yake mitatu ya kupapatika ikimaliza hiyo haijulikani ataangukia wapi inasemekana NCCR yeye na Zitto.


SIO VIBAYA KUOTA NJOZI ZA MCHANA....na fikra zenu za adumu SULTANI! Lakini mnasahau zama zake zishafika ukingoni......huyu hamad rashid unayemtajataja ndio mhusika mkuu katika ANGUKO la MAALIM SEIF kisiasa, subiri kiama chenu tar.13-march-2012.
 
SIO VIBAYA KUOTA NJOZI ZA MCHANA....na fikra zenu za adumu SULTANI! Lakini mnasahau zama zake zishafika ukingoni......huyu hamad rashid unayemtajataja ndio mhusika mkuu katika ANGUKO la MAALIM SEIF kisiasa, subiri kiama chenu tar.13-march-2012.

Wewe na hamad rashid pamoja na mahakama hamtawezi kuiua CUF, mtaaibika na kutaabika sana mnafiki mkubwa
 
HHAHAHHAHAHAHHHAhAHHA, munakereka sana mukiona wana CUF wametulia au vipi?. Musiwe na wasiwasi sisi tupo. Si munajua kama tumo kwenye serikali ya pamoja basi matunda yake ndio kioo cha CUF. Musiwe na wasiwasi tupo BENET br. an sis.
 
katika ndoa wanasema "....na ninyi si wawili tena bali mwili mmoja". Ccm na cuf walifunga ndoa, hivyo si wawili tena bali wamoja; na katika kaya (nyumba) msemaji mkuu ni baba. Hivyo ccm ndiye baba wa hiyo familia yao. Cuf (mke) na ccm(mme).

Pia kumbuka kuwa, pindi tu wawili hao wanapoamua kuingia kwenye maisha ya ndoa basi mmoja wapo anakuwa hana maamuzi kabisa khsiana nasuala la yeye kulala akiwa kavaa au hajavaa chupi!
 
KAFU is resting in pieces, especially after selling their rights to magamb@
 
Wewe na hamad rashid pamoja na mahakama hamtawezi kuiua CUF, mtaaibika na kutaabika sana mnafiki mkubwa
Kama unafiki ni katika kusimama kwenye haki na ukweli mimi aaaah!! roho kwatu na unafiki wangu lakini nijuavyo mimi unafiki ni yale yoote yanayoendelea ndani ya `CUF a.k.a Chuki Ubinafsi na Fitna` Viongozi wametanguliza Ubinafsi na uroho wa madaraka hata siku moja usitaraji kuona chama kinainuka....lazima uozo utolewe ndio CUF kama chama kisimame tena.....bila Umoja na Mshikamano hakuna CUF plus viongozi wenu hao walioko kwa personal interest mnazidi kukichimbia kaburi na wenye akili zao lazima wataondoka tu...
Mahakama haiko kwa kuiua CUF bali inasimamia HAKI na SHERIA wa kuuua CUF ni hao mlowapa madaraka na wanayatumia kwa ajili ya kujinufaisha wenyewe.
HAKi SAWA KWA WOTE.
 
Kwani kazi ya mama si kukaa nyumbani na baba ndo anaonekana barabarani kuseka mlo wa wife
 
Mawazo mgando. Hata agombee sisimizi kwa tiketi ya chadema atashinda, si ukatoliki wala nini


Mkuu umenena. Hakika Chadema imekua kwa namna ya ajabu kabisa, beyond expctations. Naamini hata wazee na wasisi wa hiki chama (Mzee Edwin Mtei na Mzee Bob Makani) wakipumzika watapumzika kwa amani wakiwa na furaha tele kwa kuliachia taifa urithi wa uhakika.

Si mchezo kwa
mazingira yetu ya mfumo kandamizi na wa kifisadi kuanzisha chama kikaimarika na hata kuaminika na umma kiasi cha sisimizi kusimama na akashinda.
Hapa mmetaja kitu ambacho daima nimekuwa nikitkitilia shaka katika siasa zetu za Tanzania. Wananchi wamekuwa wakichagua nembo na rangi za vyama na wala sio watu wa kuwaletea maendeleo. Hayo hayo ya kusimamisha sisimizi, kusimamisha kumbi, alimradi tu liwe la chama fulani linashinda, ndilo kosa walilokuwa na wanaendelea kulifanya CUF na CCM kule Zanzibar.

Tukumbuke kuwa CUF ilipata kuwa chama cha upinzani bungeni kwa msaada mkubwa wa viti kutoka Pemba ambako hata ukiweka sisimizi, wanashinda, wakati huo wakiwa na ushawishi mdogo Tanzania Bara lakini waliweza kuambulia viti vichache. Kuibuka kwa CHADEMA, kumewanyang'anya CUF tonge mdomoni. Lakini kwa Tanzania Bara si ajabu kuona chama kinakua halafu kinakufa. Waangalieni NCCR-Mageuzi, umaarufu uliokuwa nao, sasa uko wapi? Umekufa na badala yake CDM ndio imekuwa maarufu.

Kwa ufupi, vyama vyetu vya upinzani bado vina safari ndefu ya kuondokana na mawazo ya "hata ukisimamisha sisimizi tutashinda". Tuwekeze katika watu wapiganaji na tuache kusimisha sisismizi. Matokeo yake sisimizi hawa leo utakuta wako CCM, kesho CDM, keshokutwa CUF, mtondo NCCR, mtondogoo UDP.

Ujanja si kuchuma ukapata bali kukilinda ulichochuma. Ninawatakia CDM kila la heri katika kulinda walichochuma, vyenginevyo kinaweza kubaki katika historia kama kilivyobakia NCCR na CUF.
 
Mimi nafight cause siyo party..

Bado naamini CUF wako na right cause ndio maana nawaunga mkono,

Chadema hawatakuwa na mvuto siku akiwekwa mkatoliki kule ccm, sahizi wana support kubwa ya wakatoliki; watagawanyika sana come 2015..

Maskini weee.....! Kumbe bado wa hivi mpo lo..!
 
unajua kenge huwa anafikiri kwa kutumia mkia?
Sasa mkia ukiwa haupo inakuwaje?
Figure it out!!

Chama kitakachoonyesha nia ya kuboresha maisha ya watz ndio kitakachopewa dola na watz. Kama staili ya CUF naona nia ni kwenda ikulu na sio maisha ya watz.
 
Huu uchaugzi wa uzini binafsi umenipa mafunzo makuu mawili.

Kwanza:
CUF kama chama cha siasa ni kama kinaelekea kupotea ktk medani ya ushindani wa kisiasa. Kwa kuangalia siasa za zanzibar, kila mtu alijua kungekuwa na ushindani mkubwa kati ya ccm na cuf. Hata hivyo kwa matokeo ya uchaguzi mdogo wa uzini, inaonekana wananchi wameanza kupoteza imani yao kwa cuf na kuamua kukipigia ccm kura. Huenda kutokana na ukweli kwamba cuf na ccm ni chama kimoja-kutokana na cuf kuamua kuungana na ccm.

Pili:
CDM kinaanza kuota mizizi ktk medani ya siasa za zanzibar. Miaka yote ya uchaguzi wa vyama vingi, cdm hawakuwahi kusimamisha mgombea huko visiwani, na kwa mara ya kwanza wameweza kushika nafasi ya pili-ili hali watu walitegemea cuf ingekuwa ya pili na cdm pengine kushika nafasi ya tatu! Ni 'ushindi' huu wa cdm ni ishara mbaya kwa cuf ambacho ndicho kilikuwa chama kikuu cha upinzani zanzibar kabla cuf hawajaamua kuolewa na ccm.

Tusubiri tusikie cuf watatoa tamko gani kwa aibu hii kubwa ya mwaka waliyoipata! Jamani cuf, kaburi hiloooooooooo linawakaribia, poleni sana, ni aibu kwenu ktk medani ya siasa za zanzibar!

Poleni sana wana cuf kwa kudhalilishwa, na hongereni wazanzibari kwa kuamua kutafuta mkombozi wa matatizo yenu kwa kukiamini CDM!
 
Cuf chama cha mamwinyi na watu wenye fikra za kuwa wafalme hakiwezi kukubalika katika Jumuia ya watu waelewa ! to hell CUf
 
Okey,...
nilisema hapa chadema haiwezi kushinda zanzibar
bali uchaguzi huu uta wasaidia sana kujijenga huko.

"Mashabiki" wa chadema via computer wakawa wakali kweli.
haya sasa.
 
Wameyataka wenyewe na akili zao fupi kama mkia.
Waache waangukie pua.
 
a good stat to chadema. peopleeeeeeeeees!!!!!! malizia ndyoko...........
 
Back
Top Bottom